Argentina yatwaa ubingwa Kombe la Dunia - Qatar 2022

Kinachoendelea huko Qatar ni miujiza tu! πŸ˜…

Kwa mataifa ya Asia, Japan na Korea wanawawakilisha vizuri sana wenzao...πŸ‘πŸΎ

Kwa hapa nyumbani Afrika angalau Morocco, Ghana na Senegal wanatupa matumaini ya kufika Robo fainali.

Mtanange kati ya Ghana na Uruguay inatukumbusha michuano ile ya mnamo mwaka 2010 kule Afrika kusini... ni wakati wetu sasa wa Kulipa kisasi πŸ€”
 
Route to the World Cup 2022 Final
Updated
View attachment 2433071
Kwny hii betting yako umepatia kwa upande wa kulia kundi la France, France ataingia Fainali, ila kwa kushoto umechemsha Mzee...Argentina atafungwa na Nerthelands then Brazil atamfunga Spain....kisha Fainali zitaingia Brazil & France.

Tupo hapa
 
Ni sahihi lkn WC hii ina surprise nyng sana na me naona asa izi team zinazopigiwa sana upatu kuna m1 lzm atashangazwa hapo arud nymbn na vilio.
Spain & Argentina hawafiki Fainali.

Tupo hapa.
 
Morocco vs Spain
Naona inajirudia kama ile ya mwaka 2014... Spain wakabebwabebwa wakapewa ushindi kisa hao jamaa wanatokea Afrika na wana asili ya kiarabu, ila Spain alipigiwa mpira mwingi sana! Na alipigwa bao zaidi ya moja wakakataa mpaka Morocco walitaka kususia mechi watoke uwanjani. Naona yanajirudia yaleyale... hawa wazungu wanatengeneza mazingira tena kwa ajili ya maslahi/faida ya watu flani flani πŸ€”
 
Yaap, ndio maana hata timu za Africa na hizi za Asia kufika hapa ni kwa msaada wa VAR ya sasahv ambayo at least wameongeza ufanisi

Walizingua tu kwny mechi ya Ghana vs Portugal

Ila VAR wakitenda haki basi mwaka huu WC itashangaza watu
 
Wee...hiyo Brazil unayoiona hivyo itacheza Fainali na France au Portugal.

Brazil inazingua kwenye forward yake ila kiungo ni hatari na pia ni ngumu sana kufungwa (wana beki nzuri sana)
Hao Brazil wako subiri wacheze tu na USA au England uone kama hamna kitu... wala tusifike mbali, Brazil akikutana na England hatoboi au USA kama hutaki ngoja wakutane utarudi kunikumbuka hapa πŸ˜ƒπŸ‘πŸΎ
 
Wee...hiyo Brazil unayoiona hivyo itacheza Fainali na France au Portugal.

Brazil inazingua kwenye forward yake ila kiungo ni hatari na pia ni ngumu sana kufungwa (wana beki nzuri sana)
Wala Forwad Brazil hawazingui watu wanaangalia mechi mbili tu za awali Yaan Switzerland haijawai fungwa na Brazil Kwenye kombe lolote la Dunia isipokuwa hili ni team ngumu ndo ili watoa hata Ufaransa Euro ,pili ukija Kwa Serbia ni wagumu sana Yaan Kwa kimombo tunasema wana timu bora sana katika Ulaya Kwa mwaka huu
 
Haya sasa yametimia Ujeremani arudi kwao akaendeleze harakati zake. Nimefurahi sana alivyotolewa kinara wa uchoko. Wazungu wenzao wamekausha wao pereche pereche mingi.
Nilikua naona humu wapiga ramli walivyokua wanapiga hesabu kirahisirahisi za kufuzu Spain na Germany. Spain wakaona wazamishe jahazi la Geremani shepherd waende na Japan
 
Mbwembwe zingine bana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…