Angalizo: Makonda akiendeleza siasa kwenye maandalizi ya Taifa Stars atawagawa watanzania

Angalizo: Makonda akiendeleza siasa kwenye maandalizi ya Taifa Stars atawagawa watanzania

Sio tu kuwagawa....makonda huwa hafanikiwi kitu chochote
Heshima kwenu wanajamvi.
Natoa tahadhari kwa TFF na watanzania kwa ujumla kuwa makini na propaganda za kisiasa zinazofanywa na mkuu wa mkoa wa Dsm Paul Makonda kila anapozungumzia maandalizi ya mchezo wa Taifa Stars dhididi ya Uganda.

Makonda anatumia nafasi aliyopewa ya mwenyekiti wa kamati ya maandalizi kumsifia rais na serikali badals ya kuwahamasisha watanzania kuisapoti timu ya taifa.

Natoa angalizo kwa TFF kuacha kuwateua wanasiasa kwenye masuala ya mpira kwani kunawagawa watanzania badala ya kuwaunganisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heshima kwenu wanajamvi.
Natoa tahadhari kwa TFF na watanzania kwa ujumla kuwa makini na propaganda za kisiasa zinazofanywa na mkuu wa mkoa wa Dsm Paul Makonda kila anapozungumzia maandalizi ya mchezo wa Taifa Stars dhididi ya Uganda.

Makonda anatumia nafasi aliyopewa ya mwenyekiti wa kamati ya maandalizi kumsifia rais na serikali badals ya kuwahamasisha watanzania kuisapoti timu ya taifa.

Natoa angalizo kwa TFF kuacha kuwateua wanasiasa kwenye masuala ya mpira kwani kunawagawa watanzania badala ya kuwaunganisha.

Ni Kupoteza muda kutaka Kuhoji Mahusiano ya Paul Makonda kama RC, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli na Serikali ya Awamu hii ya Awamu ya Tano ( 5 ) ambayo ipo chini ya CCM ambapo Wawili hao ni sehemu ya Chama na wana umuhimu Wao mkubwa tu huku kila wanachokifanya lazima ujue kuwa wanawakilisha vyema Ilani ya Chama. Kwahiyo ili labda uridhike ulikuwa unataka Makonda kila mara awe anamtaja na anamsifia Freeman Mbowe? Kwani CHADEMA tayari imeshashika Dola? Hivi ni mara ngapi huwa tunawaona Wanasiasa wote bila kujali Itikadi zao za Vyama wakijumuika pamoja pale Uwanja wa Taifa kuzishabikia Timu zetu pendwa Simba na Yanga hadi na Timu yetu ya Taifa na huwa hakuna huo Mgawanyiko wako unaojaribu Kuuhubiri hapa? Subirini Kwanza CCM itekeleze Ilani yake kwa Vitendo na kama nanyi pia ipo Siku mtakuja Kushika Dola basi mkiwa mnafanya yenu wala Watu wa CCM hawatowaingilia. Sijaona bado Kosa lolote kwa Mkuu wa Mkoa Paul Makonda juu ya hili sana sana naona tu ' Visununu ' vingi kutoka kwa Watu wenye Chuki nae Kisiasa, Kifikra na Kimtazamo. Kibinadamu Makonda ( RC ) ana mapungufu yake ila naona sasa tunazidisha hivyo tupunguze, tubadilike na mwacheni afanye Kazi yake.
 

MAKASI SOUTH AFRICA

1553214096378.png
 
Hii iko wazi na ndio maana ukiangalia utofauti wa hamasa ya Watanzania juu ya mchezo wa Simba na AS Vita halafu huu wa Stars na Uganda Cranes utaiona tofauti.
Yalikuwa makosa makubwa kumchomeka Makonda eti awe mwenyekiti wa uhamasishaji? Tena mechi ya mwisho ya muhimu?
Huyu jamaa ukiacha kuwa ni mtu mwenye gundu na historia ya kutofanikiwa kila jambo lakini pia mpira huo anataka kuugeuza siasa na mtaji wa ccm na magu.
Hakika ni aibu watu wapambane kishujaa toka huko mwanzo Leo mwisho unataka kuwaambia hizi ni juhudi za ccm na magu Kwa sababu kawaita kula na kuidhinisha pesa (ambazo hata TFF zipo,)?
Au kuwaleta hao wasanii uchwara wauza ngono?
Naanza kuliona anguko jumapili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni nani aliye amua kumpatia Makonda nafasi ya kuwa m/kiti wa uhamasishaji kwenye pambano la soka kati ya Tanzania na Uganda ?.
Huyu jamaa ni nuksi kubwa ndani ya nchi hii.
Hivi kuna asiye jua kuwa Makonda ndiye anaye shiriki kuratibu matukio ya hovyo kabisa na yanayo liletea Taifa hili aibu ndani na nje.
Hivi si ni huyu huyu aliye pelekea waziri wetu kipenzi Nape kung'olewa kwenye wizara ya michezo?.
Ukweli ni kwamba hata Mungu hapendi na hiyo shughuli isha ingia mkosi lazima Uganda itufunge na Caf ni lazima wafuatilie vitendo vya rushwa kwenye mchezo huu.
Hata huyu Karia hafai kabisa na sijui kwa nini huyu jamaa alishinda kwenye hiyo nafasi na kuachwa kwa watu makini kama Ally Mayai.
Sasa naona Makonda akihamasisha kisiasa zaidi akidhani kuwa timu yetu ya Taifa ni tawi la CCM aibu na imrudie yeye mwenyewe kwa kuwa hana mikono safi ya kufanya jambo jema litakalo Fanya Mwenyezi Mungu aweze kuzisikiliza dua za watanzania .


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii iko wazi na ndio maana ukiangalia utofauti wa hamasa ya Watanzania juu ya mchezo wa Simba na AS Vita halafu huu wa Stars na Uganda Cranes utaiona tofauti.
Yalikuwa makosa makubwa kumchomeka Makonda eti awe mwenyekiti wa uhamasishaji? Tena mechi ya mwisho ya muhimu?
Huyu jamaa ukiacha kuwa ni mtu mwenye gundu na historia ya kutofanikiwa kila jambo lakini pia mpira huo anataka kuugeuza siasa na mtaji wa ccm na magu.
Hakika ni aibu watu wapambane kishujaa toka huko mwanzo Leo mwisho unataka kuwaambia hizi ni juhudi za ccm na magu Kwa sababu kawaita kula na kuidhinisha pesa (ambazo hata TFF zipo,)?
Au kuwaleta hao wasanii uchwara wauza ngono?
Naanza kuliona anguko jumapili

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Stars watashinda ila wamefanya makosa sana kumuweka Makonda kuongoza kamati ni sawa na ku politisize mpira, Makonda hana uzalendo kwa nchi zaidi ya uzalendo kwa Magufuli, hana uwezo wa kuwaunganisha wananchi kwa sababu ana makando kando mengi, huwa anajitahidi kutafuta events kama hizi kuwa mstari wa mbele ikiwemo misiba kutaka kujisafisha ili aonekane mwema.

Taifa Stars ingekuwa siyo timu ya taifa ningeishangilia Uganda Cranes. Ku protest uwepo wake kama mwenyekiti wa kamati sitoenda uwanjani ila nitai support Taifa Stars.
 
Mkuu Stars watashinda ila wamefanya makosa sana kumuweka Makonda kuongoza kamati ni sawa na ku politisize mpira, Makonda hana uzalendo kwa nchi zaidi ya uzalendo kwa Magufuli, hana uwezo wa kuwaunganisha wananchi kwa sababu ana makando kando mengi, huwa anajitahidi kutafuta events kama hizi ikiwemo misiba kutaka kujisafisha ili aonekane mwema.

Kwa uwepo wake, Taifa Stars ingekuwa siyo timu ya taifa ningeishangilia Uganda.
Kama ni hivo hata mim siendi
 
Mkuu Stars watashinda ila wamefanya makosa sana kumuweka Makonda kuongoza kamati ni sawa na ku politisize mpira, Makonda hana uzalendo kwa nchi zaidi ya uzalendo kwa Magufuli, hana uwezo wa kuwaunganisha wananchi kwa sababu ana makando kando mengi, huwa anajitahidi kutafuta events kama hizi ikiwemo misiba kutaka kujisafisha ili aonekane mwema.

Kwa uwepo wake, Taifa Stars ingekuwa siyo timu ya taifa ningeishangilia Uganda.
Mkuu, Uganda wakicheza soka lao la siku zote,
Stars haishindi..

Labda kuwe kuna makubaliano huko pembeni na ole CAF wasigundue..

Uwepo wa Bashite pale tayari ni NAJISI..

Nimesikia-sikia tetesi kuwa hata MO kwenye hivi vikao vya hii Kamati ambapo pia ni mjumbe haendi..

Ukakae meza moja na mtesi wako..??Haiwezekani.

Tatizo ikishinda Stars tutaambiwa ni JUHUDI nk nk..

Go Cranes Go.
 
Ni Kupoteza muda kutaka Kuhoji Mahusiano ya Paul Makonda kama RC, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli na Serikali ya Awamu hii ya Awamu ya Tano ( 5 ) ambayo ipo chini ya CCM ambapo Wawili hao ni sehemu ya Chama na wana umuhimu Wao mkubwa tu huku kila wanachokifanya lazima ujue kuwa wanawakilisha vyema Ilani ya Chama. Kwahiyo ili labda uridhike ulikuwa unataka Makonda kila mara awe anamtaja na anamsifia Freeman Mbowe? Kwani CHADEMA tayari imeshashika Dola? Hivi ni mara ngapi huwa tunawaona Wanasiasa wote bila kujali Itikadi zao za Vyama wakijumuika pamoja pale Uwanja wa Taifa kuzishabikia Timu zetu pendwa Simba na Yanga hadi na Timu yetu ya Taifa na huwa hakuna huo Mgawanyiko wako unaojaribu Kuuhubiri hapa? Subirini Kwanza CCM itekeleze Ilani yake kwa Vitendo na kama nanyi pia ipo Siku mtakuja Kushika Dola basi mkiwa mnafanya yenu wala Watu wa CCM hawatowaingilia. Sijaona bado Kosa lolote kwa Mkuu wa Mkoa Paul Makonda juu ya hili sana sana naona tu ' Visununu ' vingi kutoka kwa Watu wenye Chuki nae Kisiasa, Kifikra na Kimtazamo. Kibinadamu Makonda ( RC ) ana mapungufu yake ila naona sasa tunazidisha hivyo tupunguze, tubadilike na mwacheni afanye Kazi yake.
Hata uingereza hawamtukuzi hivyo malkia!!
 
Back
Top Bottom