Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 9,140
- 15,963
Wananchi wa kata ya Osunyai mtaa wa Ngusero wilaya ya Arusha jijini hapa wameungana kwa pamoja na kuchapisha vipeperushi mtaani vinavyoeleza kuchoshwa na uuzwaji wa madawa ya kulevya aina ya mirungi kama ilivyo mboga sokoni.
Vijana wa boda boda wamekuwa wakiingia na kutoka katika baadhi ya nyumba katika mtaa huo huku wakiwa wamebeba mafurushi makubwa ya mirungi na wengine wakiwa wanauza hapo hapo mtaani kama vile mchicha sokoni bila bughdha yoyote toka kwa uongozi wa mtaa na polisi.
Wananchi hao wamefikia uamuzi huo baada ya viongozi wa mtaa pamoja na polisi kushindwa kudhibiti hali hiyo kwa muda mrefu sasa na hivo mtaa wao kuitwa mtaa wa Mirungi.
Wananchi hao wamesema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kuona hata watoto wao na familia zao zikijiingiza katika matumizi mabaya ya madawa.
Vijana wa boda boda wamekuwa wakiingia na kutoka katika baadhi ya nyumba katika mtaa huo huku wakiwa wamebeba mafurushi makubwa ya mirungi na wengine wakiwa wanauza hapo hapo mtaani kama vile mchicha sokoni bila bughdha yoyote toka kwa uongozi wa mtaa na polisi.
Wananchi hao wamefikia uamuzi huo baada ya viongozi wa mtaa pamoja na polisi kushindwa kudhibiti hali hiyo kwa muda mrefu sasa na hivo mtaa wao kuitwa mtaa wa Mirungi.
Wananchi hao wamesema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kuona hata watoto wao na familia zao zikijiingiza katika matumizi mabaya ya madawa.