Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Kweli noma sana mkuu ubarikiwe kwa kazi yako nzur ya kutulisha chakula cha ubongo...[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 59*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

“There’s something behind here,” akasema Denmark akikuna kidevu. Kwa sekunde kama mbili hivi wakatazamana. Ila punde wakasikia kitu nje. Wakapata shaka.

Walipokuja kutoka, wakagundua kulikuwa kuna mtu ndani ya eneo lao. Kwenye perving, kulikuwa kuna nyayo mbichi za viatu.

ENDELEA

Wakatoka hata kutazama nje ya uzio wao wapate kutambua kama kuna yeyote, ila hawakufanikiwa abadani. Walichoambulia ilikuwa ni alama za matairi ya gari kuashiria kwamba mtu huyo alikuja papo na usafiri.

Wakabaki kwenye buwazo na shaka kiasi chake. Mtu huyo atakuwa amesikia kitu gani toka kwao? Ametumwa na nani na amepafahamuje hapo kwenye makazi yao?

Hata waliporudi na kuketi sebuleni wakaendelea kujiuliza. Walikuwa wanaamini wamefanya kila kitu kistadi kiasi cha kutokubakiza kivuli, sasa hii ishara ya mtu kutembelea eneo lao haikuwa njema kabisa.

Sasa ikawalazimu wawe makini sana. Na kwa kuhakikisha hilo, wakaona ni vema wakifunga kamera zao ndogo maeneo mbalimbali ya jengo hilo ili basi iwe rahisi kupata taarifa za uvamizi kabla matokeo hasi hayajachukua nafasi.

Zoezi hilo likafanyika upesi, na kila kitu kikawa kwenye mstari wakiamini kuwa mvamizi yule atarejea tu. Na punde atakapofanya hivyo basi hilo litakuwa kosa lake la mwisho kulifanya kabla hajaenda jehanam.

Ila hawakuwa wanajua. Hata wakati wanafanya ‘installation’ hiyo ya kamera, mtu yule ambaye walimkosa alikuwa anawatazama na hivyo basi akiwa anajua si muda wa yeye kufanya tena jaribio la kuzama mule.

Si kwamba mtu huyu alikuwa karibu, lah! Alikuwa ndani ya gari, kilomita kadhaa tu mbali na ile nyumba ya walengwa. Na macho yake yalikuwa yanasaidiwa na hadubini kalii yenye uwezo wa kupambana na kiza kupekua eneo analolitaka.

Alipotosheka na alichokipata, akaweka hadubini chini na kutabasamu. Na kumbe alikuwa ni Jona. Lakini alipajuaje hapa? Si muujiza. Jona na wenzake walikuwa ni watu wa kwanza kutambua utekwaji wa bwana Sheng na hata makazi ambayo alihifadhiwa kwa kutumia chip ndani ya mwili wa mchina huyo.

Na hivyo basi, watekaji hawa pasipo kujua lolote lile, wakafanya kosa la kumpeleka mateka wao nyumbani ili wamhoji na hatimaye kumtia kifaa chao kitakachowasaidia kuwapatia data.

Kiupofu wakarahisisha kazi ya wakina Jona. Sasa jicho la tai lilikuwa linawamulika kwa karibu zaidi.

“Sasa?” akauliza Miranda. “Kuna haja ya kufanya mambo?”

“Hapana,” akajibu Jona akitikisa kichwa. “Hivi Miranda hujajua kuwa hapa kuna faulo ya mchezo inachezwa? Bado tunatakiwa kuwa watazamaji kwa sasa. Muda utakapofika wa kuvaa jezi basi tutalitenda.”

“Ila kule upande wa Sheng bado wapo kimya,” sauti ya Marwa ilivuma. Kumbe alikuwa kwenye viti vya nyuma vya gari. “Unadhani na wao watakuwa wanapanga kitu?”

‘Sidhani,” akajibu Jona kisha kubinua lips zake. “Kama yule jamaa alivyosema, kuna something behind hapa. Kule kwa kina Sheng kuna jambo linafichwa, ila naamini muda si mrefu mambo yatakuwa bayana. Kama si hivyo, basi wale wazungu wasingekawia kuchukua hatua.”

Basi gari likawashwa, wakatimka. Ila si kwamba jicho la tai lilikuwa linawaacha walengwa wake wapweke, hapana. Kuna namna hapa kamilifu.


***

Saa kumi na moja asubuhi …

Kwa mbali alianza sasa kupata ufahamu. Masikio yake yalisikia sauti ya ndege wakilia huku na kule kumjuza kuwa asubuhi imewasili. Ni kweli mwili wake ulikuwa umechoshwa na purukushani za kuinusuru roho yake, ila bado alikuwa ana nia ya kurudi tena ulimwenguni kujua yanayoendelea.

Akafungua macho japo yalikuwa mazito. Akatazama kushoto na kulia na kisha akajitahidi kunyanyuka akipambana na maumivu aliyokuwa anayasikia. Alipoketi kitako, sasa akasikia vema. Huko nje sauti za watu walio kwenye mafunzo zilikuwa zinavuma. Kiwanja cha kufanyia mazoezi hakikuwa mbali sana na pale alipokuwapo. Lakini hata hivyo sauti hizi zimeanza kuvuma muda si mrefu kwani angelizisikia mapema kabla ya zile za ndege masikioni.

Akapambana kusimama. Akaweza. Ilikuwa ni ajabu mno, na kama ungelimwona jana basi ungelisema mtu huyu, kama kweli angelinusurika uhai, basi ingemchukua miezi kama mitatu au minne au mitano kusimama tena.

Hakika dawa za ‘master’ zilikuwa kali na zenye kufanya kazi mapema mno. Akajivuta kudaka shuka na kujisitiri, kisha akajikokota mpaka nje. Bado hakuwa na mwendo sawia, ila angalau husogea. Na kwa kasi ile ya dawa, basi hata juma lilikuwa kubwa kwake kutengemaa.

Taratibu akajivuta mpaka eneo alipokuwa master, akiwa anafanya meditation kama ada yake kila asubuhi ya mapema, na kusimama hapo pasipo kusema jambo. Alingoja master amalize. Ila ajabu, kama dakika mbili kukatiza, master bado akiwa amefumba macho na hata amempatia mgongo bwana Lee, akamwita kwa jina.

Akamuuliza, ina maana umepona kiasi hicho? Kisha akatabasamu na kugeuka kumtazama. Ni baridi na ametoka na shuka, tena mtu mgonjwa. Akamwelekeza waende mahali penye joto zaidi, wakapate pia na kifungua kinywa.

Baada ya muda kidogo wakawa wapo ndani ya chumba kidogo chenye zulia na mito chini, wakaketi. Punde fupi akaja mwanadada aliyebebelea trey ya kioo na vikombe viwili vya kahawa. Akawapatia.

Walipoanza maongezi Lee akaeleza staajabu yake kuwa pale maana alidhani amekwisha kufa kwenye mikono ya wadhalimu. Vita ilikuwa kali na walikuwa wamedhamiria haswa kumtoa roho.

Basi master wake akamwambia ni kama bahati. Na kama yuko sahihi, basi wadhalimu wale waliolenga kumuua, walishindwa kutimiza hilo kwa uhakiki zaidi baada ya yeye kuzama ndani ya himaya ya Wu, hivyo walivyotupa hizo risasi zao, wakaona inatosha wakajiendea.

Ila zaidi ya hapo, Lee akaeleza mkasa mzima ulivyokuwa. Namna alivyosalitiwa na yule afisa na hatimaye kukwapuliwa nyaraka zote hata zile ambazo alitakuwa kuja nazo.

Master akamtoa shaka kwa kumwambia watajua namna ya kumalizana na afisa huyo. Kwakuwa amepona dhidi ya kifo, basi ni huyo afisa ndiye ambaye ataonja kifo. Na kwa kuanzia muda huo, akamtawaza kuwa kamanda mkubwa wa kamandi ya makao makuu.

Akampa majukumu ya kuongoza kikosi chote kilichopo hapo makaoni, cha watu takribani alfu ishirini. Na hivyo akamtaka baadae nyakati za jioni wakalifanye jambo hilo kuwa rasmi kwa kuliweka bayana kwa kila mtu anayetakiwa kulifahamu.

Basi baada ya kuteta hayo kidogo, wakanyamaza na kupambana na baridi iliyopo kwa kunywa kahawa zao vikombeni. Zikapita kama dakika tatu, Lee akauliza swali, umepata chochote kile toka kule Afrika?

Master akatulia kwanza kidogo kabla hajajibu. Alishusha pumzi ndefu puani alafu akasema kwa maneno machache, hali si shwari. Lee alipotaka kujua zaidi, akamweleza kuwa kuna taarifa walizipata za kutekwa kwa Sheng na watu wasiojulikana. Ila kwa sasa mambo yapo vema kwani ameshapatikana, japo si mzima kiafya.

Lee akapata shaka hapa. Wakina nani hao waliomteka bwana Sheng? Alipoeleza shaka lake, Master akamtoa hofu kwa kumweleza kuwa anaamini Sheng atalimaliza jambo hilo kwani kama lingekuwa kubwa basi angeshalieleza huku makaoni.

Basi kikao kikawa kimezizimia hapo.

Baadae majira ya mchana, Lee akiwa peke yake anakula chakula, jambo lile la Sheng likamjia tena kichwani. Aliona kuna haja ya kuhofia sana kuhusu kile kitu. Ni mtu gani ambaye alikuwa ana uwezo wa kumteka Lee? Je ni wakina Jona? Ama watu wa bwana Brown Curtis?

Akiwa hapo anakula, akaja mtumishi mmoja kumwona. Msichana mchanga wa kichina aliyekuwa amebana vema nywele zake, mwili wake ameusitiri kwenye nguo za kitamaduni.

Msichana huyo alikuwa amebebelea nguo za Lee alizotoka nazo shurbani. Kabla hajaziweka chini akamuuliza Lee kama nguo atazihitaji tena ama akazichome. Lee akafikiri kidogo, akamruhusu msichana huyo akazichome.

Ila mwanamke huyo kabla hajatokomea, Lee akakumbuka jambo. Akamwita mwanamke huyo na kumwambia atazame mfukoni mwa nguo hizo kama kuna simu yake. Alikuwa anabahatisha tu, na kama angeliambiwa hamna,a singeshangaa.

Ajabu, msichana yule baada ya kufanya msako mdogo, akahisi kitu kigumu mfukoni. Alipozamisha mkono na kuchomoa, akatoka na simu. Akamkabidhi Lee na kisha akaenda na zile nguo akachome.

Lee, akiwa haamini, akaipekua simu yake. Na baada ya muda kidogo, kwakuwa alikuwa na hamu kujua zaidi mambo yaliyotokea kule Afrika, aka-‘switch’ laini yake ya kimatumizi kule mtandao wa whatsapp.

Muda kidogo, akapokea jumbe kadhaa. Ikiwemo zile za Glady!



***


Saa saba na nusu mchana, Shanghai, China. Kwenye ghorofa ya ishirini ya nne …


Kulikuwa kuna kikao cha watu wasiozidi watano. Watu hao wote wote walikuwa wamevalia suti nyeusi, na sura zao zikiwa kapuni. Miguu yao ilikuwa imetambaliwa na soksi nyeusi pia na chini wakimalizia na viatu barabara vya ngozi!

Ndani ya eneo hili kulikuwa tulivu, na kiyoyozi chapuliza kwa mbali.

“It is now or never,” sauti nzito ilisema. Na sauti hii kama wewe ni mtu wa kumbukumbu basi ilikuwa ndiyo ile ambayo ilikuwa inateta na Rob jana yake tu baada ya kupewa taarifa ya zoezi la kummaliza Lee.

Bwana huyo alikuwa hapa kikaoni na wenzake. Na mjadala hapa ukiwa ni kumaliza kabisa familia ya Wu kwenye uso wa dunia ili basi kuruhusu wabepari kufanya kazi yao vema na kuondoa kabisa tishio la China kushikilia uchumi wa dunia na kuiendea kombo Amerika.

“This is the time for us to finish the game,” alisema bwana yule mwenye sauti nzito. Wenzake wakaunga mkono hoja. Na hivyo basi wakakubaliana wanaume wale waliopo Afrika, the intellectual instinct, waanze kutekeleza kazi ya kufutia mbali mamlaka ya China ukanda wa Afrika ya mashariki na kati.



***
 
Back
Top Bottom