*ANGA LA WASHENZI II --- 66*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Basi wanaume watatu, Ireland, Wales na Sweden wakagawanyika kuizingira nyumba ya wakina Miranda. Wakati huo wakiwa tayari wameshajivika nguo zao za kazi.
Punde kidogo, umeme ukakatika katika nyumba hiyo na kuwa kiza totoro isijulikane mlango na dirisha lipo wapi. Hapa sasa wale ‘the intellectual instinct’ wakawa wanaona kana kwamba mchana mkavu wa saa nane.
Hakuna huruma. Hakuna mtu yeyote kutoka na uhai.
ENDELEA
Basi ndani ya dakika kadhaa, watu hao wakawa wamezama ndani ya nyumba kwa kuvunja milango. Wakafanya msako wao, na ndani ya muda mfupi wakawa wamegundua kuwa wamezamia mtegoni.
Ndio, mtegoni! Ndani hakukuwa na mtu isipokuwa Sheng aliyekuwa amelazwa kitandani. Swala hili likawashtua. Lakini wakiwa werevu wa kutosha, wakang’amua na kujinasua. Wakitumia teknolojia kubwa ya miwani waliyoivaa, wakatambua kuwa kuna nyayo za miguu mahali kadha wa kadha.
Na kama wakina Miranda wakiwa watu waliolitambua hilo jambo, wakajitokeza bayana, yeye pamoja na Lee huku Marwa akiwa ameendelea kufichama.
“Oh! Now you are here!” akasema Denmark, nyuma yake wakiwa wamesimama wenzake kwa ukakamavu. Mandhari yalikuwa ya giza, ila kwakuwa hapa walikuwa nje, basi angalau waliweza kuonana, haswa Miranda na mwenziwe, Lee, ambao hawakuwa wakitumia miwani ya kuonea.
Mbali na giza hilo, kulikuwa kimya.
“We could have killed Sheng already and left, but I wanted to see you, the people who outwitted us,” aliendelea kusema Denmark kwa dharau. Akamtazama Miranda na kisha akahamishia macho yake kwa Lee. Hapo akaganda kwa muda kana kwamba mtu amjuaye ama anamfananisha.
“The Chinese man,,” akasema na kisha kuguna kama mtu aliyekabwa na kicheko. “I think I know you, don’t I?”
Lee hakusema kitu. Kwa namna alivyokuwa anamtazama kulisema nini kipo kifuani mwake. Alikuwa ana pande la chuki. Mikono yake ilikuwa imekunja ngumi kwanguvu. Na pumzi yake ilikuwa inaenda juu na chini kwa kasi.
Denmark akanyoosha mikono juu akisema, “You don’t know who we are, lads! You don’t know anything about us, right?” akatabasamu. “Maybe you are braver more than we could imagine, stronger and bolder … but … but don’t ever mess with us.” Denmark akasema akitikisa kichwa chake na kidole akikipeleka kushoto na kulia. “Don’t ever ever do that. We are not of the same ground.”
“Neither do we,” akadakia Miranda kwa ujasiri. Basi Denmark akamsogelea na kumuuliza, “What do you say?”
“You heard me,” Miranda akamjibu akimtazama usoni. Denmark akatabasamu. Kisha akawatazama wenzake na kupiga makofi. “Wow! What’s so special about you sweet lady?”
“More than you can ever imagine,” akajibu Miranda. “More than you can ever handle.”
“Sure?” akauliza Denmark.
Kabla Miranda hajajibu, Lee akamshika bega mwanamke huyo kama ishara ya kumtaka anyamaze. Miranda hakujali, akajibu, “Totally sure.”
“Miranda,” Lee akaita. “Hatuna haja ya kufanya hili. Mwache mwanakharamu apite. Tuko outnumbered!”
“Kama kufa acha tufe,” akasema Miranda. “Tunakufa mara moja tu, Lee. Siwezi kuwa mdhaifu kiasi cha kudhihakiwa kiasi hiki.”
Lee akashindwa kumtuliza mwanamke huyo. Kwa macho yake akashuhudia wale washirika wa Denmark wakisogea nyuma kidogo kutoa uwanja, na Denmark akasema akimwambia Miranda, “Show me what you have.”
Miranda akamtazama Lee na kumpatia ishara ya kichwa kuwa ampatie nafasi. Lee akasita. Akauliza kwa kunong’ona, “Are you sure?” Miranda akajibu kwa kupandisha kichwa chake, basi Lee akasonga nyuma kwa hatua mbili tu na kisha akasimama akitazama kwa umakini.
Miranda akajiweka tenge, Denmark akamtazama. Mwanamke huyo akatanua miguu yake kutafuta balansi na kisha akakunja ngumi. Denmark akaguna kwa kebehi kisha akamwonyeshea Miranda ishara ya kumkaribisha.
Miranda akaanza kutupa ngumi zake nyepesi za kasi. Denmark akazihepa kama mchezo, ilan kwa makusudi akatengea uso wake ngumi moja iliyomkita upande wa shavu lake la kulia na kumgeuzia uso kando.
“Not bad,” akasema. “Any more than that?”
Miranda akakwazika na kauli hiyo. Sasa akafunguka kwa umahiri wake wote, akazirusha ngumi na kujifyatua mateke kama mitego ya porini. Hamaki akamkita Denmark mateke mawili ya kifua na almanusura kumwangusha chini.
Hapa sasa Denmark akatambua mwanamke apambanaye naye hakuwa wa kumpuuzia wala kumdharau. Si bure alikuwa anajiiamini. Sasa akakunja ngumi na kutanua mapaja yake kujisimika ardhini. Akamkaribisha tena Miranda.
Miranda akaja tena akionyesha umahiri wake. Na sasa akidhamiria kumwangusha mwanaume huyu kumkata ngebe. Ila hakujua … Hakujua anatakiwa kuwa mwangalifu mno kuliko anavyodhani.
Sasa akarusha ngumi zake za upesi. Pengine akimweka ‘busy’adui yake huyu ili ampatie shambulio kubwa la hatari litakalomlaza hoi. Lakini hakuwa anafahamu kuwa akiwaza hivyo, naye adui alikuwa akiwaza kingine. Sasa Denmark hakutaka kukwepa ngumi yoyote ya Miranda, na badala yake akaanza kumdhoofisha mwanamke huyo.
Kila Miranda alipotupa ngumi yake, kwa kasi ya umeme, Denmark akatengua ngumi hiyo kwa ngumi yake nzito. Miranda aliporusha ngumi kama sita na tendo hilo toka kwa Denmark likirudia, akaanza kuchoka. Mikono ikamuuma.
Basi kujikomboa, akaanza kutumia miguu yake. Akarusha mateke mfululizo na kwa mkupuo. Napo mchezo ukawa uleule. Denmark alimuumiiza miguu yake wa kupangua kila shambulizi na ngumi zake nzito za upesi. Sasa Miranda akawa amechoka, na hapo bado Denmark hajaanza kumshambulia!
Mwanaume huyo asiwe na huruma, baada ya kutambua kuwa Miranda alikuwa hoi, na sasa anahisi maumivu maungoni mwake, akaanza kutupa mashambulizi. Ngumi zake zilikuwa nyepesi ila nzito maradufu. Hata Miranda alipojitahidi kuzizuia baadhi, bado aliyumba kwa kushindwa kustahimili.
Alipojiweka bayana, akala ngumi mbili, moja ya kifua na nyingine ya tumbo, akacheua damu. Akadondokea chini na kunguruma kwa nguvu kwa maumivu makali. Denmark akatikisa kichwa chake.
“C’mon lady. We are about to start!”
Miranda akatema mate yenye damu pembeni. Akataka kusimama, viungo vilikuwa vinamuuma. Lee akammwekea mkono wake begani kumtuliza kisha akasema kwa sauti ya chini,
“Let me …”
Kisha mwanaume huyo akamtazama Denmark na kujipanga kwa ajili ya pambano. Denmark akatikisa kichwa chake kwa masikitiko. Akampatia ishara mwanaume huyo kumkaribisha. Lee akakataa. Akairudisha ishara hiyo kwa Denmark. Alitaka mwanaume huyo awe wa kwanza kushambulia.
Basi Denmark hakuona tabu. Akaanza kurusha ngumi, viwiko na kila kiungo chake cha mwili kupambani. Mapigo yake yalikuwa ya kasi na mazito. Ilimlazimu Lee awe ‘intensive focused’. Macho na akili yake iwe nyepesi kwenye kufanya maamuzi yenye tija.
Walidumu kwa kama dakika tatu pasipo yeyote kufanikiwa kufikisha shambulizi lake kwa mwenzake. Lakini kwa muda wote huo Lee alikuwa anafanya kazi ya ziada kwani alikuwa anazingatia sana na kujilazimu kufanya maamuzi mepesi mno.
Alikuwa anatumia akili yake kwa kiasi kikubwa huenda tofauti na adui yake, hivyo ilifikia mahali akawa kama mtu aliyechoka kuendana na kasi kama hapo awali. Hapa Denmark akampatia ngumi tatu na kumwangusha chini!
Akang’ata meno kwa hasira. Akanyanyuka upesi na kujiweka tenge kwa ajili ya pambano sasa akiona ni vema kushambulia kuliko kushambuliwa. Njia nzuri ya kujilinda ni kwa kushambulia kwa kasi.
Akaweka nguvu zake zote kwenye mikono yake. Akajitutumua kwa muda. Denmark akawa matatizoni, ila bado akafanikiwa kuyeya na kukwepa, akienda kushoto na kulia, chini na juu … kushoto, kushoto .. kulia, chini! Kando na kando, kushoto, chini!
Alipokaa wazi, Denmark akatumia fursa hiyo kumtwika teke zito na kummwaga chini! Denmark akacheka kidogo na kudhihaki, “that woman his better than you!”
Lee akapandwa na hasira lakini kheri kabla hajafanya lolote, akatambua hilo ni kosa. Kutwaliwa na hasira ukiwa kwenye uwanja wa mapambano hudumaza utumiaji wa akili. Huchochea utumiaji wa nguvu kwa fujo na basi hatimaye kuangamia.
Basi kwanini asitumie njia hii? Akaona kuna haja ya kufanya jambo kumkwaza bwana Denmark. Kuna sababu ya kumpandikiza mwanaume huyo hasira ili amtoe ‘mchezoni’.
“Yes, she is better than me. But at least I look like a man, not like you sweet pie. You are more beautiful than her!” Lee akasema kwa dhihaka akitabasamu kwa mbali akinyanyuka taratibu.
Denmark akabinua mdomo. “I am going to shut that piece of shit forever!” akafoka akimjongea Lee. Akamrushia ngumi nyingi sana kwa hasira. Lee akajificha kukwepa ngumi hizo. Sasa shida kwake ikiwa nguvu kubwa ya Denmark. Mashambulizi yake yalikuwa ya kilo haswa!
Ila sasa hakuwa akitumia akili tena kama hapo mwanzo. Fundo la hasira lilikuwa limemkaba na alitaka kumkomoa mpambani wake ndani ya muda mfupi! Alitaka kumtia adabu.
Huu sasa ndiyo ukawa mwanya kwa Lee. Mwanya wa kutumia akili yake zaidi ya adui yake. Alijua fika unapokuwa na hasira, mazingatio ya kujilinda hupungua, mtu huzingatia zaidi kushambulia. Basi akatafuta mwanya wa kushambulia dhidi ya ‘mvua’ alizokuwa anatumiwa.
Na alipoupata mwanya huyo, akatuma ngumi tatu za haraka, zikamlaza Denmark chini! Wenzake wakamsogelea haraka kumjulia hali.
“Let go of me!” Denmark akawaka akiwasukumia wenzake kando, Alipatwa na hasira maradufu. Uso wake ulikuwa mwekundu. Aling’ata meno yake kwanguvu, akasimama na kumtazama Lee akihema kana kwamba mbogo.
Lee akamkaribisha tena kwa kumuita kwa ishara na kusema,
“Camon my lady.”
***