New City
JF-Expert Member
- Apr 17, 2014
- 2,880
- 3,794
Watakuwa wanaleta mzaha, sheng anakufaje kirahisiHivi unaelewa kinachoendelea hapa?
Kwanza jina lake lenyewe sheng yaani kwa kiswahili shenzi [emoji16]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Watakuwa wanaleta mzaha, sheng anakufaje kirahisiHivi unaelewa kinachoendelea hapa?
Sheng itakuwa hajafa ila nina wasiwasi na Shao ndio maana mleta taarifa alikuja kwenye ofisi ya Sheng anahema sanaWatakuwa wanaleta mzaha, sheng anakufaje kirahisi
Kwanza jina lake lenyewe sheng yaani kwa kiswahili shenzi [emoji16]
[emoji3] [emoji3] [emoji2]Watakuwa wanaleta mzaha, sheng anakufaje kirahisi
Kwanza jina lake lenyewe sheng yaani kwa kiswahili shenzi [emoji16]
Hata mimi naona hivyo hivyo.Kesho mbali sana
Ila naona jona akiungana na Miranda kummaliza BC
Kweli mimi sielewi hiki kinachoendelea ila kwa mtazamo wangu Miranda atajiunga na Jona hivyo BC atajikuta mwenye wakati mgumu kuwahi kumtokea[emoji30] [emoji30] [emoji30] hayo ndo maono yangu ila cyapi aslimia nyingiHivi unaelewa kinachoendelea hapa?
Jona cna wasisi nae maana naamini Miranda hawezi kumuacha mwenyewe watalindana, ila sheing inawezekana lakini huruma zangu zinaenda kwa mzungu BC naona ule usemi walisema unaweza kumtoa nyoka kisimani asife na maji halafu akakuuma na ukafa wewe kwa sumu yake, sasa BC kajitahidi jona apone ila atakuja kumuua mwenyewe tena wakisaidiana na Miranda [emoji12] [emoji12] kitu kinakuwa [emoji621] [emoji621] [emoji621] [emoji621] [emoji621]Hivi sheng atakuwa kafa kweli mbona kirahisi hivyo na jona jaman Mungu azidi kumlinda tu
Ngoja tuone kifo chake kitagundulika vipiHuyo kamanda wa polisi alistahili kufa ila sijui kwa nini siamini kama sheng kafa acha nilale
Yule bwana anaweza kufa kirahisi kwasababu moja tuu ,, anajiamini Saaana hiyo ni shida katika vitaWatakuwa wanaleta mzaha, sheng anakufaje kirahisi
Kwanza jina lake lenyewe sheng yaani kwa kiswahili shenzi [emoji16]
And the legend never dieSheng ni rejendary wa Anga, hawa waingereza hawaujui mziki wke !!
Mwenye kujua thamani ya Jona ni Miranda, hivyo BC ameshiriki kidogo japo kwa umuhimu, tatizo ndugu yetu Jona hayupo tayari kutenda dhambi ya kumtukuza muhalifu kisa tu eti kaokoa maisha yake [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] hapa ndo ananimaliza ila kwakuwa Miranda anamjua BC na naamini hawezi muua Jona basi BC kazi anayo tangu sasaIla pamoja na yote Bc amemsaidia sana jona.....vinginevyo angekufa zamani kama isingekua miranda..... kwa akili za kazi jona lazima apewe anachostahili maana kashakua Trash
Salute kwako piaSaruti Steve mollel
*ANGA LA WASHENZI -- 43*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
“Ndio, mkuu. Kazi imeshakwisha!” akaongea mtumishi huyo mwadilifu.
Baada ya lisaa limoja …
Mtumishi huyo akafungua mlango wa sebuleni na kuangaza macho. Sura yake imebeba hofu na mazingira yalikuwa tulivu mno. Mkononi mwake alikuwa amebebelea bunduki ndogo. Haikuchukua muda, akaona mwili wa mheshimiwa pamoja na wa Nade ukiwa umelala kwenye kochi, damu zinawatiririka vichwani!
Akatahamaki. Akawatazama watu hao kwa macho ya bumbuwazi. Akakimbilia napo chumbani kutazama, Miriam hakuwapo! Chumba kilikuwa kitupu, mlango upo wazi.
ENDELEA
Hakuamini kilichotokea, akarudi tena sebuleni na kumtazama bosi wake, kwa mbali alikuwa anahema na kumbe alikuwa amejeruhiwa na risasi kifuani na hapo kichwani alikuwa amepasuliwa na kitu chenye ncha kali.
Akamtazama na Nade, mwanamke huyo alikuwa ahemi kabisa. Hakuonyesha dalili yoyote ya uhai! Mara akasikia sauti ya kuguguma toka kwa mheshimiwa, upesi akamtazama.
"Haaaammm ... "
"Unasemaje mheshimiwa? ..." akasema mlinzi yule akiweka sikio lake mdomoni mwa Eliakimu. Lakini hakusikia tena kitu, mheshimiwa akanyamaza na kutulia tuli.
Amekufa? mlinzi akajiuliza. Akamtikisatikisa mheshimiwa lakini hakufanikiwa abadani. Pengine alikuwa ameenda na maji!
Baada ya muda mchache mbele, waandishi wa habari na vyombo vya usalama vikajaa hapo kila mmoja akitenda kazi yake. Ikabainika wanaume watatu waliovalia vinyago usoni ndiyo walihusika ma mauaji hayo.
"Sijajua ni wakina nani na kwanini wamefanya haya mauaji!" Akasema Alphonce akimwambia Kamanda wa polisi mkoa.
"Hivi mtu huyu alikuwa na adui yoyote kisiasa?" Akauliza kamanda.
"Hapana! Labda pengine, huwezi jua." Akasema Alphonce akiwa anatazama waandishi wa habari wakiwa wanajitahidi kurusha matangazo yao moja kwa moja.
"Lakini mkuu ..." Alphonce akataka sema kitu. Akamtazama Kamanda kwa uso wa 'kumtonya', wakaelekea ndani ya gari la kamanda huyo wapate kuteta.
"Unaiona ile gari pale?" Alphonce akasema akinyooshea kidole taksi iliyokuwa imepaki kwenye ndani ya nyumba ya Eliakimu.
"Ndio, naiona. Ndiyo iliyobeba wauaji?"
"Hapana, ila ndiyo iliyombeba yule kasuku!"
"Kasuku? Una uhakika?" Kamanda akatahamaki.
"Ndio! nina uhakika asilimia mia saba. Ile kazi uliyotupa ya kummaliza ilikuwa inafanyika ndani ya lile gari!"
"Alphonce, embu acha ngonjera. Nyoosha maelezo!"
"Lile gari ndilo lilimbebelea Kasuku leo, na kumbe lilimleta hapa. Wakati unahojiwa na vyombo vya habari nikachukua muda wangu na kulipekua. Lina matundu ya risasi na hata damu!"
"Sasa huyo Kasuku hamkumuua?"
"Hapana, mkuu! Bila shaka atakuwa hajafa. Asingeweza fika hapa."
"Na huyo Kasuku mule ndani hayupo?"
"Hayupo! Yupo mheshimiwa na mwanamke fulani ambaye alikuwa na Kasuku yule ndani ya hilo gari!"
"Sasa Kasuku atakiwa ameenda wapi? Au unataka kunambia yeye ndo atakuwa anahusika na haya mauaji?
"Sijajua! Lakini atakuwa ana cha kueleza kuhusu haya mauaji."
"Lakini Alphonce, unajua unaniangusha sana kwenye hili! Kwanini huyo mtu unashindwa kummaliza? Na kila kitu unacho!"
"Mkuu, Kasuku ni mjanja mno. Ila itafikia mwisho akaingia tegoni tu."
"Hakikisha hiyo siku na sisi tutakuwa bado tupo hai."
"Usijali, mkuu!"
"Najali. Unadhani Kasuku huyu akija kutambua tumemuweka kwenye rada, huoni tutakuwa tupo hatarini? Kasuku yule ni mwekundu, na wa kijani! Anabadilika rangi kwa mujibu wa miale ya jua!"
Kukawa kimya kidogo. Mara, Alphonce akashika kitasa cha mlango wa gari.
"Nakuja!"
"Unaenda wapi?"
"Nimemwona mtu ambaye anaweza kutusaidia kumpata Kasuku!"
Kabla Kamanda hajasema neno, Alphonce akatoka ndani ya gari.
Kamanda akabaki akimtazama wapi anaenda. Akamwona mwanaume huyo akienda kuongea na yule mlinzi aliyesalimika kwa kwenda kumtupa Jona.
Akakodoa macho akifuatilia kila nyendo, punde akamwona Alphonce akimtaka mlinzi yule aelekee kwenye gari alilomo.
Mlinzi huyo akatikisa kichwa ishara ya kukataa, Alphonce akamlazimisha kwa sura ya msisitizo. Mlinzi akaridhia, japo kishingo upande.
Wakazama ndani ya gari wakiketi kwenye viti vya nyuma.
"Haya mwambie huyo!" Alphonce akamwamuru mlinzi yule. Alikuwa amejawa na woga, na macho yake yalikuwa mekundu.
"Tulienda kumtupa!"
"Ulienda kumtupa wapi? Kwanini mlienda kumtupa?" Akauliza Kamanda.
"Tuliamriwa na mheshimiwa. Alikuwa tayari ameshakufa kwasababu ya majeraha ya ajali! Alifika hapa akiwa hoi sana. Hakuchukua muda," mlinzi akalaghai. Mheshimiwa akatabasamu na kumtazama Alphonce kwa macho ya furaha.
"Mheshimiwa, ni mpaka tukihakikisha," akashauri Alphonce.
Basi muda mchache tu, gari la Kamanda likatoka kuelekea kule ambapo Jona alitupwa wakielekezwa na mlinzi wa mheshimiwa. Ikawachukua kama dakika ishirini wakawasili.
"Ndipo hapa!"
Wakashuka na kusonga kwa ndani, wakauona mwili mmoja, haraka Alphonce akaukimbilia na kuchuchumaa kuutazama. Haukuwa wenyewe!
"Nilijua tu! Huyu mbwa hawezi akafa kirahisi hivi!" Akasema Alphonce akisimamama.
"Una uhakika ilikuwa hapa?" Kamanda akamuuliza yule mlinzi.
"Ndiyo, ni hapa kabisa!" Akajibu mlinzi akipepesa macho yake huku na huko.
"Nakumbuka nilimtupia hapa!" Akanyooshea kidole.
"Basi atakuwa ameondoka," akajibu Alphonce, "ila nadhani hatakuwa mbali!"
Wakatafuta pasipo majibu. Jona hakuonekana wapi ameenda. Kumaliza ushahidi, Alphonce akammaliza Mlinzi kwa kumnyonga na kumtupia ndani ya msitu!
"Hakikisha mtu huyu anapatikana na kuuawa! Hakikisha hilo Alphonce!" Alisema Kamanda aking'ata meno.
***
Usiku wa saa sita, La Palma Pub.
"Nataka kuhama pale!" Akasema Glady baada ya kupulizia moshi wa sigara kando.
"Unaenda wapi sasa na kama unavyojua kodi ya pale angalau unaweza kumudu? Au umepata danga jipya mwenzetu?" Mwenzake akauliza. Wote walikuwa wamesimama nje ya pub wakiwa wanavuta sigara. Glady alikuwa amevalia sketi fupi nyeusi na topu nyeupe yenye maneno ya kichina. Mwenzake akiwa amevalia sketi nyekundu yenye mpasuo mpaka kwenye nyonga.
"Hamna si mambo ya madanga wala nini, sema nataka kubadili mazingira tu!"
"Umeanza lini hiyo tabia Glady?"
"Nitaanza hivi karibuni."
Mara mwenzake na Glady akatazama barabarani na kisha akajinyooshea kidole kifuani. Mara akamtazama Glady na kumwambia kwa sura ya kinyonge:
"Unaitwa kule!"
Glady kutazama akaona prado nyeusi. Kioo cha dereva kikashushwa vema, Alphonce akaonekana vema, akamfanyia ishara ya kumwita.
"Kwaheri shost, baadae!" Glady akaaga na kwendaze. Akapanda gari na kuondoka hilo eneo, mwenzake akimtazama.
Ndani ya muda mfupi, mwenzake huyo akasikia simu yake ikinguruma. Akaitoa na kutazama:
"Shosti lazima nipige mshindo kesho tukatumbue!" Ilikuwa ni ujumbe toka kwa Glady. Mwenzake akatabasamu na kuviweka vidole kwenye kioo cha simu, akaandika na kutuma:
"Kamua haswa shoga angu, nakuaminia!"
Akausindikiza ujumbe huo na tabasamu. Akatazama na mambo mengine ndani ya simu yake kabla hajairudisha kwenye mkoba na kuendelea kusimama.
Saa tisa usiku ... Kwachu Best Lodge, Kimara.
"Mimi siwezi kutumia kondom kabisa," alisema Alphonce. Alikuwa amekaa juu ya kitanda akiwa amevalia bukta fupi na yu kifua wazi. Glady alikuwa amebakia na sidiria na kufuli tu, vyote rangize ya pink. Yeye alikuwa amejilaza kitandani.
"Hatujakubaliana kavu!" Akaropoka Glady. "Ukitaka kavu basi ongeza pesa!"
Alphonce akacheka.
"Na vipi kama nisipokupa hiyo pesa? Utafanya nini?" Akauliza kisha akawasha sigareti yake aliyoiweka mdomoni na kuanza kuifyonza. Macho yake yamelegea ila imara. Mdomo wake ulikuwa mkavu ukipinda mithili ya wa samaki.
"Kwanini usinipe?" Glady akauliza.
"Si naamua tu," Alphonce akajibu. Glady akamtazama kwa macho ya hasira pasipo kusema kitu. Ndani yake alishaanza kutengeneza hofu juu ya mwanaume yule. Hakuwa mtu mzuri.
Lakini kwa mujibu wa fikra zake, ni kama vile aliona kitambulisho cha polisi ndani ya gari la mwanaume huyo. Mwanzoni alijihisi salama, kumbe alikosea.
Akili yake ikaanza kurukaruka na kutambalia mazingirani. Akiwa anawaza, mara Alphonce akanyananyuka na kumwambia:
"Nakuja, jiandae!"
Akaelekea chooni kukojoa baada ya kuweka kipisi chake cha sigara kwenye kisosi cha kioo kilichokuwa kipo juu ya kistuli. Aliporejea, akadaka kwanza sigara yake na kupiga pafu mbili za kumalizia.
Lakini kabla hajajimwaga kitandani, akaanza kupoteza uwezo wake wa kuona. Alikuwa anaona kama ukungu mbele yake na kichwa kikawa kinamzumguka, akachukua dakika mbili tu, akadondoka chini kama mzigo!
"Ms*nge wewe!" Glady akasema kwa kebehi kisha akanyanyuka toka kitandani na kumtazama Alphonce.
Alikuwa anavuja damu sakafuni.
Haraka Glady akavaa na kisha akatoa chupa ya mafuta na kitambaa.
Akalowanisha kitambaa mafuta kisha akapaka kwenye nyayo ya kushoto ya Alphonce na mafuta kidogo akayamiminia chini.
Alafu akaenda zake akiwa kabebelea kila kitu cha Alphonce!
****