Dkt. Gwajima D
Minister
- Nov 28, 2015
- 966
- 6,019
Salaam nyingi za za upendo kwenu wote.
Aprili 12, kila mwaka ni Siku ya Mtoto wa Mtaani Duniani.
Kaulimbiu Mwaka huu ni ‘TUWAJIBIKE’.
Uwajibikaji uanze ngazi ya familia kwa wazazi/ walezi kutimiza jukumu la kulea. Sheria ya Mtoto Sura ya 13 kifungu cha 6 – 13, kila Mlezi/ Mzazi anawajibika kuwalinda Watoto na kufanya familia mahali salama. Kutotimiza wajibu huu ni kosa kisheria na adhabu yake ni faini isiyozidi milioni 5 au kifungo miezi 6 au vyote viwili.
Vilevile, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, Kijiji, Kata, Halmashauri, Tawala za Mikoa, Taasisi za Serikali, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Asasi za Kiraia, Viongozi wa Dini, Wazee wa Kimila na Watu binafsi watekeleze sheria, ufuatiliaji na kutoa huduma za usaidizi kwa watoto na familia zenye changamoto. Aidha, waelimishe jamii kufahamu madhila ya watoto kuishi mitaani na kuzuia vihatarishi vinavyochochea watoto kuondoka majumbani na watoe taarifa ofisi za Serikali pale penye vihatarishi na dalili za mtoto kutoweka nyumbani. Ikitokea ametoweka, taarifa zitolewe kwa hatua stahiki.
Wadau pia waunganishe nguvu kuelimisha jamii umuhimu wa malezi ya watoto na vijana ndani ya familia. Wizara tutaimarisha ufuatiliaji wa utekelezaji na kutoa mrejesho kwa jamii.
Julai 2021 hadi Aprili 2024, jumla watoto 6,459 (Wavulana 4,356, Wasichana 2,103) walitambuliwa katika mikoa sita (6) yenye idadi kubwa ya kundi hilo (Dar, Mwanza, Arusha, Mbeya, Iringa na Dodoma ambapo;
Watoto 1,346 (Wavulana 919, Wasichana 427) waliunganishwa na familia zao na kati ya hao;
1. Watoto 816 (Wavulana 605, Wasichana 211) waliunganishwa na mafunzo ya ufundi stadi na kupatiwa mitaji na vifaa vya vya kazi waweze kujitegemea,
2. Watoto 3,427 (Wavulana 2,301, Wasichana 1,126) walipewa vifaa vya shule na mahitaji mbalimbali,
3. Watoto 273 (Wavulana 175, Wasichana 98) walipewa huduma ya kuimarisha uchumi wa kaya,
4. Watoto 597 (Me 356, Ke 241) wako kwenye Vituo maalum na Makao ya Watoto wakiandaliwa kwa ajili ya utengamao.
Athari za watoto kuishi mitaani; kukosa mengi ikiwemo malezi ya kiroho, matunzo, afya, elimu, kufanyiwa ukatili, kutumia dawa za kulevya na kujihusisha na uhalifu.
Wanahabari, naomba tuendelee kutoa taarifa za elimu kwa jamii. Jamii ipige pia Simu za Wizara Na. 0262 160 250 / 0734 986 503, na kuandika ujumbe 0774 112 233 / 0769 608 130 / 0766 400 168.
PAMOJA TUKIWAJIBIKA; INAWEZAKANA.🇹🇿
Ahsanteni.
Aprili 12, kila mwaka ni Siku ya Mtoto wa Mtaani Duniani.
Kaulimbiu Mwaka huu ni ‘TUWAJIBIKE’.
Uwajibikaji uanze ngazi ya familia kwa wazazi/ walezi kutimiza jukumu la kulea. Sheria ya Mtoto Sura ya 13 kifungu cha 6 – 13, kila Mlezi/ Mzazi anawajibika kuwalinda Watoto na kufanya familia mahali salama. Kutotimiza wajibu huu ni kosa kisheria na adhabu yake ni faini isiyozidi milioni 5 au kifungo miezi 6 au vyote viwili.
Vilevile, ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, Kijiji, Kata, Halmashauri, Tawala za Mikoa, Taasisi za Serikali, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Asasi za Kiraia, Viongozi wa Dini, Wazee wa Kimila na Watu binafsi watekeleze sheria, ufuatiliaji na kutoa huduma za usaidizi kwa watoto na familia zenye changamoto. Aidha, waelimishe jamii kufahamu madhila ya watoto kuishi mitaani na kuzuia vihatarishi vinavyochochea watoto kuondoka majumbani na watoe taarifa ofisi za Serikali pale penye vihatarishi na dalili za mtoto kutoweka nyumbani. Ikitokea ametoweka, taarifa zitolewe kwa hatua stahiki.
Wadau pia waunganishe nguvu kuelimisha jamii umuhimu wa malezi ya watoto na vijana ndani ya familia. Wizara tutaimarisha ufuatiliaji wa utekelezaji na kutoa mrejesho kwa jamii.
Julai 2021 hadi Aprili 2024, jumla watoto 6,459 (Wavulana 4,356, Wasichana 2,103) walitambuliwa katika mikoa sita (6) yenye idadi kubwa ya kundi hilo (Dar, Mwanza, Arusha, Mbeya, Iringa na Dodoma ambapo;
Watoto 1,346 (Wavulana 919, Wasichana 427) waliunganishwa na familia zao na kati ya hao;
1. Watoto 816 (Wavulana 605, Wasichana 211) waliunganishwa na mafunzo ya ufundi stadi na kupatiwa mitaji na vifaa vya vya kazi waweze kujitegemea,
2. Watoto 3,427 (Wavulana 2,301, Wasichana 1,126) walipewa vifaa vya shule na mahitaji mbalimbali,
3. Watoto 273 (Wavulana 175, Wasichana 98) walipewa huduma ya kuimarisha uchumi wa kaya,
4. Watoto 597 (Me 356, Ke 241) wako kwenye Vituo maalum na Makao ya Watoto wakiandaliwa kwa ajili ya utengamao.
Athari za watoto kuishi mitaani; kukosa mengi ikiwemo malezi ya kiroho, matunzo, afya, elimu, kufanyiwa ukatili, kutumia dawa za kulevya na kujihusisha na uhalifu.
Wanahabari, naomba tuendelee kutoa taarifa za elimu kwa jamii. Jamii ipige pia Simu za Wizara Na. 0262 160 250 / 0734 986 503, na kuandika ujumbe 0774 112 233 / 0769 608 130 / 0766 400 168.
PAMOJA TUKIWAJIBIKA; INAWEZAKANA.🇹🇿
Ahsanteni.