Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Lema amepinga mfumo wa VICOBA Kwa kusema ni comfort zone Kwa wanawake na wanaume walio wengi.

Nakubaliana Kwa Sababu zifuatazo;

1. Wanawake wenye vikoba wanaweka fedha zao Bila kuziingiza kwenye mizunguko wakisubiri siku ya kuvunja, japo vichache vina utaratibu wa kukopeshana na kurejesha Kwa riba ndogo.

2. Mtu anayetegemea VICOBA hasa watu wa daraja la chini wanatumia muda mwingi Sana kukaa kwenye vikao kuliko kutumia muda mwingi kuzalisha.

3. Viongozi wengi wanosimamia vikoba wanatajirika hasa wale wenye uwezo mzuri wakuzungusha kwenye biashara fedha za Wana KIKOBA. Hivyo wapo watu wanaishi Kwa mitaji ya michango ya Wana VICOBA

4. Mfumo wakuwalipisha Wana KIKOBA faini unatengeneza mizania ya wizi na kumomonyoa zaidi vipato vya wanachama. Kuchelewa Mia tano, kutokufika buku na ukisafiri pia unatozwa faini means wao wanatamani muda wote uwe nao na usipokuwepo ulipe.

5. Wanawake wengi hasa vijijini wameuza Mali za familia Kwa Sababu ya VICOBA na wakopeshaji wasio na utaratibu maalumu. Kiongozi wa KIKOBA anakwenda kukopesha fedha za KIKOBA Kwa riba na riba husika hairudi Kwa wanachama. Lakini pia ukishindwa kulipa wanakamata Mali wanauza.

6. VICOBA vimevunja Sana ndoa na sasa hivi upo utaratibu wa wanawake wengi waliovuruga future za familia zao wanaishi Kwa kujifariji Kwa KUMWAGILIA moyo.

Poverty mentality imepelekea wanawake wengi kuanzisha vikoba vya kulewa na kuishi maisha yasiyoendana na utamaduni wetu. Angalia kwenye beach nyingi au sehemu za starehe utagundua wanawake wengi washamba na masikini wamejiunga nakuweka utaratibu mbovu kabisa wakumwagilia moyo. Katika KUMWAGILIA moyo Ndipo uzaliwa magonjwa na talaka, picha zisizo na staha pamoja na mambo kama hayo.

7. Kupitia vikoba wamezaliwa wanawake masikini wasio na uwezo wa kutajirika mapema, matokeo yake wanaparamia wanaume wenye uwezo wawalipie pesa ya vikoba. Kumbuka hakuna cha bure.

Wanawake wanahubiri wamejikwamua kupitia vikoba lakini laiti wangemwelewa Lema wanaanza rasmi kushirikiana kuanzisha na kusimamia biashara kisha wagawane pesa mwisho WA MWAKA wangefika mbali sana.

Hakuna ujinga kama kupeleka pesa yako Kwa MTU akae nayo mwaka mzima then akikurudishia pesa Ile Ile unasema umevunja KIKOBA.

Kwanini isiweke pesa yako kwenye kibubu? Pesa isiyozalisha inawezaje kuleta faida?

Bora vikoba viige mfumo wa saccos at least watapata faida na watasimama kwenye mfumo rasmi.

Tuamke tufanye tathimini; tusikalie kusema tumesomesha Kwa vikoba, tuseme tumempa MTU atuwekee pesa ya Ada ili tukiitaka atukabidhi tukalipe Ada.

Kama VICOBA vingekuwa vinalipa mabenki yasingekopesha watu kwa riba, means fedha lazima izalishwe.
 
Maelezo yako ni sahihi. Lengo lake kuu ni kuweka kidogo kwenye kundi ili ikifika zamu yako upate fedha nyingi.

Je, kama waweza kuweka kidogo kidogo, kwa nini usifanye hivyo kwa kutumia mfumo rasmi wa kibenki ambapo utapata faida.

Na siku hizi mitandao ya simu imeaanzisha utaratibu huo km TIMIZA, MPAWA nk
 
Vicoba ni upuuzi.
Inasikitisha hata wanaume wanacheza hiyo michezo, huko hakuna faida wala nini, ni vile akili za wajinga haswa wanawake kujishughulisha na hayo mambo.

Vicoba ni aina ya Utunzaji wa pesa yako mwenyewe kupitia kundil la watu na mzunguko wa kugawana pesa kila baada ya muda fulani, kiufupi ni kwamba ukiweka pesa huko ni sawa na kusema umeshindwa kuitunza pesa yako hivyo unawapa watu wakusaidie kuitunza mpka baada ya muda watakaoamuwa wao.

Ni bora izo pesa mukaweke bank ama ktk vibubu kulko kuzungusha pesa mahala isipojizalisha zaid ya kupoteza muda.
Vicoba ni bank bubu uchwara zinazotakiwa kupigwa marufuku
 
Akisema anaonekana kituko, maana uongo wake unakuwa dhahiri. Lema na baibui wapi na wapi? Ni mrefu sana kwa maumbile ya kawaida ya mwanamke hasa wa kibongo, size ya mguu, mwendo na kadhalika. Hivi ni mjinga gani, achilia mbali afisa usalama (trained) au adui anayemtaka hasa, anaweza kuingia kingi kuwa huyo mvaa baibui ni mbususu! Kweli?
Labda alikuwa anaweka na kigodoro,
 
Kwanza vitu vyenyewe vinaitwa mchezo[emoji16]
 
Ila kuna angle CHADEMA inabidi watambue kwamba wanatakiwa ku move on..

Mimi kama mwananchi ukianza kuniambia story za awamu ya tano, haunisaidii chochote...

Ndio tunajua awamu ya tano ilikuwa na mambo ya hovyo.. but keep blaming doesnt change what has already happened.
Ilikuwa ya hovyo kwa watu wa hovyo. Lema ana hasira ya kutaifishiwa bureau de change yake kule arusha.
 
Lema nayeye alikuwa anavaa shanga kama yule afande wa zanzibar.!!
 
Ila kuna angle CHADEMA inabidi watambue kwamba wanatakiwa ku move on..

Mimi kama mwananchi ukianza kuniambia story za awamu ya tano, haunisaidii chochote...

Ndio tunajua awamu ya tano ilikuwa na mambo ya hovyo.. but keep blaming doesnt change what has already happened.
What if kama aliulizwa kilichomuondoa nchini?
 
Ila kuna angle CHADEMA inabidi watambue kwamba wanatakiwa ku move on..

Mimi kama mwananchi ukianza kuniambia story za awamu ya tano, haunisaidii chochote...

Ndio tunajua awamu ya tano ilikuwa na mambo ya hovyo.. but keep blaming doesnt change what has already happened.
Wewe angekuwa Mama yako au Baba yako au watoto wako wamepotea hujaona hata makaburi yao ungekubali huo ujinga

Unaongea kwa kuwa hayajagusa familia yako, Watu wanasema msiba ni kwa jirani

Watu lazima watoe uchungu wao wote wa moyoni ndio maana wanasema iundwe Tume ya maridhiano kama yalivyofanyika Rwanda baada ya mauaji ya kimbari

Lazima ukweli usemwe ili yasijirudie tena kwa wajukuu zetu

Tena hii kampeni ilipasa ccm waiendeshe nchi nzima kusema utekaji na kupoteza kwa watu

CCM kama walivyo fanya kwa Ole Sabaya ilipasa wafanye kwa DPP, Paul Makonda, Humprey Pole Pole na Bashiru Ally

Wote Walio husika na kupora Mali za watu, Kuteka, kubaka Yapasa wasemwe hadharani na wachukuliwe hatua kama Sabaya
 
Lkn ndio karud nchini kwa mara ya kwanza je haitakiw kusema madhira waliyopitia? Kusema ukwel uovu uliotaka kufanyiwa ni dhambi? Kwann mchukie watu kusema maumiv waliyopitia? Na kwann yasisemwe? Sheria ya Nchi inakataza? Kuna maumiv gan mnapata wahanga wakisema waliyopitia?
Kwenye psychology kuna kitu kinaitwa "allow the victim to vomit" Hivi haya mambo kina Lema wangeyasemea wapi Kama sio kwenye majukwaani ya mikutano ya kisiasa na kwenye media? Je awamu ya tano ingewezekana? Clouds iliyovamiwa na Bashite na Nape kufukuzwa uwaziri ingeweza kufanya mahojiano live coverage na Lema? Hivi tunakosa kabsa akili ya kuelewa kuwa Lema anatema nyongo ikizingatiwa alishakaa gereza la Kisongo Arusha zaidi ya miezi minne kwa kosa la kuota ndoto kuwa Magufuli akiendeleza unyanyasaji Mungu atamchukua. Hatujui Sugu alisha kaa gerezani? Badae alifatwa na Dr Kitila Mkumbo akishawishiwa kuunga Juhudi akagoma badae kina Pole pole wakampelekea plain cheque imesainiwa tu yeye aandike amount tu akagoma hotel yake ikapigwa x kwamba ibomolewe hapo bado Mbowe akikusimulia kuanzia bill canas mpaka kule Machame kwenye mashamba yake utashangaa. Mambo waliyofanyiwa upinzani awamu ya tano hawatakuja kuyasahau kamwe ni kama vile mwanaume aliyegundua na kushuhudia mke wake kamsaliti sasa anajaribu kumsamehe na kusahau HAIWEZEKANI KAMWE.
 
Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema mh Godbless Lema amesema alilkimbia nchi Baada ya kukoswakoswa kuuawa mara kadhaa na kutekwa pia

Lema amesema kama ilivyokuwa kwa Tundu Lisu na Ben Saanane hata yeye alikuwa akipokea vitisho vingi na Nyumba yake ya Machame ilichomwa moto

Hata alipoenda kukagua Migodi yake ya madini imlazimu avae baibui ili kuwakwepa maadui zake

Lema anasema ilifika Wakati mkewe aliwekewa madawa ya kulevya na kuna Wakati alibambikiwa kesi ya Wizi wa Gari ambalo mali yao

Lema alikuwa akihojiwa na Watangazaji nguli wa Clouds Media

Source: Clouds
Lema ni muongo mkubwa. Wamuue yeye kwa impact ipi alikuwa nayo?
 
Ila kuna angle CHADEMA inabidi watambue kwamba wanatakiwa ku move on..

Mimi kama mwananchi ukianza kuniambia story za awamu ya tano, haunisaidii chochote...

Ndio tunajua awamu ya tano ilikuwa na mambo ya hovyo.. but keep blaming doesnt change what has already happened.
Kashalamba asali na moja ya maelekezo ya kulambishwa asali ni kuikandia awamu ya tano ili kuficha madhaifu ya utawala uliopo yasijadiliwe na umma.
 
Back
Top Bottom