Arusha: Mmiliki wa Baa ya Kipong mikononi mwa Polisi kwa kutengeneza Pombe kali bandia

Arusha: Mmiliki wa Baa ya Kipong mikononi mwa Polisi kwa kutengeneza Pombe kali bandia

Mmoja wa wamiliki wa eneo maarufu Arusha ,KIPONG amekamatwa kwa kosa la kukutwa na mitambo ya kutengeneza Konyagi Feki, mitambo na stika za TRA maarufu kama TAX STAMP.John Casian anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi ambapo alikamatwa juzi usiku katika operesheni iliyofanywa na polisi kwa kushirikiana na TBL na vyombo vingine vya serikali.
MFANYABIASHARA MAARUFU NA MMILIKI WA BAR YA KIPONG ARUSHA ATIWA MBARONI AKIWA NA HAWARA WAKITENGENEZA KONYAGI FEKI,AKUTWA NA SHEHENA YA VINYWAJI FEKI ,MITAMBO NA STIKA KIBAO ZA TRA ZAKAMATWA,MKE AMRUKA FUTI MIA 'AKU'
Pole kali
 
Mmoja wa wamiliki wa eneo maarufu Arusha ,KIPONG amekamatwa kwa kosa la kukutwa na mitambo ya kutengeneza Konyagi Feki, mitambo na stika za TRA maarufu kama TAX STAMP.John Casian anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi ambapo alikamatwa juzi usiku katika operesheni iliyofanywa na polisi kwa kushirikiana na TBL na vyombo vingine vya serikali.
MFANYABIASHARA MAARUFU NA MMILIKI WA BAR YA KIPONG ARUSHA ATIWA MBARONI AKIWA NA HAWARA WAKITENGENEZA KONYAGI FEKI,AKUTWA NA SHEHENA YA VINYWAJI FEKI ,MITAMBO NA STIKA KIBAO ZA TRA ZAKAMATWA,MKE AMRUKA FUTI MIA 'AKU'
Mteja wa Pombe Kali Jijini Arusha amesema akinywa Pombe Kali sikuhizi kichwa huwa kinamuuma
 
Hata Hennessy na Moet zitakuwa zinachakachuliwa. Kuna siku nikiwa night club x Arusha nilikunywa Hennessy ambayo sikuielewa 😡
 
Tatizo la dili haramu linalipa ila ngumu kuacha. Laiti angeridhika na alichokwisha pata aendelee na dili halali yasingemkuta
 
Jeshi la polisi Mkoani Arusha, linamshikilia Mkurugenzi na mmiliki wa Bar Maarufu ya Kipong ,John Casian Shayo kwa kosa la kutengeneza na kuuza vinywaji feki aina ya Konyagi kinyume cha sheria.

Casian alikamatwa juzi usiku na mamlaka za serikali zikishirikiana na jeshi la polisi na baada ya kupekuliwa alikutwa na shehena ya vinywaji feki ambavyo amekuwa akitengeneza na kuuza na hivyo kuhujumu bidhaa halisi zinazotengenezwa kihalali,kwa lengo la kujipatia kipato na faida kubwa bila kujali afya ya mlaji .

Mbali na Casian mwingine anayeshikiliwa ni mwanamke mmoja anayedaiwa kuwa ni hawara yake (jina linahifadhiwa) ambaye alikutwa na mitambo kadhaa inayodaiwa kutumika kutengeneza pombe hizo feki kinyume cha sheria.

Mke wa Casian, Sia Casian alithibitishwa kukamatwa na kushikiliwa kwa Mume wake , akidai kwamba jambo hilo halimhusu na kwamba kwenye mkataba Casian sio Mkurugenzi wa Kipong .

"Ni kweli Casian alikamatwa walikuja watu wengi usiku kutoka idara mbalimbali za serikali wakiwemo polisi, walifanya upekuzi kila kona ila Casian alikuwa akitengeneza bidhaa hizo wakishirikiana na hawara yake na sio hapa Kipong "

Kwa upande wale meneja wa TBL Arusha, Joseph Mwaikasu alisikitishwa na kitendo kinachofanywa na wafanyabiashara wasio waaminifu kwa lengo la kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu.

"Taarifa za kuhujumu bidhaa zetu tumezipata na sisi tumelichukukia kwa uzito mkubwa suala hilo ambalo linahusisha uhujumu uchumi"

Alisema suala la bidhaa feki linawaathiri kwa kiasi kikubwa kwa kupoteza wateja na kupungua kwa mauzo kutokana na ubora wa bidhaa hizo feki na huo ni mtandao mkubwa ambao vyombo vya dola vinapaswa kuchukua hatua kali .

Alisema hatua ya wafanyabiashara kutengeneza bidhaa feki zenye nembo ya TBL zinasababishwa bidhaa zao halisi kushindwa kuuzika sokoni na hivyo kuikosesha mapato serikali.

"Aliiomba serikali kuwachukulia hatua kali wale wote wanaojihusisha na mtandao wa kutengenezaji na kusambaza bidhaa feki ili kuepusha viwanda vya ndani kushindwa kujiendesha"

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Arusha, Eva Rafael alisema wanasuburi taarifa ya jeshi la polisi baada ya kukamilisha uchunguzi kuhusu kutumika kwa nembo za TRA kwenye bidhaa feki.

"Ni kweli kuna nembo zetu zimekamatwa zikitumiwa kinyume cha sheria kutengeneza bidhaa feki ,hivi sasa polisi wanakamilisha uchunguzi ili watupatie taarifa kamili ,nitawajulisha"alisema Meneja .

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Justine Masejo hakuweza kupatikana kuzungumzia tukio hilo.

Mmoja ya wateja wa pombe kali jijini Arusha Abbas Mohamed alisema kuwa mara nyingi anapokunywa pombe kali kichwa huwa kinamuuma sana jambo ambalo anahisi huenda atakuwa akiuziwa kinywaji feki bila kujua


View attachment 2944392
FIGO ZA RAIA WA CHUGA ZIPO SALAMA KWELI?
 
Back
Top Bottom