Ashugulikiwe aliyepo nyuma ya Kagame na M23 yake kukomesha umwagaji damu mashariki ya DRC

Ashugulikiwe aliyepo nyuma ya Kagame na M23 yake kukomesha umwagaji damu mashariki ya DRC

Hata leo Kagame akiondoka hiyo vita haitaisha, M23 ni Congolese sio Rwandese, serikali ya Congo imekataa kuwatambua Banyamurenge kama raia wa Congo na imejaribu mara nyingi kuwafanyia genocide , na huyu mdude ndio yule wa Chadema? Kama ni yeye kwa akili kama hii basi Chadema wanapoteza muda tuu
Hakuna asiyewatambua kama wakongo, tatizo wao wanajiona wana haki ya kiutawala kama wanavyotawala Rwanda watusi 15% ya population.
 
Maelezo marefu yanatolewa na mtu anayewafahamu vizuri viongozi wa kiAfrika namna walivyo na haiba zenye kushabihiana!

Kwa taarifa yako ni kwamba, viongozi wa Afrika mostly ni kama nyumbu.

Nyumbu hawezi kutoa msaada kwa nyumbu mwenzake aliyekunjwa shingo na simba, kwa sababu, aliyeangushwa kuliwa si yeye, kwa hiyo jambo hilo linakuwa halimhusu.

Hata hicho kikao cha SADC na EAC kilichoitishwa Dar siku ya Juma mosi, kama hakitaweza kutoka na agenda moja yenye maamuzi ya kimshikamano, basi tujue kuwa kwa sababu mdhila ya raia wa Congo DR si yao, hivyo hayawahusu.

Uamzi uliotakiwa kufanywa kukomesha longolongo pamoja na kutoa msaada wa maana kwa DRC ni kuunda jeshi la pamoja kwa nchi zote wanachama ili kuingia kijeshi/kivita kuinusuru Congo.

Na gharama za kuliwezesha jeshi hilo zibebwe na nchi wanachama husika.

Kutegemea jeshi lolote linalopelekwa kulinda amani kwa mwamvuli wa Umoja wa mataifa ni kutokuitakia mema nchi husika.

Maana misheni nyingi za UN za walinda amani huwa haziruhusiwi kupigana ama kujibu mapigo, si za kutegemea kulinda usalama wa watu, hazisaidii na hazifai.

Kwa hiyo bw. Mdude ikitolewa hoja ya kuunda jeshi la pamoja kwenda kuwafurusha M23 na wawezeshi wa jeshi hilo wakawa ni nchi husika zitakazounda jeshi hilo, hao magaidi watabakia kuwa ni historia.

Lakini viongozi wakienda na hoja za blah blah za UN na takataka zingine za kufanana na UN, hakuna lolote lamaana linaloenda kutokea.
... hicho kikao cha EAC&SADC ni cha hovyo mno maana Ruto, Museveni na Kagame tayari ni team moja inayoingia na ajenda isiyobadilika, Saa100 yeye tutarajie neutral, UNABAKI NA NANI UPANDE WA CONGO?
UPUUZI MTUPU, ... Tshisekedi apeleke wajumbe ambao maelekezo yao ni kusikiliza tu!
 
Maelezo marefu yanatolewa na mtu anayewafahamu vizuri viongozi wa kiAfrika namna walivyo na haiba zenye kushabihiana!

Kwa taarifa yako ni kwamba, viongozi wa Afrika mostly ni kama nyumbu.

Nyumbu hawezi kutoa msaada kwa nyumbu mwenzake aliyekunjwa shingo na simba, kwa sababu, aliyeangushwa kuliwa si yeye, kwa hiyo jambo hilo linakuwa halimhusu.

Hata hicho kikao cha SADC na EAC kilichoitishwa Dar siku ya Juma mosi, kama hakitaweza kutoka na agenda moja yenye maamuzi ya kimshikamano, basi tujue kuwa kwa sababu mdhila ya raia wa Congo DR si yao, hivyo hayawahusu.

Uamzi uliotakiwa kufanywa kukomesha longolongo pamoja na kutoa msaada wa maana kwa DRC ni kuunda jeshi la pamoja kwa nchi zote wanachama ili kuingia kijeshi/kivita kuinusuru Congo.

Na gharama za kuliwezesha jeshi hilo zibebwe na nchi wanachama husika.

Kutegemea jeshi lolote linalopelekwa kulinda amani kwa mwamvuli wa Umoja wa mataifa ni kutokuitakia mema nchi husika.

Maana misheni nyingi za UN za walinda amani huwa haziruhusiwi kupigana ama kujibu mapigo, si za kutegemea kulinda usalama wa watu, hazisaidii na hazifai.

Kwa hiyo bw. Mdude ikitolewa hoja ya kuunda jeshi la pamoja kwenda kuwafurusha M23 na wawezeshi wa jeshi hilo wakawa ni nchi husika zitakazounda jeshi hilo, hao magaidi watabakia kuwa ni historia.

Lakini viongozi wakienda na hoja za blah blah za UN na takataka zingine za kufanana na UN, hakuna lolote lamaana linaloenda kutokea.
...... jeshi la Pamoja lipi hilo? ... hujuma itafanywa na vikosi vya Rwanda, Uganda & Kenya ambao watakaa kama watazamaji na ukizubaa unawahiwa!
 
Fikiria hawa ni raia wameuawa na M23 huku askari wetu wawili wa JWTZ na askari wanne wa South Africa waliokuwa wakiwalinda raia nao wakiuawa kikatili.

Nchi ya Congo ingekuwa haina madini na rasilimali zingine sidhani kama huyu Paul Kagame na Kaguta Museveni wangekuwa na kashfa ya kuwa nyuma ya Mzozo wa DRC wakisizingia kutafuta waasi wanaopinga serikali zao waliokimbilia huko. Ukiona dikteta yoyote anakaa muda mrefu madarakani halafu huoni mataifa ya Ulaya yakimlalamikia kaa ukijua kuwa dikteta huyo ni kibaraka wao. Ndivyo ilivyokuwa kwa Mubutu Sese seko.

Mobutu alikuwa kibaraka wa mataifa ya magharibi na walimuweka baada ya mataifa hayo kumuua baba wa taifa la Congo DCR Patrice Lumumba aliyepigania uhuru wa taifa hilo kutoka kwa wabelgiji. Walifanya hivyo ili iwe rahisi kuvuna rasilimali za Congo kwani ilikuwa ngumu kuvuna chini ya Patrice Lumumba ambaye alikuwa ameshaanza kuwafungia vioo. Baada ya kumuua Patrice Lumumba walianza kuvuna rasilimali za Congo kwa wanavyotaka huku wakimlinda Mobutu. Licha ya udikteta wa Mobutu wa kuteka na kuua wapinzani wake hawa nchi za magharibi hawajawahi kumkemea kwa sababu alikuwa kibaraka wao huku wakimtajirisha.

Kuna wakati akina Nyerere, Kaunda na wengine walimtenga Mobutu kwenye Mulungushi Club. Wakati huo marais wa nchi za kusini mwa Africa ambao kwa sasa ni SADC waliokuwa mstari wa mbele kupigania uhuru wa nchi za kusini mwa Africa waliunda Club iliyoitwa Mulungusi ambayo kazi yake ilikuwa ni mikakati ya kusaidia nchi za kusini mwa Africa ambazo zilikuwa hazijapata uhuru ikiwemo Zimbabwe na South Africa.

Mobutu kibaraka wa nchi za magharibi akawa anavujisha siri kwa mabwana zake mikakati yote ya Mulungusi Club. Inabidi mwalimu Nyerere na wenzake wamteme.

Baada ya anguko la Mobutu sasa Kagame akabadili nafasi hiyo ya ukibaraka wa kuwatumikia mataifa ya magharibi kufanya machafuko mashariki mwa Congo ili kupata mwanya wa kuvuna rasilimali za nchi hiyo katika eneo hilo. Kisingizio cha Kagame ni kuwatafuta waasi wa kihutu waliokimbilia Congo tangu wakati wa mauaji ya kimbali nchini Rwanda mwaka 1994. Ukweli ni kwamba huu ni uongo na waasi hao wanatumika kama kichaka tu cha kuficha uovu wa Kagame na wafadhili wake wa nchi za magharibi.

Leo tujiulize madini yanayouzwa kwenye soko la dunia kutokea Rwanda yanatoka wapi kama sio Congo? Kwanini Kagame anakuwa dalali wa kumwaga damu za waafrica wenzake kwa faida ya wazungu wa mataifa ya magharibi? Kagame anasoma biblia hivi hajui kwamba damu ina tabia ya kisasi?

Ukimuona mbuzi juu ya mti ujue kapandishwa. Kagame ni mbuzi aliyepandishwa juu ya mti. Huyo aliyempandisha ndiye ashugulikiwe. Kwa hiyo ukitaka kutatua tatizo dili na chanzo cha tatizo na sio tatizo. Viongozi wa SADC na Africa walipaswa kushugulika na aliye nyuma ya Kagame hizi nchi za magharibi ikiwemo ufaransa ambazo ndio zinampa kiburi kama walivyokuwa wanampa kiburi Mobutu. Kwa bahati mbaya nchi za SADC zinadili na Kagame huku zikiogopa kudili na boss wa Kagame nchi za magharibi kwa sababu ya kukosa mikopo na misaada.

Kama Africa bado tuna safari ndefu sana maana ndani yake wapo viongozi waoga, wezi na mamluki wa nchi za magharibi.

Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Usiseme aliye nyuma ya Kagame, ni Kagame mwenyewe!
 
kumtaja sana,PK pekeake bila mshauri wake mkuu wa uchumi .....waziri mkuu tonny Blair nikumkosea
 
Ni kweli kabisa mkuu,maana wengi wanahangaika tu na harufu, badala kuuondoa tu mzoga,ambao umejificha lakini wajulikana,,ukiondolewa tu na harufu lazima itoweke,lkn japokuwa mzoga haugusiki kirahisi hivyo na huu mzoga ni zaidi ya mmoja mjue,sasa upi uanze kushughulikiwa!?,na kivipi?
 
Hakuna asiyewatambua kama wakongo, tatizo wao wanajiona wana haki ya kiutawala kama wanavyotawala Rwanda watusi 15% ya population.
Sio kweli, acha kuamini propaganda za kipuuzi, ni ukabila tuu na ujinga tuu
 
Kama ni mfaransa au mmarekani yuko nyuma ya kagame anyukwe tu. Hayo mataifa yaambiwe ukweli. Kushinda vita si lazima utumie madege ya kisasa na silaha zingine kali za hayo mataifa. Kuna mbinu nyingi za kumtimua mfaransa na mmarekani na yeyote aliyepo nyuma ya kagame kwenye mzozo wa congo. Nani anampa jeuri kagame pamoja na M23? Watimuliwe tu huko congo pamoja na maguvu yao
 
Ukiona hadi Mdude kauingilia mgogoro wa Kongo basi mgogoro huo unatakiwa umalizwe kwa njia za maongezi.
 
"I know the leader and I know the idiot" - PK.
If you are a leader and an idiot, it's the disaster" -PK.
 
Taifa gani la Africa mashariki na kusini ambalo sio kibaraka?.

Mobutu Seseko alitolewa madarakani na akina PK na M7 na kumuweka Desire Kabila, kwahiyo vibaraka walimtoa kibaraka mwenzao.

Waambieni viongozi wa DRC wanapoitaka Ikulu wasifanye maagano ambayo utekelezaji wake unawashinda.

Suluhu la Mgogoro wa DRC sio kumpiga PK au Rwanda, maana mgogoro ulikuwepo kabla hata ya PK kuwepo hapo Rwanda, Suluhu ya huo mgogoro ni kuwatafutia suluhu watutsi wa DRC.
 
Ukiona hadi Mdude kauingilia mgogoro wa Kongo basi mgogoro huo unatakiwa umalizwe kwa njia za maongezi.
... huwa nakuheshimu sana na najitahidi sana kutojibizana na wewe, lakini kwa hili la PAKA samahani, INATAKIWA TUFURUSHE NYAU MPAKA UGANDA IKAPUMZIKE!
🤣
 
Back
Top Bottom