Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Nichukue fursa hii kuwashukuru sana wasomaji wangu wa hii simulizi kwa kufanya uzi huu kuwa TRENDING kwa muda mrefu yaani pengine uzi mwingine wowote wa simulizi ndani ya JF huku ukiwa na views lukuki.

Sitawaangusha. Nashukuruni.
Tupia vitu mkuu. Hata sisi hatutakuangusha
 
*ANGA LA WASHENZI II --- 62*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Alimpofunua usowe na kumtazama hakuwa mtu anayemfahamu.

Akiwa amemaliza kazi hiyo pevu, akampoka bwana huyo funguo wa gari atumie usafiri wao kuyeya na Sheng. Akazama ndani na kutekenya gari, akaweka ‘gear’, kabla hakanyaga mafuta, akasikia kitu kisogoni.

“shut the the car off,” akaamriwa.

ENDELEA

Basi akatii amri. Akazima gari na kuweka mikono yake juu. Kukawa kimya kidogo. Alipotazama sight mirror, kioo kikaacho juu ya kichwa cha dereva, akaona sura nyeusi na si ya kizungu kama ambavyo alikuwa anawaza. Na kama haitoshi, sura ile aliyoiona haikuwa ngeni machoni pake.

“Sheng yupo wapi?” sauti ikauliza. Basi Lee akasita kidogo kusema. “Nimekuuliza Sheng yupo wapi?” Swali likarudiwa. Lee akajifikiri kidogo, kisha akasema, “Yupo upande wa kaskazini wa mahalii tulipo.”

“Tumwendee,” akaamriwa. Basi akatia moto kwenye gari na kutimka kwenda huko ambapo Lee alipasemea. Lakini kichwani mwa mchina huyu hakukuwa salama. Alikuwa anawaza mambo ya hatari. Alikuwa anawaza namna ya kujinasua hapa ahepe zake salama.

“Kamwe usije ukafikiri ujinga,” mwanaume yule aliyemwonyeshea bunduki akamtahadharisha. “Punde tu utakapofanya ujinga wako, basi nitatoboa kichwa chako na kukuacha mfu uliwe na mbwa koko!”

Basi hapa Lee akasitisha kwanza mipango yake. Akawaza huyu mtu ni wa namna gani na kivipi aliwaza alchokuwa anakiwazia yeye kichwani. Katika fikra hizo ndipo sasa fahamu zikamjia, kumbe mwanaume yule alikuwa ni Jona.

Ndio! Akili yake ikawa inazoza yenyewe. Ni Jona huyu. Ina maana naye amekuja na wale wazungu au amekuja kwa mambo yake binafsi? Lakini amejuaje haya? Akajikuta akipata mawazo maradufu.

Lakini zaidi akajikuta pia ana sababu ya kuhofia mara mbili. Kwake Jona hakuwa mtu wa masikhara hata kidogo. Kabla ya songombingo lolote lile, alikuwa ni mwanaume waliyemtafuta na kuhangaika kummaliza pasipo mafanikio.

Gari likasimama.

“Yupo pale!” Lee akasema akionyeshea kwa kichwa.

“Shuka, kamlete!” Akaamriwa. Naye pasipo ajizi akashuka na kutembea hatua tano kwendea kizani. Alipotazama kwa macho yake ya wizi, akaona mdomo wa bunduki ukimuelekea. Hakuwa anaweza kutoroka. Aidha akifanya hivyo aenende akiwa majeruh kama atafanikiwa kunusuru roho yake.

Ni kweli. Mwanga wa mbalamwezi haukuwa unamdanganya. Alichokiona kiliikuwa ni sahihi kabisa.

Basi akamnyanyua bwana Sheng aliyekuwa amelala chini, pengine katika hali ya kutojitambua. Akauweka mkono wa Sheng begani mwake na kisha akaanza kujongea kuuendea usafiri.

Ila akilini mwake bado akiwaza. Bado akifafanua. Na macho yake yakiwa yanaangazaangaza kule dirishan ambapo mdomo wa bunduki ulikuwa umetokeza nje tayari kwa ajili ya shambulio.

Akawaza kumtelekeza Sheng. Amweke mbele kama ngao yake kisha yeye akapotea zake salama. Ila akaona si kheri. Hata kama angelifanikiwa kutoka hapo, nini kingelifuata? Si kwamba kazi na juhudi zake zote zitakuwa za kutwangia maji kinuni?

Aliweza kuyawaza haya yote kwasababu ya mwendo wa taratibu aliokuwa anakokotana na mgonjwa Sheng. Mgonjwa huyo alikuwa mzito, na tena hivi hajiwezi, basi uzito ndiyo huwa maradufu. Ilimpasa Lee kutumia nguvu nyingi sana kusonga.

Basi akiwa bado hajafika mlangoni mwa usafiri, mara ghafla akasikia jambo la kumshtua. Ilikuwa ni kama sauti ya kishindo na kaupepo pia. Akatazama upande wake wa kaskazini kwa mashaka. Huko akaona mtu mmoja kwa mbali kama kweli macho yake yalikuwa yanaona sawia.

Mtu huyo alikuwa mweusi kwanzia kichwa mpaka miguu na mkono wake wa kuume ulikuwa umebebelea bunduki yenye mdomo mrefu. Yalikuwa ni mang’amun’amu ya giza? Akajiuliza. Hapana! … Hapana! Sauti ikateta kichwani mwake. Na kwa kumwondoa shaka, mara taa za gari alilomwacha Jona akiwa ndani likawasha ‘full light’, akamwona mtu huyo vema.

Ni kweli alikuwa ni mtu. Ni kweli mkononi alikuwa amebebelea bunduki. Na ni kweli alikuwa amevalia mavazi meusi kuanza juu mpaka chini. Mavazi haya yalikuwa ndiyo yaleyale ambayo alikuwa ameyavaa yule bwana wa kizungu aliyetoka kumuua muda muda si mrefu.

“Panda upesi!” Jona akafoka. Na haikuchukua punde, risasi zikaanza kumwagwa haswa kushambulia gari! Ni kheri Jona alikuwa amefungua mlango wa gari na basi risasi zilizokuwa zinamwelekea Lee na Sheng zikagotea mlangoni. Takriban risasi nane!

Lee alipojitupia humo, pamoja na Sheng, gari likakanyagwa mafuta na kuchomoka kwa kasi mno! Hata mlango ukafungwa wakiwa mwendoni. Gari, kwa pupa na kwa kasi, likamfuata bwana yule aliyekuwa anawashambulia kwa nia ya kumsomba.

Kabla halijafanikiwa, bwana huyo akatoweka. Ilikuwa ni upesi mno kiasi cha kuweza dhani pengine ameyeyuka, ila la hasha! Bwana huyu alikuwa amekwenda hewani mithili ya paka mweusi wa misitu ya Amazonia.

Na kama vile ngedere, akatua kwenye paa la gari liendalo kasi, na akalikamata kwa nguvu mno. Wakati nguo yake ikiwa imeshaji - tune na kuwa yenye mabakamabaka yenye matobo madogomadogo yaliyovimba. Na mikononi kucha zilikuwa zimetokama kana kwamba chui.

Hivyo basi haikujalisha gari lilipelekwaje, hovyo kiasi gani, bwana huyo akawa bado yu paani. Jona akayumbisha gari kwanguvu, akaendesha kwa mwendokasi wa hali zote, bado hakufanikiwa kumng’oa njemba huyo paani!

Na kutulia kidogo, njemba huyo akaanza kumwaga risasi akitoboa paa. Shukrani gari lilikuwa na paa gumu. Waliolitengeneza walilenga liwe hivyo, na si tu kwenye paa, hata huko pande zingine, gari lilikuwa gumu kumeza risasi.

Na punde bwana huyo alipokuwa akishambulia paa kwa risasi, Jona akatambua kuwa adui huyo kwa huo muda atakuwa ameshikilia paa kwa mkono moja, mwingine akiutumia kuushambulia, hivyo akaongeza kuyumbisha usafiri huo kwa pupa na kumnyima nafasi ya kufanikisha zoezi lake.

Akafanikiwa kwa hilo. Na pale adui alipopata upenyo wa kushambulia tena, Jona akafanya mahesabu ya upesi kichwani. Ni hivi, wakati anamwona adui yule akiwa amebebelea bunduki wakati ule alipomulika full light, adui huyo alikuwa amebebelea bunduki mkono wake wa kuume.

Kwahiyo basi adui huyo hutumia mkono huo, wa kuume, kushambulia. Na kwa maana hiyo mkono wa kushoto ndiyo hudaka paa. Na kwa makadirio yake basi, itakuwa vigumu sana kwa adui huyo kuangukia upande wa kulia, kwani atakuwa kajaza balansi upande huo. Hivyo … hivyo upande wa kumwangushia ulikuwa ni huu huu wa kushoto alipoekea mkono.

Basi akamwacha adu afyatua risasi. Akazihesabu, moja … mbili … tatu … nne! Akabinya breki ya ghafla na kuliemazia gari upande wa kushoto kwa kukata kona ya ghafla mno! Mpango ukaitika. Adui alikawia kudaka paa kwa mkono wake wa kuume, na hivyo akawa sasa ananing’inia na mkono wake wa kushoto, upande wa kushoto wa gari.

Bado akawa ngangari. Akanyooshea mdomo wa bundki ndani ya gari. Lakini kabla ajafyatua, Jona akatupa teke lake kutengua mlango wa gari, mlango ukatenguka na kumsomba adui huyo na kumwaga chini! Akabiringita mara tano kabla hajatulia tuli akiskizia maumivu makali. Na huku akitazama gari likiyoyoma.

“https://jamii.app/JFUserGuide!!” akalaani akipiga kofi ardhini kisha akaweka kidole chake sikioni na kusema, “I’ve lost them!”


**


Gari lilisimama na pasipo kupoteza muda, Jona akachumpa nje na kumwamuru Lee ashuke pamoja na Sheng. Wakatii amri. Lee akiwa anajikokota, akamtua Sheng na kisha wakafuata amri ya Jona ya kumfuata aelekeapo.

Baada ya hatua kadhaa. Wakakuta gari lingine, range rover sport nyeupe. Ndani alikuwapo Miranda, Marwa na Kinoo. Wakapanda humo na kuhepa wakiwa wamelitelekeza gari lili la maadui lililowaleta mpaka hapo.

Zikapita kama dakika nane, na mara gari lingine likafika hapo likiwa na wanaume wanne. Wale ‘the intellectual instinct’. walishuka na kulitazama gari lao, hakuna mtu. Wakanyofoa mfumo wa GPS na kifaa fulani kilichokuwa kinafuatilia ‘chip’ aliyopandikiziwa Sheng mwilini.

Basi wakarejea ndani ya gari lililowaleta na kutimka. Wakaendelea kufuatilia mahali alipo Sheng kwa kutumia chip ile. Na baada ya kama robo saa, wakawa wamefika mahali ambapo ilionyeshwa kwenye ramani kuwa ‘chip’ ipo hapo.

Basi wakashuka na kusogelea hilo eneo. Ajabu wakakuta kuna kikopo kidogo cheupe chenye mfuniko mwekundu. Mmoja akakiokota na kuifunua. Ndani akakuta ‘chip’ yao na karatasi nyeupe yenye ujumbe uliosomeka,

“Welcome to the sky of the damned.” Kumaanisha karibu kwenye anga la washenzi.



***
 
Back
Top Bottom