*ANGA LA WASHENZI II --- 55*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Na hata lile cadillac nyeusi waliyoiona wakati wanakuja, nayo haikuwapo. Wakatazamana kwa bumbuwazi.
Wakatazama huku na kule, hakukuwa na kitu mbali na kiwanda kilichochoka na kufubaa. Mazingira yalikuwa kimya mno. Majani na matawi ya miti yaliyumbishwa na upepo, kisha yakatulia.
ENDELEA
Ndani ya dakika moja na sekunde mbili, watu wale watano waliokuwa wamembebelea Sheng kumwokoa, wakawa wamedondoka chini isijulikane nini kiliwaangusha.
Alah! Baada ya muda kidogo vichwa vyao vikaanza kuvuja damu kulowanisha nyasi na mchanga. Na kumbe vilikuwa vimetobolewa na ncha za risasi!
Risasi hizi zilikuwa zimetokea wapi? … kwa umbali wa kilomita moja na hatua kadhaa, kule juu kabisa ya chumba kimojawapo kilichopo ndani ya kiwanda, ndipo risasi zilipotoka.
Na basi hazikupiga kelele hata kidogo maana midomo ya bunduki ilikuwa imemezwa na viwamba vya kumezea sauti.
Watu hao watano, the intelectual instinct, wakatoka wakiwa wanatembea mwendo wa kubarizi fukweni mwa bahari, wakawaendea watu hao wavamizi, ambao kwa sasa wamekuwa miili tu, wakamnyanyua bwana Sheng na kurudi naye ndani.
“How did they know we are here?” akauliza mwanaume mmoja wa kizungu. Nadhani kwa sasa ni vema tukawatambua kwa majina ili iwe vema, huyu aliyeuliza aitwa Denmark, wenzake wanne ni, Sweden, Ireland, Scotland na Wales.
“We have to know that,” akasema Scotland kisha akamtazama bwana Sheng aliyekuwa amelala hajiielewi. “And we have to before it’s too late.”
“There must be a thing here,” akadakia Denmark. Naye pia akimtazama bwana Sheng. Macho yao wote yalikuwa ya kijanjajanja sana. Na sura zao za watu wa mafikirio ya mbele. “I think we have to take him home,” akashauri bwana Denmark.
Basi wakamtoa bwana Sheng na kumweka kwenye gari yao mpaka eneo wanapokaa. Huko wakamfanyia bwana Sheng ‘scanning’ ya mwili na kubaini ana chip ndani yake. Wakaitoa na Denmark akadhamiria kuiharibu.
“No, don’t do that,” akasema Scotland. Alikuwa ni mwanaume mwenye mwili mpana kuzidi wote. “We need that chip.”
“Yah!” akadakia Wales na kuongezea, “It’ll help us getting the rest of them.”
***
Saa nane mchana ….
Beep … beep … beep … beep
Sauti kwa mbali ilisikika masikioni mwake. Alihisi mwili wake mzito. Alijaribu kufurukuta ila alishindwa. Alihisi viungo vyake vya mwili huenda vimepooza.
Ila hakuchoka kujaribu kupambana kutoka katika wimbi hili la giza. Alihangaika na hatimaye, kama mtu aliyetoka kunusurika kuzama kwenye maji ya kina kirefu, akakurupuka akivuta hewa mafundo makubwa makubwa.
Akatazama kushoto na kulia. Tumbo likamvuta kwa maumivu makali ambayo alishindwa kupambana nayo, akajikuta anarudisha kichwa chake upesi kwenye mto akigugumia maumivu.
Tumboni alikuwa ana bandeji iliyohifadhi jeraha lake la risasi. Pia kwenye mguu wake wa kushoto alikuwa na jeraha la risasi iliyomparasa. Kichwa kilikuwa kinamuuma na fikira zikiwa nzito kuvutika.
Akashusha pumzi ndefu. Akaperuzi chumba alichomo, akagundua ni hospitali tena ya kisasa. Akajiuliza amefikaje hapo, kuna mtu aliyemleta? Hakukumbuka hata tone. Akatazama tena kushoto na kulia.
Kidogo baada ya kutulia akakumbuka namna alivyoingia matatizoni. Mara ya mwisho kuwa na fahamu alivamiwa na kupokonywa kila alichokuwa nacho. Kulitambua hilo kukamfanya azame zaidi mawazoni. Ilikuwa ni kama vile amechokoza fikra.
Akawaza tukio zima na namna ilivyokuwa. Ina maana yule afisa wa serikali alimzunguka? Alijiuliza. Mara mlango ukafunguliwa akaingia nesi, mwanadada mchanga wa kichina. Uso wake ulikuwa mfupi wenye miwani ndogo ya kumsaidia kuona.
Alipomwona mgonjwa wake, akatabasamu na kumuuliza hali yake. Lee, ambaye ndiye mgonjwa, akamwambia anaendelea vizuri. Ila naye akarusha swali juu ya nani aliyemleta hapo maana kuwapo hospitali kama ile, yenye hadhi, haileti mantiki kuletwa na wasamaria.
Nesi akatabasamu, akiwa ameweka mikono yake kwenye mifuko ya koti, akamwambia Lee kuwa ni wasamaria ndiyo walimleta. Na kwasababu ya kitambulisho chake ndiyo maana wakamleta mahali hapo.
Baada ya kujibu hivyo, akamuaga na kumtaka apumzike. Atakuja kumwona tena baadae. Basi akaendaze.
Lee akabaki akiwaza kuhusu hicho kitambulisho ambacho nesi alikiongelea. Akakumbuka ni cha ‘member’ wa familia ya Wu. Alikiweka kitambulisho hicho nyuma ya mfuko wake wa suruali baada ya kusisitiziwa afanye hivyo kabla hajatoka makao makuu.
Akiwa bado fikirani, ghafla anasikia sauti ya kelele na mara inakoma na kuwa kimya kama awali! Anapata shaka. Punde kidogo, anaona kivuli cha mtu mlangoni. Kwa maana mlango ulikuwa umegawanywa nusu ya chini ‘material’ ya mbao na ile nusu ya juu, kioo cha kufifia.
Kivuli hicho kilikuwa ni cha mwanaume mwenye mwili mpana, na kichwa chake alikuwa amekihifadhi na kofia ya wale wapanda farasi.
Mlango ukafunguka …
**
Saa tatu usiku …
Sauti ya mtu akiteta kwenye simu akitumia lugha ya kichina ilisikika toka dirishani. Sauti hiyo ilidumu kwa dakika tatu tu alafu simu ikakata. Baada ya muda mfupi wakaja wanaume watano ndani ya hiyo nyumba, na maongezi yakafanyika.
Bado sauti zao zilikuwa zinatoka dirishani. Na kwasababu dirisha lilikuwa mbali kidogo na sebule, hawakusikika vema nini wanateta. Baada ya kama robo saa, wale wanaume wakatoka na kwenda zao. Nyumba hii ikadumu mwangani kwa dakika kumi, kisha ikawa gizani.
**
Saa nne usiku …
“It’s time,” Wales alimtonya Denmark aliyekuwa ameketi sebuleni. Mwanaume huyo wa kizungu akanyanyuka na kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha mwisho. Hata sasa kwakuwa ni usiku wa kulala wote walikuwa wamevalia nguo nyepesi na si suti zao kama ilivyo ada.
Kwenye chumba hicho cha mwisho, ndani alikuwapo Sheng akiwa amewekwa kitini. Alionekana mdhaifu asiye na nguvu. Macho yake yalikuwa yanarembua na hata mdomo wake alikuwa anapata shida kuufumba.
“Hey …” Denmark akaita akimpigapiga Sheng vikofi vya shavu. Kisha akaketi kwenye kiti mbele ya Sheng, nyuma yake Wales na Scotland wakiwa wamesimama.
“Don’t worry it is going to be easy and fast. I won’t last long,” alisema Denmark akimtazama Sheng ndani ya macho yake madhaifu.
“So tell me who are you?” Denmark akauliza.
“My name is Sheng Ping. The East African zonal manager of Wu clan and family from Hongkong, China,” Sheng akajibu vema, hata Denmark akatabasamu na kuwatazama wenzake., “I think we’ve got it.”
Kila alilouliza, Sheng akawa mwepesi wa ndimi basi akafunguka anavyotakiwa. Watu wale walipopata kila walichokitaka katika ‘tape’, Denmark akanyanyuka na kukoki bunduki yake.
“It’s time to die, pal.” akainyooshea mdomo wake kwenye paji la uso la mwanaume huyo, ila kabla hajaifyatua, Scotland akamgusa bega lake na kumwambia, “We still need him.”
“Are you sure?” Denmark akauliza. Kidole chake kilikuwa tufeni.
“Yes, I am sure, we do,” Scotland akajibu. Basi Denmark akashusha silaha yake na kuichomeka kiunoni.
***
Saa nne asubuhi …
“Ndiyo hapa!” akasema mwanaume mmoja mwenye sura mbovu. Alikuwa ni dereva wa gari hili, Murrano rangi ya fedha. Ndani yake kulikuwa na wanaume watano waliobebelea silaha. Na hapa walipokuwa wamesimamisha gari ilikuwa mbele ya nyumba fulani, ghorofa, ambayo haijamaliziwa.
Basi wanaume wale wakashuka wote, na hao wakazama ndani ya jengo hilo. Ndani ya muda mfupi wakatoka wakiwa wamembeba Sheng.
Walimkuta akiwa amelala chini hajiwezi. Wakamsweka ndani ya gari na kutimka pasipo kupoteza muda.
Basi Scotland akatokea mbali kidogo na nyumba hiyo akiwa anatazama gari likiyoyoma, na simu yake ipo sikioni, akasema, “It is on the right track.” kisha akakata simu na kuidumbukiza mfukoni.
***