Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!

Sijakuelewa hapa una maanisha nini!!
 
Acha uchawa! Unaweza kusimama mbele ya Mh. Mbilinyi aka Sugu na kusema hilo kweli? aliyepigwa mpaka sasa afya yake haijatengemaa. Unaweza kusema kwa watt waliotekwa na kutupwa mahututi katika mapori baada ya vipigo!. Acha unafiki!!! Wewe ni wakiume lakini ikifika 2025 uchaguzi kwa unafiki na uchawa utavaa hijab nyekundu!!!!
 
Sijakuelewa hapa una maanisha nini!!
Mkuu Stuxnet , pole sana, baadhi ya mabandiko yangu sio ya watu wote, ni coded message kwa watu maalum tuu.
Ngoja nikusaidie to decode
Hii ni zawadi yangu kwa Birthday ya Mama leo, nilipanga kumpa wiki ya mwisho ya October 2025,
Kila wiki ya October kila baada ya miaka 5 huwa kuna fanyika nini?. Kuna wengi wamepania kumzawadia zawadi fulani Rais Samia
Ili zawadi hii iwe na manufaa kwake, nikisubiri mpaka hiyo 2025, it might be a bit too little too late, kuna ubaya hiyo zawadi, kutolewa mapema mwaka huu ili iweze kutumika mwaka kesho?.
Nikisubiri hiyo 2025 it might be a bit too little too late.
Zawadi yenyewe ni Salaam tuu za Birthday zenye ki parcel fulani!
Zawadi yenyewe ni ki parcel fulani
Hiyo ndio parcel ya zawadi yenyewe
Hivyo endelea na ule mpango wako wa 2025!, na Watanzania wanaolitakia mema taifa letu hili, wote tutakuwa Tuko nyuma yako,
Tuko pamoja nawe,
Tuko nawe!.

Mungu Akubariki Sana!.
HBD Mamaa!.
Paskali
Natumaini umeelewa

P
 
Ameliponya amekuwa Mungu??? Acheni ujinga basi!!!
 
Tusonge mbele tu kwa kuwa mimi si mlengwa haina shida
 
Tusonge mbele tu kwa kuwa mimi si mlengwa haina shida
Asante, sio lazima kusoma kila kitu humu, kuna mabandiko mengine yanakuwa yana kimo fulani, unajikuta yamekuzidi kimo, lakini as days go by na wewe unazidi kukua, hivyo utafikia stage unayafikia, vinginevyo jipitie tuu, mfano ni bandiko kama hili Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa! sio la kitoto, watoto wote hawawezi kupata kitu hivyo unajipitia zako.
P
 
Una hulka kama za Mwijaku na Baba Levo. Inasikitisha sana.
Kila mtu ana levels zake anazowaweka watu, kama mimi kwako ndio umeniweka levels za hao machawa, then hiyo ndio level yangu according to you, I accept. Hao machawa wako wanaweza kushuka na mada kama hizi?.
View: https://youtu.be/kws2YUVqNq0?si=86Z4Lyd9UVXV2Cko na hapa
View: https://youtu.be/Ta0URHvUlko?si=mOGUZE6vfppl03krNa sio na Rais wetu tuu, hata marais majirani zetu
View: https://youtu.be/VS3dGmNY1XQ?si=otyjzZ5p2aNGvNyETuheshimiane jemeni!.
P
 
Sina shaka na uwezo wako. Unafanya makusudi kujishushia heshima kwasababu ya tumbo lako ndio maana nimesikitika
 
Sina shaka na uwezo wako. Unafanya makusudi kujishushia heshima kwasababu ya tumbo lako ndio maana nimesikitika
No sijishushi bali mimi ni mtu wa chini sana ground zero, tena kazi yangu ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, silipwi na yeyote, najitolea tuu, na sasa pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea kwa kujitolea kwa kujikita kwenye utoaji elimu ya katiba, sheria na haki kwa umma kwa kujitolea na solipwi na yeyote
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=P5ugJmkuULieyX5E all that I do is noble job ni kazi ya kanisa, kazi ya kujitolea kwa kujitoa kutumikia watu bure kabisa.
P
 
Sawa, fanya self reflection kama ni sahihi kutoa makala kama hizi ambazo mnatukuza watu.
 
Absolutely. Tatizo threads zako zina contradict each other. Pascal wa asubuhi na jioni ni watu wawili tofauti.
Atadai anaongea kwa code hivyo sisi wa mitaani hatuna uwezo wa kumwelewa hadi atutafsirie anachosema!
 
Absolutely. Tatizo threads zako zina contradict each other. Pascal wa asubuhi na jioni ni watu wawili tofauti.
Kuna kitu kinaitwa reality na perception, reality ni mtu ukweli wa jinsi ulivyo, na perception ni jinsi watu wanavyo ku perceive ulivvyo kutokana na perception yao, sasa kama wewe unajijua the reality ukoje, you will keep being the way you are bila kujali how people perceived you. Mfano mimi najijua kabisa sio chawa, sijawahi kuwa chawa, ila nikisifu mazuri ya ukweli yanayofanyika, some people perceives kama ni uchawa, kwasababu mimi najihua sio chawa, I just let it go.
Pasco ni yule yule juzi jana na leo.
P
 
Hii kadi unaweza kucheza kwa watu wenye uelewa mdogo bahati mbaya I'd like to think I'm not one of them. Bwana Pascal with all due respect we can see right through your BS. Ukitaka kujidanganya that's fine lakini maandishi unayoandika yatakuja kusomwa na kuchambuliwa na vizazi vyako huko mbeleni. All the best.
 
Thanks, na kwenye maandishi ndiko ninakolalia, mfano angalia tarehe ya bandiko hili and rationale behind it Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!
P
 
Pascal Mayalla unakumbuka zamani ukiwa unatangaza nikiripoti kutoka ITV miki ni pasco mayalla wa ITV .

SO ningeomba ubakie hivyo hivyo uache uchawa kwa hawa viwavi jeshi . Hakuna mtu anayeponya kama Mungu ni yeye tu anaponya hawa wengine kama rais haponyi. Kitu. Jingine hupendezei uchawa unapendezea haki.
NChi hii haina maji,haina hospitali za kutosha,haina miundo mbinu unaenda mahali utasema mnadhurika,sijasomea mipango miji ila ,ninachojua kuna mji mkuu ,mji wa kati na vijijini. Samia na Serikali yake hawajafikia vijijini ni wamefika miji ya kati kuelekea huko afanye utafiti atajua bado anakazi za kufanya asopende kuteua tu apende kwenda kujionea hali halisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…