Mheshimiwa Godbless Lema anachokisema kuhusu bodaboda kina ukweli wa asilimia 90, bodaboda wengi wamekata tamaa ya maisha na hata ukiwaangalia wengi wao unaona kabisa hawana option B zaidi ya kuendesha bodaboda.
Moja ya dalili kuonesha kuwa bodaboda wengi wamekata tamaa ya maisha ni style yao ya uendeshaji wa hizo bodaboda wengi wao hawajali wanaendesha kwa mwendo kasi hata sehemu za hatari.
Yaani wana base na ule msemo wa liwalo na liwe kweli, bodaboda ni kazi ya laana wengi wao wanaofanya hii kazi hawana option.
Lema kukaa nje kidogo karudi mjinga hasa
Haelewi kuwa bodaboda wako wanaozimiliki wenyewe wengi tu
Benki ya NMB imekopesha maelfu ya bodaboda kuwa wamiliki sio madereva tena
Taasisi nyingi zimekopesha na wanalipa vizuri tu marejesho
Anafikiri anaongea na madereva tu
Wako wengine ni madereva na wamiliki.wa bodaboda hadi kumi
Angefanya utafiti kwanza kuwa anaoongea nao ni nani
Wako wengine wafanyakazi wa serikali muda wa mapumziko huendesha bodaboda kuongeza kipato .Wengine hununua bodaboda na kuajiri madereva wa kuwaletea hesabu hadi wabunge wamo nawajua wanaomiliki bodaboda zaidi ya 30 na wanaletewa hesabu
Lema anaposema bodaboda ni umaskini anatukana kuanzia wamiliki kuwa bodaboda zinawapa umaskini wakati sio.kweli zinawapa utajiri na anatukana hadi madereva kuwa ile sio ajira!!! Haelewi kuna ajira rasmi na zisizo rasmi.Wenyewe wanajua ile ni ajira
Sekta ya bodaboda imebadilika sana Lema hana habari sababu hapandi anawaangalia tu akiwa kwenye gari yenye kiyoyozi
Atoe tamko tu mfano kuwa bodaboda nchi nzima wagome kutoa huduma hata kwa siku moja tu aone bodaboda watakavyomparamia kwa hasira kumpinga