Antony Komu na Said Kubenea waivua nguo CHADEMA

Antony Komu na Said Kubenea waivua nguo CHADEMA

hapa nchini mpinzani wa kweli ni Zitto Kabwe pekee na ACT yake

hao wengine wanafarakana wao kwa wao kila uchwao na hawawezi kuiondoa ccm
 
Wapambane wao halafu unituhumu kuwa ninaleta propaganda!

Angalia pia hii video ya audio ya pili iliyovuja!
VIDEO:

Hujaelewa tena. Ninachokisema ni kuwa hayo mambo yalishajadiliwa na kuisha. Wewe unayarudisha na kuyafanya mapya ili kuchanganya na mchakato wa uchaguzi wa sasa ndani ya CHADEMA. Hapo ndipo propaganda zako zinaposhindwa vibaya. Umeelewa?
 
Hujaelewa tena. Ninachokisema ni kuwa hayo mambo yalishajadiliwa na kuisha. Wewe unayarudisha na kuyafanya mapya ili kuchanganya na mchakato wa uchaguzi wa sasa ndani ya CHADEMA. Hapo ndipo propaganda zako zinaposhindwa vibaya. Umeelewa?
Kama yangekuwa yameisha, kwa nini Mbunge Msigwa anayarudia tena wakati huu wa Uchaguzi wa viongozi ndani ya CHADEMA na hasa baada ya Audio nyingine kuvuja?
 
hapa nchini mpinzani wa kweli ni Zitto Kabwe pekee na ACT yake

hao wengine wanafarakana wao kwa wao kila uchwao na hawawezi kuiondoa ccm
Sasa Zitto atafarakana na nani wakati ACT-Wazalendo ni Zitto?

Siku Zitto akitoweka ACT-Wazalendo hata chama kitatoweka Tanzania Bara! Ninajua Maalim Seif na kundi lake wamejishikiza tu ndani ya ACT-Wazalendo lakini sio wanachama wa itikadi bali wanachama wa madaraka Zanzibar!
 
Mkuu MsemajiUkweli , ni wazi kuwa umeiweka habari kishabiki na hujaielewa. Unajaribu kuitumia habari iliyopita kujenga propaganda zako nyepesi na kuchanganya na mchakato wa uchaguzi ndani ya CHADEMA. Kwa hilo hujafanikiwa. Msigwa alikuwa anazungumzia Kikao kilichokwishafanyika huko nyuma. Na hata huo msamaha ulishatolewa. Ona soni na propaganda zako nyepesi dhidi ya vyama vya watu!
....afadhali wewe nimekuelewa;

huyu mleta mada siku zote anafahamika msimamo wake dhidi ya upinzani hasa CDM, so simshangai sana, kidogo namshangaa siku hizi kapunguza kuleta thread za kumsifia 'boss' wake!
 
Kuna siku watamtaja aliyemmiminia risasi Tundu Lisu kutoka hapo Ufipa....... Ndipo taifa zima la Tanzania litapatwa na mshangao!!!
Yes, watamtaja aliyeondoa walinzi kwenye makazi ya TAML; na aliyetoa cctv cameras watamtaja!
 
Sasa wewe Msigwa nyumbani kwa Mbowe ulikwenda na Biblia ya nini kwani Kubenea alimtumia majini au wale pepo wachafu wanaowafugaga?!
Wacheni uchonganishi hii ishu ni ya siku nyingi na hili jambo lilishamalizwa katika ngazi ya chama ila wewe msema uongo umeliketa kimkakati kwa malengo unayoyajua wewe na mabosi wako hapo Lumumba.
 
Hawezi kukuelewa wametoa ubongo wote
Kama hivi
1572191514899.jpeg
 
Katika Mahojiano na vyombo vya habari kupitia Mtandao wa Darmpya, Mbunge Peter Msigwa amefunguka na kuwatuhumu wabunge wenzake wa CHADEMA, Antony Komu wa Jimbo la Moshi Vijijini na Saed Kubenea wa Jimbo la Ubungo.

Msigwa amesema, "Hakuna shaka kuwa watu hawa Kubenea na Komu wamekuwa wenzetu kimwili tu, lakini kiroho wapo kwingine. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba hawa wabunge wawili, mara ya kwanza sauti zao zilinaswa wakipanga kumuua na kumpoteza Mhe mbowe na Meya Boniface wa Ubungo"

"Ni mimi niliyekwenda nyumbani kwa mwenyekiti Mbowe usiku usiku nikiwa na biblia yangu ikiwa ni siku moja kabla ya kamati Kuu ya CHADEMA kuketi, lengo langu likiwa ni kumtaka mwenyekiti wetu, Mhe. Mbowe arudishe upanga wake kwenye ala, atoe msamaha kwa wabunge hao"

"Pamoja na wakati mgumu tulionao katika kukabiliana uonevu na ukandamizaji unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, wenzetu hawa wamekuwa "busy" kutushambulia sisi wenzao tulio mstari wa mbele dhidi ya CCM na vyombo vyake vya dola"

"Tena hili limenifanya nitafakari na kukumbuka kwanini wabunge hawa wawili hawakuwahi kufika hata Segerea wakati Mwenyekiti Mbowe alipofungwa miezi karibuni minne. Hawakuwahi pia kufika hata Kisutu kujua mwenendo wa kesi yetu, kuonesha upendo, umoja na mshikamano’’

Mbunge Msigwa anamaliza kwa kusema, "Licha ya mbunge kama Kubenea kuishi Dar es salaam, hajawahi hata mara moja kukanyaga Kisutu kwenye kesi ya viongozi wenzie wa CHADEMA. Bila shaka amekuwa akituombea dua mbaya ili wenzie tufungwe ndipo afurahi"

NOTA BENE: Historia inaonyesha kila ukikaribia Uchaguzi Mkuu wa ndani ya CHADEMA lazima kuna viongozi wa juu hupata misukosuko na kufukuzwa ndani ya CHADEMA. Kikombe cha misukosuko kwa sasa watakinywa kina Kubenea na Komu!

Kubenea alifanya juu chini ili Zitto Kabwe afukuzwe ndani ya CHADEMA wakati wa Uchaguzi ndani ya CHADEMA 2014, kwa sasa naye ni zamu yake kufukuzwa ndani ya CHADEMA.

Karma at its finest!

Tusishangae kumuona Kubenea kesho anaomba kuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo, chama ambacho Kiongozi wake Mkuu alimfanyia fitna ili afukuzwe CHADEMA!
Ni kwanin haya yanafanyika wakati huu kuelekea uchaguxi wa kitaifa?
 
Chadema km hampendani wenyewe itakuaje
Chama ni mkusanyiko wa watu mbali mbali na usitegemee wapendane wakati kilichowaunganisha ni madaraka na vyeo.

Mapambano haya ndani ya CHADEMA chimbuko lake ni vyeo na madaraka
 
Kuna siku watamtaja aliyemmiminia risasi Tundu Lisu kutoka hapo Ufipa....... Ndipo taifa zima la Tanzania litapatwa na mshangao!!!

Vipi ile Interejinsia yenu mpaka leo haijawabaini wale waliotenda hiyo Jinai.
Wakati mwingine Mbatizaji unajitoa ufahamu sana,

Ndani ya viunga vya makazi ya Wabunge ,Mchana kweupe Mwakilishi wa Wananchi anashambuliwa, alafu unaleta Porojo kwenye mambo ya msingi.
 
Chadema km hampendani wenyewe itakuaje
CCM ndiyo hampendani hadi mawaziri waandamizi wa awamu ya tatu walitaka kumtoa roho JPM, mna roho mbaya sana sasa hii midege na reli mpya kama mngefanikiwa tungezipata wapi. Hata Rais wa awamu ya nne aliwahi kulisema kuwa imefikia wana CCM hawaaminiani tena kiasi mtu hawezi kutoka mezani akaacha kinywaji chake.
 
Back
Top Bottom