Ashugulikiwe aliyepo nyuma ya Kagame na M23 yake kukomesha umwagaji damu mashariki ya DRC

Ashugulikiwe aliyepo nyuma ya Kagame na M23 yake kukomesha umwagaji damu mashariki ya DRC

Wewe ndiye umetumia akili?
Ndiyo, wewe je?? Vikwazo havijaleta madhara kwa Urusi?? Jibu kwa kutumia akili.

 
Miguu utadhani ya Flamingo.
1738589405520.jpg
 
Fikiria hawa ni raia wameuawa na M23 huku askari wetu wawili wa JWTZ na askari wanne wa South Africa waliokuwa wakiwalinda raia nao wakiuawa kikatili.

Nchi ya Congo ingekuwa haina madini na rasilimali zingine sidhani kama huyu Paul Kagame na Kaguta Museveni wangekuwa na kashfa ya kuwa nyuma ya Mzozo wa DRC wakisizingia kutafuta waasi wanaopinga serikali zao waliokimbilia huko. Ukiona dikteta yoyote anakaa muda mrefu madarakani halafu huoni mataifa ya Ulaya yakimlalamikia kaa ukijua kuwa dikteta huyo ni kibaraka wao. Ndivyo ilivyokuwa kwa Mubutu Sese seko.

Mobutu alikuwa kibaraka wa mataifa ya magharibi na walimuweka baada ya mataifa hayo kumuua baba wa taifa la Congo DCR Patrice Lumumba aliyepigania uhuru wa taifa hilo kutoka kwa wabelgiji. Walifanya hivyo ili iwe rahisi kuvuna rasilimali za Congo kwani ilikuwa ngumu kuvuna chini ya Patrice Lumumba ambaye alikuwa ameshaanza kuwafungia vioo. Baada ya kumuua Patrice Lumumba walianza kuvuna rasilimali za Congo kwa wanavyotaka huku wakimlinda Mobutu. Licha ya udikteta wa Mobutu wa kuteka na kuua wapinzani wake hawa nchi za magharibi hawajawahi kumkemea kwa sababu alikuwa kibaraka wao huku wakimtajirisha.

Kuna wakati akina Nyerere, Kaunda na wengine walimtenga Mobutu kwenye Mulungushi Club. Wakati huo marais wa nchi za kusini mwa Africa ambao kwa sasa ni SADC waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa nchi za kusini mwa Africa waliunda Club iliyoitwa Mulungusi ambayo kazi yake ilikuwa ni mikakati ya kusaidia nchi za kusini mwa Africa ambazo zilikuwa hazijapata uhuru ikiwemo Zimbabwe na South Africa.

Mobutu kibaraka wa nchi za magharibi akawa anavujisha siri kwa mabwana zake mikakati yote ya Mulungusi Club. Inabidi mwalimu Nyerere na wenzake wamteme.

Baada ya anguko la Mobutu sasa Kagame akabadili nafasi hiyo ya ukibaraka wa kuwatumikia mataifa ya magharibi kufanya machafuko mashariki mwa Congo ili kupata mwanya wa kuvuna rasilimali za nchi hiyo katika eneo hilo. Kisingizio cha Kagame ni kuwatafuta waasi wa kihutu waliokimbilia Congo tangu wakati wa mauaji ya kimbali nchini Rwanda mwaka 1994. Ukweli ni kwamba huu ni uongo na waasi hao wanatumika kama kichaka tu cha kuficha uovu wa Kagame na wafadhili wake wa nchi za magharibi.

Leo tujiulize madini yanayouzwa kwenye soko la dunia kutokea Rwanda yanatoka wapi kama sio Congo? Kwanini Kagame anakuwa dalali wa kumwaga damu za waafrica wenzake kwa faida ya wazungu wa mataifa ya magharibi? Kagame anasoma biblia hivi hajui kwamba damu ina tabia ya kisasi?

Ukimuona mbuzi juu ya mti ujue kapandishwa. Kagame ni mbuzi aliyepandishwa juu ya mti. Huyo aliyempandisha ndiye ashugulikiwe. Kwa hiyo ukitaka kutatua tatizo dili na chanzo cha tatizo na sio tatizo. Viongozi wa SADC na Africa walipaswa kushugulika na aliye nyuma ya Kagame hizi nchi za magharibi ikiwemo ufaransa ambazo ndio zinampa kiburi kama walivyokuwa wanampa kiburi Mobutu. Kwa bahati mbaya nchi za SADC zinadili na Kagame huku zikiogopa kudili na boss wa Kagame nchi za magharibi kwa sababu ya kukosa mikopo na misaada.

Kama Africa bado tuna safari ndefu sana maana ndani yake wapo viongozi waoga, wezi na mamluki wa nchi za magharibi.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Maelezo marefu yanatolewa na mtu anayewafahamu vizuri viongozi wa kiAfrika namna walivyo na haiba zenye kushabihiana!

Kwa taarifa yako ni kwamba, viongozi wa Afrika mostly ni kama nyumbu.

Nyumbu hawezi kutoa msaada kwa nyumbu mwenzake aliyekunjwa shingo na simba, kwa sababu, aliyeangushwa kuliwa si yeye, kwa hiyo jambo hilo linakuwa halimhusu.

Hata hicho kikao cha SADC na EAC kilichoitishwa Dar siku ya Juma mosi, kama hakitaweza kutoka na agenda moja yenye maamuzi ya kimshikamano, basi tujue kuwa kwa sababu madhila ya raia wa Congo DR si yao, hivyo hayawahusu kuyashughulikia kwa ukamilifu.

Uamzi uliotakiwa kufanywa kukomesha longolongo pamoja na kutoa msaada wa maana kwa DRC ni kuunda jeshi la pamoja kwa nchi zote wanachama ili kuingia kijeshi/kivita kuinusuru Congo.

Na gharama za kuliwezesha jeshi hilo zibebwe na nchi wanachama husika.

Kutegemea jeshi lolote linalopelekwa kulinda amani kwa mwamvuli wa Umoja wa mataifa ni kutokuitakia mema nchi husika.

Maana misheni nyingi za UN za walinda amani huwa haziruhusiwi kupigana ama kujibu mapigo, si za kutegemea kulinda usalama wa watu, hazisaidii na hazifai.

Kwa hiyo bw. Mdude ikitolewa hoja ya kuunda jeshi la pamoja kwenda kuwafurusha M23 na wawezeshi wa jeshi hilo wakawa ni nchi husika zitakazounda jeshi hilo, hao magaidi watabakia kuwa ni historia.

Lakini viongozi wakienda na hoja za blah blah za UN na takataka zingine za kufanana na UN, hakuna lolote lamaana linaloenda kutokea.
 
Kuna kitu nimejaribu kuwaza. Nchi za Tanzania na Kenya haziwezi kumwekea vikwazo kwenye bandari kumlazimisha kumaliza hii vita?

Sioni kama ana njia nyingine kupitisha bidhaa zake mbali na Tanzania na Kenya.
Hii ni njia rahisi sana. Lakini ngumu kutekeleza
 
Ni pale unapokuwa na hasira za kumpiga mwizi, kumwangalia vizuri kumbe ndo faza yako. Aliyepo nyuma ya Kagame ndio anaetoa 70% ya misaada yenu yote. Hadi chandarua unacholalia na mke wako ni yeye kakupa bure, kwa hio acha makasiriko.

Ukiwa ombaomba tegemea na wewe kuombwa, sasa usianze kurusha miteke, ukikataa watakamata hiyo miguu, ndio Kongo hiyo, mzigo lazima...
 
Ndiyo, wewe je?? Vikwazo havijaleta madhara kwa Urusi?? Jibu kwa kutumia akili.
Nitajie nchi moja kwenye hizo G7 ambayo haijaathiriwa na vikwazo walivyomwekea Russia. Tatizo mnasoma kile wanachotaka wao msome.
 
Kuna kitu nimejaribu kuwaza. Nchi za Tanzania na Kenya haziwezi kumwekea vikwazo kwenye bandari kumlazimisha kumaliza hii vita?

Sioni kama ana njia nyingine kupitisha bidhaa zake mbali na Tanzania na Kenya.
... kama sio njaa ya Ruto hili lingewezekana, lakini kwa sasa Ruto tayari kaishanunuliwa na anaendeleza wimbo uleule wa M23 NI WACONGOLESE!
 
Dawa ya Paul Kagame siyo kushughulika na wanaomtuma (nchi za magharibi), bali ni kumshughulikia yeye mwenyewe.

Huyu Kagame ni wa kupigwa risasi tu kama ambavyo amekuwa anawaua mahasimu wake.

Na hili haliko mbali
Hata leo Kagame akiondoka hiyo vita haitaisha, M23 ni Congolese sio Rwandese, serikali ya Congo imekataa kuwatambua Banyamurenge kama raia wa Congo na imejaribu mara nyingi kuwafanyia genocide , na huyu mdude ndio yule wa Chadema? Kama ni yeye kwa akili kama hii basi Chadema wanapoteza muda tuu
 
Back
Top Bottom