Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Apple, Google, Tesla na Microsoft ni baadhi ya makampuni yaliyotajwa katika kesi ya madai ya fidia ya vifo na majeraha ya wachimbaji watoto wa migodi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,DRC.
Kesi hii ilifunguliwa na mawakili wa kimataifa wa haki za binadamu kwa niaba ya familia 14 DRC.
Wanayashutumu makampuni hayo kwa kujua kwamba madini aina ya kobalti yanayotumiwa katika bidhaa zao, yanatokana na ukiukwaji wa sheria kwa kuwaruhusu watoto wadogo kuchimba madini hayo.
DRC inazalisha asilimia 60 ya Kobalti inayosambazwa duniani kote.
Madini hayo yanatumiwa kutengenezea betri aina ya lithium-ion zinazotumika kuwasha magari ya umeme, komputa mpakato na simu janja.
Lakini, hatua za uchimbaji zimekuwa zikizua wasiwasi kuhusu uchimbaji haramu, ukiukwaji wa haki za binadamu na ufisadi.
Kesi hii iliyofunguliwa nchini Marekani inadai kuwa kampuni hizo za teknolojia walikuwa na ''uelewa wa kutosha'' kuwa kobalti inayotumika katika bidhaa zao inaweza kuhusishwa na kufanyishwa kazi kwa watoto kinyume cha sheria.
Wanasema makampuni hayo yameshindwa kudhibiti mifumo ya usambazaji wa bidhaa zao na badala yake kufaidika kutoka kwa utumikishwaji wa watoto hao.
Makampuni mengine yaliyotajwa katika kesi hiyo ni pamoja na kampuni ya kutengeneza kompyuta mpakato Dell na kampuni mbili za uchimba madini za Zheijang Huayou Cobalt na Glencore, ambao wanamiliki migodi ambayo kwa mujibu wa familia za waathirika wanasema ndipo watoto hao walipokuwa wanafanyia kazi.
Glencore iliiambia gazeti la Telegraph nchini Uingereza kuwa ''hainunui, kusindika wala kufanya biashara yoyote ya madini yaliyochimbwa na wachimbaji wadogo,'' na haiungi mkono utumikishwaji wowote wa watoto, uwe wa kulazimishwa au hata ule wa kujitolea.''
BBC
Kesi hii ilifunguliwa na mawakili wa kimataifa wa haki za binadamu kwa niaba ya familia 14 DRC.
Wanayashutumu makampuni hayo kwa kujua kwamba madini aina ya kobalti yanayotumiwa katika bidhaa zao, yanatokana na ukiukwaji wa sheria kwa kuwaruhusu watoto wadogo kuchimba madini hayo.
DRC inazalisha asilimia 60 ya Kobalti inayosambazwa duniani kote.
Madini hayo yanatumiwa kutengenezea betri aina ya lithium-ion zinazotumika kuwasha magari ya umeme, komputa mpakato na simu janja.
Lakini, hatua za uchimbaji zimekuwa zikizua wasiwasi kuhusu uchimbaji haramu, ukiukwaji wa haki za binadamu na ufisadi.
Kesi hii iliyofunguliwa nchini Marekani inadai kuwa kampuni hizo za teknolojia walikuwa na ''uelewa wa kutosha'' kuwa kobalti inayotumika katika bidhaa zao inaweza kuhusishwa na kufanyishwa kazi kwa watoto kinyume cha sheria.
Wanasema makampuni hayo yameshindwa kudhibiti mifumo ya usambazaji wa bidhaa zao na badala yake kufaidika kutoka kwa utumikishwaji wa watoto hao.
Makampuni mengine yaliyotajwa katika kesi hiyo ni pamoja na kampuni ya kutengeneza kompyuta mpakato Dell na kampuni mbili za uchimba madini za Zheijang Huayou Cobalt na Glencore, ambao wanamiliki migodi ambayo kwa mujibu wa familia za waathirika wanasema ndipo watoto hao walipokuwa wanafanyia kazi.
Glencore iliiambia gazeti la Telegraph nchini Uingereza kuwa ''hainunui, kusindika wala kufanya biashara yoyote ya madini yaliyochimbwa na wachimbaji wadogo,'' na haiungi mkono utumikishwaji wowote wa watoto, uwe wa kulazimishwa au hata ule wa kujitolea.''
BBC