April '09 Bomb Blasts in Dar (Mbagala) and responses

Nasikia majambazi yameisha ingilia mbagla na kuaanza kuwaibia watu. Si mambo ya aibu hayo. Umasikini huuu jamani kazi kweli kweli.
 
Huge explosions rocked an ammunition dump at an army camp in Tanzania's commercial capital Wednesday, killing three people and injuring more than 150, officials said.

Haya maswala ya makazi kuchanganyika na kambi za jeshi, zifikie maala uongozi wa nchi kuangalia upya. Miaka 30-40 nyuma idadi ya wakazi wa Mbagala haikuwa kubwa kiasi cha kuwa karibu sana na kambi hizi za jeshi.

Hali imekuwa tofauti na sasa... Mji unapanuka watu wanafikia kuishi just few yard kutoka kwenye kambi za jeshi.

Hii yote ni kutokana na mipango miji kuwa mibovu. Wataalam wetu huwa wanashindwa kufanya makadirio ya ongezeko la idadi ya watu kwenye miji mikubwa kama DSM. Ni bora sasa ilo linalo itwa ammunition dump aidha liamishwe na kubakia just infantry with out so called ammunition dump au
wakaazi wa eneo lililo karibu na makazi ya jeshi waamishwe na kulipwa fidia ya usumbufu na mali zao.

Hizi mbinu za nchi za kijamaa jeshi kukaa karibu na raiya ili kuweza kulitumia jeshi pindi tu watu watakapotaka kufanya mapinduzi au maasi, inaonekana sasa imepitwa na wakati.

Hatuhitaji tena tena kambi za jeshi kuwa karibu na raiya, ukizingatia kuwa kambi zenyewe ndizo hizo hizo zenye kuifadhi expired ammunition.

Tena kwenye Ghala lililo zungushiwa mabati kama sikosei kama si under ground. Tz ni kubwa sana katika nchi za East Afrika, kuna maeneo Tz tangia kuumbwa kwa hii dunia binadamu hajawai kukanyaga huko. Kwanini serikali/Jeshi lisihamue kupeleka huko mbali kabisa na kwenda kuangamiza hayo mabomu na ammunition zinazo semekana zimepitwa na muda wake...(!?) Hapa mi nashindwa kupata picha halisi... Hivi ni kweli this so called Ammo zinafikia ku'expire ni zile ambazo zipo tangia enzi ya kina Tip tip na Mkwawa au ni zile zilizo tumika kwenye vita vya maji maji?

Ninavyo fahamu mimi Ghala la siraha linakuwa kept clean, cool and dry na kufia mpaka those Ammo kuwa expire may take many, many years to reach a point of unsuitability, hapa tunazungumzia kuanzia miaka 50-70 or longer.
Sasa hizi ambazo zinafikia mpaka kuripuka tu, mbona haiingii akilini? Au ndio zile ambazo wakati wa production ndizo zilizo kuwa rejected, kisha tukazi nunua kwa bei ya kutupa...!? Na hata hii sidhani kama inakubalika.
Au ni zile ambazo tulizirithi toka mkoroni!? Nashindwa kuelewa...! I'm shocked.

This is serious matter tena ime'involve maisha ya raiya, bora yangewakumba hao hao wanajeshi tungesema ajali kazini. Lakini kuwakuta raiya wasio juwa hata mbinu za kujihokoa pindi maafa kama haya yakitokea ni jambo kubwa sana hili.

Tufikie wakati sasa tusema kuwa TUMECHOKA HATUTAKI TENA.
Kwani hii ni dhurma kubwa sana kukatiza uhai wa raiya na wakazi wasio na hati.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un... Tuna wapa pole sana wakazi wa mbagala kwa maafa yalio wakuta. Insha'Allah M'Mungu azipokee roho za marehemu na kuzipumzisha kwa Aman.

Ila sisi ambao bado tu HAI tusimame sasa kwani wahenga walisema Amkani si shwari tena. Ni lini itafikia kipindi tutasema BASI.
 
Last edited:
Angalia taarifa ya BBC BBC NEWS | Africa | Deadly blasts rock Tanzanian city. Inaonekanakile kinacholipuka ni ramia za mizinga pamoja na mabomu ya kutega. kama ni kweli inaonyesha ukosefu wa nidhamu upande wa jeshi na pia ukosefu wa usimamizi ndani ya vyombo vya usalama. Kila jeshi duniani latakiwa kusimamia silaha zake bila kuwa hatari kwa wananchi.

Kwa sasa maombi na sala zetu ni kwa wote wanaoathiriwa na balaa hii!
 
Duh cheki watu walivyochoka.....eti sijui hawa ni askari wa zimamoto..(picha kwa hisani ya Michuzi)

 
This type of unfortunate event has the effect of exposing our military capacity.
Unfortunately we have been undressed in the eyes of the world intelligence community, like a bunch of children who don't know how to handle explosives.

I know it's not very patriotic and all that jazz to say this, and I will probably catch some backlash for this, it needs to be said.

This is worse than Plaxico Burress, worse than scoring against your own team, worse than a marine drowning in Comoro because he couldn't swim, since the mutiny of January 1964, which really did not come from this army, we have arguably never faced a more shameful period in the Tanzanian defence fraternity.

This day will go down in history with a peculiar and unprecedented infamy due to the degree
of negligence and number of people effected which is toned down by the government as is
always the case.
 
This type of unfortunate event has the effect of exposing our military capacity.

Capacity? What capacity? Capacity ya kunyanyasa wananchi?

know it's not very patriotic and all that jazz to say this, and I will probably catch some backlash for this, it needs to be said.

I disagree. It is very patriotic to check your government/ country/powers that be and whatnot when they make stupid and costly blunders.
 
Naombea serikali isitoke na kusema tunatoa billion 100 kuhamisha mabomu yote kwenye kambi zilizoko karibu na makazi ya watu na kupeleka porini! 2010 around the corner..anything is possible.
 
Hofu kuu!! Mabomu yalipuka ghala la JWTZ yatikisa Jiji la Dar es Salaam.

Imeandikwa na Halima Mlacha



Vilio, nyumba kubomoka, watoto kupotea na vifo, ndiyo hali iliyotawala jana eneo la Mbagala Kizuiani, Temeke, Dar es Salaam baada ya milipuko kutokea katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Milipuko hiyo ilitokea mfululizo katika maghala ya kuhifadhi silaha katika kambi hiyo na kusababisha mtikisiko mkubwa katika maeneo ya jirani na katikati ya Jiji na kusababisha hamaniko kwa watu waliokuwa wakihaha kujiokoa.

Mabomu hayo ambayo yalianza kulipuka takribani saa 5.45, asubuhi yalisababisha wakazi wa Mbagala kukimbia makazi yao huku baadhi ya nyumba zikishika moto na kuteketea kutokana na mabomu kulipuka na kutua kwenye nyumba hizo.

Ingawa taarifa rasmi ya athari zilizotokana na tukio hilo ilikuwa haijatolewa jana, lakini za awali zilizothibitishwa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk. Aisha Mahita, zilisema maiti watatu na majeruhi zaidi ya 150 walifikishwa hospitalini hapo kwa matibabu. Taarifa zilizopatikana katika maeneo ya tukio, zilidai kuwapo mtoto aliyekufa akijaribu kuvuka Mto Kizinga, Mbagala wakati wa hekaheka za kujiokoa na watoto wengine wapatao 30 walikusanyika katika kituo kidogo cha Polisi Makangarawe kwa ajili ya hifadhi. S

erikali kupitia Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Emmanuel Nchimbi, ilitangaza kuwa Baraza la Uchunguzi limeundwa kuchunguza tukio hilo na akawataka wananchi wawe watulivu ili baraza hilo liweze kutoa taarifa juu ya tukio hilo, ambalo pia liliathiri shughuli za kazi katika maeneo mbalimbali. Wafanyakazi wengi walilazimika kukimbia ofisi zao kwa hofu ya kuathiriwa na milipuko hiyo huku waliobaki wakijawa hofu kubwa na kukaa kwa tahadhari. Hali hiyo ilichangiwa na mtikisiko katika majengo.

Gazeti hili lilishuhudia wakazi wa Mbagala wakiwa wametanda pembeni mwa barabara ya Kilwa wakiwa na hofu iliyosababishwa na kishindo. Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Nchini Paul Chagonja, alisema chanzo cha kulipuka kwa mabomu hayo ni tatizo la kiufundi lililosababisha kuzuka kwa moto ghafla katika moja ya maghala hayo.

Β“Bado hatujui chanzo cha moto ni nini kama ni hitilafu ya umeme au kitu gani, ila moto huo ndio ulisambaa na kusababisha mlipuko wa mabomu,Β“ alisema Chagonja. Alisema jambo la msingi wanalofanya ni kuhakikisha usalama wa wananchi ambao hawakutakiwa kuwa katika eneo hilo lililo karibu na makazi ya watu, kutokana na hatari iliyopo kwani bado mabomu yalikuwa yakiendelea kulipuka.

Alisema vikosi mbalimbali vya Jeshi na Polisi viliwasili kuhakikisha vinaokoa maisha ya watu na kuwatoa wengine katika eneo hilo na kikosi kingine kwa ajili ya kuangalia namna ya kuzuia moto huo na kutegua baadhi ya mabomu yaliyokuwa kwenye maghala ambayo hayakuwa yamefikiwa na moto huo. Mmoja wa mafundi wa minara ya simu za mkononi wa TIGO aliyekuwa eneo la kambi hiyo, James Msowoya, aliliambia gazeti hili kuwa alishuhudia bomu la kwanza likilipuka, lakini kwa kuwa mlipuko ulikuwa mdogo walidhani ni wa transfoma.

Β“Bomu la pili lilikuwa hatari kwani nilijikuta niko chini ghafla na baada ya mtikisiko niliinuka nikakimbia huku nikifuatiwa na baadhi ya askari wa Jeshi, kwa kweli tulikuwa tunakimbia hatujui hasa ni nini kimetokea,Β“ alisema. Alisema alipofika barabarani alishuhudia umati mkubwa ukikimbia hovyo barabarani huku wengine wakianguka na kupoteza fahamu na wengine bila kujali, wakiwakanyaga wenzao walioanguka na kuendelea kukimbia na katika tafrani hiyo alipotezana na rafiki aliyekuwa naye.

Wakati 'HabariLeo' ikiwa eneo la tukio ilishuhudia pia magari ya Polisi na Zimamoto STK 1971 na PT 1524 yakiranda eneo hilo huku yakitangaza wananchi waondoke. Β“Tahadhari wananchi tunaomba muondoke eneo hili si salama kaeni umbali wa meta 100.Β“ Hali ilikuwa ngumu kwa askari hao ambao pamoja na kujitahidi kuwadhibiti wananchi wasikaribie eneo hilo ambalo lilizungushiwa utepe wa njano, walijikuta wakiwa katika wakati mgumu zaidi baada ya baadhi ya wananchi kubainika kuiba baadhi ya silaha na mabomu.

Gazeti hili lilishuhudia vijana wawili waliokamatwa na mabomu na silaha za kutungulia ndege wakiadhibiwa kwa kuchapwa viboko na askari Jeshi. Kwa mujibu wa askari Mgambo, Abeid Mchopa aliyewakamata vijana wanne, walikutwa wakiwa katika bonde jirani na kambi hiyo wakiwa na silaha hizo. Eneo hilo ambalo lilijaa moshi pamoja na harufu kali ya moto, pia lilikuwa na mabaki kadhaa ya mabomu huku wananchi, polisi na askari Jeshi wakijitahidi kuwahi mabomu yaliyorukia kwenye nyumba za raia kabla hayajalipuka.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Manumba aliwaonya waandishi wa habari kutoendelea kuwa katika eneo hilo kutokana na uwezekano wa kulipuka kwa maghala mawili yenye silaha kali ambazo zinaweza kuteketeza eneo lote la Mbagala. Β“Jamani nawaombeni mkae mbali au muondoke kabisa hili eneo ni hatari sana kwenu, kuna silaha mbaya sana hazijalipuka tunahofia zikilipuka hatabaki mtu hapa,Β“ alionya.

Baadhi ya redio za jijini Dar es Salaam zilisikika zikitangaza kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha, amewataka watu warudi majumbani kutokana na hatari ya mabomu yaliyobakia hali ambayo ilizidisha hofu. Naye Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alikaririwa na redio akiwataka wananchi wasiende Mbagala kwa kuwa eneo hilo ni hatari. Akizungumza na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC Taifa), Kamanda huyo pia aliwataka wananchi walioko huko wazime simu za mkononi kwa kuwa zinavuta mabomu.

Kamanda Kova alisema, baadhi ya mabomu yaliangukia nyumba, hivyo vikosi vya zimamoto na Chama cha Msalaba Mwekundu waliitwa kwa ajili ya uokoaji. Awali kulikuwa na taarifa zilizodai kuwa nyumba kadhaa za wananchi zilikuwa zikiungua na moshi ulitanda eneo la Mbagala. Tukio hilo lilivuruga pia taratibu za usafiri baada ya magari kusimamisha safari za kwenda maeneo ya Temeke hususan yaliyo karibu na Mbagala huku wakazi wa maeneo husika, wakikwama kupata usafiri wa kuwapeleka maeneo salama.

Wakati huohuo, watu waliokuwa katika maeneo mbali na Mbagala, walikuwa wakifanya juhudi za kuwasiliana na ndugu zao kwa simu. Baadhi ya watu waliwasihi ndugu zao wafungashe mizigo watoke Mbagala kwa kuhofia mabomu hayo kuendelea kulipuka. .
 
Mpaka sasa sijasikia lolote kutoka kwa Amir Jeshi Mkuu ( Mh. Jakaya Mrisho Kikwete), sijasikia kutoka kwa mkuu wa Majeshi. Nimesikia kuna special team iliyoundwa na Jee imeundwa kuchunguza nini? Na ni muda gani italeta majibu? Jee majibu yatakwenda kwa raisi tuu kisha kama ilivyo ni mila na desturi yake kukaliaa report? Sijasikia kama kuna anybody kwenye uongozi amesha jiuzulu sababu ya hili.

Huu ni muda muafaka wa kuwajibishwa walio zembea, serikali inabidi ilipe fidia za losses zote zilizotokana na uzembe wao. Jakaya as a leader inabidi awe ameshaitishi prime time news conference kuelezea kwamba hali inaendelea vipi.
 

Mkuu, serikali hii inatia aibu sana katika inaction yake. Tumwache huyo Amiri Mkuu wa Jeshi, labda alikuwa anatalii nje, lakini hata basi Makamu rais angetembelea wahanga hospitali, au waziri wa Ulinzi (siyo naibu) au waziri mkuu angetoa pole. Jana Pinda alionekana TBC akiwa amekaa mpaka saa 2 usiku katika bunge tupu akisikiliza miswaada!!! Inatia aibu sana. Kwanza Pinda angetakiwa aombe ruhusa mchana arudi mara moja, si tumeambiwa ile idara ya maafa iko chini ya ofisi yake. Sasa wote wanakuja na kisingizio eti wanasubiri kamati ilete majibu. Kamati? Kamati ndo itawaeleza wakatoe pole au la?
I have only one sentence to define what happened to these guys : THEY JUST DON'T CARE!
 

Hi ni kweli jamani au ndo uongo wa viongozi unaendelea. Hii inaniboa, maana hawa viongozi wetu utakuta wanajifanya sana. Kumbe ni mbumbumbu tu! Has this been proven scientifically? Simu zinavuta mabomuπŸ˜•...hehehhee. Kichekesho hichi sasa.
 
Hi ni kweli jamani au ndo uongo wa viongozi unaendelea. Hii inaniboa, maana hawa viongozi wetu utakuta wanajifanya sana. Kumbe ni mbumbumbu tu! Has this been proven scientifically? Simu zinavuta mabomuπŸ˜•...hehehhee. Kichekesho hichi sasa.

Hehehe ndo Jesho letu hilo!!! Cell phone seeking bombs!!
 




Susuviri!

Usinitie majonzi huyu Amiri Jeshi si ni Kanali mstaafu wa JESHI au alipewa zawadi ya ukada kama Luteni Makamba? ( Nimekumbaka walikuwa intake moja kule Monduli pamoja na Jaka Mwambi sijui kama Mkuchika alikuwepo)
Si alitakiwa atembelee hapo kuonyesha ujeshi wake! What is important to him ni kwenda kuuza sura Arusha- Namanga kuzindua ujenzi wa barabara ambayo fedha za ujenzi wake anategemea kutembeza bakuli kwa wadosi!!

It's a big shame hiyo fast truck ya federation ni ya nini kama hakuna barabara ya kwenda Nairobi! East Africans acheni usanii!! look at the ugly face of Kibaki!!! Narudia huwezi kujivunia umahiri wa kuomba hivi Kikwete ana akili kwenye hicho kichwa! M7 naye anawania u first presida wa fed !!Why ngangania kumkumbusha kupewa msaada!! ukimwomba mtu kitu ukiona hakupi au ameminya ujue imekula kwako!!!

Huyo Pinda ingekuwa Oysterbay kwa wakubwa au Upanga kwa mabwana zao bunge lingesimama. Lakini kwa sababu Mbagala wanaishi kapuku it's business as usual!!! The tume syndrome shall wapa wanatume heifty allowances lakini itabaki kuwa siri ya jeshi!

Msipoteze muda kumsikiliza huyo chizi Nchimbi na taahira Lukuvi! Je Lukuvi atadhubutu kutusomea CV yake kwanza he has only a formal education unatarajia nini kwa kada wa umoja wa vijana kama yule!! Amezoea kubebwa tu!!
 
Wazee wa tume naona tayari wana andaa matumbo yao na bla bla kibao kutathimi.
Tunacho omba wahanga wote wa hii milipuko walipwe, walipwe nyumba zao,walio jeruhiwa nao walipwe maana huu ni uzembe wa serikali pamoja na jeshi watawekaje kambi na ghara la siraha nzito nzito jilani na makazi ya watu?
Kwanza kabisa tunaomba waziri muhusika ajiuzuru ili taratibu zingine ziweze kwendelea.
 

Tume gani tena.......mwaka jana kale kamlipuko kambi ya gongo la mboto..matokeo ya tume yalisemaje??? tume..tume..tume!!

kikwete kashindwa kazi ya kutawala hata kazi ya jeshi anayodaiwa kusomea nayo inamshinda..au alikuwa
akiimba kwaya tu jeshini???
 
Rais mwenyewe hafai,

Watu wame stoop low mpaka kum photoshop Salim katika a nasty propaganda campaign, kuna ustaarabu hapo?
?

mkuki kwa nguruwe...dhambi aliyomfanyia salim ya kuunga picha aonekane yupo na sultani...leo hii watoto wa mujini wamemtoa ..analia ...dhambi zinalipwa hapahapa duniani...ahera mbona mbali!!
 
Thank you andindile!

Poleni sana wote mliopo Dar es salaam. Mshikamano kiwe kitu cha kwanza katika kukabiriana na hali hii ya kutisha



Mbagala Jeshini
 
Last edited:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…