Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

CCM wawe makini na kauli hizo za lema, kwenye mikutano yao ya hadhara wanamjibu kwa kujipendekeza kwenye makundi hayo wakati inaonekana wazi bodaboda na VICOBA ni ishara ya wazi kabisa kuwepo kwa umasikini na ufukara katika jamii
 
Maisha yetu magumu sana lakini hamna mzazi anayelipa ada ili mwanae aje kuwa bodaboda.

Hamna mzazi anayepata mimba na kuwish atakaye mzaa aje kusajili line
Wishing and getting are different. Unaweza kuwish lakini uhalisia ukawa mwingine
Lema hana substance. Anaeleza end result ya tatizo bila kuleta suluhisho la tatizo lenyewe.
Alikuwa mbunge wa Arusha mjini kwa miaka 10. Kulikuwa hamna bodaboda?Kulikuwa hamna wasajili line, wamama wauza nyanya ?

Alifanya nini kuondoa hali hiyo?Jiji la Arusha wakati huo lilikuwa chini ya Chadema alitoa mchango gani? Madiwani wote walikuwa Chadema isipokuwa kata moja ya kati Arusha mjini. Lema amekuwa populist wa kupiga kelele. Malkia mmoja wa Ufaransa kabla ya mapinduzi ya Ufaransa alisimama kwenye balcony na kushangaa watu wanaandamana kupinga uhaba wa mikate.Akasema kama kuna uhaba wa mikate kwanini wasile keki.

Lema amekuwa mjinga baada ya kupata exposure. Nilidhani kukaa Canada kutamuongezea uwezo wa kutafakari. Anashauri watu wasiokuwa na means zingine wafanye nini?
 
Shida ni kwamba na wanaoleta taarifa za Lema humu wanadokoa statement tata wanaleta hivyohivyo bila maelezo ya ziada au source of information,watu wanaanza kujadili kila mtu na fikra zake.

Mfano kuna Uziuliwekwa humu,Lema kasema kujenga ukuta Mererani ni ushamba(hio ilikuwa heading)ila source haikuwekwa,nilipofualitilia ni kweli alisema hivyo ila kuna maelezo mengi alitoa kuhusu hilo na alitoa ushauri mzuri tu,na akasema kwa kuwa viongozi wote wapo Arusha(semina) atawashauri mawazo yake.

Nadhani tunahitaji media serious imualike kwa mahojiano atoe ufafanuzi juu ya kauli zake hizi,tujue hasa anamaanisha nini.

Leo East Africa radio walikuwa na uongozi wa Bodaboda Dar,wale viongozi nao walilaumu hio kauli wakisema kwamba watu wanasomesha wanajenga na kwa siku boda hakosi 30,000(Siku mbaya) kwamba kwa mwezi hakosi 800,000 na kwamba wanawazidi hata kada fulani ya waajiriwa serikalini.

Baadae mtangazaji akaanza kuwadadisi,kama mna kipato hicho inakuwaje mnakosa bima ya afya ya 1,200,00 kwa mwaka?wakaanza bla bla kwamba hio tumetaja ni kama ukiweka akiba,wakaambiwa kwa takwimu za muhimbili kila siku wanapokea majeruhi 6 wa bodaboda pale,wakadai eti hao sio bodaboda ila ni vijana wa mikoani wameletwa kubeba mayai kusambaza kitu ambacho ni uongo.

Je unaweza kufanya kazi ya Bodaboda kuanzia ujana hadi uzee?Je utapenda mtoto wako arithi kazi yako? hawakuwa na majibu ya maana.

Ukweli ni kwamba kauli ya Lema kwa juu juuu inakera ila ukiingia ndani ukweli upo,Ilikuwa wamtafute Lema bahati mbaya naona hawakufanikiwa mpaka kipindi kinaisha.
Mwache Lema atupe hiyo 'exposure' ya kuishi CANADA kwa mwaka mmoja na atufundishe jinsi maisha yanavyopaswa kuwa hata kama ni kwa kutusimanga.Kuna wengine wameishi huko miaka zaidi ya 20 lakini hawajapata 'exposure' kama ya Mh.Lema. What a genius man,mwaka mmoja tu amerudi ni mwalimu wa kila kitu [emoji3]
 
Jamaa ni kama yule kipofu alieona punda

Kufika Canada ameona kama miujiza ameshangaa na ni ushamba tu kuona maisha ya huko ni tofauti

Angekaa miaka 10 angetukana wanaokula Ugali Walahi
Nawajua baadhi ya watu wanapokuja nje na wwkirudi nyumbani hujiona wamebadili maisha na kuwaona wengine kama mbuzi tu

Nimekaa nje karibia miaka 50 ila hata siku moja sijawashangaa maisha ya jamaa zetu huko ila nawaombea always maisha yawabadilikie

Anawatukana watu wakati yeye na familia wanakula hela za wakimbizi
Amejilipua ukimbizi na kujidhalilisha kwa wazungu
Watoto wanasoma kwa jasho la walipa kodi Canada

Badala aseme njia mbadala yeye anayashangaa maisha aliokulia mpaka kafika hapo

Anafananisha Canada na Tanzania anataka wawe sawa

Jamaa kumbe ni mshamba kiasi hicho
Ulimbukeni mbaya sana
Kufika Canada kaanza kutukana washikaji
Mzabeni makofi huyo [emoji1]
 
Unaposema boda boda ni kazi ya laana, kusajili laini ni kazi ya kipuuzi hutaki mwanao umuone anaifanya utamfukuza kwako, vikoba ni laana sijui hutaki mkeo ajihusishe navyo kabisa.

From a standing point wewe ni mkimbizi wa kisiasa umebebwa huko Canada for over a year. Umepata PR na familia yako na privileges nyingi huko. Umeyaona maisha kwa utofauti hilo hatukatai. Najua kwa sasa wewe watoto wako wanaweza wakaishi huko Canada for whatever reasons, huko ada hazilipwi ni serikali kila kitu. Mzazi kazi yako ni kulipa kodi ya nyumba na utilities tu.

Viwanda na Private companies ziko kibao kiasi kwamba ishu ya kupata cha kufanya wakimaliza vyuo ni wao kuamua tu kukaa kwenye corporate sphere, kwenda kuuza migahawa, kukwangua mabarafu na kutawaza wazee.Maybe sio kazi za hovyo atleast kwa uchumi wa Canada maana hata wazungu wenyewe wa huko hawazitaki.

That being said, wewe unapata wapi guts za kusema kuwa Watanzania wanafanya kazi za laana esp. Boda boda, wasajili line na wauza mboga wanaocheza vikoba? Okay, hizo kazi ni za laana atleast kwa fikra zako lakini ushajiuliza kuna ugumu kiasi gani kwa hapa Tanzania when it comes to making ends meet?

Sidhani kama una idea kwamba graduate aliyemaliza chuo anaetoka familia hohehae anapitia ugumu kiasi gani na fedhea ilioje pale anapokosa ajira na hana mtaji! Usicheze na maisha ya watu kabisa, huna ajira una mke na mtoto huna chanzo cha pesa unafikiria kitakachofuata nini?

Utakaa chini unaangalia familia iangamie? Boda boda ndio quick fix ya maisha yetu ya dhiki walau familia zile na maisha yaende, vikoba ndio quick fix ya mikopo ya benki bila masharti magumu.

Toa solution watu wafanye nini baada ya kuachana na hizo kazi za laana. Sio unaropoka hovyo tu bila kuwa na substance. Tanzania sio Canada watu wanakolipwa dollar 15-20 kwa kazi ya saa 1. Huku unapigishwa mzigo masaa 12 unalipwa elfu 4 na hamna kitu utaongea.
Bodaboda wengi wanakubaliana naye. Wanakubali kuwa kazi yao ni ya laana kwa namna wanavyochukuliwa, pia kwa mambo wayafanyayo kupitia hiyo kaxi.
Zaidi hata wao kuna wanasema wanaiganya kwa kuwa hawaona namna nyingine na kuna wanaoifanya lakini wanapambana zaidi ili waachane nayo.

Ushauri wangu. Watafuteni hao bodaboda ili mbadilishane kazi, wapeni zenu, mchukue za kwao
 
Lema amekuwa mjinga baada ya kupata exposure. Nilidhani kukaa Canada kutamuongezea uwezo wa kutafakari.Anashauri watu wasiokuwa na means zingine wafanye nini?

Tatizo anajiona yeye ndiyo amekuwa mtu wa kwanza Mtanzania kwenda kuishi Canada tena kwa mwaka mmoja tu.Zamani nilikuwa namsikiliza lakini kwa sasa namuona kama limbukeni flani tu.Usije kuta kwa sasa hata chakula atawaambia wampikie kama alichokuwa anakula Canada.
 
Unahitaji akili gani kufanya kazi ya bodaboda au kusajili laini??
Hiyo inayomfanya ajue wapi ni wapi
Kwani hao wenye PhD wamesaidia nini katika kukuza ajira zaidi ya akili za mikopo?

Vijana wanahitaji muwasaidie kama hamtaki wafanye hizo kazi
Sawa haihitaji taaluma kubwa ila suluhu ni ipi?
 
Bodaboda wengi wanakubaliana naye. Wanakubali kuwa kazi yao ni ya laana kwa namna wanavyochukuliwa, pia kwa mambo wayafanyayo kupitia hiyo kaxi.
Zaidi hata wao kuna wanasema wanaiganya kwa kuwa hawaona namna nyingine na kuna wanaoifanya lakini wanapambana zaudi ili waachane nayo.

Ushauri wangu. Watafuteni hao bodaboda ili mbadilishane kazi, wapeni zenu, mchukue za kwao
Huo ndio ushauri wangu kwa ndugu Lema. Naamini hamna mtu atakataa kazi ya kuwa Kamishna wa TRA au Naibu waziri
 
Jamaa ni kama yule kipofu alieona punda

Kufika Canada ameona kama miujiza ameshangaa na ni ushamba tu kuona maisha ya huko ni tofauti

Angekaa miaka 10 angetukana wanaokula Ugali Walahi
Nawajua baadhi ya watu wanapokuja nje na wwkirudi nyumbani hujiona wamebadili maisha na kuwaona wengine kama mbuzi tu

Nimekaa nje karibia miaka 50 ila hata siku moja sijawashangaa maisha ya jamaa zetu huko ila nawaombea always maisha yawabadilikie

Anawatukana watu wakati yeye na familia wanakula hela za wakimbizi
Amejilipua ukimbizi na kujidhalilisha kwa wazungu
Watoto wanasoma kwa jasho la walipa kodi Canada

Badala aseme njia mbadala yeye anayashangaa maisha aliokulia mpaka kafika hapo

Anafananisha Canada na Tanzania anataka wawe sawa

Jamaa kumbe ni mshamba kiasi hicho
Ulimbukeni mbaya sana
Kufika Canada kaanza kutukana washikaji
Mzabeni makofi huyo [emoji1]
Afadhari nyie mliokaa nnje kwa muda mrefu msaidieni apunguze ujuaji wa kuishi Canada kwa muda mfupi.Anakoelekea anageuka kuwa kichekesho
 
Inawezekana Lema ameshindwa kukielezea anachowaza kwa ufasaha.

Bodaboda ni ajira kwasababu vijana hawana namna lakini kwa Taifa masikini binafsi naamini ni upotevu wa nguvu kazi na wakulaumiwa sio Bodaboda bali ni watawala kushindwa kuwa na mipango mizuri na sahihi kwa vijana.

Tunapaswa kuilamu Serikali kwa kushindwa kutanua uwanja na kuifanya jamii kuwa na fursa nyingi zenye vipato na kuboresha maisha ya wati kuliko hivi sasa.
 
Lazima kama Nchi tuhakikishe vijana wanapata ajira za viwandani au mashambani , kule Kyela siku za nyuma kidogo kulikuwa na vijana waliokuwa wakifanya biashara ya kusafirisha mizigo mizito kwa baiskeli , walijulikana kwa jina la NJEMUKE ( kwa kiswahili ni kama kuchemka au kutobweteka )

Hawa walitumia baiskeli ya Phoenex , sijui ilitengenezwa wapi , walibeba mizigo mizito sana huku wakiendesha baiskeli hizi , lakini baadaye wakaanza kupukutika kwa maradhi ya kifua hadi tukaaanza kuwapa elimu kwamba ni bora waingie kwenye kilimo .

Kwahiyo watu waweza kuwa wanafanya jambo linaloonekana linawasaidia lakini kumbe nyuma yake kuna madhara makubwa
Leo mmemgeukia JPM na sera ya viwanda?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nisaidie kumuuliza hii boda yangu nauza nipige mishe gani isiyo ya laama kwa uwezo wangu?
 
Wakuu huyu bwana anayeongea kama amekatwa kichwa Arusha imejaa wauza mitumba kila kona toka ubunge wako mpaka sasa lakini haukusema ni kazi ya laana wala kuonyesha juhudi za kuwasaidia vijana wa Arusha
 
Unaposema boda boda ni kazi ya laana, kusajili laini ni kazi ya kipuuzi hutaki mwanao umuone anaifanya utamfukuza kwako, vikoba ni laana sijui hutaki mkeo ajihusishe navyo kabisa.

From a standing point wewe ni mkimbizi wa kisiasa umebebwa huko Canada for over a year. Umepata PR na familia yako na privileges nyingi huko. Umeyaona maisha kwa utofauti hilo hatukatai. Najua kwa sasa wewe watoto wako wanaweza wakaishi huko Canada for whatever reasons, huko ada hazilipwi ni serikali kila kitu. Mzazi kazi yako ni kulipa kodi ya nyumba na utilities tu.

Viwanda na Private companies ziko kibao kiasi kwamba ishu ya kupata cha kufanya wakimaliza vyuo ni wao kuamua tu kukaa kwenye corporate sphere, kwenda kuuza migahawa, kukwangua mabarafu na kutawaza wazee.Maybe sio kazi za hovyo atleast kwa uchumi wa Canada maana hata wazungu wenyewe wa huko hawazitaki.

That being said, wewe unapata wapi guts za kusema kuwa Watanzania wanafanya kazi za laana esp. Boda boda, wasajili line na wauza mboga wanaocheza vikoba? Okay, hizo kazi ni za laana atleast kwa fikra zako lakini ushajiuliza kuna ugumu kiasi gani kwa hapa Tanzania when it comes to making ends meet?

Sidhani kama una idea kwamba graduate aliyemaliza chuo anaetoka familia hohehae anapitia ugumu kiasi gani na fedhea ilioje pale anapokosa ajira na hana mtaji! Usicheze na maisha ya watu kabisa, huna ajira una mke na mtoto huna chanzo cha pesa unafikiria kitakachofuata nini?

Utakaa chini unaangalia familia iangamie? Boda boda ndio quick fix ya maisha yetu ya dhiki walau familia zile na maisha yaende, vikoba ndio quick fix ya mikopo ya benki bila masharti magumu.

Toa solution watu wafanye nini baada ya kuachana na hizo kazi za laana. Sio unaropoka hovyo tu bila kuwa na substance. Tanzania sio Canada watu wanakolipwa dollar 15-20 kwa kazi ya saa 1. Huku unapigishwa mzigo masaa 12 unalipwa elfu 4 na hamna kitu utaongea.

Huyo muache alivyo. Anadanganya umma mchana kweupe bila ya soni. Eti anasema Canada 90% ya wananchi wake wanamiliki nyumba. Hivi anajua kweli gharama ya kumili nyumba kwa nchi za ulaya na marekaniii.
 
Lema anaweza kuwa na hoja, tatizo ni uwasilishaji wa hoja zake, anavyoongea namuona kama mtu anayejifikiria mwenyewe, anatakiwa aseme sasa badala ya kusajili line wafanye kazi gani nyingine ili wajikimu kimaisha.
 
Back
Top Bottom