Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Du!! Kama utamu unakata vile Lakini Stive mtu wetu mambo yakikaa sawa atatoboza tu. I will never give up.
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 56*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Walimkuta akiwa amelala chini hajiwezi. Wakamsweka ndani ya gari na kutimka pasipo kupoteza muda.

Basi Scotland akatokea mbali kidogo na nyumba hiyo akiwa anatazama gari likiyoyoma, na simu yake ipo sikioni, akasema, “It is on the right track.” kisha akakata simu na kuidumbukiza mfukoni.

ENDELEA

Baada ya dakika moja tangu mlango ulipogongwa, ukafunguliwa na kichwa cha mchina kutokeza nje. Kutazamana, akaona Sheng akiwa kabebelewa na wanaume aliowaagiza basi akawapokea na Sheng akaingizwa ndani na kisha maongezi machache yakachukua nafasi.

“Hatukukuta mtu yeyote, isipokuwa mwili wake tu,” yule dereva mwenye sura mbovu aliteta.

“Hatujajua wamemfanyia nini, na hatujajua ni wakina nani kwa lengo gani.”

Basi yule mchina akaguna akimtazama Sheng kwa macho makini. Akatulia kidogo na kusema mawazo yake.

“Kwa asilimia zote watakuwa ni watu wa yule mzungu ambaye Sheng alimuua. Ila kwanini hawakummaliza kwa muda wote huo? Ni nini walikuwa wanafanya naye?” Hata yeye akapatwa na maswali.

Basi isiwe na haja kwa muda huo, ilikuwa ni lazimu bwana Sheng apewe huduma haraka asije fia kwenye ‘mikono salama’. Daktari wa mule mule ndani akaitwa na kumfanyia ‘diagnosis’, baada ya hapo akamtundikia dripu na kutaka kufanya maongezi machache na yule bwana wa kichina.

Daktari huyu alikuwa ni mwanaume mzee mwenye kiwaraza kichwani. Sura ya upole na macho ya hekima za utu uzima. Alivalia koti jeupe ambalo lilionekana kumvaa kutokana na ufupi wake.

Akasafisha koo na kusema, “Bwana huyu ametiliwa sumu.” Aliongea kwa uhakika, ila sauti yake ikiwa chini. “Afya yake ni dhalili hivyo anahitaji uangalizi wa juu mno.” aliposema hayo akakohoa kidogo na kuvuta hewa ndefu kwa pua, kisha, “Namhitaji kule eneo langu la kazi kwa uangalizi zaidi.”

Sasa ameshasema daktari, yule bwana wa kichina akawa hana kipingamizi. Kikubwa akaongozana na daktari mpaka huko ambapo Sheng alipelekwa, akaingizwa ndani ya chumba maalum, ndani ya jengo litumikalo kama sehemu ya kutoa huduma za matibabu ndani ya eneo hilo.

Humo ndani kulikuwa kuna mazingira tulivu, na hata wahudumu wa kutosha, wa China na hata wa hapa nchini.

“Inatosha, yupo mikono salama, waweza kwenda,” alisema Daktari akimtazama bwana yule wa kichina. Naye pasipo kubisha akaendaze. Ila akiwa na maswali kichwani.

Sasa ufisadi wake ulikuwa hatiani. Endapo Sheng akisimama kwa miguu yake ni wazi hatabakizwa na pumzi. Hata akajikuta tumbo likimuuma na kichwa pia.

Baadae, kwenye majira ya saa mbili usiku, akatoka ndani, akiwa amejipaki ndani ya gari nyeusi aina ya discovery, akaelekea zake viwanja akiwa ameongozana na vijana wake watatu wa kazi.

Alilenga kupumzisha kichwa chake kwa mawazo, lakini pia alikuwa na mawazo fulani ambayo alitaka kuwashirikisha hawa vijana wake watatu ambao alikuwa amependezwa nao.


***

Saa sita kuelekea saa saba usiku …

Kuna sauti kubwa ya muziki hapa. Watu wengine wapo ndani ya kiwanja wakijibetua na kunengua kwa mujibu wa midundo ya muziki huo. Wengine walikuwa wamekaa kwenye makochi, na wengine wakiwa wameshikana, wanatomasana ama wamesimama tu wakiongea kana kwamba wanasikiana dhidi ya muziki huu mkubwa.

Mwanga ulikuwa hafifu, ila hewa ya kutosha. Kote palikuwa pametawaliwa na kiza, ila vijitaa vidogodogo vyekundu, vya njano, vya kijani na vya kila rangi vikipitapita huku na huko.

Mahali hapa palikuwa ni klabu ya usiku.

Wakiwa wamekaa kaunta, kila mmoja ana kinywaji chake, na hapo tayari wameshakunywa kadha wa kadha, yule bwana wa kichina, aidha kwa kuona sasa ni muda muafaka wa kuteta, akasema,

“Mmetosheka?”

Wale mabwana alioongozana nao wasiseme kitu, wakatabasamu. Ishara ya kwamba bado ni muda mchanga. Basi yule bwana wa kichina akawaambia wanywe mpaka waseme wenyewe basi.

Lakini wakiendelea huku kunywa, akaendea adhma yake.

“Nataka muwe watu wakubwa sana. Nafikiria kuwapa nafasi nyeti sana pale kitengoni. Mwaonaje?” japo muziki ulikuwa mkubwa, sauti yake nyembamba ya kichina ilipasua na kusikika vema. Wale mabwana wakatabasamu.

Ni wazi pande la nofu la nyama liliwekwa mezani mwa mabwana fisi.

“Aaah safi tu!” akasema bwana mmoja. “Tupo tayari kabisa, au mwasemaje?”

“Yah! Sisi hatuna shida kabisa!” wenzake wakamuunga mkono na tena huku usoni wakijawa na matabasamu ya kiroho, na hata kujichekesha pasipo na msingi.

“You know, nimetazama nikaona mnanifaa sana,” akasema bwana yule wa kichina. “kati ya watu wote nikaona ninyi ndiyo watu wa kutenda kazi na mimi … mna nguvu, na intelligent …” bwana huyu wa kichina akaweka kituo kwa kunywa kwanza fundo moja la kinywaji chake, kisha akaendelea wakati hadhira wake wakimsikiza kwa umakini.

“Ila sasa kuna tatizo moja, moja tu, moja!”

“Lipi hilo?” akauliza mmoja wa mabwana wale. Basi yule bwana wa kichina akanyamaza kwanza, kama mtu anayefikiria, kisha akauliza,

“How far can you go to get this?”

“Uncountable miles,” akasema bwana mmoja. Huyu alikuwa karibu zaidi na bwana huyu wa kichina. Na maneno yake haya yakamfurahisha bwana huyo, akatabasamu, “That’s nice. If then, I have a work for you to do.”

Basi akawaeleza kazi hiyo na alipomaliza kuwaeleza, wakapeana mikono ya kukubaliana. Ila bwana mmoja, yule aliyekaa mbali na bwana huyu wa kichina, akawa na shaka. Akauliza,

“Vipi kuhusu wengine?”

“Wengine!” mwenzake aliye jirani akatahamaki. “Hapa duniani ulizaliwa na nani? Jiangalie wewe ndugu yangu, acha ufala!”

Kuliunga hilo mkono, wengine wakacheka na kisha wakaendelea kunywa na kunywa. Baadae kwenye majira ya saa nane kasoro, bwana yule wa kichina akaona inatosha, basi akawataka waondoke. Ila akaona ni vema kama akipata mwanamke mmoja wa kwenda kumpunguza uzito kwa usiku huo.

Akamwamgiza mmoja wa wale jamaa aliokuja nao amtafutie mwanamke mzuri wa kwenda naye. Pasipo hiyana mwanaume huyo akafanya kazi na ndani ya muda mfupi akarejea na mwanamke mzuri kabisa, mweupe mwenye figa ya kuzembesha.

Na mwanamke huyu, kama bahati au nuksi, alikuwa ni Glady.

Bwana yule wa kichina akapendezwa naye hakika, wakaondoka naye kwenda kujipaki garini warudi makaoni.


**

Mazingira haya hayakuwa mageni. Ni kama vile aliwahi kufika huku, kumbukumbu zake zilimweleza bayana. Alijitahidi kutazama barabara na mazingira, akajikuta anapata picha fulani.

Na kweli hakuwa amekosea kabisa. Macho yake hayakuwa yanamdanganya, hili eneo si geni kwake. Na alipotuliza kichwa vema sasa akakumbuka. Mahali huku alishawahi kumleta yule mwanaume wa kichina aitwaye Lee.

Glady akaminyua mdomo wake. Hapa kidogo akamkumbuka mwanaume yule wa kichina, Lee. Na basi akajikuta anachukua simu yake na kupekua kama jina lake lipo kwenye simu. Akaliona.

Akataka kutext, akasita. Litakuwa jambo la kipumbavu akifanya hivyo. Basi akatulia kwanza akiwaza ujinga fulani kichwani mwake. Punde sauti ya honi ikamtoa fikirani. Walikuwa wameshafika getini. Geti likafunguliwa, wakazama ndani.

Ndimo humu humu! Akaendelea kuhakikisha. Ndimo humu humu alipomleta Lee. Macho yake ya wizi yakawa yanaangaza sana, huku na kule mpaka gari kusimama na kuongozana na wanaume wale kwenda kwenye makazi ya yule mchina.

Yeye akaamriwa aingie ndani, na yule bwana wa kichina akabaki na wale mabwana wengine pale mlangoni. Akateta nao kwa sauti isiyosikika vema, na kisha wakafunga mjadala kwa mchina yule akisema, “Msiniangushe!” wanaume hao wakaondoka zao, bwana yule wa kichina akazama ndani.

Akavua nguo na kwenda kuoga akimwacha Glady peke yake.

Glady akatazama huku na kule. Kimini chake akakivuta akibadilisha pozi la kukunja nne. Punde akanyanyuka na kuchungulia dirishani. Akaangaza nje akijaribu kufikiria ni upande upi yalipo makazi ya Lee. Muda kidogo, akasikia mlango wa bafu ukifunguliwa, basi akarejea kitini.

“Kaoge,” yule mchina akamwambia Glady. Glady akanyanyuka na kwenda bafuni. Akaoga akiwaza kuhusu Lee. Kabla hajatoka, akasikia sauti ya yule mchina huko chumbani. Alikuwa anaongea na simu.

“Hakikisha anakufa kabisa, sawa?”

Glady akashtuka. Akapatwa na maulizo kichwani. Sasa akapata picha juu ya nini yule bwana wa kichina alikuwa anaongea na wale wajamaa. Akaguna. Akapiga moyo konde na kutoka bafuni. Akaketi kitandani.

Bado bwana yule wa kichina alikuwa anaongea na simu.


***
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 56*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Walimkuta akiwa amelala chini hajiwezi. Wakamsweka ndani ya gari na kutimka pasipo kupoteza muda.

Basi Scotland akatokea mbali kidogo na nyumba hiyo akiwa anatazama gari likiyoyoma, na simu yake ipo sikioni, akasema, “It is on the right track.” kisha akakata simu na kuidumbukiza mfukoni.

ENDELEA

Baada ya dakika moja tangu mlango ulipogongwa, ukafunguliwa na kichwa cha mchina kutokeza nje. Kutazamana, akaona Sheng akiwa kabebelewa na wanaume aliowaagiza basi akawapokea na Sheng akaingizwa ndani na kisha maongezi machache yakachukua nafasi.

“Hatukukuta mtu yeyote, isipokuwa mwili wake tu,” yule dereva mwenye sura mbovu aliteta.

“Hatujajua wamemfanyia nini, na hatujajua ni wakina nani kwa lengo gani.”

Basi yule mchina akaguna akimtazama Sheng kwa macho makini. Akatulia kidogo na kusema mawazo yake.

“Kwa asilimia zote watakuwa ni watu wa yule mzungu ambaye Sheng alimuua. Ila kwanini hawakummaliza kwa muda wote huo? Ni nini walikuwa wanafanya naye?” Hata yeye akapatwa na maswali.

Basi isiwe na haja kwa muda huo, ilikuwa ni lazimu bwana Sheng apewe huduma haraka asije fia kwenye ‘mikono salama’. Daktari wa mule mule ndani akaitwa na kumfanyia ‘diagnosis’, baada ya hapo akamtundikia dripu na kutaka kufanya maongezi machache na yule bwana wa kichina.

Daktari huyu alikuwa ni mwanaume mzee mwenye kiwaraza kichwani. Sura ya upole na macho ya hekima za utu uzima. Alivalia koti jeupe ambalo lilionekana kumvaa kutokana na ufupi wake.

Akasafisha koo na kusema, “Bwana huyu ametiliwa sumu.” Aliongea kwa uhakika, ila sauti yake ikiwa chini. “Afya yake ni dhalili hivyo anahitaji uangalizi wa juu mno.” aliposema hayo akakohoa kidogo na kuvuta hewa ndefu kwa pua, kisha, “Namhitaji kule eneo langu la kazi kwa uangalizi zaidi.”

Sasa ameshasema daktari, yule bwana wa kichina akawa hana kipingamizi. Kikubwa akaongozana na daktari mpaka huko ambapo Sheng alipelekwa, akaingizwa ndani ya chumba maalum, ndani ya jengo litumikalo kama sehemu ya kutoa huduma za matibabu ndani ya eneo hilo.

Humo ndani kulikuwa kuna mazingira tulivu, na hata wahudumu wa kutosha, wa China na hata wa hapa nchini.

“Inatosha, yupo mikono salama, waweza kwenda,” alisema Daktari akimtazama bwana yule wa kichina. Naye pasipo kubisha akaendaze. Ila akiwa na maswali kichwani.

Sasa ufisadi wake ulikuwa hatiani. Endapo Sheng akisimama kwa miguu yake ni wazi hatabakizwa na pumzi. Hata akajikuta tumbo likimuuma na kichwa pia.

Baadae, kwenye majira ya saa mbili usiku, akatoka ndani, akiwa amejipaki ndani ya gari nyeusi aina ya discovery, akaelekea zake viwanja akiwa ameongozana na vijana wake watatu wa kazi.

Alilenga kupumzisha kichwa chake kwa mawazo, lakini pia alikuwa na mawazo fulani ambayo alitaka kuwashirikisha hawa vijana wake watatu ambao alikuwa amependezwa nao.


***

Saa sita kuelekea saa saba usiku …

Kuna sauti kubwa ya muziki hapa. Watu wengine wapo ndani ya kiwanja wakijibetua na kunengua kwa mujibu wa midundo ya muziki huo. Wengine walikuwa wamekaa kwenye makochi, na wengine wakiwa wameshikana, wanatomasana ama wamesimama tu wakiongea kana kwamba wanasikiana dhidi ya muziki huu mkubwa.

Mwanga ulikuwa hafifu, ila hewa ya kutosha. Kote palikuwa pametawaliwa na kiza, ila vijitaa vidogodogo vyekundu, vya njano, vya kijani na vya kila rangi vikipitapita huku na huko.

Mahali hapa palikuwa ni klabu ya usiku.

Wakiwa wamekaa kaunta, kila mmoja ana kinywaji chake, na hapo tayari wameshakunywa kadha wa kadha, yule bwana wa kichina, aidha kwa kuona sasa ni muda muafaka wa kuteta, akasema,

“Mmetosheka?”

Wale mabwana alioongozana nao wasiseme kitu, wakatabasamu. Ishara ya kwamba bado ni muda mchanga. Basi yule bwana wa kichina akawaambia wanywe mpaka waseme wenyewe basi.

Lakini wakiendelea huku kunywa, akaendea adhma yake.

“Nataka muwe watu wakubwa sana. Nafikiria kuwapa nafasi nyeti sana pale kitengoni. Mwaonaje?” japo muziki ulikuwa mkubwa, sauti yake nyembamba ya kichina ilipasua na kusikika vema. Wale mabwana wakatabasamu.

Ni wazi pande la nofu la nyama liliwekwa mezani mwa mabwana fisi.

“Aaah safi tu!” akasema bwana mmoja. “Tupo tayari kabisa, au mwasemaje?”

“Yah! Sisi hatuna shida kabisa!” wenzake wakamuunga mkono na tena huku usoni wakijawa na matabasamu ya kiroho, na hata kujichekesha pasipo na msingi.

“You know, nimetazama nikaona mnanifaa sana,” akasema bwana yule wa kichina. “kati ya watu wote nikaona ninyi ndiyo watu wa kutenda kazi na mimi … mna nguvu, na intelligent …” bwana huyu wa kichina akaweka kituo kwa kunywa kwanza fundo moja la kinywaji chake, kisha akaendelea wakati hadhira wake wakimsikiza kwa umakini.

“Ila sasa kuna tatizo moja, moja tu, moja!”

“Lipi hilo?” akauliza mmoja wa mabwana wale. Basi yule bwana wa kichina akanyamaza kwanza, kama mtu anayefikiria, kisha akauliza,

“How far can you go to get this?”

“Uncountable miles,” akasema bwana mmoja. Huyu alikuwa karibu zaidi na bwana huyu wa kichina. Na maneno yake haya yakamfurahisha bwana huyo, akatabasamu, “That’s nice. If then, I have a work for you to do.”

Basi akawaeleza kazi hiyo na alipomaliza kuwaeleza, wakapeana mikono ya kukubaliana. Ila bwana mmoja, yule aliyekaa mbali na bwana huyu wa kichina, akawa na shaka. Akauliza,

“Vipi kuhusu wengine?”

“Wengine!” mwenzake aliye jirani akatahamaki. “Hapa duniani ulizaliwa na nani? Jiangalie wewe ndugu yangu, acha ufala!”

Kuliunga hilo mkono, wengine wakacheka na kisha wakaendelea kunywa na kunywa. Baadae kwenye majira ya saa nane kasoro, bwana yule wa kichina akaona inatosha, basi akawataka waondoke. Ila akaona ni vema kama akipata mwanamke mmoja wa kwenda kumpunguza uzito kwa usiku huo.

Akamwamgiza mmoja wa wale jamaa aliokuja nao amtafutie mwanamke mzuri wa kwenda naye. Pasipo hiyana mwanaume huyo akafanya kazi na ndani ya muda mfupi akarejea na mwanamke mzuri kabisa, mweupe mwenye figa ya kuzembesha.

Na mwanamke huyu, kama bahati au nuksi, alikuwa ni Glady.

Bwana yule wa kichina akapendezwa naye hakika, wakaondoka naye kwenda kujipaki garini warudi makaoni.


**

Mazingira haya hayakuwa mageni. Ni kama vile aliwahi kufika huku, kumbukumbu zake zilimweleza bayana. Alijitahidi kutazama barabara na mazingira, akajikuta anapata picha fulani.

Na kweli hakuwa amekosea kabisa. Macho yake hayakuwa yanamdanganya, hili eneo si geni kwake. Na alipotuliza kichwa vema sasa akakumbuka. Mahali huku alishawahi kumleta yule mwanaume wa kichina aitwaye Lee.

Glady akaminyua mdomo wake. Hapa kidogo akamkumbuka mwanaume yule wa kichina, Lee. Na basi akajikuta anachukua simu yake na kupekua kama jina lake lipo kwenye simu. Akaliona.

Akataka kutext, akasita. Litakuwa jambo la kipumbavu akifanya hivyo. Basi akatulia kwanza akiwaza ujinga fulani kichwani mwake. Punde sauti ya honi ikamtoa fikirani. Walikuwa wameshafika getini. Geti likafunguliwa, wakazama ndani.

Ndimo humu humu! Akaendelea kuhakikisha. Ndimo humu humu alipomleta Lee. Macho yake ya wizi yakawa yanaangaza sana, huku na kule mpaka gari kusimama na kuongozana na wanaume wale kwenda kwenye makazi ya yule mchina.

Yeye akaamriwa aingie ndani, na yule bwana wa kichina akabaki na wale mabwana wengine pale mlangoni. Akateta nao kwa sauti isiyosikika vema, na kisha wakafunga mjadala kwa mchina yule akisema, “Msiniangushe!” wanaume hao wakaondoka zao, bwana yule wa kichina akazama ndani.

Akavua nguo na kwenda kuoga akimwacha Glady peke yake.

Glady akatazama huku na kule. Kimini chake akakivuta akibadilisha pozi la kukunja nne. Punde akanyanyuka na kuchungulia dirishani. Akaangaza nje akijaribu kufikiria ni upande upi yalipo makazi ya Lee. Muda kidogo, akasikia mlango wa bafu ukifunguliwa, basi akarejea kitini.

“Kaoge,” yule mchina akamwambia Glady. Glady akanyanyuka na kwenda bafuni. Akaoga akiwaza kuhusu Lee. Kabla hajatoka, akasikia sauti ya yule mchina huko chumbani. Alikuwa anaongea na simu.

“Hakikisha anakufa kabisa, sawa?”

Glady akashtuka. Akapatwa na maulizo kichwani. Sasa akapata picha juu ya nini yule bwana wa kichina alikuwa anaongea na wale wajamaa. Akaguna. Akapiga moyo konde na kutoka bafuni. Akaketi kitandani.

Bado bwana yule wa kichina alikuwa anaongea na simu.


***
Wow santeee mkuu Steve , nmekomebt na ku like kabla hata sjasoma
Najua mambo ni [emoji95] [emoji95] [emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91]
 
Innovator97 una quotije episode ndefu kaa hii, unatujazia page bure bwana, hii sio thread ya siasa ,unahalibu mtiririko.
 
Wow santeee mkuu Steve , nmekomebt na ku like kabla hata sjasoma
Najua mambo ni [emoji95] [emoji95] [emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91]
Fyuuumbaaafyuuu thana weee....

Kwahiyo hizo coment na like zinashibisha??! Mfyuuuu acha ujinga banaa lioneee
 
Back
Top Bottom