Chama dola kongwe kimeishiwa mbinu zote walizozoea kutumia kama silaha, ambazo ni Bunge, Mahakama, Sheria za Uchu wa Kubaki Madarakani, Propaganda Mfu Amani ipo Tanzania n.k
- 2024 September Mauaji yapigiwa kelele waziwazi mbele ya waziri wa mambo ya ndani Eng. Masauni ktk maziko ya mzee Ali Mohamed Kibao
- 2024 Mahakama Kuu inajitutumua kuacha kutumiwa kama silaha ya vitisho na CCM- KESI YA TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa mitaa, vitongoji na vijiji pingamizi la serikali latupiliwa mbali
- 2024 Agosti - Watu wa nyikani Ngorongoro wajiunga ktk wingi wao kama jamii ya kiMaasai, serikali ya CCM yasalimu amri Kabudi na Lukuvi waenda kuomba msamaha
- 2024 Agosti serikali ya CCM yatumia chakula kama silaha ya kivita kwa kuweka mageti barabarani kuzuia chakula kisifike Ngorongoro
- 2024 kuelekea Siku ya Vijana Duniani tarehe 12 Agosti 2024 jijini Mbeya wafuasi 500 wa CHADEMA wasukumwa mahabusu na kutishiwa kufunguliwa kesi,
- 2023 November CCM yatumia bunge lake la chama kimoja Dodoma kama silaha ya ugandamizi, kwa kupuuza kuweka viraka vya sheria ya uchaguzi Tume Huru ya Uchaguzi INEC isiweze kusimamia uchaguzi wa November 2024
- 2023 Tundu Lissu na CHADEMA Kanda ya kaskazini wazuiwa kuingia Ngorongoro Loliondo na kufunguliwa kesi, ambazo serikali imeshindwa kuendlea na kesi