Asili na Maana ya Jina/majina ya sehemu mbalimbali Tanzania

Bonge la Elimu.

Ila inaonesha zamani palikuwa na mfumo mzuri mno
 
Mkuu mziki wa zamani ulikuwa na tunzi nzuri sana kwa vile katika wimbo wowote watunzi wanaweza kuwa bendi nzima.
Kulikuwepo na solo guitar no 1 na no 2, halafu rythym guitar, mbali na bass guitar.
Wabunifu kama Mbaraka Mwinshehe alileta na Hawaian guitar yenye manjonjo yake.
Pembeni kunakuwa na trumpets na saxaphone.
Kiujumla kila mwenye chombo aliweka manjonjo yake ya kuvutia.
Na hapo bado waimbaji wenye sauti za kuvutia siku hizo wakiitwa vocalists.
Sauti ya kwanza, pili, tatu hadi nne.

Kwa ujumla mziki ulishiba tungo na ufundi wa watu zaidi ya 15.
Siku hizi mziki nia wa mwimbaji mmoja au wawili na computer generated graphics zinazojirudia nyimbo nyingi.
 
Moja ya sababu zilizo changia kufa kwa kamata ni barabara mbovu za mikoani na zakwenda nchi jirani. Barabara chache sana za lami enzi hizo .
 

Ng'wanamalundi, Jidu La Mabambasi

nawashukuru kwa kufafanua suala hili la mabasi ya DMT, nilishtuka hapo mwanzo wachangiaji wanaishia Scandinavia tu, nikajiuliza hakuma MLENGA humu kweli?
nakumbuka mabasi hayo yalikuwa yakitembea usiku, miaka ya 1969 mpaka 1970 niliyapanda kuelekea Mtwara maana Baba yangu alikuwa akifanya kazi serikalini Newala km Mganga /Tabibu
na kweli mabasi ya Umma kama Railways pia tuliyatumia kati ya Iringa na Moshi usumbufu ukiwa hivyo hivyo kuharibika na kulala Bonga Kondoa eti gari bovu asubuhi linapona
 
Ni kweli kabisa Ng'wanamalundi miaka ya 1980 ziliruhusiwa CHAI MAHARAGE yaani pich-up za tani 3 mnakaa mkiangaliana kwa sasa naona mtindo huo upo Zaznzibar nyingi zilikuwa ni KIA zikifanya biashara ya abiria na hapo wengi wakatoza sh 5/ (km ulivyosema dala moja) na hata pick-up ndogo zikaruhusiwa kuingizwa Nchini badala ya gari za saluni kwa amri ya Marehemu Sokoine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…