Pre GE2025 Anguko la CCM linazidi kuonekana chini ya utawala wa Awamu ya 6

Pre GE2025 Anguko la CCM linazidi kuonekana chini ya utawala wa Awamu ya 6

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
12 September 2024
Dodoma, Tanzania

Mnyika - Akemea Vyama vya Siasa Kutoheshimiwa, Dhamira mbaya ya CCM, Vitendo vya kutengeneza hofu


View: https://m.youtube.com/watch?v=Zz0R5vqfYjo

Raia huru, kukataa kuwa mateka ndani ya nchi yako, kutembea bila hofu pia haki ya kuwakilishwa na viongozi tuliowachagua kupitia uchaguzi ulio huru na haki

Hatuwezi kuwa wafungwa wa sheria mbovu ingawa wanataka tusisie uchaguzi wa November 2024 ili wabaki madarakani ngazi ya vijiji, mtaa na vitongoji.

Katibu mkuu wa CHADEMA anasema tutamalizana nao mitaani, vitongoji na vijijini kwa kujiandikisha katika daftari la mpiga kura ngazi ya serikali za mitaa na kuanzia leo ...
 
ARUSHA YAUNGA MAANDAMANO YA TAREHE 23 SEPTEMBER 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=JSC1wY7LsLk

Maandamano hayo ni kupinga mauaji ya kada wa CHADEMA mzee Ali Mohamed Kibao pia utekaji wa viongozi wa CHADENA unaoendelea kufanywa na vyombo vya dola chini ya utawala wa chama dola kongwe CCM
 
Kama ni kusubiria anguko la chama dola, na kuhakikishia utasubiri sana kwasababu CCM sio tuu ni chama cha siasa, ni chama dola, ni dola!. CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola!
P
Achilia mbali "chama dola", hata dola yenyewe huanguka na kupotea kabisa...

Dola ya Rumi, Dola ya Misri ya kale chini ya Farao zilizowahi kuwa na nguvu sana duniani, zilianguka na kupotea hadi leo....

Mwisho wa jambo lolote haupimwi wala kuangaliwa kwa namna unavyoangalia wewe kwa kuwa unaona ukubwa wake, nguvu zake na uwezo wake kwa macho yako tu ya damu na nyama...

Mwisho wa kitu au jambo hupimwa kwa kuangalia majira na ishara za nyakati....

Watu wa Sodoma na Gomorra waliangamia wote kwa sbb ya ujinga wao wa kutosoma ishara za nyakati na majira. Walikuwa wanajiona wako fresh, wana kila kitu, nguvu na mapesa ya kula maraha. Bahati mbaya ni kuwa walikuwa wajinga kama walivyo CCM leo....!

Kizazi cha Nuhu (Noah) kilichoangamizwa na mafuriko ya maji (gharika) ya Mungu kilikuwa na kila kitu, kilijiona kina akili na nguvu nyingi, lakini kikaangamia chote kwa sababu ya ujinga wa kushindwa kuzielewa ishara za nyakati na majira kama walivyo CCM....

Ishara za nyakati na majira, zinathibitisha mwisho wa CCM umefika haijalishi mnajiona mna nguvu kiasi gani maana hazitawasaidia kwa kuwa MAJIRA na NYAKATI zina nguvu zaidi ya hizo zenu

Kumbuka kanuni hii muhimu ya asili: Kwamba, hakuna kilicho na mwanzo kikakosa kuwa na mwisho wake....!!
 
Kama ni kusubiria anguko la chama dola, na kuhakikishia utasubiri sana kwasababu CCM sio tuu ni chama cha siasa, ni chama dola, ni dola!. CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola!
P

Paskali, never say never. Ni makundi tofauti ndani ya dola yenye kutaka dola yatakayoleteana shida. Mwalimu Nyerere alisema ipo siku itapasuka na kutakuwa na upinzani halisi. Siku zote kikulacho ki nguoni mwako. Kuna mambo usijaribu kuyabeza.

Kuna siku jamaa mmoja aliwahi kuniambia USSR isambaratike. IMPOSSIBLE. Kule nilikokuwa kulikuwa na warusi wananunua nguruwe mzima kila mtu ili wakale. Nilikuwa nawashangaa sana. Kumbe ile ilikuwa dalili kuwa kwao kuna njaa. Na njaa haina adabu kabisa. Lakini hapo hapo, sababu ya mahaba yetu, mtu mwingine anasema IMPOSSIBLE. Infact, Mwenyezi Mungu peke yake ndiye atatawala milele
 
Achilia mbali "chama dola", hata dola yenyewe huanguka na kupotea kabisa...

Dola ya Rumi, Dola ya Misri ya kale chini ya Farao zilizowahi kuwa na nguvu sana duniani, zilianguka na kupotea hadi leo....

Mwisho wa jambo lolote haupimwi wala kuangaliwa kwa namna unavyoangalia wewe kwa kuwa unaona ukubwa wake, nguvu zake na uwezo wake kwa macho yako tu ya damu na nyama...

Mwisho wa kitu au jambo hupimwa kwa kuangalia majira na ishara za nyakati....

Watu wa Sodoma na Gomorra waliangamia wote kwa sbb ya ujinga wao wa kutosoma ishara za nyakati na majira. Walikuwa wanajiona wako fresh, wana kila kitu, nguvu na mapesa ya kula maraha. Bahati mbaya ni kuwa walikuwa wajinga kama walivyo CCM leo....!

Kizazi cha Nuhu (Noah) kilichoangamizwa na mafuriko ya maji (gharika) ya Mungu kilikuwa na kila kitu, kilijiona kina akili na nguvu nyingi, lakini kikaangamia chote kwa sababu ya ujinga wa kushindwa kuzielewa ishara za nyakati na majira kama walivyo CCM....

Ishara za nyakati na majira, zinathibitisha mwisho wa CCM umefika haijalishi mnajiona mna nguvu kiasi gani maana hazitawasaidia kwa kuwa MAJIRA na NYAKATI zina nguvu zaidi ya hizo zenu

Kumbuka kanuni hii muhimu ya asili: Kwamba, hakuna kilicho na mwanzo kikakosa kuwa na mwisho wake....!!

Kitu chochote kinachoendeshwa bila nidhamu kina nafasi kubwea ya kusambaratika. Hizi dola kubwa zilianguka. Tusibeze hata kidogo kuanguka kwa chama. Kama kitawasahau watanzania walio wengi, kikaendekeza interest ya kundi dogo lenye ubinafsi na hila, lazima wataachana na wataachana mazima
 
Chama dola kongwe kimeishiwa mbinu zote walizozoea kutumia kama silaha, ambazo ni Bunge, Mahakama, Sheria za Uchu wa Kubaki Madarakani, Propaganda Mfu Amani ipo Tanzania n.k
  • 2024 September Mauaji yapigiwa kelele waziwazi mbele ya waziri wa mambo ya ndani Eng. Masauni ktk maziko ya mzee Ali Mohamed Kibao
  • 2024 Mahakama Kuu inajitutumua kuacha kutumiwa kama silaha ya vitisho na CCM- KESI YA TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa mitaa, vitongoji na vijiji pingamizi la serikali latupiliwa mbali
  • 2024 Agosti - Watu wa nyikani Ngorongoro wajiunga ktk wingi wao kama jamii ya kiMaasai, serikali ya CCM yasalimu amri Kabudi na Lukuvi waenda kuomba msamaha
  • 2024 Agosti serikali ya CCM yatumia chakula kama silaha ya kivita kwa kuweka mageti barabarani kuzuia chakula kisifike Ngorongoro
  • 2024 kuelekea Siku ya Vijana Duniani tarehe 12 Agosti 2024 jijini Mbeya wafuasi 500 wa CHADEMA wasukumwa mahabusu na kutishiwa kufunguliwa kesi,
  • 2023 November CCM yatumia bunge lake la chama kimoja Dodoma kama silaha ya ugandamizi, kwa kupuuza kuweka viraka vya sheria ya uchaguzi Tume Huru ya Uchaguzi INEC isiweze kusimamia uchaguzi wa November 2024
  • 2023 Tundu Lissu na CHADEMA Kanda ya kaskazini wazuiwa kuingia Ngorongoro Loliondo na kufunguliwa kesi, ambazo serikali imeshindwa kuendlea na kesi
Mene mene tekeli na peresi!
 
Chama dola kongwe kimeishiwa mbinu zote walizozoea kutumia kama silaha, ambazo ni Bunge, Mahakama, Sheria za Uchu wa Kubaki Madarakani, Propaganda Mfu Amani ipo Tanzania n.k
  • 2024 September Mauaji yapigiwa kelele waziwazi mbele ya waziri wa mambo ya ndani Eng. Masauni ktk maziko ya mzee Ali Mohamed Kibao
  • 2024 Mahakama Kuu inajitutumua kuacha kutumiwa kama silaha ya vitisho na CCM- KESI YA TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa mitaa, vitongoji na vijiji pingamizi la serikali latupiliwa mbali
  • 2024 Agosti - Watu wa nyikani Ngorongoro wajiunga ktk wingi wao kama jamii ya kiMaasai, serikali ya CCM yasalimu amri Kabudi na Lukuvi waenda kuomba msamaha
  • 2024 Agosti serikali ya CCM yatumia chakula kama silaha ya kivita kwa kuweka mageti barabarani kuzuia chakula kisifike Ngorongoro
  • 2024 kuelekea Siku ya Vijana Duniani tarehe 12 Agosti 2024 jijini Mbeya wafuasi 500 wa CHADEMA wasukumwa mahabusu na kutishiwa kufunguliwa kesi,
  • 2023 November CCM yatumia bunge lake la chama kimoja Dodoma kama silaha ya ugandamizi, kwa kupuuza kuweka viraka vya sheria ya uchaguzi Tume Huru ya Uchaguzi INEC isiweze kusimamia uchaguzi wa November 2024
  • 2023 Tundu Lissu na CHADEMA Kanda ya kaskazini wazuiwa kuingia Ngorongoro Loliondo na kufunguliwa kesi, ambazo serikali imeshindwa kuendlea na kesi
Hizi ni harakati zile zile za siku za nyuma haswa awamu ya Kikwete, awamu ya Samia ni marudio ya awamu ya Kikwete, hakuna jipya lolote ambalo halijaipa nchi uzoefu wa miaka ya nyuma.
 
Tuache kujidanganya ccm ni taasisi imara sana ingawa ina mapungufu yake kwenye mambo kadhaa ila imeviacha mbali sana hivi vyama vingine huo ndio ukweli, 2025 ccm itashinda kwa kishindo sioni wa kuisumbua ccm kwa sasa
CCM ipo mpaka kule mpakani Kigoma na Katavi, ipo kila sehemu na inafanya vikao kwa mujibu wa katiba yake huko ilipo.

Huwezi kulinganisha na vyama vya mifukoni mwa watu, vyama vya kurasa za kwanza za magazeti ya mijini.

Kuna kipindi JPM alitufikisha uchumi wa kati hatua za chini, Samia anatupelekea uchumi wa kati hatua ya juu na anatoa ushirikiano kwa taasisi na watu makini na ambacho anakipata katika huo ushirikiano kinakuwa na faida kwa Tanzania nzima.
 
Una miaka mingapi toka kuzaliwa kwako?
Umebakiwa na miaka mingapi yakuishi hapa duniani?

Ccm itakufa kama wewe utakavyokufa.

Najua kinachowapa kiburi ni bunduki na wala sio kukubalika.
Mimi na wewe pia tutakufa, tofautisha siasa za kiunaharakati anazofanya Mbowe na uhalisia wa mapambano ya kiuchumi anaoufanya Samia kila siku.

Kutanguliza suala la vifo ni siasa zile zile za kukosa ubunifu, hakuna kilicho na uhai ambacho hakitakufa.
 
Chama dola kongwe kimeishiwa mbinu zote walizozoea kutumia kama silaha, ambazo ni Bunge, Mahakama, Sheria za Uchu wa Kubaki Madarakani, Propaganda Mfu Amani ipo Tanzania n.k
  • 2024 September Mauaji yapigiwa kelele waziwazi mbele ya waziri wa mambo ya ndani Eng. Masauni ktk maziko ya mzee Ali Mohamed Kibao
  • 2024 Mahakama Kuu inajitutumua kuacha kutumiwa kama silaha ya vitisho na CCM- KESI YA TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa mitaa, vitongoji na vijiji pingamizi la serikali latupiliwa mbali
  • 2024 Agosti - Watu wa nyikani Ngorongoro wajiunga ktk wingi wao kama jamii ya kiMaasai, serikali ya CCM yasalimu amri Kabudi na Lukuvi waenda kuomba msamaha
  • 2024 Agosti serikali ya CCM yatumia chakula kama silaha ya kivita kwa kuweka mageti barabarani kuzuia chakula kisifike Ngorongoro
  • 2024 kuelekea Siku ya Vijana Duniani tarehe 12 Agosti 2024 jijini Mbeya wafuasi 500 wa CHADEMA wasukumwa mahabusu na kutishiwa kufunguliwa kesi,
  • 2023 November CCM yatumia bunge lake la chama kimoja Dodoma kama silaha ya ugandamizi, kwa kupuuza kuweka viraka vya sheria ya uchaguzi Tume Huru ya Uchaguzi INEC isiweze kusimamia uchaguzi wa November 2024
  • 2023 Tundu Lissu na CHADEMA Kanda ya kaskazini wazuiwa kuingia Ngorongoro Loliondo na kufunguliwa kesi, ambazo serikali imeshindwa kuendlea na kesi
Mtaweweseka sana kwa CCM.
 
Back
Top Bottom