Are spies made or born?

Are spies made or born?

Nyongeza: kwa maeneo ya shule hasa sekondari,wakuu wa shule huwa na role kubwa ya kuanza kuwaona na kupeleka mapendekezo.
Pia Head Prefects wa Enzi zile .
Kuna shule zilipandikizwa"scouts". Wakishachagua vijana wao,scouts huacha shule ghafla.
Shule kama Ilboru, Mzumbe,Songea boys, mazengo,vkilakala kwa girls.
 
Kwa hawa wanaoanza mapema kama sekondari, kwa kweli sijui hata ni saa ngapi wanakuwa trained, yaweza kuwa ni watu waliokwishakuuwa trained somewhere halafu wakaingia shule kama wanafunzi, labda!,ila wewe ambaye bado, huwezi kujijua kuwa unafuatiliwa ili uwe hivyo mpaka baada ya muda fulani, hutofuatwa na kuambiwa au kuombwa ufanye kazi hiyo, utafuatiliwa kimya kimya baada ya kuonekana kuwa unaweza kuwafaa, hutojua kuwa unafuatiliwa, kuna mtu atasogezwa close na Wewe, huyo ndiye atakaye kutune mpaka utafika huko, anaweza kuwa mjomba wako ambaye naye yumo huko, mwalimu, jirani au rafiki yako, kuwa na wewe karibu kutamfanya akujue zaidi na kupeleka information, na anakuwa anakulead kwenye njia ya kukufikisha huko bila wewe kujijua, utakuja kujielewa baadae kuwa wewe ni nani, na hapo ndipo utaanza kuwa msiri zaidi na mambo yako, mtu aliyewekwa kuwa close na wewe, atakushauri mambo mengi ambayo ukiyafuata yatakufikisha huko bila wewe kujijua mwanzoni but ni mambo ya manufaa tu kwako, na kwa hao wanaokusubiri wakuingize kwao, kwa mfano, unaweza ukawa unapenda kusomea kitu fulani, lakini huyo mtu akakushauri mara mbili mbili kusomea kitu kingine, akakusisitiza mno, akakupa faida zaidi za kusomea hicho anachokushauri, akakuhaidi au akakuweka katika connection nzuri na ya uhakika ya kuzidi kufanikiwa katika kitu hicho, yaani anakuwa mshauri wako anayekufanikisha kila mara, unamuamini, kila atakapo kueleza jambo unalifuata cause unafanikiwa mwisho unajikuta tayari umeshafika mlango, kwenye hivyo vyuo vyao utafika hivyo, utashauriwa na washauri wako wa siku zote mpaka utafikia huko, unaambiwa jiendeleze kwenye hili, kachukue diploma ya hili, embu kasome chuo fulani kitu fulani, kuna sehemu nitakuunganishia kuna mtu namfahamu etc. unaweza hata ukawa hutumii hela zako sometimes, unaweza akatukoa wa kukufadhili au ukafadhiliwa na ofisi aliyokupeleka, ukasoma kwa raha, unafanyiwa mambo yako faster kuliko wenzako, ukishaingia kwenye vyuo vyao utakuwa tayari umejijua, na utakuwa msiri zaidi, usije ukapata matatizo outside, hawa watu wana raha mambo yao wanafanyiwa faster, mnaweza kujikuta wengine kwenye ofisi, mnasahaulika, hamshughulikiwi haraka mnapoomba kwenda kusoma, lakini yeye ni faster anashughulikiwa, hawatakiwikuwa waropokajiropokaji , lakini unaweza kukuta mtu wa aina hiyo anaropoka kitu fulani mbele yako ili akujue wewe una maoni gani au unakijua vipi, anakuchunguza tu, yuko kazini, nahauoi au kuolewa hovyohovyo, mtu unayetaka kuoana naye anachunguzwa kwanza, akionekana ok kwao wewe kuwa naye, mtaoana, ukikataliwa kuoana naye, hutomuoa, la sivyo uchague ofisi au yeye, nahata ukimchagua yeye ukiacha ofisi utakipatapata, cause you have siri nyingi waweze payuka huko unakoenda, mara nyingi wanaoana wao kwa wao, hii kazi wengine unaweza kusikia kastaafu lakini huwa ni till death, sio kustaafu totally kama kazi nyingine, unaendelea kimya kimya, kama nyie wazazi mko humo mtoto wenu ni rahisi kuingizwa humo, sio mtu yule wa kuchunguzwa saaana, muda mreeefu kwa kuwa nyie tayari mnajulikana ni watu wa aina gani, wasiri, na moja kwa moja mtoto wenu mtakuwa mmemkuza kuwa hivyo, kutokana na mazingira yenu nyumbani au atakuwa amestaadopt kuwa hivyo, atawafaa, watamuongoza/ mtamuongoza tu kuwa anavyotakiwa kuwa, kuwa barabara itakayomfikisha/ itakayomfanya kuwa hivyo
Kweli umenena.
 
Mbona kama michango yako inaonesha kama unajua vile au kuna Infantry soldier wawili???
Au una research kujua ubora wa mbinu yenu kama vipi mbadilishe. Mukulu naona una knowledge kuzid swal ulouliza.
Umefikiri vema
 
kimsingi hakuna aliyezaliwa nakusema kwa akili zangu hizi napaswa kufanya kazi ya kijasusi, uhasibu ualimu nk...

kuna mawazo mengi sana miongoni mwenu hasa juu ya hawa watu..na pengine wengine kudhani hawa watu wapo special kabis akwa kazi hiyo tu...
kimsingi mara nyingi wengi wao kwanza huwa hajui kama ana karama kutumikia kazi hii..mara nyingi watu hawa kwanza huonwa na watu wengine waliobobea kwenye fani hiyo ya ujasusi.. wakipendezawa na mamabo kadha wa kadha kwa mtu fulani na wakaona anazo ''potentials'' na anafiti criteria yao basi huanza kumfatilia kwa undani ili kujua dira na mweleko wa maisha yake yakoje na mambo mengine kama hayo.
mara nyingi mtu anayefuatliwa anaweza kuwa mtu mzima na elimu yake na anafanya kazi nyingine tofauti kabisa..pengine ni mhunzi, mwalimu , daktari, dreva tax, bar maid nk.. na asijue kabisa kuwa kuna watu wana agenda nae. kuna wengine wanatengenezwa wakiwa toto wadogo kabisa kuanzia wakiwa wachanga... hawa watakusanywa na kupelekwa ''shambani'' ambako watalelewa na kufundishwa kila aina ya vitu lugha, itkadi mbalimbali kwa madhumuni na malengo maalumu.. wakishai iva vizuri wanatumika meneo mbali mbali nje na ndani ya nchi

ki msingi kuna sifa za kuingi katika kundi hili...si kali mtu anaweza kuingi..kuna wengi wanatamani sana kujua na kuingia huku lakini kwa kuwa hawana sifa ama uwezo basi wanaishia kutamani tu am pengine kujifanya kama na wao ni wa kundi hili...kuna wengine mpaka wanaghushi na kupatia pesa kwa njia hiyo kisa akili yake inatamani kufanya kazi hiyo na hana lakini hana sifa...hawa ni wengi ndio hao kila uchao mnasikia afisa usalama feki akamatwa...ndio hao kila uchao anajesema mimi ni afisa usalama nk..wale walioiva na wanaojua kai hii na wlaiomo hata siku moja hwezi kusikia anajidai hadharani au bar...labda kama maadili yamebadilika na miiko haifatwi...

nitataja baadhi ya sifa kwa kifupi sana ambazo kimsingi kila mtu anazo ila zinatofautiana kiwango cha kuelewa mambo nk

1. lazima mtu huyu awe na uwezo wa kuchunguza jambo..lazima akili yake iwe ina rekod mambo na matukio haijalishi yuko wapi na anafanya nini..

2. ni lazima pia awe na kumbukumbu nzuri..hili ni tatizo la wengi sana..wengi vijana wa siku hizi wanaangukia kundi la
7+_ 2 ...maana yake ni kwamba ukimuuliza mtu ataja sifa za jambo fulani (mfano sifa kuu za maji au matumizi yake) anaweza akakutajia sifa tan na akijitahidi sana anaweza kufuka tisa lakini si zaidhi ya hapo.. jasusi lazima awe na kumbukumbu ya hali ya juu kabisa...mtu hana haauwezo wa kushika namba sita za simu za watu tofauti halafu analilia kuwa jasusi....hili haliwezkani..lazi kumbukumbu iwe ya hali ya juu vinginevyo huwezi kazi hii

3. siku zote jasusi anatumia mantiki (logic) kuelewa mambo, vitu ..sifa hii ni muhimu sana..lazima ajuwek kwa nini hiki kiko hivi na hiki kiko hivi na pia lazimaajue namna ya kukibadili kuwa kati muonekanao mwingine tofauti na wa awali si katika muonekano bali katika ufahamu pia..

4. jasusi lazima ajue kubadilika kulingana na mazingira na watu wanaomzunguka, nini wanataka , ni watu wa aina gani hii tamsaidiaaenende vipi katika mazingira hayo..jasusi lazima ajue kucheza na hisi za watu...

5. lazima ajue kujifunza na kusikiliza milango yote ya fahamu na achambue kwa haraka nin cha kufanya kama yu katika hatari...katika ubongo wa binadamu kuna maelekezo mengi sana yanayomuonya binadamu juu ya hatari yoyote..lazima uyasikilize hayo ...

6. lazima asiwe mkurupukaji katika katika kufnaya maamuzi ya jambo lolote..

7..uwezo wa kutunza siri lazima uwe mkubwa....hili ni tatizo hasa kwa wengin wengu...wengi hamna chumba cha siri na hamjui kuweka mambo chini ya kitovu.

kwa kifupi ziko sifa nyingi sana juu ya watuwa kundi hili...sasa mtu anawez kuw ana sifa nyingi zote hizo hapo juu na akaoenkana anafaa lakini baada ya kupatikana na akaanza kufanyiwa usaili hasa juu ya psychology yake anaweza kuonekana ahafai...kuna series ya test nyingi sana nyingi mno upande huu ili kuona kama kweli huyu mtu anafaa nk..ukifanikiwa kupita test zote basi utafaa ukifeli hata moja basi hufai...

kwa hiyo kujibu swali la huyu muuliza swali kwamba ni lazima mtu awe na akili ya kutosha nailiyotulia IQ yake iwe juu...hivi ni vitu tunavyozaliwa navyo lakini tunaweza kujifunza na kuviendeleza vipawa kama tutapitia makuzi sahihi na mazingira rafiki.basi ukibahatika kuonekana na ukaonwa basi utafundishwa namna ya kutumia vipawa vyako.
huwa tunasema we choose the right people not necessarily the best one...

walau kidogo nimesaidia
Umetoa soma kubwa kama ni watu wa kulewa wameelewa.....pia huwa sipendi mtu wa misifa.unajua mi nani?
 
katika bandiko langu nilijaribu kugusia kidogo sana juu a mambo mihimu yanayohitajika kwa watu wa aina hiyo wanaoongelewa kwenye mada....katika kuzisoma umeona kuwa kwa hali ilivyo huko Tanzania hakuna anayeweza kufaa na sababu kubw auliyoongelea ni mabadiliko ya kimaadili yanayoletwa na utandawazi kuwa yanaathiri kwa kiasi kikubwa zoezi zima la upatikanaji wa watu hawa.
yawezekana hoja yako ni ya msingi lakini nipende kukwambia kuwa huko nyumbani kuna vijana wake kwa waume wengi ambao vichwa vyao havijachafuliwa na mambo hayo lakini pia mabadiliko ya kiteknolojia sio sababu ya msingi sana maana jasusi yoyote lazima ajue matumiz ya technolojia mbali mbaliili aweze kufanya kazi zake kwa ufasaha. siku hizi haihitaji mtu kutembe na AK47 mtu anaweza kutembea na ki-USB flash disk kidogo tu ambacho kiknaweza kuwa na madhara makubwa sana katika jamii.
pengine niseme kuwa wapo watu wengi sana vichwa vyao havina uchafu mwingi na wanafiti katika eneo flani kulingana na mahitaji...huko juu kwenye bandiko langu nilisema wanahitajika watu wa aina mbali mbali kulingana na mahitaji yaliyopo...

sasa hizo ulizoita criteria naomba nikwambie kuwa kila mtu anao uwezo huo wa kila moja wapo hapo juu isipokuwa namna ya kuzitumia... uelewa wa mambo ni jambo la msingi sana...kuna wakati flani huko nikiw ahuko nyumbani nilimuuliza kijana mmoja kwamba..ili kijiji kiwe kijiji ni hatua zipi zinachukuliwa mpaka eneo flani linaitwa kijiji, na pia katika kijiji kuna safu zipi za uongozi.... kijana yule alishindwa kunijibu swali liel akabaki kurukia rukia vitu vya ajabu ...sasa swali kama hili haliihitaji eti mabadiliko ya teknolojia ...bali ni upana wa uelewa wa mambo..ni swali dogo lakini kama hujui namna ya kujibu basi huwezi

ukija kwenye swala la kumbu kumbu..kila mtu anazo kumbukumbu za kiwango flan...wapo watu wanaoweza kutaja majina ya wenzao karibu 40 waliokuwa wanasoma shule ya msingi lakini hawezi kutaja majina ya marafik zake 5 aliosoma nao sekondari...nk nk nk.... naomba nikupe changamoto ukienda kwene mishuguliko yako ya siku ..na jioni ukirudi nyumbani hebu jaribu kuandika report yako ya sku nini umefanya, umekutana na nani...alivaa nini, mliongea nini, ulipita wapi ulkaona nini....kama kuna jambo utalisahau na ulilifanya kwa siku hiyo basi jua uwezo wa kukumbuka na umakini uwapo eneo flani ni kiasi...au nenda bar hata kama hunywi pombe agiza maji kisha ukiwa mle ndani angalia kuna watu wa aina gani, umesalimiana na nani humo ndani, kuna bar-maids wangapi walivaa nini, kaunta ikoje mle ndani watu walikaa vipi,,mtu wa upande upi alikuwa anavuta sigara, uliongea na nani na mliongea nini....kumbuka iwe ni bar yenye mziki na watu wanacheza...kisha rudi nyumbani tengeneza report ya kila kitu ulichoona mle ndani....hili nalo haliihitaji mabadiliko ya tabia nchi au technolojia bali ni aili ya mtu jinsi ilivyo tulia na uwezo wake kurekodi mambo na kutunza kumbukumbu....


Niliposoma post yako nikakumbuka jambo moja miaka mingi ya nyuma siku moja mimi na mdogo wangu tulichukuliwa na baba kwenda hadi katikati ya mji na kisha baba akanionyesha dirisha moja lililokuwa wazi kwenye jengo flani la gorofa , dirisha lilikuwa kwenye gorofa ya 4.baba akaniambia unaliona dirisha lile basi nenda mpaka pale ndani ya ile ofis na fanya ufanyavyo baad aya dakika saba ningependa sana kukuona kwenye balcony ya ofis hiyo ukiwa na mtu utakayemkuta humo ndani na hakikisha mkononi umeshikilia moja ya file utakalolikuta humo na ukikosa file basi ushike hata glasi ya maji mkononi uwe unakunywa......piga picha ungekuwa ni wewe hatua zipi ungechuku na ungeanzia wapi hadi kufanikisha swala hilo ndani ya dakika saba?...mdogo wangu yeye aliambia aene mpaka mapokezi aangalie ndani ya daftari la wageni jina la mwisho la mtu aliyejiandikisha na achukue na namba za simu alipewa dakika 4.....wewe ungeanzia wapi ?..na je unadhani mabadiliko ya technolojia yanachangia lolote juu ya kufanikisha hayo mawili tuliyoambiwa na baba mimi na mdogo wangu?....

kwa hiyo napenda nikwambie kuwa mabadiliko ya globalization hayaathiri upatikanaji wa watu hawa bali kwa namna flani yanasaidia kuweza kupata vijana wanaofaa..chini ya mchango wangu pale juu nimesema wanaochaguliwa ni the right person note necessarily the best one.....

nimalize kwa kuukuuliza swali hivi unadhani kusema uongo ni dhambi?...
Sio dhambi kwa sababu uongo hutumika kutatua matatizo kutokana na mazingira husika
 
Mtoa mada nenda kaangalie movie ya SALT itakujibu swali lako
 
Spies please try to help. Mtoto wangu aliyekuwa anatumikia jkt kwa mujibu wa sheria baada ya kumaliza kidato cha sita Umbwe secondary mwaka huu amepigwa na wanajeshi wa huko jkt bulombora kigoma inasemekana khali yake ni mbaya sana na wanataka kumuhamishia lugalo. Nawezaje kupata habari za uhakika.?
[emoji23][emoji23][emoji23]chanzo cha hbr au taarifa hiyo ni nani kakupa taarifa hizo.kwanini mwanao apigwe?ulijuaje kama yupo lugalo?pia navyofahamu mtu yeyote akipatwa na tatizo ns yupo serious lzm watawasiliana na mzazi
 
mtoto akizaliwa katika jamii huwa anabembelezwa na na kila mtu atamuona kama malaika...hana dhambi, hajui lolote juu ya dunia hii...kadri anavyokuwa na ubongo wake ulio katika kundi la ''tabula lasa'' taratibu unaanza kushika vitu anaanza kuelewa mambo kwa hatua...mtoto huyu akikuwa na akawa mtu mzima na akawa na tabia za ajabu kama ujambazi kila mtu atashangaa malaika huyu aliyekuwa mdogo amepatwa na nini.....

kuna vitu tunazaliwa navyo...viko ndani lakini vingine tunajifunza kwa kadri tunavyokuwa..binti akitoa mimba na kuua kicanga au kukitupa chooni sijui kama nae huyu kazaliwa na tabia ya kuua au amejifunza ukubwan baada ya kuona maisha magumu basi akaamua kufanya vile....

nikijikitaka tika swali lako nianze kwa kusema hivi...mauaji mengi hupangwa mara baad aya kuona hatari ya mtu falni katika jamii..kuwa uwepo wake ni hatari kwa ustawi na usalama wa eneo au nchi kwa ujumla na hivyo akiondolewa kuna mengi ya heri na usalama yatapatikana..kwa hiyo ni lazima faida za kumuondowa ziwe ni nyingi na za maana.,,mipango yote hii ni lazima ifanywe kwa siri na hairihusiwi kuandika mahali popote pale.

sasa ili kufanikisha jambo hli ni lazima kujua kabisa kwamba yule mlengwa anafahamu juu ya maisha yake...je anafahamu kuwa anaweza kuuwawa? je hafahamu kama yu katika hatari? analindwa? halindwi?

kama hafahamu kuwa anaweza kuuwawa na hana ulinzi basi hatua ya kumuondoa huitwa ''rahisi''(simple) , kama anafahamu yu katika hatari na ana ulinzi basi hatua ya kumuondoa huitwa '' fukuza'' na kama analewa na analindwa huitwa''ulinzi''....sasa baada ya kuona mlengwa yu katika hali gani basi kusudio la kumuondoa na mipango husukwa kwa ustadi wa hali ya juu kabisa kumbuka no paper work ni kichwani tu!!! mipango hii hasa ni lazima izingatie maisha ya mlengwa na ratiba zake, anapenda nini,anaishi wapi, ni mlevi au si mlevi anapenda wanawake sana? nk... maisha yake lazima yawe yanajulikana kila kitu.

hilo likikamilika hatua inayofuata ni kupanga nani akakamilishe kazi ile na aikamilishe kwa namna ipi? kama ni kuikamilsha na yeye kubaki hai basi process hiyo huitwa ''salama''(safe) kama nae itabidi kufa wakati wa kukamilisha zoezi basi process hiyo hiutwa ''poteza''(lost)...anaweza kuandaliwa kulingana na mazingira ya utekelezaji wa tukio hilo kama nani lazima awe na sifa zifaazo (must be determined,intelligent, resourceful and physically active.)..mtu mwnye moyo kwa kwale hatakiwi hata kidogo....kupoteza maisha ya mtu si mchezo...so mtu muoga muoga hatakiwi kabisa ..kuna watu hawawezi hata kuuwa mbwa!!...kama muuaji itampasa kuuwawa basi lazima aangaliwe mtu mwenye mlengo flani wa kidini, kisiasa au mwenye haja ya kulipiza kisasi...

hayo na mengine mengi yakifanyika basi njia ya kukamilisha zoezi hupangwa mchoro mzima lazima uandaliwe....remember no paper work!!...mda wa kukamilisha zoezi na wapi hupangwa....haijalishi itachukua mda gani kikubwa yule targeti lazima apotee ndani ya mda uliopangwa...zipo mbinu kibao sana ni nyingi mno ..za maumimvu makali, zisizo na maumivu makali ....na yule muuaji ni lazimaaandaliwe au waandaliwe na ni muhimu pia asijue/wasijue rule of the game ikoje sababu hasa ni nini ya kukamilisha zoezi...wao ni kukamilsha zoezi tu.

wapo walizaliwa wakiwa na roho ngumu sana hasa wanawake ni wazuri sana katikakukamilisha mambo haya hasa kama unataka kutumia njia isiyo na maumivu na kama targeti anapenda mambo yetu yalee...(mmiliki mmoja wa mahoteli huko dar alipotea kwa njia hiyo)..alikwa anapenda sana blowjob...

kuna jamaa mmoja anaitwa chepuga miaka ya mwanzoni 2000 huko kwnye mbuga za wanyama ruaha yeye alikuwa bingwa wa kuuwa tembo..jamaa alikuwa katili sana yule...hakuwa na huruma kabisa...pengine huyu ne alizaliwa akiwa hivyo maana hakutengenezwa mahali...kuna siku askari wanyamapori walikuta kijana mmoja aliekwenda nae kuwinda anachoma nyma ya swala porini na jamaa huyo alikuwa ameenda kukusanya kuni..askari wale walimkata miguu yule kijana kwa risasi wakamwacha pale yule ..chepuga akarudi na kuni zake na kumkuta kijana analia pale akajua moja kwa moja waliotenda hivi ni askari wanyama pori...alichokifanya pale ni kummalizia yule kijana kwa risasi na akamzika kule kule..yeyey akarudi mpaka kijijini kwake madibira...akajipanga ....akarudi porini siku nyingine safari hii alikwenda si kuwinda tembo bali kuwasaka askari wa wanayama pori..akaliona gari likiw alimesheheni askari..kwa njia zake anazozijua yeye aliwauwa askari 12 pale pale akabaki dreva wa gari...akamuamuru akusanye silaha za askari wenzake na apakie miili ya wenzake kwenye gari..yule askari akatii....baadaya hapo akamuamuru aendeshe gari lile mpaka kituo cha polisi madibira...kupfika pale polisi chepuge akafyatua risasi na kumuua yule dreva...kisha akaowambia polisi mizigo yenu hiyo....akaondoka.....

alitafutwa kwa njia zote hadi alipopatikana na na iliamliwa asiuwawe...akapelekwa dsm ..baadaya hapo wakamuomba aachane na kazi ya kuwinda tembo bali sasa awe mlinzi wa kuwalinda tembo..akakubali...akapewa piki piki na silaha akarudishwa ruaha akawa anakaa huko ni weli allisaidia sana kukamata majangiri akisaidiana na askari wa wanyamapori..baada ya miaka kama mitatu ilitengenezwa fomula nzuri sana kisha akaungana na wale askari aliowauwa...

nimalize kwa kusema kuwa wapo waliozaliwa na roho ngumu na wengine nyepesi....na wengine hufunshwa ujasiri wa kutekeleza mambo hayo hataka kama wana roho nyepesi...zoezi hili hufanyika kwa usiri mkubwa na pengine muuaji asijue sababu hasa ni ipi...lazima wahusika wawe na wachache..waliojipanga sawa sawa....


ngoja niulze swali....hivi ikiotokea siku moja sukari ikapigwa marufuku (yaani ikawekwa kwenye kundi moja na cocaine au heroin) kutumiwa na binadamu unadhani nini kitatokea katika jamii?..

jion njema
Nadhani taifa litakuwa na watu wengi waliodumaa akili pamoja na kudhoofika afya.......
 
Back
Top Bottom