ASAS kuwapa Polisi Gari na Pikipiki ni kutaka kuiweka mfukoni dola

ASAS kuwapa Polisi Gari na Pikipiki ni kutaka kuiweka mfukoni dola

Huu mtindo wa serikali kupokea misaada toka kwa kampuni au taasisi zisizo za kiserikali au mtu binafsi ni kutengeneza mianya ya ukwepaji kodi kwa dhana ya kulipa fadhila kwa kupokea hiyo misaada. Makampuni yataona ni kawaida kuisaidia serikali. Hayo makampuni kama yanaona ya misaada yapeleke kwa taasisi zingine zisizo za kiserikali, zipo za kuhudumia watoto, wazee na makundi mengine yanayohitaji misaada. Kwanza msaada huo ni kituko, ni sawa na kupeleka maji kwenye bahari kwa kutumia kikombe cha chai ili ijae maji wakati serikali ni kubwa na ina rasilimali nyingi kuweza kuhudumia vyombo vyake
 
Sidhani kaka ni sawa kwa hiki kilchofanyika tena hadharani, Kampuni ya ASAS kutoa msaada wa Pikipiki na Gari kwa Jeshi la Polisi sio jambo la kukaliwa kimya. Hii ni taasisi ya Utoaji Haki inapotokea wanatoa msaada huo je wakipatwa na makosa yanayohitaji Polisi kuwawajibisha watachukua hatua sawa au watawalinda kwakuwa ni wadau wao?

Kwenye nchi zinazofuata misingi ya Utawala Bora hili jambo lilitakiwa kupingwa kwa nguvu zote. Kitendo hicho kinamaanisha ASAS watakuwa hawachukuliwi hatua kwa lolote.
Mara zote imekuwa hivyo
 
Back
Top Bottom