Angezungumza kama alivyozungumza Emmanuel Nchimbi angepungukiwa nini?

Angezungumza kama alivyozungumza Emmanuel Nchimbi angepungukiwa nini?

la muhimu zaidi ni kwamba,
Amani ya Tanzania tutailinda kwa Gharama yoyote 🐒
Huwezi kulinda watu 60 kwa kutugemea vyombo vya ulinzi huku ukiwakamata na kuwaua kama kuku...haijawahi kufanikiwa....ni suala la muda tu
 
viongozi wanasali makanisani ni vyema wachungaji watumie madhabau kukemea hao waumini kuikataa dhambi..ni unafiki kuswali mara kumi kwa siku bila kumwambia muumini wako acha kuuwa watu acha kuonea watu lazima viongozi wa dini wawe mstari wa mbele kuikemea dhambi
WASIWE NA DOUBLE STANDARDS SASA,AKIWA MWANAKONDOO WANAINAMISHA VICHWA CHINI HAWAMBWAMBIII...AKIWA MVAA KOBAZI MIWARAKA KIBAAOOO...
 
WASIWE NA DOUBLE STANDARDS SASA,AKIWA MWANAKONDOO WANAINAMISHA VICHWA CHINI HAWAMBWAMBIII...AKIWA MVAA KOBAZI MIWARAKA KIBAAOOO...
Mwanakondoo yupi ambaye aliinamiishiwa kichwa chini? Unafikiri BAKWATA wale?
 
Baada ya Chadema kutangaza maandamano kupinga kutekwa na kuuwawa kwa Wanachama wao na Watanzania kulitokea ka tension kadogo.

Tension hii ilipata msisimko baada ya Viongozi wa dini kuanza kukemea.

Kwa kuwa tuhuma hizi zilikihusu Chama cha Mapinduzi na vyombo vya Serikali yake hasa Polisi na TISS ilihitajika kauli thabiti na yenye hekima kutoka Chama cha Mapinduzi.

Tuseme ukweli Press aliyoifanya Comred Emmanuel Nchimi ilituliza sana mioyo ya watanzania ingawa haikuwapa majibu juu ya mustakabali ya haki yao kuu ya kuishi!

Nchimbi kama Mwanasiasa aliyelelewa na wazee wenye exposure hekima na busara aliongea vizuri sana na kwa sehemu kubwa kuweza kutuliza tension ya Wananchi.

Kituko kilikuja kutokea jana. Kusema kweli Mwenyekiti jana ametia petrol na kiberiti kwenye moto alioweza kuuzima kidogo Comrade Nchimbi.

Mbaya zaidi kanunua ugomvi na wakubwa ambao ndiyo wanamlisha na kuendesha miradi yake mingi kwa misaada na mikopo yao.

Nimefuatilia maoni ya wananchi kwa jana na leo, mitaani na kwenye mitandao. Kusema ukweli Mwenyekiti wetu jana aliharibu sana.

Wananchi wanatoa maoni bila kificho tena kwa account zenye majina yao kulaaani maneno yake ya jana.

Swali nililojiuliza ni kuwa, baada ya Comrade Nchimbi kuzungumza vizuri siku ile na kutuliza upepo. Kulikuwa na haja ya yeye jana kuzungumza maneno yale aliyozungumza?

Ushauri wangu kwake,

" Gombana na Nchi za Magharibi ukiwa na internal support na kamwe usianzishe ugomvi na Magharibi ukiwa hohehahe kwenye internal support "
NCHIMBI siyo sawa na SAMIA hao ni watu wawili tofauti
 
Kwa vp make watu wanatekwa wanauwawa au ndo kulinda uko!
Licha ya changamoto zozote zile za kisiasa au za kiusalama ambazo ni jambo la kawaida sana dunia nzima,

Amani ya Tanzania italindwa kwa nguvu na gharama zote bila mbambamba yoyote gentleman, upende usipende 🐒
 
la muhimu zaidi ni kwamba,
Amani ya Tanzania tutailinda kwa Gharama yoyote 🐒
Amani au uoga wa waTanzania mtaulinda kwa gharama yoyote? Kizazi kimebadilika hiki, sio kile cha kusujudia viongozi majizi kwa kichaka cha amani.
 
Baada ya Chadema kutangaza maandamano kupinga kutekwa na kuuwawa kwa Wanachama wao na Watanzania kulitokea ka tension kadogo.

Tension hii ilipata msisimko baada ya Viongozi wa dini kuanza kukemea.

Kwa kuwa tuhuma hizi zilikihusu Chama cha Mapinduzi na vyombo vya Serikali yake hasa Polisi na TISS ilihitajika kauli thabiti na yenye hekima kutoka Chama cha Mapinduzi.

Tuseme ukweli Press aliyoifanya Comred Emmanuel Nchimi ilituliza sana mioyo ya watanzania ingawa haikuwapa majibu juu ya mustakabali ya haki yao kuu ya kuishi!

Nchimbi kama Mwanasiasa aliyelelewa na wazee wenye exposure hekima na busara aliongea vizuri sana na kwa sehemu kubwa kuweza kutuliza tension ya Wananchi.

Kituko kilikuja kutokea jana. Kusema kweli Mwenyekiti jana ametia petrol na kiberiti kwenye moto alioweza kuuzima kidogo Comrade Nchimbi.

Mbaya zaidi kanunua ugomvi na wakubwa ambao ndiyo wanamlisha na kuendesha miradi yake mingi kwa misaada na mikopo yao.

Nimefuatilia maoni ya wananchi kwa jana na leo, mitaani na kwenye mitandao. Kusema ukweli Mwenyekiti wetu jana aliharibu sana.

Wananchi wanatoa maoni bila kificho tena kwa account zenye majina yao kulaaani maneno yake ya jana.

Swali nililojiuliza ni kuwa, baada ya Comrade Nchimbi kuzungumza vizuri siku ile na kutuliza upepo. Kulikuwa na haja ya yeye jana kuzungumza maneno yale aliyozungumza?

Ushauri wangu kwake,

" Gombana na Nchi za Magharibi ukiwa na internal support na kamwe usianzishe ugomvi na Magharibi ukiwa hohehahe kwenye internal support "
Watu wanaomzunguka huwa wana screenshort comments za akina Lucas Mwashambwa , ChoiceVariable na wenzao na kumpelekea kumuonyesha anavyokubalika mitandaoni. Siku hizi hawamruhusu aiongie mwenyewe mitandaoni wakimdanganya kuwe eti siku hizi pagers zinaripuka
 
PENGO ALIONGEA CHOCHOTE??KKKT ILIONGEA NINI KIPINDI KILE??

ACHENI DOUBLE STANDARDS KAMA KWELI MNAMAANISHA
Ingiia youtube ndugu yangu....sisi wagalatia tunakumbuka Serikali ya Magufuli ilichanwa mara za kutosha
 
kuku wako fuga huko huko bandani kwako,

Amani ya Tanzania italindwa kwa gharama yoyote upende usipende 🐒
Kama gharama ni kutoa uhai wa wapinzani na wakosoaji wa serikali hata nyinyi mnaojiona mmeshikilia mpini uhai wenu utatolewa tu ....ni suala la muda
 
Amani au uoga wa waTanzania mtaulinda kwa gharama yoyote? Kizazi kimebadilika hiki, sio kile cha kusujudia viongozi majizi kwa kichaka cha amani.
serikali makini na madhubuti sana ya Dr. Samia Suluhu Hassan, haipuzii wala kuleta mzaha kwenye kitisho cha Amani ya nchi hata kama ni cha mlevi, mvuta bangi au mwenye shida ya akili..

atadhibitiwa kwa nguvu ya kiwango kile kile kama atakavyodhibitiwa kibaka, jambazi na muhalifu atakaethubutu kushiriki maandamano haramu ya Chadema 🐒
 
Kama gharama ni kutoa uhai wa wapinzani na wakosoaji wa serikali hata nyinyi mnaojiona mmeshikilia mpini uhai wenu utatolewa tu ....ni suala la muda
kwenye suala la umoja, amani na utulivu wa wananchi wa waTanzania hakuna mpini wala jembe,

Jembe na mpini wake vikatumike shambani kwaajili ya uzalishaji gentleman 🐒

kumbuka,
tunalinda amani ya waTanzania, sio hao wapinzani au kikundi Fulani cha watu ni amani ya waTanzania wote bila kujali vyama, ukabila au dini zao 🐒
 
Unafikiri kilichokuleta mitandaoni tena kwa ID ya kujificha ni kipi? Si kwasababu huko ground wewe ni mwenzao hali ni mbaya lakini unawang'ing'a na ili kuwasifu unalazimika kutumia ID fake ?
Hali ni mbaya? Hali gani hiyo mbaya? Mitandaoni ni sehemu yangu ya burudani na kuwachora kama sio kuwacheka mnaojifariji humu jf,sawa tuu na Mafuriko ya Lowasa mitandaoni 🤪🤪

Wapiga kura wako Mitaani na ni Hawa hapa 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C_8QrndITIq/?igsh=bWEzbjNiMGpieXVn
 
Back
Top Bottom