Asanteni Radio One, Watangazaji Bora Afrika Farhia Middle na Abubakary Sadick kwa Kuniheshimisha na Kuuheshimisha Mtandao wa JamiiForums leo

Aiseee mbona siwaoni au ngoja niwasubiri afu ntajua cha kuwafanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umezaliwa cku aliyofariki mwanangu leo Niko nyumbani naangalia picha zake video alifariki 9:30 mchana nasubiria muda ufike nibusu pichazake nimwombee kwamungu
Umeandika kwa Uchungu sana.
Pole sana mwamba ..
 
Apost hicho kipande walichomtaja.
 
Onelove peace muombee
 
Apost hicho kipande walichomtaja.
Sina muda huo wa Kupoteza ila ninachojua leo Radio One na Watangazaji hao Wameniheshimisha kwa Kunitaja mwisho wa Kipindi walipokuwa Wanaaga pamoja na Kuutaja Mtandao huu wa JamiiForums.

Kwahiyo niwadanganye au nidanganye Kwenu hapa ili iweje na kwa faida gani? Wanafiki na Waswahili wakubwa GENTAMYCINE kutajwa Hewani Redioni mnakataa na hamuamini ila mngesiikia kuwa nimetajwa kwa mabaya ( ubaya ) ndiyo mngeamini na hata Kufurahia pia.
 
Hicho kipindi bahati mbaya huwa sikipendi kimekaa kiumbea umbea, hongera kwa kutajwa huko.
 
Hicho kipindi bahati mbaya huwa sikipendi kimekaa kiumbea umbea, hongera kwa kutajwa huko.
Ukiona hukipendi Kipindi hicho jua Wewe ni Mpumbavu, Muhuni, Mnafik, mwana Yanga SC na Mgonjwa wa Akili.
 
Kipindi ni kizuri ila abubakari sadiki hakiwezi, naona hata Farhia amegundua huyu kijana ni mswahili anadakiadakia maneno wakati mwingine farhia anaongea cha maana anadakiadakia tu, hiki kipindi Mwaipaya ndo alichokiweza, kama kuna uwezekano wajaribu kutafuta mtu mwingine ashirikiane na Farhia lakini huyu abubakari sadiki ni zero kabisa hajaweza kuvaa viatu vya mwaipaya,kwanza anaonekana hana hata upeo wa maisha ni kijana wa kitaa tu.....ili kurudisha ubora wa hichi kipindi mtoeni huyu kijana mapema

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Uandishi wako na huu Uwasilishaji wako unaonyesha kuwa Wewe una Chuki zako tu binafsi na Abubakary Sadick na kwamba huenda ulikuwa na lako Jambo na aliyekuwepo Mtangazaji Abdallah Mwaipaya ( sasa DC wa Mwanga )

Halafu ni Upuuzi uliopitiliza wa Kumtaka Mtu mpya akiingia mahala basi awe anamuigiza Yule aliyemkuta mkisahau ya kwamba kila Mtu ana 'taste' yake pale mahala ambako huwa yuko.

Ndiyo nyie nyie Wavivu wa Kufikiri na wenye Ubongo unaotikisika mlikuwa mnataka Hayati Rais Dkt. Magufuli awe anaongoza kwa 'Style' ya Rais Mstaafu Kikwete mwisho wa Siku alipokuwa anaongoza kwa anavyojua Yeye mkaanza Kumchukia na mpo ambao hata mlifurahia Kifo chake ila cha Kushangaza leo mnamkumbuka na Kumlilia.

Hoja yako ya kusema au kushauri Uongozi wa Radio One umtafute Mtu mwingine kwakuwa humped tu Abubakary Sadick ni ya Kitoto na Dhaifu sana. Kwa Taarifa yako tu ni kwamba Wabobezi wa Utangazaji na Mabosi hapo ( pale ) Radio One walishajaribisha Watangazaji wengi katika hicho Kipindi ila wengi Wao walikuwa hawatengenezi 'Chemistry' nzuri na Dada Farhia Middle na wakawa 'Wanatuboa' tu ila alivyokuja Mtangazaji huyo Mkongwe Abubakary Sadick na aina ya Utangazaji wake wenye 'Comedy' fulani ndani yake, Uchokozi wa Mada, Udadisi wa Mada na Utani wake akaonekana kuwa anaweza na kweli anaweza tena binafsi namuona amemzidi Vitu kadhaa DC wa Mwanga na mwana Yanga SC Mwenzako Abdallah Mwaipaya ambaye ndiyo Mwanzilishi Mwenza wa Kipindi hicho cha Mazungumzo ya Familia akiwa na mwana Simba SC Mwenzangu Dada Farhia Middle.

Kama Balozi Kazi yangu ni Kuwatetea!!!
 
Basi tufunge mjadala Abubakar sadik, anafaa ila waskilizaji na wafuatiliaji wa hichi kipindi wataendelea kupungua hapo ndipo management ya radio one itazinduka

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…