Annunaki created Man: Binadamu tunaoishi sasa tulitengenezwa (tuliumbwa) na Annunaki

Annunaki created Man: Binadamu tunaoishi sasa tulitengenezwa (tuliumbwa) na Annunaki

Inaonekana hata maana ya tamko "logic" huijui japo umekusudia "maana". Msingi wangu umejikita katika kuhakiki habari na kuujua ukweli kama ulivyo. Huwezi kuniambia habari ambayo haijulikani mtu wa mwanzo ni nani ? Kisha ukategemea michoro kuelezea asili ya jambo, mwisho wa siku hao mnao warejea wakaja na dhana.

Umetoka nje ya mada hapa hatuoengelei hisia na malalamiko, hapa tunajadili uhalisia na elimu.

Hakuna alite tika nje ya mada ndiyo maana tukamuomba atupe uthibitisho wa kuwa Mwanadamu aliumbwa na Annunaki. Matokeo analeta kauli za jumla zisizo kuwa na ushahidi. Nimeuliza swali la msingi nani wa kwanza kuelezea habari za Annunaki ? Mnadai kuwa ni Sumerians, nikasema hapa hujajibu swali unatakiwa uainishe ni nani. Matokeo yake ni sarakasi.

Kuna vyanzo vinasema habari za Annunaki zimemkuta Adamu na kuna vyanzo vingine vinasema wali kuwa Majini.

Mola wetu sisi ni mmoja ila hao Annunaki tunaambiwa walikuwa wengi. Swali nani wa kwanza kuelezea hizi habari ? Msiruke ruke kama bisi.

Famili tree haijaja hivi hivi ukisoma vitabu vya Historia vinaonyesha "chain" sasa hao walio tunga habari za Annunaki ndiyo walienda kuiga habari za kwenye vitabu vya Dini.

Kingine ithibati siyo mpaka iwe picha au video, bali ni ile namna madhubuti ya kuhifadhi habari mpaka kufika kwa mtu wa kwanza, hii elimu ipo na imedhibitiwa, na ukifata njia zake lazima uujue ukweli wa mambo.

Ndiyo maana mtoa mada nikampa uhuru mimi natumia kitabu changu akihakiki na mimi nahakiki vitabu alivyo soma ili tujue nani mkweli, lakini ameshindwa kulifanya bali hakuna atakaye weza kulifanya.
ndiyo walipitia kwny vitabu vya dini kw sababu, vimedanganya, hivyo walitaka waweke wazi ukweli ambao hamuutaki.
 
Hili swali lilikuwa rahisi sana na nimemjibu kwa ufasaha na ukamilifu ulio tosheleza ndiyo maana hakurudi tena na swali hili, kama kuna kosa katika nilicho jibu onyesha na onyesha wapi nimeruka ruka, hili najua huwezi kulifanya nakupa miaka kumi.

Hilo nimeshalijibu na kulitolea mfano na uzuri nilianza mbali kidogo na nikatoa mfano wa njaa, njaa haionekani ila ina viashiria na ndivyo ilivyo katika mambo mengine, lakini pia mmeshindwa kulijengea hoja.
hujamjib, hebu tuonyeshe majibu yako hapa, usiruke ruke
 
Sawa Mkuu, hao viumbe annunaki ni viumbe walio physical in shape kama viumbe wengine. Yaani wana miili na wanazaliana.

Kwanini?
Kwa sababu umesema yupo kiumbe "Me" (Anu) na "Ke" (Ki). Kwa maana hiyo hao viumbe Anu na Ki, wameumbwa na Muumbaji aliewaumba kwanza wao jinsia Me na Ke ndio wakazaa hao watoto.

Hivyo, KILA KIUMBE CHENYE MWILI, KILICHO PHYSICAL IN SHAPE KINA MUUMBAJI WAKE ALIEKIUMBA KIUMBE HICHO.

Kwa Muktadha huo, wewe umewahi kufanya juhudi ya kumjua aliewaumba kiumbe ANU na KI kwanza?
ww nae mbona unakuw kama mgumu kuelew, unajibiw majibu huyataki, alafu umekomalia swali lile lile tu uzi mzima utazan huku tunafany debate za o level, hapa tunajadili kama greater thinkers, hujarizika n majib, anzishia uzi swali lako, maana umekomaa kwl, annunaki hawakuumbwa, walijiumba n ndiyo mungu wenu anu=annunaki =miungu=Mungu, hizi dini hazitak kuwapa ukweli kama huo.
 
Mkuu kama unamjua muumbaji wa kiumbe Anu na Ki tuambie, maana hao ni viumbe wenye mwili kama viumbe wengine lazima wawe wameumbwa na muumbaji.



Mungu ndie alieumba ULIMWENGU WOTE kama nyota zote, mwezi , jua na sayari zote, kutoka katika sayari zote alizoziumba akaichagua sayari dunia akaumba vyote vilivyomo ili kuweka mazingira rafiki kwa viumbe hai wote na kutuweka viumbe hai tuishi katika sayari hii DUNIA.

Hao viumbe wa kufikirika anunaki unasema wametoka sayari nyingine, kuja duniani. Bila kujua sayari zote alieziumba ni Mungu. Sasa hao viumbe anunaki wametoka kwenye sayari aliyoiumba Mungu na kuja kwenye sayari aliyoiumba Mungu. Sasa nakuuliza hao viumbe aliewaumba ni nani? Maana wana mwili tu kama viumbe wengine, na kila kiumbe chenye mwili lazima kiwe kimeumbwa na Muumbaji.

Nikuulize kwanza wewe unaijua solar system vizuri? Kabla sijakujibu kukuonesha kwamba Mungu ndie alieumba ulimwengu wote (including hiyo sayari mnayosema wametoka hao viumbe wa kufikirika).
No Mungu wenu hajulikani, hawezi kuumba ulimwengu na vilivyomo, na hauna uwezo wa kuthibitisha ilo.
 
Fungua akili anu=annunaki =miungu=Mungu, hutaki kuamini, endeleeni kusubiri mabikra mbinguni wa bure.
Kwanini unasema sitaki kuamini? Hapa si tunajadiliana watu wenye mitazamo tofauti mkuu au ulitaka nikubali kila unachoeleza na kuamini?

Annunaki walikuwa miungu au ni viumbe tu vyenye nguvu?
Fungua akili anu=annunaki =miungu=Mungu, hutaki kuamini, endeleeni kusubiri mabikra mbinguni wa bure.
 
Unaweza kuonesha uthibitisho (Scientifically) kwamba kiumbe chenye mwili, kilichoumbwa na muumbaji kimeumba kiumbe mwingine mwenye mwili na kumpa uhai wa kuishi?
reproductive cloning, gene cloning ingia mtandaoni usome hapo huone wanachokifanya.
 
Tatizo lako unaangalia historia ya Abraham Kwa jicho la kawaida Sana Kumbuka yeye alitoka Mesopotamia ilikozaliwa nadharia ya Mungu/Miungu hivyo hata yeye alikua kwenye chain Ile Ile hakuna maajabu yoyote nae alimwabudu Mungu El/YWH/JEHOVAH
Moja ya Miungu ya Summerians ila yeye ndie alitoka kwao na nadharia ya Mungu El Mpaka Kaanan kitendo kilichowafanya wenyeji wa nchi aliyoifikia kumshangaa maana alikua ni Mtu mkuu na tajiri wa Mali na dhahabu vile vile alikua ni Mzee mwenye hekima kiasi kwamba aliweza shawishi jamii nyingi zikamuelewa na kumsikiliza ndio maana Kila alipoenda alipokelewa vizuri kitendo ambacho ni kigumu Sana hasa Kwa jamii zile na maeneo aliyopita walikua Barbarian ila Kwa Abraham walimheshimu Sana mpaka kumruhusu apite nchi zao bila kikwazo maana aliacha Neema Kwa wenyeji,

Hicho kitendo kiliwafanya watu wengi waanze kufuata hekima zake maana alionesha matendo mengi Civilized maana alitokea jamii za Mesopotamian zenye ustaarabu wa Annunak Toka hapo kale,

Kingine Kipindi ambacho Abraham anazaliwa ANNUNAK walikua wameshaondoka miaka zaidi ya elfu Moja nyuma yake Hata yeye aliona ustaarabu wa kujenga Pyramids umeshapita miaka mingi mno kama tuonavyo Mimi na wewe Leo,

Haya Kamanda kuhusu kutengeneza story za Ibrahimu ni yeye na kizazi chake walikua na ujuzi wa kutunza kumbukumbu maana huo ndio ustaarabu wao na Wajukuu yake ambao ni Israelites waliendelea na utamaduni huo mpaka Leo hii kumbukumbu zao zipo kuanzia walipotokea mpaka idadi ya wafalme wao wote,
Hiyobilichagizwa na Asili Yao ambapo watu wa Mesopotamia na jamii nyingi zilizopitia utamaduni wa ANNUNAK hua wanahifadhi kumbukumbu kwenye tablets
Kuanzia kule
Sumerian, Babylon, Egyptian, Mexico, Aztec, Maya, Peru, Indus valley, china, India,Dogon wote Hao walipitia Accient civilization za kale Kwa kupewa na ANNUNAK Wana kumbu kumbu hizo na still Hata ukienda Leo Unaona KAZI za mikono Yao Kwa ushahidi na idhibati,

Kwahiyo Haya mambo hayapo kama unavyofikiria Soma historia wewe acha kukariri Aya za vitabu vya kiyahudu kama chanzo kikuu utapotea na kuona Malue Lue!
😁🔥
hapa lazima apakimbie, au aje na vihoja hoja tu.
 
Kama ndiyo hivyo kwa Nini unasema dini ya kikristo ni ya uongo? Na ndini annuanaki ndiyo ya kweri??. Tena unaendambali kwa kusema wakrito na waisilamu wanadanganywa tu?. Unatoa wapi kigezo Cha kusema hivyo???. Maana Kama ukristo ni wa kufikrika tu je hiyo annuanaki siyo ya kufikrika tu???. Kunawakati binadamu tunasubuliwa na Tamaa ya kujitafasilia wenyewe.
dini zote ni annunaki.
 
Safi Mkuu, atleast wewe una ufahamu mzuri. Ila naomba nikurekebishe kidogo tu. Kwenye kauli yako kwamba Mungu hausiki hapo ondoa. Mungu anahusika kwa 100%

Kwanini?
Kwa sababu yeye Mungu ndie alieumba kiumbe "ME" na "KE", akawaumbia mifumo mbalimbali katika miili ya viumbe Me na Ke, mfumo kama ya uzazi, organs mbalimbali n.k

Mifumo hiyo ndio husaidia kuzalishwa kwa mbegu na urutubishwaji wake mpaka kiumbe kinapatikana na kuzaliwa.

Hivyo Mungu amehusika kwa 100%, kama Mungu asingeumba kiumbe "Me" na "Ke" unafikiri kungekua na kuzaliana?
Mungu hatahusikaj ww wakati hazai? Hamumujuh kama n ke/me, au ndo yale kwamb amejiumba.
 
watu wapoteze muda, kusoma vitabu vinavyofundisha kukata watu vichwa na kuwapiga mawe hadi kufa.
watu wapoteze muda, kusoma vitabu vinavyofundisha kukata watu vichwa na kuwapiga mawe hadi kufa.
Hayo ndio unayoyajua kwenye hicho kitabu wengi hamjasoma hicho kitabu hamjui yaliyomo, ina maana wewe hapo katika vitabu vya dini umesoma biblia na kuishia hapo kwahiyo umetoka kuwa mkristo na kuangukia kuamini habari za Annunaki basi.
 
Umeathirika kimtazamo mpaka uulizaji wako unadhihirisha udhaifu ulionao

Kama unajielewa huwezi uliza swali 'ni na nani' alifanya moja mbili tatu

Maana inakuwa kama unalazimisha jibu lije kwa muktadha gani

Kwanini usiulize waliwezaje kufanikisha hilo au kipi kiliwezesha hilo
😂😂 jamaa uzi mzima swali moja, anajibiw hatak kuelewa, yaani haelewek anatak nini
 
400 BC ndio Unaona zamani sana Kamanda?
Yaani unamzungumzia kina Socrates,Plato, Algebra NK ambao wamekuja juzi kipindi ambacho Kila kitu Cha Accient civilization kimeshakua magofu Kwa zaidi ya miaka 350,000 BC Huko nyuma na ndio tatizo la wengi sana humu wabishi kama wewe historical time chatline inawapiga chenga Kwa kiwango kikubwa mno,

Accient civilization za kale zilianzia miaka zaidi ya million Moja Huko nyuma yaani
Pre human cloning project
Dunia ulianza kaliwa na Annunak kwanza kabla hawajawafanyia cloning Nephilims au giants

Jicho ni kipindi ambacho ENLIL anajenga mji wa ERIDU na kuwatumia Igigi Aliens kama workers kwenye
Accient gold mining,
Kipindi vita ya kwanza ya Dunia inavyopigwa,
(hapa utastaajabu Najua)
Vita kubwa inayohusisha Nuclear power weapons kati ya Igigi na Annunak binadamu walikua hawajaexist Kabisa katika Uso wa Dunia na baada ya hiyo vita Annunak wanaacha kuwatumia Igigi kama workers na kumproject Nephilims wenye ujuzi na maarifa then wanamproject na Adamu
Ilikua ni miaka mingi mno nyuma

Ila wengi humu habari kuhusu hii Dunia imeanzia Kuumbwa Kwa Adamu na maajabu Hata muumbaji wa huyo Adamu hammjui mnamwita Mungu ila hamjui ni Mungu Gani,Ndie mnayemwabudu na hamjui mnachoabudu
Mnaamini katika nadharia ya Mungu ila hamna ufahamu kumhusu,
Mpo mpo tu mnaleta ubishi wa kijinga jinga hapa
Dini zenyewe mmeletewa na wahuni Ili wawapige wao hawazifuati kamwe sababu wanajua ukweli wa mambo,

Shame to you Brain washed Afrikan!
hap watapakimbia, hawajuh time chart ya dunia kabisa
 
Mbona wapo wengi tu hatujawahi kuwaona lakini kutokana na historia tunaamini walikuepo kama vile hao akina socrates,plato na wengineo..

kwa kuwa hatujawahi kuwaona haimaanishi kwamba tusiamini kama walikuepo,tukienda hivi tutawaondoa watu wengi sana kwwmba hawakuwepo zamani.

Nitajie technolojia gani ambayo imechunguza na ikasema kwamba kutokana na mabaki ya mifupa fulani basi binadamu kaumbwa na annunaki.

Ni ipi hiyo technology ?
geological time scale nini, lead-uranium, carbon 14 dating n.k technology ni nini hizo? Au siyo teknology hizo, unatak useme ni sayansi
 
wewe jamaa hivi unajielewa kweli
Habari za Annunak kule India zilitoka kwenye ukristo?
Habari za Annunak kule mexico na Meso America zimetoka kwenye ukristo?
Habari za Annunak kule Mali kwenye kabila la Dogon zimetoka kwenye ukristo?
Habari za Annunak kule Misri na Mesopotamia zimetoka kwenye ukristo?
Habari za Annunak kule Antarctica zimetoka kwenye ukristo?

Vipi habari za Annunak walizokuta kule Mwezini wanaanga na NASA zimetokana na ukristo?

Acha kua brain washed Kamanda inaonesha jinsi Gani ulivyo mtupu kichwani na hutaki kujifunza ila kuleta ubishani wa kijinga tu

Huo ukristo wa kina Constantine pale Nicea committee Constantinople Uturuki mwaka 100AD unafahamu Nini kuhusu Accient civilization za kale kama Sumerians,Assyrian,Babylon Egyptian, Kush, Aztec,Maya, Peru Indus valley, china, India na Dogon ?
Una masikhara wewe!
Hahaha, haujui history ya dini ya kikristo Mkuu. Ungeijua usingebisha. Roma imeitawara Israel, ugiriki imeitawara Israel, misiri imeitawara Israel, kushi, Ethiopia, wachina, India, America imehusika na shuguli za Israel. Unaijua contact ya kibiashara ya kipindi Cha Ibrahim Hadi Joseph mtoto wa yakobo anauzwa misiri???. Hao wafanyabiashara waliomnunua walikuwa wanatoka wapi na wanaenda wapi?. Roma ilipoitawara Israel ujue kulikuwa na contact baina ya America, ulaya na Asia katika maswala ya kibiashara. Mkuuu Mambo ni mengi ya kukueleza. By the way Mimi nimesomea history of the Earth from it's formation na ujio wa viumbe kuanzia mimea Hadi binadamu. Ukweri ni Kuwa viumbe vya kiroho vipo Hilo sipingi hata kwenye biblia Hilo swala kulikuwa kumuzo ndiyo Paulo katika barua kwa wakolosai alitoa jibu
Wakolosai 1:15-16
[15]naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Who is the image of the invisible God, the firstborn of every creature:
[16]Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
For by him were all things created, that are in heaven, and that are in earth, visible and invisible, whether they be thrones, or dominions, or principalities, or powers: all things were created by him, and for him:
Tambua pia ukuu wa binadamu ni mkubwa kuliko viumbe vya kiroho yaani malaika, hao pepo wote majini, alliens, annuanaki etc hivyo hayawezi kuhusika na kumuumba binadamu, original ya viumbe vya kiroho ndiyo original ya binadamu pia. Ote viumbe vilivyoumbwa. SoMo Hilo ni pana Sana. Soma waebrania sura ya 1na ya 2 yote pia utaona ukuu wa binadamu
Waebrania 2:5-6
[5]Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema,
For unto the angels hath he not put in subjection the world to come, whereof we speak.
[6]Mwanadamu ni nini hata umkumbuke,
Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?
But one in a certain place testified, saying, What is man, that thou art mindful of him? or the son of man, that thou visitest him?
 
Unastaajabu Nini Kamanda kuhusu hiyo miaka Toka gold ianze kuchimbwa?
Nenda Kush kajionee historia hapo ndipo gold ilipogunduliwa miaka zaid ya laki nne BC

Unashangaa Nini unajua machimbo ya Mwenemutapa Zimbabwe Yana miaka mingapi na alichimba nani zile dhahabu kule miaka elfu nyingi Tena pre human civilization?
Unajua Accient civilization zote walikua wazalishaji wakubwa wa dhahabu kuliko bidhaa yoyote kiasi kwamba mpaka kumbu kumbu inayoonesha KAZI zao ikiwemo bronze mbali mbali zinazoonesha Mifumo ya kisasa ya uchimbaji dhahabu kiasi ambacho sisi Leo hatujafikia hiyo tech?
Naenda Google uone hizo migodi za lini. Yaani story za karine ya 15-18 ndiyo unasema civilization ya zamani. Duhu???.
Haya maajabu sasa
 
Kwahiyo mkuu kila alichokieleza

Kwahiyo mkuu kila kilichoelezwa kwenye hizi habari za Annunaki kimehakikiwa na wataalamu?

Habari za anunaki ni dhana iliyo kwenye maandishi kama ilivyo kwa dhana nyenginezo za kiimani

Mtoa anajajaribu kutumia utashi alionao katika kuhakiki dhana azijuazo kupitia nyenzo za uhakiki wa kitaalam ili kupata mtiririko uletao maana

Na sisi tunakubaliana nae katika hili analofanya Hakuna tatizo

Sasa kama una hoja za kupinga mtiririko alioanisha kwenye kutetea hoja yake weka
 
hebu tuambie kwanza sayansi nini?, alafu uwe unasoma mada vzr, hujaona sayans zilizoelezwa kabisaa?
Hiyo sayansi fiction. Mambo ya kale yapo chini ya archeology na hakuna inayozungumuzia viumbe vya kiroho. It's only physical organism Mkuu. Ninachokataa vitu vilivyofanya na binadamu vinalazimishwa Kuwa nilifanya na viumbe vya kiroho.
 
Back
Top Bottom