Antony Mtaka aambiwe kwamba sera ya elimu ni ya kitaifa na siyo mkoa kwa mkoa

Sera haiko ivyo mkuu,sera ni ya kitaifa sio juhudi za mkuu wa mkoa,RC anapaswa afanye kazi kwa kufuata sera za taifa, hakuna sera za kielimu kimkoa maana ikiwa ivyo basi kila mkoa uwe mamlaka kamili inayojitegemea aka serikali za majimbo
Kuna mijitu akili imedumaa. Makonda alipowapelekesha mitaani wakalilia rais yuko wapi. Sasa tena wanataka mkuu wa mkoa aachwe na mambo yake mkoani. Fallacy!
 
Vicious! Unajua TAMISEMI iko chini ya ofisi ya rais? Unafahamu rais ndo aliyemteua waziri wa elimu? Unafahamu rais ndo aliyemteua waziri mkuu? unafahamu mkuu wa mkoa yuko chini ya ofisi ya waziri mkuu? Jibu lako ni lipi????
 

Wewe ndiye hufahamu kitu...

Sera ya elimu ni moja tu nchi yote. Hakuna kipande cha sera ya elimu kwa ajili ya RC Mtaka na mkoa wa Dodoma...!!!

Kutoka kwenye sera ya elimu tunapata KANUNI na MIONGOZO mbalimbali ya kielimu ya namna ya kuitekeleza sera hiyo...

Miongozo hii hutolewa na nani?

Hutolewa na wizara yenye dhamana ya elimu Tanzania chini ya waziri husika. Kwa sasa wizara hii ya elimu iko chini Waziri Bi. Joyce Ndalichako na kamwe siyo RC Anthony Mtaka...!!

TAMISEMI (ukiwemo mkoa wa Dodoma chini ya RC Mtaka) kamwe hazijihusishi na utoaji wa miongozo na sheria zao wenyewe. Wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa ni LAZIMA na SHARTI watekeleze miongozo itolewayo na serikali kuu kupitia wizara za kisekta....

Ni upumbavu na ujinga wa kukosa ufahamu kutumia ubovu wa shule za serikali za walala hoi kutaka Ku - justify uvunjaji wa sheria, miongozo na kanuni za usimamizi wa elimu unaofanywa na RC huyu...

Anachokifanya RC Mtaka ni vurugu and pure insubordination dhidi ya mamlaka iliyo juu yake and he deserves to be punished...

Ni ujinga tu na upumbavu wa wananchi wa kutoelewa kama wewe ndiyo maana hawaoni tatizo la RC huyu. Hii ni Magufuli mentality ya kufanya mambo nje ya utaratibu...

Serikali za mitaa chini ya TAMISEMI i.e halmashauri, miji, manispaa na majiji ni wakala (agencies) kwa ajili ya kutekeleza maelekezo ya kisera za kisekta toka serikali kuu...

Jukumu kubwa na la kipekee la serikali za mitaa ambalo wanaweza kufanya ni kutunga sheria ndogo ndogo (bylaws) ili kuwezesha utekelezaji wa sera za kitaifa za kisekta mfano elimu, afya, ulinzi na usalama nk na kamwe siyo kwenda nje ya mstari...

This is undeniable fact. Ukubali ukatae RC Mtaka, amevuka mstari wa uwajibikaji kwa alichokisema ili kumshambulia Waziri wa elimu Bi Joyce Ndalichako kijinga bila sababu...
 

NAKUBALIANA NA WEWE MKUU KWA ASILIMIA MIA, NASHUKURU UMEKUBALI MARC NA DC WAPO TAMISEMI.

TUJE KWENYE MUONGOZO AMBAO HAPA SIYO SERA BALI NI MTAALA. MTAALA UMETOA MINIMUM TIME YA KUSOMA, MASAA 6 . MTAALA HUO HUO UMERUHUSU KUWE NA "EXTRA CURRICULAR ACTIVITIES" IKIWEMO MASOMO KAMA ZIADA KWA AKILI YA KUJIJENGEA UWEZO.

HAPA NDIPO KINA MTAKA WANAPOTOKEA MKUU.
 
Muacheni MTAKA awanyanyue wagogo kielimu .

Lakini asinyanyue wagogo kama akina NDUNGwaii
 
Sera zenu za elimu ni mbovu Sana mkuu na zinzalisha vilaza weñgi wenye ufaulu tu mkubwa refer BRN since iko introduced tunapata adi watot wasiojua kusoma na kuandika vizur lakini wapo sekondari hiyo yote ni kuonesha tu vijana wanafaulu Sana kumbe nyuma ya pazia ni upuuzi tu unafanyika Kwan n uongo ilo boss
 
Nchi yetu tuna tatizo na tatizo lenyewe sio dogo ni la kimfumo.Mtu akiwa mkweli anaanza kubanwa kwa mfumo lakini Ukweli unabaki uuwazi. Kwa mfano Kuna watu wanategemea mawaziri au wabunge walete hoja za maana kuhusu kuboresha elimu yetu hasa shule za sekondari za kata na msingi.Hili haliwezekani kwa sababu viongozi wakubwa wote HAWANA IMANI na elimu inayotolewa katika shule za kata lakini pia viongozi wengi wanamiliki shule za private. Mtaka alisema Ukweli anapigwa mawe kimfumo.
 
Katiba mpya itasimamia aina ya Elimu itolewayo kitaifa iwe na maslahi bora KWA watanzania wote bila kubaguana kama ilivyo Sasa!

Pia itatuepusha na KUTUMIA utashi wa mtu kuamua Elimu yetu iweje kama ilivyo Sasa hivi!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA!!
 
Yap, kwanza makambi ya kitaaluma ni mizigo tu kwa wazazi, wazazi wanatozwa pesa kubwa lkn ufanisi wake ni minor, wakuu wanapiga hela sana kupitia hayo makambi.
wewe ni muongo nanafiki na unaongea hata usiuo yajua na hata hujui hizo kambi zinaendeshwaje.
 

Katiba ya nchi gani inasimamia elimu?
 
Unadhani hao wa st wanasoma je? Yaani wanakuwa overdosed kupita maelezo wapo busy mda wote. Ila hawa kayumba munataka wawe free wapumzishe ubongo wakati darasani wanakaa 100 nakuendelea.
Ulizeni huko private wanasoma je? Mkuu wa mkoa akaze.
 
Hao mawaziri wanamatatizo utazuiaje mtoto kusoma? Wakati watoto wao wanasoma intenational school
 
We jamaa ni mjinga kinoma. Katiba haisimamii elimu. Halafu pia kwa mujibu wa sheria ile rasimu ya Warioba sio katiba. Inabidi ijadiliwe na bunge la mabadiliko ya katiba kisha wapitishe katiba pendekezwa ambayo wananchi wataipigia kura. Kusema rasimu ya Warioba ndo iwe katiba ni kuvunja sheria na kutomaliza sehemu muhimu ya mchakato
 
Mwacheni Mtaka apige kazi.
 
Mkuu robinson crusoe , kwanza naheshimu mawazo yako ila sikubaliani na wewe. Kwenye hili la makambi, mimi nasimama na RC Mtaka. Kiongozi mzuri hapimwi kwa jinsi anavyo jua kuongea, bali hupimwa kwa matokeo chanya ya utendaji wake. Kwa wanao ijua Simiyu kabla ya RC Mtaka na Simiyu ya Mtaka ndio watanielewa.
Shuhudia hapa P
 
Ukafie mbele.
Ulimdis huyu mwamba mwaka 2021.
Lakini mawazo yake yanatumika nchi nzima makambi yamejaa
 

Nani amekuambia Tanzania ina sera ya elimu? Tungekuwa na sera ya elimu tungekuwa na mabadiliko makubwa makubwa kila tunapopata waziri mpya wa elimu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…