Uchaguzi 2020 Asante sana Rais Magufuli, kiukweli ninashukuru

Uchaguzi 2020 Asante sana Rais Magufuli, kiukweli ninashukuru

Nami namtizama kwa umakini kama kuna kitu mbele yake anasoma, lakini si kweli maana anaongra akiwatazama wasikikizaji.
Kama ni kweli hana chochote kinacho mwongoza Kusoma hotuba yake, Huyu atakuwa si Binadamu wa kawaida! Amini mkuu!

Na hiyo, kama ni kweli tafadhari watu wanaohusika kuwaingiza watu katika vinyang'anyilo za watu waliovunja record mbalimbali kuhusu vitu tendwa hapa duniani, wafanye Yao aisee, huyu si Binadamu wa kawaida
 
Nina shaka,nyie ndio wale wavurugao amani au wanaotaka kutumia mianya fulani kwa malengo yao Binafsi

Uhuru bila Mipaka,ni sawa na Ujambazi tu
Yajayo.......... Yanafurahisha......... Alisikika mtu akisema bungeni saiz hapa.
 
Ni mtu wa aina pekee kwani amejaliwa vipaji vingi sana. Leo ananishangaza kuhutubia Bunge bila kusoma na kwa takwimu.
Mkuu kwamba huoni akisoma au.... Labda hujaona anasomea wapi 😂
 
Ninapenda tumia muda huu kukushukuru Mzee wangu Rais wa Jamuhuri ya Muungano ya watu watanzania kwa safari ndefu ya miaka mitano kutuongoza wa Tanzania hasa ktk kipindi kigumu chakubadilisha fikra za watanzania nakutufanya kufanya kazi kwa bidii na kutopenda kuwa omba omba. Hii haikuwa Rahisi na kamwe haitokuwa rahisi kwa awaye yote.

Mengi yametokea mengi yamesemwa ila ukweli utabakai kuwa ukweli wewe ni aina ya kiongoz umesimamia kwa mkono wa chuma yale kama kiongoz una yaamini na uwenda sisi kama taifa kuna nyakati tumekuchukia na kusema huyu nikiongoz asie na huruma kwa watu wengine au kusema hata wewe sio baba mwenye huruma ila siri na ukweli ya kile umekisimamia itabaki kuwa kwako na vyombo vya ulinzi na usalama.

Palipo na ukweli tuseme ukweli hili taifa lilikuwa ktk mahali palimuhitaji Rais kama wewe na nikweli chamoto tumekiona ila pamoja na yote umetufungua macho wengi na sasa tuna elewa maana ya vijana kuwa wabunifu na kuchapa kazi.

Rushwa ni adui wa haki na kwa hakika kwa maneno mafupi sana waliokula rushwa cha moto wamekiona na uwenda watasimulia vizazi vyao yale yamewakuta kwa kupenda Rushwa.

Uzembe na ulevi wa madaraka ulifanya Raia waka ktk msongo wa mawazo wasijuwe nani wakuwasaidia leo adabu nikama zote na Raia ndio mfalme afikapo ktk ofisi ya serikali.

Mafisadi wa ardhi walitesa Raia masikini na kufanya masikini kukosa mahali pakupeleka malalamiko ofisi za ardhi zilijaa rushwa na mafisadi walizitumia ofisi za ardhi kujinufaisha kwa ardhi isio kuwa yako ila umesimama pitia Waziri Lukuvi na ardhi pamekuwa mahali pakuheshimika. Binafsi nishuhuda wa haya na mara kadha pale ikulu tukija kama raia wakawaida tulipata huduma bora sana.

Kwa miaka mitano umeme umekuwa vizuri sana kiukwel kama sio wewe kusimamia kodi zetu na ruzuku unawapa tanesco umeme ungekuwa janga na bill kupanda bila sababu. Leo umeme ni historia kukatika na walanguz wa magenerator wamekuwa wanyonge.

Umeme wa Rea vijijini umesaidia sana kutanuwa upatikanaji wa umeme vijijini na sasa vijiji vingi vina umeme yule kijana alikuwa anamiliki smart phone mjin pia sasa anamiliki kijijini. Hakuna tofauti ya kijijini na mjini.

Umefanya mambo mazuri mengi ila usisahau kutengeneza akina Magufuli wengi. Marekani ina marais zaid ya arobain na tati laikin wanao kumbukwa hawazidi watano hivyo sio bure na wewe ukaingia ktk historia za taifa hili kwa kuwa Rais ulie thubutu na ukafanikiwa.
Njaa za watu ni mbaya sana wanaweza hata kuua ilimradi matumbo yashibe.
 
Back
Top Bottom