ANUNNAKI: Nadharia za Mungu, miungu, fumbo la sciencenscience na Teknolojia kubwa katika Dunia ya kale, kuanguka Kwa civilization na kuinuka Tena

Ni kama eti kwa sababu kwenye intaneti kuna porno basi tuzuie intaneti nchi nzima haiwezi kuwa sahihi. Bali tuone namna ya kuyaboresha maisha yetu kwa kutumia intaneti vizuri.

Waliopewa elimu ya uwepo wa Mungu hapo mwanzo kama waliamua kuibadili na kuanza kuwakandamiza wenzao kuwafanya watumwa waliitumia vibaya. Sasa tumeshafahamu hatutamkataa Mungu bali tutaukataa mfumo wa kiukandamizaji ambao hauko logical na idea ya Mungu mmoja anyway maana: Ikiwa sote ni wa Mungu mmoja, basi wote tu sawa, tu ndugu katika ufalme wa mbinguni hapana mmoja wa kumkandamiza mwenzie. Idea ya dini na Mungu ni nzuri ikifuatwa kwa ukweli na ukamilifu na uadilifu - Kama tu Yesu mwenyewe alivyoibainisha. Nasisitiza sio kama sheikh/mchungaji/mtume fulani alivyosema ila ni kama Yesu alivyobainisha.
 
Haijaandikwa popote juu ya Asili ya hao hayawani Bali Annunak waliwakuta tu wanasurvive hapa hapa Duniani!
1.Kama ANNUNAKI walikuja duniani na kuikuta duniani ikiwa na vimbe mbalimbali je huoni kama hawa ni viumbe inferior?
2.Inaonekana kama hawa ANNUNAKI wana uwezo wa kuumba je uko walikotoka walishindwa kiuunda dhahabu.
 
1.Kama ANNUNAKI walikuja duniani na kuikuta duniani ikiwa na vimbe mbalimbali je huoni kama hawa ni viumbe inferior?
2.Inaonekana kama hawa ANNUNAKI wana uwezo wa kuumba je uko walikotoka walishindwa kiuunda dhahabu.
Watu wengi wameuliza Hilo swali na nilishajibu humu,
Hivi Kwa Akili Yako ya kawaida unaona inawezekana kuunda dhahabu maabara?
Hivi kwanza unajua dhahabu inaundwa na Nini ampaka ikatokea?
Ni Sawa na mtu Leo tunazalisha watoto maabara aje na swali kwanini hatuzalishi mawe!

Dhahabu ni natural resource sio artificial
Na ndio maana ilikua rahisi Annunaki kuumba mtu kuliko dhahabu hata Leo tukitumia technology za human manipulation na cloning tutaunda Watu wenye ufanano na sisi Kwa Kila kitu Hilo linawezekana na Lina ushahidi wa kiidhibati,
Ila dhahabu tutadanganyana na ndio maana hata wao katika Accient civilization waliifuata duniani!
 
Aisee we jamaa bwana unapenda blabla kwenye mambo muhimu,
1.Yaani kwa akili yako unaona mtu ni rahisi sana kumuumba kwa sababu tayari process ilishakamilka na mtu kawekewa mbegu ndani yake!!!?

2.Kwako wewe kwa kuwa research za cloning zinaweza kufanyika unaona kama vile mtu hana thamani?

3.Binadamu wa sasa anapotaka kuchimba dhahabu ameweza kufanya ugunduzi na kujitengenezea Machine very complicated kwa ajili ya kuchimba dhahabu,Mtu aliyedhaifu ana nguvu gani ya kuchimba dhahabu matani na matani na kupelekwa uko unakokuita wewe Nibiru?Na lazima ufikirie ya kwamba mbingu ni kubwa kuripea hiyo mbingu yao kungehitaji dhdhabu nyingi, mtu dhaifu hawezi kufanya hiyo kazi.

Angalia mtu asiye na mitambo anachimbaje dhahabu hivi leo?
 
Uwe unasoma kuelewa Acha kukurupuka nibiru kinaitwa Mbinguni sababu ni single planet sio Galaxy kama Akili zako zinavyokuendesha,kitu kingine Kupitia cloning project hata binadamu wa Leo wanafanya viumbe mbali mbali ambao ni advanced mfano kuku wa Kisasa,ng'ombe,Nguruwe na mimea mbali mbali ya Kisasa mfano mbegu za GMO

Annunak kutokana kua high advanced Katika science and technology wakafanya human manipulation wakitumia mfano wa DNA Zao ndio maana tablets za Sumeria zinasema ENKI, ENLIL INNANA na wale ANNUNAKI Saba walioshuka Duniani walisema na tumuumbe mtu Kwa mfano wetu sawa na kitabu Cha Genesis katika biblia kinasema hivyo hivyo

Tena Kwa msisitizo kikakazia Kwa mfano wa Mungu binadamu mke na mume waliumbwa Kwa Akili Yako ya kawaida unadhani huyo Mungu aliyefanana na binadamu aliyemuumba ndie nani kama sie ENKI Ambaye katika michoro ya Wasumeria anaonekana ni mfano wa giant na wings mbili?
 
Nakuelewa unachosema, Mimi mwenyewe ni mkristo safi kitambo tu.
Shida inaanza nikianza kujiuliza kwanini kusingekuwa na dini Moja?, Mungu aliwafikiriaje watu wa mataifa mengine alipoichagua Israel liwe taifa lake teule?, Mungu alidhani kuwafanya wazungu wamjue yeye alafu, halafu wao wakaeneze habari zake duniani kote, alikuwa anadhani watu watakubali kirahisi?. Kwanini Mungu kwenye midahalo ya dini hatoi hoja, haoni kama binadamu tunaendelea kuchanganyana?.

Nina maswali mengi sana kichwani Yanayonifanya nione kama Mungu kwamaana ya supreme Being, siyo huyu tunaefundishwa kwenye hizi dini zetu, naona kama Mungu wa kweli( supreme being) Hana mpango na hizi dini zetu
 
Kumbuka supreme power haiwezi kua Mungu kamwe sababu katika difinition na asili ya Neno MUNGU
ni
'Master of high chamber'
Ambapo Wasumeria walimaanisha mtawala wa
12th Planet Nibiru (Heaven) ambako Annunaki walitoka
Hivyo wote wanaoamini Nadharia ya dini wanawaabudu deities kama kina
Allah,Elohim, Jehovah,NK Ambao kimsingi ni Moja ya miungu ya jamii Fulani pale middle east!
 
Naelewa, ila na assume ndo supreme power kama tunavyohubiriwa
 
Naelewa, ila na assume ndo supreme power kama tunavyohubiriwa
Hawa wa Nadharia za Mungu wa Israelites yaani Elohim/Jehova Mungu wao Hana tofauti na deities Wengine kama kina Budha,Brahma NK Ambao kimsingi ni wanaabudiwa na jamii au kikundi Cha Watu wachache,mfano ndio Huyo Mungu Elohim/YWH ambae Aliabudiwa na Abraham family na vibaraka wao Ambao Leo wamefanya modernization!
 
Kuna mambo ya utaifa, na utamaduni yamekuwa yakichanganya sana na dini ya kweli.

Lakini kwa kuwa ni 'mkristu' basi una bahati njema kazi kwako ni ndogo. Ukitaka kuielewa namna ya kuenenda katika dini na kumjua Mungu wa kweli basi mfuate Yesu na msikilize yeye anasemaje. Kuwa MKRISTU kweli kweli.
 
Angalia labda unataka kuiruka fact moja muhimu;

Ni kwamba kila watu waliamini katika Mungu kwa namna mbalimbali lakini kila mara wamekuwa wakija walimu kutufundisha namna nzuri ya kuabudu. Haya mabadiliko yalianzia kutoka kila ukoo kuwa na miungu yao [ghost/mizimu] hadi kwenda
miungu wengi wa jamii fulani [polytheism] hadi mungu mmoja[monotheism]. Mungu mmoja ndio top truth
 
Lete uthibitisho wa Huyo Mungu mmoja kua Ndie top truth,nataka pia vigezo vilivyotumika kumpa top truth Kwa Ushahidi wa kiidhibati!
 
Huo wa kiithibati sijui [in fact siuelewi]

Mimi uthibitisho wangu ni wa ki analojia. Nikijaribu kupima mantiki nakuta unamake sense. Huo ushahidi upo hapa Mwanabaiolojia na uhalali wa wazo la Mungu
Refer maana na difinition niliyoitoa kuhusu neno 'MUNGU' na asili yake likisimama kama cheo Cha mtawala wa Nephilim 12th Planet Nibiru katika accient tablets aliitwa
(Master of high chamber)

Je Kwa tafsiri Yako unavyodai Huyo Ndie Mungu Muumbaji wa Ulimwengu huoni unaleta mkanyiko katika tafsiri ukimtaja deity ambaye anafungwa na kanuni za Ulimwengu?
 
Huyo wa tafsiri yako ndio anafugwa🤣.... sorry anafungwa na hizo kanuni.

Tafsiri yangu haina mkanganyiko, mkanganyiko ni pale tu wewe unapolazimisha mimi nikitaja Mungu niwe natumia tafsiri yako.

Sikia Dumas the terrible ni kwambaa hiyo tafsiri yako ilitumika na watu wengi tu kila watu na jamii zao walikuwa na mungu wao. Lakini baadaye ufunuo na elimu inavyokua ndio unakuta watu/manabii wanamzungumzia Mungu wa vyote na kusisitiza kuwa hana kisawe chake. Ndio kina Muhamad SAW na YESU. Watu wa zamani wao walikuwa confortable na kuishia tu mungu wa ukoo fulani, kabila/race fulani lakini huo haukuwa ukweli wote
 
Yaani unachopinga kwangu Haina maana,narudia kukupa msisitizo ukitaja Mungu Kwa Watu Ambao tunajua asili na mwanzo wa Hiyo Nadharia Halafu ukampa sifa za uumbaji wa huu Ulimwengu nitakubishia daima maana Kwa tafsiri rasmi ambayo naijua Mimi hakuna Huyo Mungu mnaemdai kaumba Ulimwengu huu mkubwa na huko yeye akiwa Ndani ya huo huo Ulimwengu,huoni contradiction hapa?
Mungu anafungwa na kanuni za Ulimwengu na ndio maana anasifa za viumbe wa kawaida kama tulivyo sisi mfano
Mungu Elohim/YWH/Jehovah
Ana character ya kibinadamu Kuna mbaya kama Hasira,Wivu,chuki,ubaguzi,
Mabavu,ubabe,visasi,
Pia anazo nzuri kama
Upendo,rehema,Upole,maarifa,
ujuzi,Huruma NK
Vile vile ana character ya Ufalme akiwa kama top of command
Akiongoza kundi la viumbe mbali mbali Katika falme na milki yake mfano
Malaika, maserafi, Mashetani,Majini NK

Sasa basi kutokana na character hizo napinga huyo sio Supernatural power Bali ni deity tu ambaye anaongoza milki mojawapo katika Galaxies

Nataka nisemaje hizo sifa zote Israelites walicopy kwa Maandiko ya Sumeria ambayo Babu Yao Abraham alitokea Kwenye jamii hizo ambazo kimsingi ziliongozwa na Annunaki/Watchers/Angels Ambao kimsingi na Katika Ushahidi wa kihistoria wakitokea
Nephilim 12th Planet Nibiru ambayo Watu wa kale walikuita Heaven kwa kwa lugha ya kingereza au Mbinguni Kwa kiswahili,
Sasa kutokana na Nadharia hizo dini na kuabudu viumbe kutoka huko Mbinguni ndio ulipoanzia huko Mesopotamia Karne hizo
BCE!

Understand?
 
Duh hapa kuna kazi kwa kweli. Nimesoma huko juu ulivyopinga hadi mishipa ya vidole ikakakamaa. Asee kwanza pole bro.

Sasa tufanye kitu kimoja. Nimegundua kuwa wewe upo logical katika maelezo yako. Na nimegundua pia kuwa premise yako ipo kwenye hilo dubwana linaitwa 'Nephilim 12th Planet Nibiru'

Sasa tufanye zoezi la akili, je unaweza kuishikilia hiyo mantiki yako hata kama hiyo Nephilim 12th planet Nibiru ikidondoka. Namaanisha leo tukithibitisha kwamba hakujawahi kuwapo Nephilim 12th planet Nibiru. Je utaweza kuaccount kwa uwepo wa kila kitu leo?
 
Dumas the terrible ukiachana na hao anunaki walichokuambia kwamba ukitaka kumuona Mungu utamkuta Nephilim 12th planet Nibiru. Haina tofauti na walioamini mungu anakaa katika mlima fulani au mlima mwingine sikia hii hapa:

Yn 4:23-24​

Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.​

 
Hizo zote ni Nadharia tu ambazo Israelites waliamini na Hata rejea zako ukitumia bible na maandiko mengine kumthibitisha Huyo Mungu unaemdai itakua ni uwendawazimu tu,
Nje ya Abrahamic religion Ambazo walizikopy huko Mesopotamia kuzungumzia Hizo habari na Nadharia ya MUNGU/MIUNGU

Usingezijua ila Kwa sababu utamaduni wao ulikua strong umejikuta Umemezwa Ndani yake na upo Kwenye dome nje ya hapo huna fact kumprove Huyo Mungu bila kurejea maandiko Yao,
Think twice!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…