Asante Rais wetu kwa hotuba yako, Watanzania tupo tayari kuhesabiwa

Asante Rais wetu kwa hotuba yako, Watanzania tupo tayari kuhesabiwa

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Kwanza pole kwa kazi mh Rais wetu na Asante kwa Hotuba yako ya kutuhamasisha ili tujiandae kuhesabiwa, mh Rais napenda kukuambia kuwa watanzania huku mitaani wamehamasika vizuri na wameelewa umuhimu wa sensa na wapo tayari kuhesabiwa

Mh Rais napenda kukufahamisha pia kuwa zoezi Hilo limepokelewa na watu wote kwa mikono miwili bila kujali itikadi ya vyama vya siasa, kwani sisi kwa sisi tunahamasishana kuwepo nyumbani au kuacha mtu atakayekuwa na uelewa na taarifa zote zinazohitajika, kwa kuwa pia tumeshayaona maswali husika kupitia mitandao, kwa hiyo ushirikiano utakuwa mkubwa utakao tolewa na kupewa makarani wa sensa.

Asante kwa kujenga umoja wa kitaifa ulio Rahisisha watu kuwa na hamasa maana sote Ni wamoja na wote tunaona zoezi hili Ni letu sote kwa manufaa yetu wote kwa pamoja katika kupanga mipango ya maendeleo kwa Taifa letu.

Mwisho ni ushauri wangu kwako mh Rais kutoa maagizo kwa waratibu wa zoezi hili ngazi za mikoa wahakikishe makarani wote wanapatiwa vifaa vyote muhimu katika kufanikisha zoezi hili, pia kutomfumbia macho atakayeleta dosari katika zoezi hili nyeti na muhimu kwa mstakabari wa Taifa letu, Asante.
 
Kakutuma uke hapa KUTOA uzi wa kusifia.??
Mie kazi yangu inanihitaji saa 10 kuwa nimetoka sivyo usafiri mjini hakuna!!
Kwani unaishi peke yako hapo nyumbani, Kama unaishi peke yako acha hata mawasiliano kwa jirani yako wa karibu ili kulahisisha upatikanaji wa taarifa zako atakapopita karani wa sensa
 
Yaani ulivyo tusemea, kama kuna mtu anatoka dunia nyingine anaweza akashangaa!
Kumbe asilimia kubwa ya wananchi wanaona hilo zoezi lenyewe kama ni la kidwanzi tu.

Maana wanajua kitakacho tokea baada ya hapa ni kuanzishiwa kwa tozo mpya ya kuhesabiwa, ili kufidia gharama ya posho mlizogawana.
 
Yaani ulivyo tusemea, kama kuna mtu anatoka dunia nyingine anaweza akashangaa!
Kumbe asilimia kubwa ya wananchi wanaona hilo zoezi lenyewe kama ni la kidwanzi tu...
Acha mawazo potofu, sensa si kwa ajili ya tozo Bali kwa ajili ya mipango ya maendeleo yetu wenyewe Kama Taifa
 
Karani wa sensa ushalambishwa asali na vijisenti vya sensa umepata upofu wa fikra kabisa. SMH
Hapana Wala Mimi siyo karani Bali kijana mzalendo wa nchi yangu ambaye natambua umuhimu wa Sensa kwa maendeleo ya Taifa letu

Tujiandae kuhesabiwa ili tujuwe tunapangeje mipango yetu ya kimaendeleo kupitia serikali yetu
 
Acha mawazo potofu, sensa si kwa ajili ya tozo Bali kwa ajili ya mipango ya maendeleo yetu wenyewe Kama Taifa
Mawazo potofu ya wapi! Hivi kuna jambo lolote kwa sasa hao viongozi wako wanaliwaza vichwani mwao zaidi ya kuanzisha kila aina ya tozo ili kuwaumiza wananchi?
 
Hatari, wana JF tuukatae umasikini kwa nguvu zetu zote na akili zetu zote ili vizazi vyetu vijavyo visije kuwa watumwa kama mleta uzi.
Ndio maana unaona juhudi za mh Rais kuhakikisha kuwa anatutoa katika umasikini na kutuinua kiuchumi, ili hayo yafanikiwe tujiandae kuhesabiwa ili kuliwezesha mh Rais wetu katika upangaji wa mipango ya maendeleo, huwezi ukapanga mipango wakati huelewi unaongoza Taifa la namna gani, mh Rais wetu mpendwa anataka maendeleo yatakayopatikana yakamguse kila mmoja wetu, haraka mtu yeyote Yule aachwe nyuma,

Ili hili lifanikiwe hatuna budi kutoa ushirikiano wetu katika zoezi hili la Leo kuhakikisha kuwa tunahesabiwa
 
Mawazo potofu ya wapi! Hivi kuna jambo lolote kwa sasa hao viongozi wako wanaliwaza vichwani mwao zaidi ya kuanzisha kila aina ya tozo ili kuwaumiza wananchi?
Sensa siyo kwa ajili ya tozo ndugu yangu, Sensa Ni kwa ajili ya mipango yetu ya maendeleo, tuhesabiwe ili maendeleo yatakayo pangwa yakamguse kila mmoja wetu

Tumuunge mkono mh Rais wetu mpendwa kwa kuhesabiwa Leo ili apate picha na Hali halisi tuliyo nayo wananchi wake anao tuongoza
 
Sensa siyo kwa ajili ya tozo ndugu yangu, Sensa Ni kwa ajili ya mipango yetu ya maendeleo, tuhesabiwe ili maendeleo yatakayo pangwa yakamguse kila mmoja wetu

Tumuunge mkono mh Rais wetu mpendwa kwa kuhesabiwa Leo ili apate picha na Hali halisi tuliyo nayo wananchi wake anao tuongoza
Hiyo ilikuwa zamani. Ila kwa akili za viongozi wako wa sasa, hii sensa kwao ni fursa nyingine ya kuja kuwatesa wananchi kupitia tozo kandamizi! Ubunifu wa kutafuta vyanzo vingine vya mapato hawana! kwa sasa wanachowaza ni tozo pekee na kukopa kwa mabeberu.

Nakuhakikishia mkiendelea kumuendekeza yule mpiga dili wenu mwenye dharau na majivuno, basi huyu mama yako atachukiwa mpaka siku yake ya kiama.
 
Chawa kazini
Hapana Mimi siyo chawa ndugu yangu mwana nyanda za juu kusini, Jiandae kuhesabiwa kwa maendeleo ya Taifa letu, tuhesabiwe ili mh Rais wetu mpendwa ajuwe namna keki ya Taifa unapaswa iende wapi na wapi, jiandae kutoa ushirikiano ili mh Rais wetu apate picha na uhalisia wa mambo yalivyo na namna ya kupanga mipango ya maendeleo itakayo mgusa kila mmoja wetu

Jiandae kuhesabiwa ili mipango itakayo pangwa ikatoe fursa kwa kila kundi hapa nchini pasipo kuachwa nyuma au kusahaulika kiuchumi, sensa siyo kwa ajili ya kusajili wanachama wa vyama vya siasa au mpira Wala tozo Bali kwa manufaa yetu wenyewe watanzania
 
Back
Top Bottom