Angalizo: Tunatarajia muswada wa marekebisho kuhusu nishati

Angalizo: Tunatarajia muswada wa marekebisho kuhusu nishati

jingalao

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
36,197
Reaction score
29,717
Nichukue Fursa hii kumpongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusukuma mbele gurudumu la maendeleo nchini Tanzania. Yapo mambo mengi yaliyobadilishwa naye katika kipindi kifupi kwa mustakabali wa Tanzania mbele ya Uso wa kidiplomasia.

Mengi ni mazuri na ni muendelezo na marekebisho wa awamu ya Tano.

ANGALIZO
Tunatarajia kuletewa marekebisho mbalimbali ya kisheria yanayogusa rasilimali zetu hususani katika eneo la nishati.

Ikumbukwe kuwa tulikuwa na sheria mbovu zilizokosa meno katika usimamizi wa rasilimali zetu za asili jambo lililopelekea tuje nasheria za umiliki wa rasilimali zetu za asili.

Tulitumia nguvu na mali nyingi ili kufanikisha suala hilo na hatimaye tukawa na sheria bora za udhibiti wa rasilimali hizo za asili.

Tunapoelekea kushangilia ufutaji wa mzigo wa kodi na tozo mbalimbali katika mafuta/nishati kamwe tusije KUCHOMEKEWA jambo bovu litakaloondoa milestone tuliyoifikia.yaani umiliki wa rasilimali zetu.

NASAHA KWA BUNGE
Tusome na kuelewa in details kile kitakachowasikishwa katika mapendekezo ya marekebisho ya sheria. Tukumbuke kuwa tunachokibadilisha kinaweza kubadilishwa pia lakini maamuzi ya leo yana athari ya kesho.

#CATEGORICAL#

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Kuna mbunge yeyote mwenye uelewa wa mikataba na Sheria za Nchi hii kwa Sasa bungeni?

Kama Rais anakosa mtu wa kumteua kuwa Waziri bungeni ije iwe kupata wabunge wa kutengeneza Sheria na mikataba?

Anagalia mbunge kama Slaa anafukuzwa bungeni kihuni vile wanabaki wakina msukuma.

Tunaenda kupigwa Kama kwenye Gesi.
 
Tunapoelekea kushangilia ufutaji wa mzigo wa kodi na tozo mbalimbali katika mafuta/nishati kamwe tusije KUCHOMEKEWA jambo bovu litakaloondoa milestone tuliyoifikia.yaani umiliki wa rasilimali zetu.[emoji1534][emoji1545]
 
Haya ndio madhara ya magufuli kutaka kuua upinzani. Bungeni wamejaa vilaza alio waweka ili siku skitaka kujiongezea muda wa madaraka asiwepo wa kuhoji.

Swali ni je, hao vilaza waliowekwa na mwendazake wana uwezo wa kuchambua mambo mazito kama hayo?
 
#NASAHA KWA BUNGE
Tusome na kuelewa in details kile kitakachowasikishwa katika mapendekezo ya marekebisho ya sheria.Tukumbuke kuwa tunachokibadilisha kinaweza kubadilishwa pia lakini maamuzi ya leo yana athari ya kesho!

[emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541][emoji1546][emoji1541] kwa aina ya bunge tulilonalo hakuns kitu hapo.. Ukiachana na uvivu wa kusoma na kuchambua vitu hata uelewa wenyewe ni janga.. Na kwa bahati mbaya sana mabadiliko husika yanaweza kuletwa kwa maandishi ya kiingereza ...lugha ambayo ni mtihani mkubwa kwa 'wahishimiwa' wetu!
 
Wabunge ambao kwenye tozo za simu walisema eti walishtukia tu sheria imetungwa kama wangejua wasingekubali na muda huohuo walikua Bungeni, hawana msaada na bunge la chama kimoja halina tija ya kulinda maslahi ya wananchi wao husimama kulinda maslahi ya chama chao na sio tofauti
 
Kuna mbunge yeyote mwenye uelewa wa mikataba na Sheria za Nchi hii kwa Sasa bungeni?

Kama Rais anakosa mtu wa kumteua kuwa Waziri bungeni ije iwe kupata wabunge wa kutengeneza Sheria na mikataba

Tunaenda kupigwa Kama kwenye Gesi.
Aibu tupu
 
Kuna mbunge yeyote mwenye uelewa wa mikataba na Sheria za Nchi hii kwa Sasa bungeni?

Kama Rais anakosa mtu wa kumteua kuwa Waziri bungeni ije iwe kupata wabunge wa kutengeneza Sheria na mikataba

Tunaenda kupigwa Kama kwenye Gesi.

8F699D55-D2F6-49E0-B72B-8F5FCA8CF8A0.jpeg
 
Wabunge ambao kwenye tozo za simu walisema eti walishtukia tu sheria imetungwa kama wangejua wasingekubali na muda huohuo walikua Bungeni, hawana msaada na bunge la chama kimoja halina tija ya kulinda maslahi ya wananchi wao husimama kulinda maslahi ya chama chao na sio tofauti
Hakuna bunge hapo hilo ni genge la wahuni tupu
 
Back
Top Bottom