Arusha: Mwandishi wa habari mwingine adaiwa kupelekwa kusikojulikana

Arusha: Mwandishi wa habari mwingine adaiwa kupelekwa kusikojulikana

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
IMG_20220616_042831_722.png

Breaking News: Mwandishi wa Habari Mkoani Arusha, Lilian Oddo ambaye anafanya kazi na mwandishi wa Wasafi tv Bw. profit Mmanga, na yeye amekamatwa akiwa maeneo ya darajani/vibandani njia ya kwenda Kwa Morombo Jijini Arusha, na amepakiwa kwenye gari nyeusi ambayo ndani yake yupo Profit, bado haijulikani wamepelekwa wapi.


===================
Arusha: Mwandishi Lilian Oddo Hajulikani Alipo

Taarifa kutoka Mkoani Arusha inadaiwa Mwandishi wa Habari, Lilian Oddo hajulikani alipo.

Lilian anayefanya kazi kwa ukaribu na mwandishi wa Wasafi TV, Potte Mmanga ambaye naye alichukuliwa na watu wasiojulikana mapema Juni 15, 2022, inadaiwa amechukuliwa na watu wanaodhaniwa ni walewale waliomchukua Potte.

Taarifa za awali zinaeleza Lilian alichukuliwa akiwa maeneo ya Darajani/Vibandani njia ya kwenda Kwa Morombo. Taarifa zaidi zitafuata, vyombo vya usalama havijapatikana kuzungumzia taarifa hizo.


Pia soma: Mwandishi wa Habari wa Wasafi Media - Arusha, Potte Mmanga adaiwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana

Chanzo: Gadi TV
 
Wafuasi wa... Walisema yule bwana ndiye alikuwa anafuga makundi ya watekaji na wasiojulikana[emoji23] chaajabu watekaj wapo bado ijapokuwa sponsor kafariki, who's behind the game?

Anyway utekaji upo kwa kila nyakati za Uongoz, inategemeana na mtekwaji aliingilia vip mambo yasiyomuhusu[emoji23].

Au basi usikute hata huyo mtekwaji anakesi ya kutembea na mme wa mtu, so alionesha kiburi na dharau kwa mwenye mme, matokeo ndio hayo[emoji23].

Au basi tufanye ni matukio ya ngorongoro waandishi kuanza kuchimbua data ambazo wenye nchi hawataki ziguswe wala kuwa published in public [emoji23].

Kati ya hayo moja wapo ni jibu japo laweza kuwa si sahihi sana[emoji23]
 
Watakuwa wameripoti habari mbaya kuhusu mtu au ....
Kuna press conference ilifanywa na wamasai niliona maiki ya Wasafi Media ikiwa kwenye meza basi kisanga ndo icho japo press haikuwa na madhumuni mabaya ila kilichopo hawata uwataje ata wamasai kwenye haki.
 
Kuna press conference ilifanywa na wamasai niliona maiki ya Wasafi Media ikiwa kwenye meza basi kisanga ndo icho japo press haikuwa na madhumuni mabaya ila kilichopo hawata uwataje ata wamasai kwenye haki.
Watoto hawajui Dola ni nini, ngoja wakaijue... chezea ndevu siyo dola
 
Samia usiruhusu haya mambo yatakuharibia.
Damu za watu nzito
 
Back
Top Bottom