Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah! sawa Mkuu umeeleweka vema kabisa.Lizaboni maana yake Eliza born alizaliwa binti alikua anaitwa Eliza...
Kama hutak bas.
LUKULEDI (Look ladies) Wazungu walikuwa wakioneshana wanawake wakati wanaoga mtoni, baadae ikawa jina la mto1.KIBORILONI & KIBOSHO[MOSHI].
Kiboriloni ni neno lililotokana na maneno mawili KIBO ALONE. Hii ilikuwa sehemu ambapo wazungu walisimama na kuona kilele cha Kibo pekee bila kukiona kilele cha Mawenzi, Kibo na Mawenzi ni vilele vya Mt. Kilimanjaro.Kibosho lilitokana na maneno KIBO SHOW, hii ni sehemu ambapo Kibo kilionekana vizuri zaidi.
2.KARIAKOO.
Inasemekana Kariakoo ilikuwa kituo cha Askari wa kikoloni CARRIER COP, Wabantu wakarahisisha kwa kupaita Kariakoo.
3.KOLOMIJE[BUNDA].
Inasemekana mahali hapo alifika Mzungu aliyeitwa James.Yule Mzungu akataka watu wamwiite 'J' badala ya kutamka jina lote. Hivyo akawaambia CALL ME J, wabantu wakatamka KOLOMIJE na kutengeneza jina la lile eneo.
4.CHEKERENI[MOSHI].
Hili ni eneo ambapo barabara inakatiza kwenye reli.Sasa wazungu waliweka alama ya bararani ya tahadhari kabla ya kuvuka reli CHECK THE LINE, watu wakatamka CHEKERENI na kuliita hivyo lile eneo hadi leo.
5.NEWALA [MTWARA].
Inasemekana kwamba waingereza walipofika Mtwara walikuta kisima kilichojengwa na wajerumani ambacho kilikuwa cha kizamani kwa wakati huo.Hivyo walijenga kisima kipya na kukiita NEW WELL, watanganyika wakatamka NEWALA, hatimaye likawa jina la ile sehemu.
N:B SOURCE yake ni HEARSAY STORIES....unaweza kusahihisha ama kuongeza majina mengine.
Mkuu huo mto upo wapi? bado lediz wanaoneshwa?😀😀😀😀LUKULEDI (Look ladies) Wazungu walikuwa wakioneshana wanawake wakati wanaoga mtoni, baadae ikawa jina la mto
Wape link ili wafanye kazi vyema mkuuMod unga huu Uzi,Upo mwingine una title asili ya najina ya maeneo.
Mkuu we ni wa dar?Kuelekea dareda kuna sehem inaitwa Logia. Hi inatokana na Low Gear, ikiwa ni tahadhari kwa madereva kubadilisha gia kwa sababu barabara hapo ina mwinuko mkali.
Huko wabarbeig ndo wakata majina wazuri wa maeneo walikopitia alafu wairak wanazikolezeaSea breeze= Chibirizi (Kigoma)
Ila samahani mleta mada kuna majina huku Manyara yanaishia na consonant sijui chanzo chake mf. Katesh, Hanang, Endabash, Endasaq,
Ukiangalia maeneo mengi yanayokaliwa na wairak majina ya hayo maeneo ni ya kibarbaigMkuu Wairaq sidhani kama ni wabantu wenzetu[Mimi siyo mbaguzi] wao pamoja na jamii mbalimbali za wafugaji wana asili tofauti na ya watu wengine.
Ndio maana Lugha zao hazijachangia neno lolote kwenye lugha ya Kiswahili[pia sina uhakika] hivyo kuziondoa miongoni mwa lugha za kibantu na ndio sababu iliyonifanya niseme siyo wabantu......Kuna neno linatamkwa Haidom nalo lina niacha hoi sana.
Sawa kabisa wana lafudhi ya kufanana.....pia wanashea mambo mengi sana.Ukiangalia maeneo mengi yanayokaliwa na wairak majina ya hayo maeneo ni ya kibarbaig
Kabila rafiki nadhani kwasababu mbarbaig hajui uwizi, wala hataki kitu cha mtu , na hawapendi kulima.Sawa kabisa wana lafudhi ya kufanana.....pia wanashea mambo mengi sana.
Yale maeneo ya Iringa yalivamiwa na wagiriki walima tumbaku na wajerumani, sasa wakati wanapima mashamba yao ili wagawane wakawa wanasema keep on zero kama reference point. Wahehe wakajua pale ni kiponzero !!!!!!Dah yaani linaleta mantiki kabisa Mkuu.....hii lugha ilikuja kwa meli aisee.
kakueleza ni kijerumani. Nenda google ulizia maana yake. Tunatumia kijerumani sababu ndo walioanzisha shule bara. Tanga ikiwa kianzio.Schule siyo neno la Kingereza.
Nafahamu ni la Kijerumani, ila mimi nilitaka maneno ya Kingereza.kakueleza ni kijerumani. Nenda google ulizia maana yake. Tunatumia kijerumani sababu ndo walioanzisha shule bara. Tanga ikiwa kianzio.
Hahahahaaa......dah! nimecheka sana aisee....kutoka keep on zero hadi Kiponzero? kweli Wahehe hawapendagi ujinga,....unawaongelesha kithungu kwani uliwapeleka Shule?Yale maeneo ya Iringa yalivamiwa na wagiriki walima tumbaku na wajerumani, sasa wakati wanapima mashamba yao ili wagawane wakawa wanasema keep on zero kama reference point. Wahehe wakajua pale ni kiponzero !!!!!!
Nawapenda Wahehe, sababu mkoa mzima hakuna majina ya kizungu kwenye mitaa yao, ila kijiji kimoja tu, Pomern (jerumani), kipo kilolo.