JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Watu sita wamefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa katika ajali ya gari baada ya Toyota Noah kugongana na Lori aina ya Scania katika eneo la Alkatani, Kata ya Sepeko, Tarafa ya Kisongo Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha usiku wa kuamkia leo Aprili 20, 2022.
Ajali hiyo imetokea katika barabara ya Arusha – Babati, RPC wa Arusha, Justine Masejo amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Lori aliyeshindwa kulimudu gari na kuhamia upande mwingine, ambapo anashikiliwa na Jeshi la Polisi.
“Lori lilikuwa likitokea maeneo ya Makuyuni, Noah ilikuwa ikitokea Arusha Mjini, majeruhi walikimbizwa katika Hospitali ya Jeshi iliyopo Monduli, miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Maunti Meru.
“Hatujafahamu majina kamili ya watu waliopoteza maisha, uchunguzi unaendelea,” - RPC wa Arusha, Justine Masejo.
Ajali hiyo imetokea katika barabara ya Arusha – Babati, RPC wa Arusha, Justine Masejo amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Lori aliyeshindwa kulimudu gari na kuhamia upande mwingine, ambapo anashikiliwa na Jeshi la Polisi.
“Lori lilikuwa likitokea maeneo ya Makuyuni, Noah ilikuwa ikitokea Arusha Mjini, majeruhi walikimbizwa katika Hospitali ya Jeshi iliyopo Monduli, miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Maunti Meru.
“Hatujafahamu majina kamili ya watu waliopoteza maisha, uchunguzi unaendelea,” - RPC wa Arusha, Justine Masejo.