Arusha: Polisi auawa kwa panga akijaribu kumkamata mwizi usiku nyumbani kwake

Arusha: Polisi auawa kwa panga akijaribu kumkamata mwizi usiku nyumbani kwake

Mnasema ndo taaluma ya uandishi lakini naona inachosha kukirudia kichwa cha habari mara nne kwenye habri moja. Kahabari kafupi lakini maandishi ni mengi.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Askari polisi katika kituo kidogo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Mkoani hapa, ameuawa kwa kukatwa na panga kichwani wakati akijaribu kumkamata mtuhumiwa.wa wizi.

Tukio hilo limetokea Jana majira ya saa tano usiku katika Kijiji Cha Makiba wakati Askari huyo( jina linahifadhiwa) alipoenda nyumbani kwa mhalifu kwa lengo la kumkamata.

Kwa mujibu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP-Justine Masejo askari huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuvunja damu nyingi.

"Askari wetu katika kituo kidogo cha polisi Mbughuni alikatwa panga kichwani na kufariki dunia baada ya kwenda nyumbani kwa mhalifu majira ya saa tano usiku lengo la kumkamata, hivi Sasa polisi wanaoendesha operesheni ya kumsaka ili afikishwe kwenye vyombo vya dola"alisema Masejo

Kamanda alifafanua kwamba askari huyo alienda Nyumbani kwa mtuhumiwa kwa nia ya kumkamata kuhusiana na matukio ya wizi wa mazao na kwamba wakati akijaribu kumkamata ndipo alipotokea mhalifu mwingine Nyumba ya jirani ambaye alimkata panga moja kichwani askari huyo nakupoteza Maisha.

Aidha Masejo aliongeza kuwa kabla ya tukio hilo mwananchi mmoja alifika katika kituo cha polisi Mbughuni kulalamika.juu ya mtuhumiwa wa wizi wa mazao yake ambapo polisi walianza msako wa kumvizia mtuhumiwa huyo.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa uchunguzi, aliweza kufanikiwa kutoroka baada ya tukio hilo na polisi wameanzisha msako Mkali dhidi ya Watuhumiwa hao .

Ends
Kwa hiyo polisi alienda peke yake kumkamata mhalifu saa 5 usiku ?!
 
Askari polisi katika kituo kidogo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Mkoani hapa, ameuawa kwa kukatwa na panga kichwani wakati akijaribu kumkamata mtuhumiwa.wa wizi.

Tukio hilo limetokea Jana majira ya saa tano usiku katika Kijiji Cha Makiba wakati Askari huyo( jina linahifadhiwa) alipoenda nyumbani kwa mhalifu kwa lengo la kumkamata.

Kwa mujibu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP-Justine Masejo askari huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuvunja damu nyingi.

"Askari wetu katika kituo kidogo cha polisi Mbughuni alikatwa panga kichwani na kufariki dunia baada ya kwenda nyumbani kwa mhalifu majira ya saa tano usiku lengo la kumkamata, hivi Sasa polisi wanaoendesha operesheni ya kumsaka ili afikishwe kwenye vyombo vya dola"alisema Masejo

Kamanda alifafanua kwamba askari huyo alienda Nyumbani kwa mtuhumiwa kwa nia ya kumkamata kuhusiana na matukio ya wizi wa mazao na kwamba wakati akijaribu kumkamata ndipo alipotokea mhalifu mwingine Nyumba ya jirani ambaye alimkata panga moja kichwani askari huyo nakupoteza Maisha.

Aidha Masejo aliongeza kuwa kabla ya tukio hilo mwananchi mmoja alifika katika kituo cha polisi Mbughuni kulalamika.juu ya mtuhumiwa wa wizi wa mazao yake ambapo polisi walianza msako wa kumvizia mtuhumiwa huyo.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa uchunguzi, aliweza kufanikiwa kutoroka baada ya tukio hilo na polisi wameanzisha msako Mkali dhidi ya Watuhumiwa hao .

Ends
Wameru noma sana....
 
Huyu kajitakia utaendaje kukamata mtuhumiwa peke yako tena saa tano usiku ni uzembe..
 
Askari polisi katika kituo kidogo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Mkoani hapa, ameuawa kwa kukatwa na panga kichwani wakati akijaribu kumkamata mtuhumiwa.wa wizi.

Tukio hilo limetokea Jana majira ya saa tano usiku katika Kijiji Cha Makiba wakati Askari huyo( jina linahifadhiwa) alipoenda nyumbani kwa mhalifu kwa lengo la kumkamata.

Kwa mujibu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP-Justine Masejo askari huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuvunja damu nyingi.

"Askari wetu katika kituo kidogo cha polisi Mbughuni alikatwa panga kichwani na kufariki dunia baada ya kwenda nyumbani kwa mhalifu majira ya saa tano usiku lengo la kumkamata, hivi Sasa polisi wanaoendesha operesheni ya kumsaka ili afikishwe kwenye vyombo vya dola"alisema Masejo

Kamanda alifafanua kwamba askari huyo alienda Nyumbani kwa mtuhumiwa kwa nia ya kumkamata kuhusiana na matukio ya wizi wa mazao na kwamba wakati akijaribu kumkamata ndipo alipotokea mhalifu mwingine Nyumba ya jirani ambaye alimkata panga moja kichwani askari huyo nakupoteza Maisha.

Aidha Masejo aliongeza kuwa kabla ya tukio hilo mwananchi mmoja alifika katika kituo cha polisi Mbughuni kulalamika.juu ya mtuhumiwa wa wizi wa mazao yake ambapo polisi walianza msako wa kumvizia mtuhumiwa huyo.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa uchunguzi, aliweza kufanikiwa kutoroka baada ya tukio hilo na polisi wameanzisha msako Mkali dhidi ya Watuhumiwa hao .

Ends
Fake story. Mtu kauwawa wanashindwa vipi kutaja jina lake wala kuonyesha picha yake. Jambazi na yeye jina lake linahifadhiwa ili iweje?
 
Saa tano usiku , peke yake anavizia mtaani, je kama alikuwa anavizia mke wa mtu? Maana askari hawachelewi kugeuza kesi.

Mie mtuhumiwa wa kwanza ni huyo aliyeripoti wizi wa mazao yawezekana huyo ndio aliyengeneza mtego mzima. Njagu kajipeleka akajikuta ameingia mtegoni.

Pamoja sifurahii kifo Ila polisi wajifunze kuishi na watu, hilo panga wangekatwa wote wanaobambikizia watu kesi
 
Sijawahi kuelewa wala kuamini statements za mapolisi[emoji848]
 
Halafu utasikia nyumbu mmoja anasema kwanini jambazi fulani alietwangwa risasi hajakamatwa afikishwe mahakamani!
Statement za polisi huwa zina ukakasi

Na we umeamini kabisa kilichoelezwa hapo?
 
huyo alifumaniwa sema wameamua watuzuge ki’hivo.

we unaendaje kukamata mwizi usiku wa saa 5 usiku peke yako ?

ila hata hivo nikisikia polisi amepatwa na lolote baya hua nafurahi maana hawana roho ya utu hao jamaa
 
Hilo ni GENGE LA POLISI CCM yaani lilikwenda kwenye ugoni haya likazikwe tu hakuna namna
 
Good angemchoma na moto kabisa ili kupoteza ushahidi.


Kutokuwa na shule bwana! utaendaje kukamata mwizi usiku ukiwa mwenyewe?

Huyu alienda kuomba rushwa bila shaka!!

Pole pole Karma!

Rekebisha title. Kauwawa na sio Kaua
 
Kwa maelezo haya inaonyesha hakukuwa na tukio la kiaskari katika kutekeleza majukumu yake,inawezekana ni ugomvi binafsi au tukio la kufumaniana.Iweje jina la mtuhumiwa lifichwe? Kwa nini aende pekeake kumkamata mharifu usiku saa tano?mwenyekiti wa mtaa/kijiji alikuwa wapi?vipi auawe na jirani kwa panga na si mtuhumiwa mwenyewe? kuna maelezo mengi hayajakaa sawa kwa taarifa hii ufafanuzi wahitajika zaidi.
 
Back
Top Bottom