Kiukweli mkuu niwe muwazi niliiondoka dakika ya 37 baada ya Di Maria kufunga bao la pili, maana huko kibanda umiza nilikuwa nazodolewa mpaka nikawa nakosa amani
Kelele za mashabiki vibanda umiza baada ya Mbappe kusawazisha ndio zilizoniamsha ikabidi niucheki tu kwenye TBC.
Aisee mpira nimeangalia kwa dakika ya 80 nimeshangaaa sana yani kiukweli hii ndio mechi yenye hadhi ya fainali.
Moyo wangu umekuwa mweupe yale makasiriko niliyoyapata baada ya kuona tunaongozwa yashayeyuka.
Siwezi kuacha kumsifia Messi jinsi alivyokuwa anashuka hadi chini kuzuia mashambulizi na kwa juhudi zake hususani katika bao la tatu, ila Mbappe ni kiumbe kingine.
Hongereni Argentina mmechukua kombe kihalali japo mapito yenu yalikuwa yana sintofahamu nyingi ila by now mmestahili.