Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Unajua kuna watu mnakesha kuwatafutia watu ban
Maan ake nin kuquote Uzi alafu wa zamaani zen hauandiki kitu ila ukaona ngoja utusumbue tunaotumia simu au sio?
[emoji119] umeshind mkuu na mbona umetuweza saan
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 46*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Wale wanaume wakampatia masikio. Bwana huyo akawaeleza juu ya Jona. Anataka mwanaume huyo afe kwani aliyempatia hiyo kazi haamini kama ataitekeleza.

Pia akawasihi, “if the woman trouble you, jus kill her."

ENDELEA

Wale wanaume wakabeba maagizo hayo na kwasababu usiku ulikuwa umeingia, wakaenda kupumzika wakilenga kufanya kazi hiyo kesho na huku wakitaka kazi nyingine itafutwe mapema kwani hiyo waliyopewa haitawia hata dakika.

Basi BC akafurahishwa na hilo. Huu usiku wake ukawa mwororo kabisa. Alivuta sigara mpaka akajichokea. Pia akanywa kwa raha zake kamili.

**

Saa saba usiku ...

Japo Shao hakuwa kwenye mipango yake, jambo hili la kuuawa kwake kulimshtua haswa bwana Sheng. Inakuwaje adui anaingia ndani na kummaliza mtu kama Shao?

Adui huyo ni nani na anajiamini kiasi gani hivyo?Na ni kweli alikuwa amemlenga Shao ama yeye?

Akiwa amesimama kandokando ya kaburi la Sheng ambalo lilikua limetoka kuchimbwa muda si mrefu, aliwaza sana. Hata siku hiyo hakuwa na hasira kama kawaida yake.

Alikuwa ametulia na kwa kumtazama tu alionekana kumezwa na lindi kubwa la mawazo. Macho yake yalikuwa mekundu, lips kavu na uso wa njano.

Mwili wa Shao ukazama ndani ya ardhi na kisha ukafukiwa upesi. Yote hayo Sheng akitazama ila asione chochote kwani alikuwa mbali haswa.

Hata kila kitu kilipokamilika, ilibidi Sheng ashtuliwe kwamba kila kitu kimekwisha na sasa akapumzike.

Wakati huo walinzi wakiwa wanatetemeka kwa hofu. Walijua Sheng atawamaliza kwa kile anachokiita uzembe.

Ila kinyume kabisa na mawazo yao, Sheng hakutia neno. Na kwa ukimya kabisa akajigeukia na kwendaze. Akajiweka kitini sebuleni na kuendelea kuwaza sana.

Alikosa amani na raha kabisa. Alijitathmini namna mambo yalivyoenda hapa karibuni. Pasipo kutarajia akajikuta anatoa chozi. Chozi la simba.

Aling'ata meno yake kwanguvu akimeza mate yaliyokuwa na ladha ya klorokwini.

Mara hodi ikagonga. Hajasema kitu, mtu akazama ndani. Alikuwa ni mwanaume yule aliyekuja kumpasha habari ya kifo cha Sheng. Mwanaume mrefu aliyevalia tisheti nyepesi nyeupe na suruali ya kadeti rangi nyeusi.

Alikaa kitini na kumtazana Sheng kwa sekunde kadhaa kabla hajashusha pumzi ndefu na kuanza kuteta. Ni kama vile Sheng hakuwa anajali anachosema kwani alikuwa anatazama pembeni kwa umakini.

Ila masikio yake yalikuwa yanadaka kila jambo hapa. Yalikuwa makini kuliko kawaida.

“Wauaji walikuwa ni wazungu. Waliruka ndani na kuwamaliza walinzi takribani nane kabla hawajafika nyumbani kwa Shao. Ni watu wenye ujuzi wa hali ya juu. Walikuwa ni watatu ila walifanya tukio hilo kwa muda mfupi.

Na japo waliua watu wengi, ilifanyika ndani ya muda mchache mno kiasi cha kutokujulikana! Na baada tu ya kummaliza Shao waliondoka zao. Hatujajua walitumia usafiri gani kwani hawakubakiza alama yoyote ile.

Na hatujajua kwanini wamemuua Shao. Na walilenga haswa kummaliza yeye kwani walimnyookea na kummaliza na kisha wakapotea!"

Sheng akafikicha pua yake pasipo kusema jambo. Akamtazama kijakazi wake huyo na kumwonyeshea ishara ya kichwa akimtaka aende, naye kijakazi akaenda zake kumpatia faragha.

Sheng akaendelea kuwaza. Na baada ya muda ndipo akafungua kinywa na kusema neno moja, “Brown!"

Kisha hakusema tena neno lingine lolote mpaka usiku huu unaishilia zake.

**

Saa nane usiku...

Tap! Sauti ya chupa ililia baada ya kugonga meza. Kinoo akanguruma kama simba kupooza koo lake kwa pombe kali aliyogida.

Akapiga kichwa chake kofi na kukitikisa kisha akamtazama mkewe, bibie Sarah. Macho ya mwanaume huyu yalikuwa mekundu haswa yakirembua.

Kwenye sebule yao mezani kulikuwa kuna ‘bapa' mbili na kopo kubwa la juisi ya embe. Juisi hii ilikuwa ni ya Sarah na bapa hizi zilikuwa ni za Kinoo. Tayari alishamaliza moja, hii ya pili ilikuwa nusu sasa.

Tayari Kinoo alishachanganya waya kichwani. Hakuwa sawa na alikwishalegea, ila kwa upande wa Sarah bado alikuwa ngangari. Japo macho yake yalikuwa mekundu kwa usingizi, alikuwa anajitahidi ‘kukaza'.

Kuna lengo alitaka litimie. Hakutaka kulaza jahazi.

“kwahiyo wewe sasa umeamuaje? Umekubali kirahisi hivyo?" Akauliza akimkuna Kinoo kidevu.

“ah-ah! Mimi sio bwege unajua!" Kinoo akajitapa kilevi. “mimi natazama tu. Najua watazama kwenye anga zangu tuuu ... Mimi," akajipigapiga kifua. “mimi ndiyo Kinoo wa Kunikavu! Kisiki walichoshindwa wakata mkaaa!"

Aliposema hayo akatulia kama mtu aliyepitiwa na usingizi.

“ila mume wangu mi' n'na wazo," Sarah akateta akichezea kifua cha Kinoo. “wewe sasa hivi si waekutenga, wanakuona hufai, huna mana! ... Unaonaje na sisi tukamwaga mboga kabisa!"

Kinoo akaguna kwa mbali kuitikia. Sarah akaendelea kunena,

“Unaonaje tukatoa taarifa za yule jamaa, tukapiga mpunga mrefu tukafanya yetu mbele kwa mbele huko. Nani atajua?"

Kinoo akagunia kooni, “mmmmhhh!" Kisha akapambana kufungua macho yake ya kilevi. Akamtazama mkewe.

Sarah akaendelea kunena, “usiwe kama boya, watu washakuchoka, shika lako tembea mbele. Utakuja kujuta baadae nakwambia."

Kinoo akanyaka kwanza chupa ya kileo, akanyonya mafundo kadhaa kana kwamba anakunywa juisi. Kisha akaiweka chupa mezani na kusema, “tatizo nini unajua .. Sijajua wapi walipomweka huyo bwege!" Akakohoa kidogo na kusema, “ila ngoja..." Akayoosha kidole juu.

“nitafanya mchongo mmoja, mmoja tu, nitajua kila kitu alafu kama mbwai na iwe mbwai tu," akajivuna kilevi kisha akanyanyua tena kilevi na kupiga fundo kadhaa, sasa akamaliza na yeye akalala papo hapo.

**

Saa tano asubuhi ...

“Kino! Kino!" Sauti ya kike ilisikika kwa mbali ikiita. “we Kino, amka bana simu yako inaita!"

Kinoo akaufinyanga uso wake na kuangaza. Kichwa kilikuwa kinamgonga haswa, alijilaza palepale kitini kwa usiku huo mzima.

Macho mekundu na mwili wa kichovu.

Kabla hajasema kitu Sarah akamkabidhi simu inayoita mkononi. Kutazama akaona ni Miranda. Akapokea na kuiweka sikioni.

“... Nipo home! ... Saa hii? ... Kuna ishu gani? ... Basi nipe kama robo saa ..."

Simu ikakatwa.

“kuna nini?" Sarah akawahi kuuliza. Kinoo akajikusanya na kunyanyuka zake. Alisema maneno kadhaa tu, “mambo yameharibika huko!" Kisha akayeya zake.

Sarah akapaza sauti kumkubushia kile walichoongea usiku wake.

“usisahau basi ile ishuu!"

Kinoo akafungua geti na kwenda zake. Sijui kama alisikia ama alipuuzia.

**

Saa nane mchana ...

“I think there is something for you, boss," alisema jamaa mmoja wa wale wanaume wa kazi toka Uingereza. Mkononi alikuwa amebebelea mfuko mkubwa mweusi wa rambo. Macho yake yalikuwa yanamtazama BC aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha mbao bustanini.

“what is that?" BC akauliza kabla hajapokea mfuko huo.

“I don't know. Somebody on a bike delivered it," alisema bwana yule wa kizungu. Bado mkononi akiwa ameshikilia mfuko huo.

“we have scanned it. It is not a bomb."

“Open it," BC akaagiza.

Bwana yule aliyeleta mzigo akauweka chini na kuufungua. Ndani akakuta kichwa cha binadamu!

Kichwa hiki kilikuwa cha bwana Graham, bwana aliyeenda zake asubuhi ya siku hii kwenda kutimiza agizo la Bwana Brown la kummaliza Miranda na Jona.

Kwenye mdomo wake alikuwa ana karatasi yenye ujumbe.

**
 
Tank you Steve tupo active sana na ww kaka acha nisome kabisa hesabu y kesho ni ingine hiyo
 
Duh huu moto habari brown kaisha hapo Miranda + jona
Njooni ni wahadithie xxx men hili movie
 
Steve mkuu wangu pls ongeza kamoja bosi wangu dah!!!
 
Miranda na Jona washaanza kutema cheche kwa BC sasa kazi imeanza na akija kujua sheng yupo hai atakufa kwa hasira, huyu jamaa alopeleka mfuko wenye kichwa atakua Jona huyu maana ndo namjua kuwa akili zake zinamtosha mwenyewe
 
Uzidi kubarikiwa sana mkuu kwa kazi nzur unayojitolea ya kutuburudisha
 
Back
Top Bottom