Arusha: Lengai Ole Sabaya afikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi, Utakatishaji Fedha

Huyu jamaa ni mafia wa hatari sana..

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana - 2020, Jimbo la HAI ndilo lilikuwa la kwanza kutangaza matokeo ya ubunge masaa mawili tu baada vituo vya kupigia kura kufungwa siku hiyo huku majimbo mengine yakitumia masaa zaidi ya 18 kutoa matokeo...!

Yaani jimbo la Hai, tulijua Mbowe kashindwa hata kabla kura hazijahesabiwa mpaka Yoel Museven, Rais wa Uganda "akatoa tuzo" kwa Mwendazake Magufuli na kijana wake Sabaya...!!!!!!
 
Kazi yote aliyofanya Sabaya ya kumng'oa Mbowe pale Hai leo hii analipwa kwa kushikiwa "bastola" kama jambazi?
Aisee!!!!!
Huyo jambazi mwenzio Sabaya alimung'oa mbowe hai kwa njia haramu. Kwa kutumia uhalifu. Chama Cha Mapinduzi hatukumtuma kwenda kufanya uhalifu kwa wapinzani, wananchi na wafanyabiashara wa kilimanjaro na Arusha.

Matendo ya Sabaya yakihalifu hayawezi kuharalishwa kwa kumuondoa mbowe hai. Mbona kina Sugu waliondolewa mbeya lakini wakuu wa wilaya kule hawakufanya uhalifu?
 
Ndege mjanja hunasa na tundu bovu. Kunyanyasa watu na kuiba mali zao ndio terms of reference ya kazi zake? Ndio imetoka toka hiyo. Asahau kabisa mambo ya kupata madaraka
 
Ngoja nitume jamaa awapelekee wana vumbi la Congo huko Kisongo kitafunwa kinakuja.
 
Naona hii itakuwa habari njema sana kwa wafuasi wa Mbowe.
Sasa watachekelea utafikiri jimbo la Hai watalipata tena.
By the way, Sabaya alipaswa kupewa tuzo ya heshima na CCM na siyo kushtakiwa. Huu ni usaliti kwa mpiganaji kama huyu.
Ona ulivyo na Akili za kijinga
 
Dah nyie kizazi cha sasa nyie. mnajiooona.
Kila kitu mnajua. Hata ukipita makongo jeshini pale ukaleta fyongo ukiogeshwa maji ya mtaro kwa sabuni utakuja anzisha thread hapa za Sheria sijui kanuni.
 
Ni kweli. Nashangaa kwanini aliachiwa aendelee kuwa DC. Hakufaa toka mwanzoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…