MotoYaMbongo
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 2,146
- 886
Kwa Tume hii ya uchafuzi, Gambo mapema mshindi.Nasikia fununu kuwa Gambo huwenda akachukua fomu kwa tiketi ya CCM kugombea ubunge wa Arusha mjini.
Kwa hali ilivyo nnapata Uhakika 100% sana Gambo hawezi kushinda katika uchaguzi huo, tukumbuke kua tayari Gambo ana kidonda kibichi kabisa cha kutumbuliwa na Raisi, hivyo basi kama Raisi ameona hufai.
Je, wananchi utawaambia nini? Gambo pia si mzoefu wa siasa za majukwani, hapa pia Lema atatumia uzoefu wake kupita na Gap.
Trust me, ikitokea mtinange ukawa kati ya Lema Vs Gambo, basi mapema mnoo Lema ananyanyua Kikombe.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa tume ipi?SAAA MBILI TU ASUBUI TU
Gambo kusimamishwa kazi siyo kwa bahati mbaya, Gambo hawezi kuchukua fomu ya ubunge ilihali ni RC, kuachishwa kazi ni hatua ya gambo kuweza kuchukua fomu na kuanza kujinadi majukwani. Hata RC wa DSM yapo mawili akachia ngazi au akapewa UBUNGE WA KUTEULIWA HATMAYE UWAZIRI. TRUST ME, THE TIME WILL TELL hahahaaa kiswangilishNasikia fununu kuwa Gambo huwenda akachukua fomu kwa tiketi ya CCM kugombea ubunge wa Arusha mjini.
Kwa hali ilivyo nnapata Uhakika 100% sana Gambo hawezi kushinda katika uchaguzi huo, tukumbuke kua tayari Gambo ana kidonda kibichi kabisa cha kutumbuliwa na Raisi, hivyo basi kama Raisi ameona hufai.
Je, wananchi utawaambia nini? Gambo pia si mzoefu wa siasa za majukwani, hapa pia Lema atatumia uzoefu wake kupita na Gap.
Trust me, ikitokea mtinange ukawa kati ya Lema Vs Gambo, basi mapema mnoo Lema ananyanyua Kikombe.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ndiyo huzijui siasa za arusha mgoroko, siasa za arusha ni ngumu na rahisi mno!! First and foremost arusha ni anti-CCM,hilo ni la kwanza na la muhimu kuliko mengine,pia arusha wanaweza kukupiga chini huku wanakupenda na kukulilia, Arusha wanaweza kukuchagua huku wakiwa hawakuamini,hawakupendi,wala hawakutegemei uwasaidie,( mf Mh Lema)kumbuka siku ile pale council wananchi walikuwa wakiimba nyimbo za kutokuwa na imani na lema kama hatauza ushindi wake,ila wao wana uhakika kuwa kura walizompigia zinatosha kumpeleka bungeni,wanajua wanachikifanya na pia wanajua matokeo yake!! Ndiyo maana huwezi kuta mwana arusha halisi akilalamika kuwa sijui Lema hajatusaidia hili au lile,zaidi sana utawasoma tu wakina Magonjwa Mtambuka wakimlalamikia kutokea nangulukuluAnashinda mapemaaa. Watu hawajui siasa za Arusha. CCM wamsimamishe Gambo, anakubalika na wananchi
Mtangaza matokeo ndiye mwenye maamuzi ya mwisho ya nani awe mbunge! Na yeye mwenyewe amevaa jezi ya ccm na kadi yake inaonekana dhahiri kwenye mfuko wa koti lake!! Tusubiri tuone.Hizo zote ni kelele, wapiga kura ndo wana maamuzi ya mwisho.
Awali sikuwa nakuelewa vizuri na kukasirika nisomacho ulicho andika.Hiyo ipo wazi Gambo asubuhi anashinda.
Hii inaitwa kupakaziana.....zaidi sana utawasoma tu wakina Magonjwa Mtambuka wakimlalamikia kutokea nangulukulu
anaSHINDA njaa labda[emoji3]Hiyo ipo wazi Gambo asubuhi anashinda.
Mnaweweseeka. Mnamfanyia Gambo fitna. Kwa taarifa yenu siamini Kama CCM itasikiliza majungu, na mkumbuke CCM ndo chama kinachoongoza serkali,watafanya uchunguzi na itabainika haya Kama Ni kweli. Mna fitna za kizamani Sana. Na nyie mkiendekezwa ndo mtaleta mpasuko kwenye chama. Acheni unaaUshindi wa kura za maoni kwa aliyekuwa Mgombea wa jimbo la Arusha mjini, Mrisho Gambo umezidi kupingwa na makada mbalimbali wa CCM wakiwemo waliokuwa wagombea wenzake wakidai kwamba uligubikwa na rushwa iliyokithiri.
Taarifa zaidi zimeeleza kwamba baadhi ya wajumbe walioshiriki kumpitisha Gambo siku moja kabla walipokea fedha kiasi cha sh 150,000 kila mmoja na hivyo wakati wakiwa katika ukumbi wa uchaguzi tayari walikuwa na mgombea wao mfukoni.
Mmoja wa wajumbe wa uchaguzi huo Peter Mbise kutoka kata ya Lemara alidai kwamba siku moja kabla ya uchaguzi huo Gambo alilala katika hotel ya Mount Meru ili kukutana na wajumbe nyakati za usiku baada ya mazingira ya nyumbani kwake kutokuwa rafiki.
Pia Gambo anadaiwa kufanikisha kulipia ukumbi wa kura katika hotel hiyo jambo lililochangia yeye kujiweka katika mazingira mazuri ya ushindi .
Duru za kisiasa jijini hapa zimedai kwamba iwapo Gambo atapitishwa jimbo la Arusha Mjini litaenda upinzani mapema kwani Gambo hakubaliki kwa wananchi lakini amekuwa akitumia fedha kuwahadaa wananchi ili wamuunge mkono.
Hata hivyo baadhi ya wagombea ambao wamejipanga kutoa malalamiko yao ngazi za juu baada ya kukamilisha kukusanya vielelezo wamedai kwamba msimamizi wa uchaguzi huo, Mary Kisaka amewahujumu kwa kutoonyesha vizuri karatasi ya kura hivyo kujikuta kura zao akipewa Gambo kwani walikuwa haonyeshi ipasavyo karatasi ya kura.
Wafuatao ni baadhi ya makatibu kata wa CCM na viongizi wengine wa CCM waliokuwa wakitumia pikipiki nyakati za usiku kuwakusanya wajumbe na kuwapa fedha, Felix Lemoi mwenyekiti wa CCM kata ya Ngarenaro, Aisha Mbaraka katibu kata Levolosi, Saipuran Rams mwenyekiti UVCCM wilaya ya Arusha.
Wengine ni Juliana Paulo mwenyekiti wa CCM kata ya Sekei, Ally Menu mwenyekiti wa CCM wazazi wilaya, Labora Ndarvoi mwenezi kata ya Themi, Joseph Masawe mwenyekiti wa CCM wilaya, Mary kisaka msimamizi wa uchaguzi na mwenyekiti wa UWT wilaya.
Wengine ni Juma Mohamed katibu wa CCM kata ya Muriet ,Abdi Madava Mwenyekiti wa CCM kata ya Osunyai, Sakina Mpuju Mjumbe wa kamati ya siasa wilaya, Abraham Mollel (Cobla)mwenezi wa CCM wilaya na Yajaya Njalita mmiliki wa shule ya Green Valley na mbunge viti maalumu aliyemaliza muda wake.
Kwa mujibu wa uongozi wa hotel ya Mount Meru (jina limehifadhiwa) Gambo alitumia chumba namba 403 Gorofa ya NNE kulala katika hotel hiyo kwa siku tatu akikutana na wajumbe .
Washalikoroga walinywe tu Sasa[emoji3][emoji3][emoji3] na wakae kwa utulivu dawa ifanye kazi vizuriNaona wapinzani mmeanza kuweweseka ....subirini dawa iwaingie
Sema Arusha ina wenyewe, ww huna ulijualo zaidi ya kula bangi na milungi.Huyo Gambo awe mbunge wa nani , mm ni mkazi wa Arusha hapa kaloleni naijua in and out ,
Kiufupi tu Gambo hana uwezo wowote wa kupamban na lema ,
Hii ni Arusha mzee tunaijua wenyewe huyo gambo atapigwa asubuhi tu ohoooooooo!!! Lema hajaanza leo and tunamchagua lema kwakuwa katekeleza wajibu wake vizr and tunajua uovu wote unaofanywa na ccm , hawatutishi katu asilani abdani
uongo utakusaidia nini ?