Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazo zungumzia jambo lolote la kisiasa, kiuchumi au kijamii lenye maslahi kwa taifa. Makala hizi huja kwa mtindo wa swali na hoja halafu jibu utatoa wewe mwenyewe.
Uteuzi wa Prof. Palamagamba Kabudi una maslahi makubwa kwa taifa hili lililojaa wanasheria vilaza kuanzia serikalini, Bungeni hadi mahakamani. Kwa vile Prof. Kabudi ni mwalimu wa sheria somo la katiba, kazi yake hapo wizarani sio tuu kutekeleza majukumu ya uwaziri, bali atawafundisha sheria na katiba na Mwanafunzi wake No. 1 ni Maza mwenyewe.
Mada ya leo ni pongezi na shukrani kwa Rais Samia kumteua tena Prof. Palamagamba John, Aidan Mwaluko Kabudi, kuwa waziri wetu wa Sheria.
Kwa maoni yangu binafsi, ulimuondoa Prof. Shivji , Prof. Chris Peter Maina, na Prof. Gamalieli Mgongo Fimbo kwenye unguii wa katiba, anayefuata ni Prof. Kabudi, ila tukija kwenye overall the best of the best, Prof. Palamagamba Kabudi is the best, amewapita wote on several avenues.
Prof Kabudi is one of the best brains this country has and has ever had. The best brain inapimwa kwa IQ test. Sisi Tanzania hatuna amplitude test za kupima IQ za watu wetu, tunatumia matokeo ya mitihani ya kidato cha 4, 6 na GPA za chuo kikuu.
Soma Pia: Kwa uteuzi wa Prof. Kabudi katiba na sheria tukubaliane tu Mwambukusi atanyoosha mikono kama ilivyokuwa kwa Lissu na kudhibitiwa
Japo sijui scores za Prof. Kabudi za form 4 na form 6,
ni division 1 ya points ngapi, ila enzi zile kusoma sheria ilikuwa ni lazima uwe na division 1 kali.
Kwenye nchi za Afrika Mashariki, chuo kikuu cha kwanza kufundisha sheria ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kilichoanzishwa October 1961, siku chache kabla ya uhuru wa Tanganyika na kilichukua wanafunzi kutoka nchi zote tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda.
Na mimi pia nilisomea sheria yangu LL.B chuo kikuu cha Dar es Salaam na kupita mikononi mwa Prof. Palamagamba Kabudi, sio tuu kama mwalimu wangu bali yeye ndiye alikuwa supervisor wangu wa my LL.B dissertation, hivyo ni mtu ninayemfahamu kwa karibu.
Wakati nikiwa mikononi mwake mpaka ninamaliza UDSM kuna vitu sikuvifahamu kumhusu Prof. Kabudi, ila mwaka 2011 wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam kinaadhimisha Diamond Jubilee, Prof. Palamagamba Kabudi alitunukiwa tuzo ya outstanding GPA, kwa muda wote wa miaka 50 ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, recoding ya GPA ya Prof. Kabudi, ya 4.9 haukuwahi kuvunjwa mpaka wakati huo, na sikuwahi kusikia kama kuna Mwanafunzi mwingine yeyote amewahi kuifikia, hivyo kuna uwezekano Prof. Kabudi ni one of the best brains of the best that we have!.
Nimesema one of, kwasababu kuna uwezekano tuna best brains kuliko Prof. Kabudi lakini hawakwenda shule hivyo hawajulikani lakini kuna watu wanafanya mambo makubwa kimya kimya, na kuna Watanzania wengi best brains waliosoma au wanaosoma ughaibuni, huwa hawarejei nchini, Wazungu wanawashika and tap their brains for their own gain yaani wanafanya brain drain ya best brains.
Kitu kingine cha ziada kumhusu Prof. Kabudi, ni multi talented, ana kipaji cha usimulizi, oratorio talent, ana kipaji cha kupiga kinanda na ni mcha Mungu aliyelelewa kwenye uchamungu.
Hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Kabudi kuteuliwa Waziri, aliteuliwa na Magufuli kwenye serikali ya awamu ya 5, Rais Samia akamuondoa, sasa ni Samia amemteua tena Wizara ile ile ya sheria.
Mtu kuwa the best brain, high IQ na bingwa wa Katiba ni jambo moja, na uelewa wa katiba, na utekelezaji wa majukumu yake kiweledi ni jambo jingine, swali ni will he deliver this time. Last time alisimamia makinikia, tukaambiwa hakitoki kitu, makinikia yanatoka kama kawa.
Serikali inafanya kazi kwa mtindo wa uwajibikaji wa pamoja, a collective responsibility hata kama jambo fulani haliko sawa lakini waliowengi wanakubaliana nalo, wewe ukiliona haliko sawa na hukubaliani nalo, kanuni ya uwajibikaji wa pamoja inakutaka ukae kimya. Kwa vile yeye ni bingwa wa Katiba, na katiba ndio Biblia yetu na Msahafu wetu, tunamuomba asikubali katiba yetu inajisiwe na vilaza wa sheria wa serikalini, Bungeni na Mahakamani, ili kutunza heshima yake, kuliko kukubaliana na uwajibikaji wa pamoja wa kututungia sheria batili, ni bora akajiweka pembeni kuliko kuunyamazia ubatili huu wa ajabu wa Katiba yetu unaofanywa na wanasheria manguli wabobezi na wabobevu lakini ni vilaza wa katiba!.
Prof. Kabudi ni mwalimu wa somo la katiba pale UDSM, amefundisha mamia ya wanafunzi, kanuni kuu ya katiba inasema Katiba ndio sheria Mama, Sheria nyingine yoyote atakayotenda kinyume cha Katiba ni Sheria batili, Prof. Kabudi asiache huu ubatili wa Katiba yetu na ubatili wa sheria zetu uendelee chini ya nguli wa Katiba. Ijue Katiba kwa Jicho la Mtunga Katiba: Mtunga Katiba alimaanisha nini aliposema "Katiba ni Sheria Mama"? Ni kweli Katiba ni Sheria Mama?
Prof. Kabudi ni miongoni mwa wale ma Amicus Curiae (marafiki wa mahakama) watatu wa ile kesi ya Mtikila ambapo Mahakama Kuu ilitoa hukumu kuhusu ubatili wa Katiba yetu kunajisiwa na sheria batili ya uchaguzi inayokwenda kinyume cha Katiba.
Ushauri wao ni Mahakama isiliingilie Bunge kwenye utungaji wa sheria lakini anajua kuwa Bunge letu lilitunga sheria batili, likafanya mabadiliko batili ya katiba, likauchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu kiubatili.
Mahakama Kuu ikaamuru huo ni ubatili, mabadiliko ya katiba ni batili na sheria hiyo pia ni batili, ila kwa heshima ya Bunge, kwa vile ni Bunge ndilo lililofanya ubatili huo, mahakama ya Rufani ikajizima data na kusema "the Court is not the custodians of the will of the people", yaani Mahakama sio mtunzaji wa mahitaji ya jamii, mtunzaji wa mahitaji ya jamii ni Bunge kwasababu ndilo linawawakilisha wananchi.
Mahakama ya Rufaa ikalirudisha jambo hilo la ubatili wa Katiba na Ubatili wa Sheria kwa Bunge ndilo lirekebishe. Bunge letu mpaka hivi ninavyo andika hapa, halikuwahi kuurebisha ubatili huo wa katiba na ubatili huo wa sheria, hii ina maana mpaka hii leo Tanzania tuna katiba yenye ubatili na tuna sheria batili!.
Rais Samia alipoingia akaunda kikosi kazi kuhusu katiba, watu tukaitwa kutoa maoni yetu kuhusu mustakabali mwema wa siasa za nchi yetu.
Mimi ni miongoni mwa tuliotoa maoni na mimi nilipata fursa kuzungumza mara 3.
Kitu cha ajabu sana ni serikali hii ya Rais Samia ikatunga muswada wa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama kwa kutumia kifungu kile kile batili cha Katiba kilichochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu!.
Bunge letu nalo lilivyo Bunge la ajabu, likaipitisha sheria hiyo hivyo hivyo ilivyo pamoja na ubatili wake, na kumpelekea Rais Samia kuisaini kuwa sheria na Rais Samia ameisha isaini sheria hiyo batili ya uchaguzi na tunayokwenda kuifanyia uchaguzi mkuu wa 2025, huku tukijiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa bila uwepo wa sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa!.
Naamini uteuzi huu wa Prof. Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa sheria ni mpango wa Mungu kwa Tanzania, kumletea Rais Samia watu bold watakao mwambia ukweli kuwa Tanzania imekuwa ikilaaniwa kutokana na dhulma kubwa hii ya kupoka haki za Watanzania za kuchagua na kuchaguliwa zimeporwa na kipengele batili ndani ya katiba yetu na sheria batili.
Kiukweli pale mwanzo Prof. Kabudi alikuwa anamuogopa sana Rais Magufuli hadi kuteleza ulimi kumuita mungu!, na yeye kujiita ameokotwa Jalalani.
Swali sasa ni je this time around atakuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake?. Atamweleza Rais Samia kuhusu ubatili wa Katiba yetu na sheria yetu mpya ya uchaguzi ambayo Rais Samia ameisani hivi majuzi?, au atajizima tena data kama alivyojizima enzi za JPM?
Time will tell.
Mungu Mbariki Prof. Kabudi kusimama kwenye kweli.
Mungu Mbariki Rais Samia kukubali kuambiwa ukweli wa ubatili wa Katiba na Sheria na kuufanyia kazi
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali.
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazo zungumzia jambo lolote la kisiasa, kiuchumi au kijamii lenye maslahi kwa taifa. Makala hizi huja kwa mtindo wa swali na hoja halafu jibu utatoa wewe mwenyewe.
Uteuzi wa Prof. Palamagamba Kabudi una maslahi makubwa kwa taifa hili lililojaa wanasheria vilaza kuanzia serikalini, Bungeni hadi mahakamani. Kwa vile Prof. Kabudi ni mwalimu wa sheria somo la katiba, kazi yake hapo wizarani sio tuu kutekeleza majukumu ya uwaziri, bali atawafundisha sheria na katiba na Mwanafunzi wake No. 1 ni Maza mwenyewe.
Mada ya leo ni pongezi na shukrani kwa Rais Samia kumteua tena Prof. Palamagamba John, Aidan Mwaluko Kabudi, kuwa waziri wetu wa Sheria.
Kwa maoni yangu binafsi, ulimuondoa Prof. Shivji , Prof. Chris Peter Maina, na Prof. Gamalieli Mgongo Fimbo kwenye unguii wa katiba, anayefuata ni Prof. Kabudi, ila tukija kwenye overall the best of the best, Prof. Palamagamba Kabudi is the best, amewapita wote on several avenues.
Prof Kabudi is one of the best brains this country has and has ever had. The best brain inapimwa kwa IQ test. Sisi Tanzania hatuna amplitude test za kupima IQ za watu wetu, tunatumia matokeo ya mitihani ya kidato cha 4, 6 na GPA za chuo kikuu.
Soma Pia: Kwa uteuzi wa Prof. Kabudi katiba na sheria tukubaliane tu Mwambukusi atanyoosha mikono kama ilivyokuwa kwa Lissu na kudhibitiwa
Japo sijui scores za Prof. Kabudi za form 4 na form 6,
ni division 1 ya points ngapi, ila enzi zile kusoma sheria ilikuwa ni lazima uwe na division 1 kali.
Kwenye nchi za Afrika Mashariki, chuo kikuu cha kwanza kufundisha sheria ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kilichoanzishwa October 1961, siku chache kabla ya uhuru wa Tanganyika na kilichukua wanafunzi kutoka nchi zote tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda.
Na mimi pia nilisomea sheria yangu LL.B chuo kikuu cha Dar es Salaam na kupita mikononi mwa Prof. Palamagamba Kabudi, sio tuu kama mwalimu wangu bali yeye ndiye alikuwa supervisor wangu wa my LL.B dissertation, hivyo ni mtu ninayemfahamu kwa karibu.
Wakati nikiwa mikononi mwake mpaka ninamaliza UDSM kuna vitu sikuvifahamu kumhusu Prof. Kabudi, ila mwaka 2011 wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam kinaadhimisha Diamond Jubilee, Prof. Palamagamba Kabudi alitunukiwa tuzo ya outstanding GPA, kwa muda wote wa miaka 50 ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, recoding ya GPA ya Prof. Kabudi, ya 4.9 haukuwahi kuvunjwa mpaka wakati huo, na sikuwahi kusikia kama kuna Mwanafunzi mwingine yeyote amewahi kuifikia, hivyo kuna uwezekano Prof. Kabudi ni one of the best brains of the best that we have!.
Nimesema one of, kwasababu kuna uwezekano tuna best brains kuliko Prof. Kabudi lakini hawakwenda shule hivyo hawajulikani lakini kuna watu wanafanya mambo makubwa kimya kimya, na kuna Watanzania wengi best brains waliosoma au wanaosoma ughaibuni, huwa hawarejei nchini, Wazungu wanawashika and tap their brains for their own gain yaani wanafanya brain drain ya best brains.
Kitu kingine cha ziada kumhusu Prof. Kabudi, ni multi talented, ana kipaji cha usimulizi, oratorio talent, ana kipaji cha kupiga kinanda na ni mcha Mungu aliyelelewa kwenye uchamungu.
Hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Kabudi kuteuliwa Waziri, aliteuliwa na Magufuli kwenye serikali ya awamu ya 5, Rais Samia akamuondoa, sasa ni Samia amemteua tena Wizara ile ile ya sheria.
Mtu kuwa the best brain, high IQ na bingwa wa Katiba ni jambo moja, na uelewa wa katiba, na utekelezaji wa majukumu yake kiweledi ni jambo jingine, swali ni will he deliver this time. Last time alisimamia makinikia, tukaambiwa hakitoki kitu, makinikia yanatoka kama kawa.
Serikali inafanya kazi kwa mtindo wa uwajibikaji wa pamoja, a collective responsibility hata kama jambo fulani haliko sawa lakini waliowengi wanakubaliana nalo, wewe ukiliona haliko sawa na hukubaliani nalo, kanuni ya uwajibikaji wa pamoja inakutaka ukae kimya. Kwa vile yeye ni bingwa wa Katiba, na katiba ndio Biblia yetu na Msahafu wetu, tunamuomba asikubali katiba yetu inajisiwe na vilaza wa sheria wa serikalini, Bungeni na Mahakamani, ili kutunza heshima yake, kuliko kukubaliana na uwajibikaji wa pamoja wa kututungia sheria batili, ni bora akajiweka pembeni kuliko kuunyamazia ubatili huu wa ajabu wa Katiba yetu unaofanywa na wanasheria manguli wabobezi na wabobevu lakini ni vilaza wa katiba!.
Prof. Kabudi ni mwalimu wa somo la katiba pale UDSM, amefundisha mamia ya wanafunzi, kanuni kuu ya katiba inasema Katiba ndio sheria Mama, Sheria nyingine yoyote atakayotenda kinyume cha Katiba ni Sheria batili, Prof. Kabudi asiache huu ubatili wa Katiba yetu na ubatili wa sheria zetu uendelee chini ya nguli wa Katiba. Ijue Katiba kwa Jicho la Mtunga Katiba: Mtunga Katiba alimaanisha nini aliposema "Katiba ni Sheria Mama"? Ni kweli Katiba ni Sheria Mama?
Prof. Kabudi ni miongoni mwa wale ma Amicus Curiae (marafiki wa mahakama) watatu wa ile kesi ya Mtikila ambapo Mahakama Kuu ilitoa hukumu kuhusu ubatili wa Katiba yetu kunajisiwa na sheria batili ya uchaguzi inayokwenda kinyume cha Katiba.
Ushauri wao ni Mahakama isiliingilie Bunge kwenye utungaji wa sheria lakini anajua kuwa Bunge letu lilitunga sheria batili, likafanya mabadiliko batili ya katiba, likauchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu kiubatili.
Mahakama Kuu ikaamuru huo ni ubatili, mabadiliko ya katiba ni batili na sheria hiyo pia ni batili, ila kwa heshima ya Bunge, kwa vile ni Bunge ndilo lililofanya ubatili huo, mahakama ya Rufani ikajizima data na kusema "the Court is not the custodians of the will of the people", yaani Mahakama sio mtunzaji wa mahitaji ya jamii, mtunzaji wa mahitaji ya jamii ni Bunge kwasababu ndilo linawawakilisha wananchi.
Mahakama ya Rufaa ikalirudisha jambo hilo la ubatili wa Katiba na Ubatili wa Sheria kwa Bunge ndilo lirekebishe. Bunge letu mpaka hivi ninavyo andika hapa, halikuwahi kuurebisha ubatili huo wa katiba na ubatili huo wa sheria, hii ina maana mpaka hii leo Tanzania tuna katiba yenye ubatili na tuna sheria batili!.
Rais Samia alipoingia akaunda kikosi kazi kuhusu katiba, watu tukaitwa kutoa maoni yetu kuhusu mustakabali mwema wa siasa za nchi yetu.
Mimi ni miongoni mwa tuliotoa maoni na mimi nilipata fursa kuzungumza mara 3.
Kitu cha ajabu sana ni serikali hii ya Rais Samia ikatunga muswada wa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama kwa kutumia kifungu kile kile batili cha Katiba kilichochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu!.
Bunge letu nalo lilivyo Bunge la ajabu, likaipitisha sheria hiyo hivyo hivyo ilivyo pamoja na ubatili wake, na kumpelekea Rais Samia kuisaini kuwa sheria na Rais Samia ameisha isaini sheria hiyo batili ya uchaguzi na tunayokwenda kuifanyia uchaguzi mkuu wa 2025, huku tukijiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa bila uwepo wa sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa!.
Naamini uteuzi huu wa Prof. Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa sheria ni mpango wa Mungu kwa Tanzania, kumletea Rais Samia watu bold watakao mwambia ukweli kuwa Tanzania imekuwa ikilaaniwa kutokana na dhulma kubwa hii ya kupoka haki za Watanzania za kuchagua na kuchaguliwa zimeporwa na kipengele batili ndani ya katiba yetu na sheria batili.
Kiukweli pale mwanzo Prof. Kabudi alikuwa anamuogopa sana Rais Magufuli hadi kuteleza ulimi kumuita mungu!, na yeye kujiita ameokotwa Jalalani.
Swali sasa ni je this time around atakuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake?. Atamweleza Rais Samia kuhusu ubatili wa Katiba yetu na sheria yetu mpya ya uchaguzi ambayo Rais Samia ameisani hivi majuzi?, au atajizima tena data kama alivyojizima enzi za JPM?
Time will tell.
Mungu Mbariki Prof. Kabudi kusimama kwenye kweli.
Mungu Mbariki Rais Samia kukubali kuambiwa ukweli wa ubatili wa Katiba na Sheria na kuufanyia kazi
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali.