Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Hod kwenye Anga la wenyewe...!! Bado amjafungua kumbe... [emoji22][emoji22][emoji86][emoji86][emoji86]
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 61*


*Simulizi za series*



ILIPOISHIA


“Tumekawia. Na hili linaelekea kugharimu maisha yake. Tumegundua ndani ya dripu kulikuwa na sumu. Hatujui imefikaje, na mbaya zaidi majibu yake yameshaanza kuonekana mwilini. Amepooza upande wake wote wa kulia. Matumaini yake ya kupona ni hafifu hafifu mno.”


Akiwa hapo, bado taarifa hizi zikiwa ngumu kuzimeza, mara akasikia king’ora cha hatari kikilia kwanguvu! Punde akaja mwanaume mmoja hapo akiwa amebebelea silaha mkononi. Akasema, “Tumevamiwa!”


ENDELEA


Lee akamtazama daktari na kumwambia, “Ningoje hapa, nakuja.” kisha akaenda zake na yule jamaa aliyekuja kuleta taarifa. Wakaelekea mpaka huko inaposemekana kuna mashambulizi. Lakini hawakukuta kitu chochote. Zaidi kulikuwa kweli kuna miili ya watu waliokufa ikiwa imezagaa huku na kule.


Jambo hili likamshangaza sana Lee. Walipata kusikia sauti za milio ya bunduki na hata kilio na magugumizi ya watu wakililia uhai lakini kila walipokwenda kutazama, hawakukuta mtu huko zaidi ya maiti.


Lee akatahamaki. Basi akapata wazo. Haraka akaenda control room apate kutazama kinachoendelea kwa kutumia rekodi ya kamera za cctv ambazo zimetundikwa ndani ya jengo hilo maeneo mbalimbali. Lakini alipofika huko, napo akakuta maiti za watu wanaohusika na kitengo hicho. Wote, sita kwa ujumla, walikuwa wameshindiliwa risasi kadhaa wakiwa chini wanamwaga damu. Alipotazama televiisheni, hakuona kitu. Zote zilikuwa na rangi ya bluu kuonyesha kwamba hakuna kinachodakwa na kurushwa kwa muda huo.


Ina maana wavamizi walikuwa tayari wameshaharibu mifumo yote ya kamera! Bado akiwa hapo, mara umeme ukakatika ghafla na eneo lote likabakia totoro gizani. Hapo sasa mambo yakawa magumu kupita kawaida.


Watu wakaendelea kuuawa na maadui wakiwa wanafanya namna ya kutoonekana kwa wepesi. Kwa takribani nusu saa, watu wengi mno wakawa wameuawa. Lee hakuwa na msaada wowote ule, zaidi ya kila mahala kushuhusia maiti na maiti na maiti.


Hapa akapata walakini mkubwa. Haraka akakimbia kwenda kule hospitali kumkuta Sheng.



**


Sauti ya mtu akigugumia ilisikika, na mara ikanyamaza kimya. Upande wa kushoto, akadondoka mtu akiwa anamimina damu kifuani mwake baada ya kukitwa na kisu kirefu chenye ncha nyembamba ndefu.


Hapo muuaji akaonekana akiwa mwanaume aliyevalia mavazi meusi ya kubana kana kwamba wale watu wazamao ndani ya maji. Muuaji huyo hakuwa amebakiza sehemu yoyote ya mwili wake wazi. Nguo yake hiyo ilikuwa imefunika mpaka kinywa na pua, macho yakiwa yamemezwa na miwani iliyobana kuta za uso.


Miwani hiyo ilikuwa inamwezesha kuona vema katika giza hili. Kwenye nyonga zake, alikuwa amebebelea mkanda mwembamba ulioning’iniza bunduki mbili ndogo. Na mikononi alikuwa ana visu viwili vinzvyochuruza damu.


Upesi, baada ya mtu yule aliyekitwa na kisu kudondoka chini, akatokea mtu mwingine mlinzi wa jengo. Alipomwona mvamizi, hakujiuliza mara mbili akarusha risasi kama tano kwa mfululizo. Lakini ajabu hakufanikiwa kumpata mlengwa wake kabisa.


Bwana yule mvamizi alichumpa na kujibiduabidua hewani, na mara kufumba na kufumbua akawa haonekani. Kuja kutahamaki, yule mlinzi akiwa anatazama huku na huko, mara akasikia kishindo cha mtu nyuma yake. Akatazama upesi kwa woga. Na katika haraka ya ajabu, kabla hajabinya kitufe cha risasi, akachomekwa kisu cha shingo.


Akiwa anapapatika na kifo, akabinya kitufe cha risasi kwanguvu, risasi zikamiminika kama mvua, lakini zote zikaenda kombo maana mvamizi alikuwa ameshaelekezea mdomo wa risasi pembeni. Basi bwana yule mlinzi alipoishiwa nguvu, akadondoka chini na kujifia.


Mvamizi akaweka kidole chake sikioni na kuuliza,


“What’s your position?” Sauti ikamjibu kwa mbali isisikike vema isipokuwa kwake mwenyewe. Basi akaongezea kwa kusema. “The building is under control. Seize the man and let’s finish the business.”


Akatoa kidole chake kwa sikio na kupotelea gizani.



**


Kulikuwa ni kimya sasa kupita kiasi. Hata watu hawakuwa wanaonekana wakikatiza huku wala kule tofauti na ilivyozoeleka siku zote.


Hata hapa hospitali palikuwa kimya. Ila hali hiyo haikudumu kwa muda mrefu, wanaume watano wakajiri wakitoa upande wa kushoto wa jengo. Wote walikuwa wamevalia sare, nguo nyeusi zinazobana miili na usoni wakiwa na miwani zilizobana na kushikilia vema nyuso zao.


Wakazama ndani ya hospitali, wakinyookea chumba alichokuwa amelazwa Sheng. Kufungua mlango kutazama, hakukuwa na mtu! Kitanda kilikuwa tupu. Mashine, mipira na waya, zilikuwa pembeni.


“Shit!” akalaani Denmark. Alitambulika kwa sauti yake. Sheng hakuwa ndani!


Basi akamgeukia mwenzake na kusema, “Scot, go look where he is.”


Haraka aliyepewa agizo hilo, Scotland, akatoka ndani na kwenda kule walipokuwa wamepaki gari lao, nje ya Jengo upande wa kulia, kama kilomita moja na nusu hivi. Alienda huko kwa kukimbia. Na hawakutaka kwenda wote kwa maana Denmark alikuwa anaamini Sheng atakuwa amefichwa ama amejificha ndani ya jengo.


Hivyo ni swala la kupewa taarifa na kuifanyia kazi tu.


Baada ya punde, Scotland akatoa taarifa, “He is out of the building!”


Hakuongezea ttaarifa nyingine, akasikia kiganja cha mtu kikimgusa begani. Kutazama, alikuwa ni Lee.


“I’ve got a little problem here,” Scotland akasema akiwa amebinyia kidole chake sikioni. “Let me deal with it, be in touch.” akamalizia taarifa na kisha akaufunga mlango kumkabili Lee.


“Who are you?” Lee akauliza.


“Your destroyer,” Scotland akajibu. “Your breath taker,” akaongezea.


“Who sent you here? Are you are the one who kidnapped Sheng?” Lee akauliza tena. Bwana Scotland akasikika akiguguma kwa kicheko, kisha akasema, “Hell yeah!” na kuongezea, “I don’t think if you have to know who sent us here ‘coz you are going to die in anyway. What help will it give?”


Aliposema hayo, Scotland akachomoa visu vyake nyuma ya kiuno.


“Where’s Sheng?” akauliza.


“You have to go through me to get him,” Lee akajibu kwa kujiamini.


“Ok, if that’s what you want,” akasema bwana Scotland na vita ikaanza. Lee hakuwa na silaha yoyote mkononi mwake. Aliamini kwenye uwezo wake kumlinda na hata kummaliza adui.


Na kwakuwa hakuwa anafahamu uwezo wa adui yake, akaona ni vema ampatia nafasi ya kumuanza. Kwa wakati huo akiwa anaamini adui wake huyo hatakuwa mtu mwepesi kutokana na matukio waliyoyafanya ndani ya jengo.


Hakuwa amekosea. Scotland alikuwa mwepesi mno na zaidi akiwa mwenye nguvu. Lee alijitahidi kukwepa lakini bado akajikuta akipokea ngumi kadhaa na mateke yaliyomrudisha nyuma.


Akaona endapo naye asiposhambulia basi muda si mrefu atajikuta yu hoi na kuwa chakula cha adui. Akaanza naye kujikakamua.


Akatupa ngumi, ikayeya, akatupa tena nyingine nayo ikadakwa, kabla hajaviringitwa, akaruka juu na kuchoropoa mkono wake kisha akajifyatua mateke. Nayo yakapanguliwa.


Scotland akatuma mikono yake yenye visu, Lee akajitahidi kuizuia, lakini Scotland akamzidi ujanja na kumchanja mkono wake wa kuume. Kisha haraka akaviringita miguu ya Lee na kumwangusha chini. Lee akapiga kiwiko mkono wa kushoto wa Scotland, kisu kikaangukia kando, sasa akabaki na kisu kimoja cha mkono wa kuume.


Akawa analazimisha kumtoboa Lee kifuani, Lee naye akikazana kuzuia mkono huo kwa mikono yake yote miwili. Ila ni dhahiri alikuwa anaelekea kushindwa. Ncha ya kisu ilikuwa inasogea taratibu, na ilibakiza kama robo sentimeta kugusa paji la uso la Lee.


Ilibidi afanye jambo la sivyo alikuwa anakufa. Basi akatumia akili yake. Kwakuwa nguvu kubwa Scotland alikuwa ameiweka kisuni, Lee akaachilia mikono yake upesi na kukunja shingo yake haraka. Kisu kikatoboa chini. Na sasa kwakuwa mikono ya Lee ilikuwa huru kwa muda huo mfupi, akagonga shingo ya Scotland maeneo ya pembeni chini kidogo mwa taya, Scotland akalegea.


Lee akachojoa miguu yake na kumkita mwanaume huyo kwenye kende, na kabla hajalalama kwa maumivu, akawa ameshasomba kisu na kumkita nacho shingoni. Akamsukumia pembeni bwana huyo na kuhema kwanguvu. Kazi haikuwa nyepesi hata kidogo!


Alimpofunua usowe na kumtazama hakuwa mtu anayemfahamu.


Akiwa amemaliza kazi hiyo pevu, akampoka bwana huyo funguo wa gari atumie usafiri wao kuyeya na Sheng. Akazama ndani na kutekenya gari, akaweka ‘gear’, kabla hakanyaga mafuta, akasikia kitu kisogoni.


“shut the the car off,” akaamriwa.




***
 
Msema kweli mpenzi wa Mungu, mimi hii story ilishanikata stimu maana imekuwa ya kusubiriwa sana mpaka mtu hamu inamuisha. Asante sana Stive kwa nilichokipata toka kwako maana siihaba, Mungu akupe afya njema ili tulijenge Taifa.
 
Msema kweli mpenzi wa Mungu, mimi hii story ilishanikata stimu maana imekuwa ya kusubiriwa sana mpaka mtu hamu inamuisha. Asante sana Stive kwa nilichokipata toka kwako maana siihaba, Mungu akupe afya njema ili tulijenge Taifa.
Una uhakika hutasoma tena hii story, au ndo kutupa majivu then unafuatilia na kutoa arosto kimyakimya !!
 
Back
Top Bottom