Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Wanajf, naomba mnijuze jambo hili, kila cku tunatoa shikamoo kwa wa2 waliotuzidi umri. cjapata mantiki ya neno hili, je hii ni kuonyesha heshima au ni kwa mazoea tu.

naomba kuwasilisha.
 
shikamoo maana yake niko chini ya miguu yako ilitumiwa na waarabu watumwa waliitumia kuwasalimu mabwana wao
 
Sijui kwa nini tunaitumia.Mi nadhani ukimwamkia mtu,habari yako! au habari ya saa hizi! Heshima haitapungua.
 
Nipo chini ya miguu yako?
Hayo ni maneno wameweka wazee wetu ili kupaka rangi shikamoo.
Mie naamini tafsiri yake ni hii
Shika=Shika
Moo=Kuna herufi moja mwanzo wameifuta.
OTIS
 
Nipo chini ya miguu yako?
Hayo ni maneno wameweka wazee wetu ili kupaka rangi shikamoo.
Mie naamini tafsiri yake ni hii
Shika=Shika
Moo=Kuna herufi moja mwanzo wameifuta.
OTIS

huo ni uhuni
 
Marhabaa. Neno hili (shikamoo) limezoeleka mno kama salam kwa kiswahili na wengi wanatambua kuwa ni neno lililotokana na Kiarabu kwa maana ya mdogo kukiri adabu kwa mkubwa. Juzi tu nilikuwa nasikiliza TBC radio na kugundua kumbe neno hilo (shikamoo) ni neno la Kireno likimaanisha kushika sehemu ya chini ya mguu kuonesha utii (kuomba radhi) kwa mkubwa. Sasa inakuwaje litumike kama salam ya kiswahili wakati hata lenyewe tu halionekani ni salam?
 
Salamu si lazima iwe na maana sawa ni ile ambayo 'wewe' unategemea.
Mfano, lugha nyingi zina 'salamu' ambazo ukitafsiri maana yake utaishia kucheka. Lugha ni utamaduni..pia lugha ni kiashiria cha jinsi watu katika jamii husika wanavyofikiri.
Kwa maoni yangu Shikamoo ni nzuri sana..Waingereza 'hawana' salamu inayolingana uzito na shikamoo.

Mfano: Kwa Kiingereza utasikia mtu akiuliza, 'How old are you' = tafsiri ya neno-kwa-neno utasamaje?

Lugha si maneno pekee, ni jinsi watu tunavyofikiri.
 
Ni sawa na kusema naomba baraka zako.....
Hapana, nilimsikia mzee mmoja TBC Taifa akifafanua maana na asili ya neno hili ni kumuamuru mkosaji akushike chini ya kikanyagio chako cha mguu ili umsamehe. Mfano umenitukana sasa ili nikusamehe nakuambila 'shikamoo' yaani uniguse sehemu ya chini ya mguu wangu na ntakuwa nimekusamehe.
 
Salamu si lazima iwe na maana sawa ni ile ambayo 'wewe' unategemea.
Mfano, lugha nyingi zina 'salamu' ambazo ukitafsiri maana yake utaishia kucheka. Lugha ni utamaduni..pia lugha ni kiashiria cha jinsi watu katika jamii husika wanavyofikiri.
Kwa maoni yangu Shikamoo ni nzuri sana..Waingereza 'hawana' salamu inayolingana uzito na shikamoo.

Mfano: Kwa Kiingereza utasikia mtu akiuliza, 'How old are you' = tafsiri ya neno-kwa-neno utasamaje?

Lugha si maneno pekee, ni jinsi watu tunavyofikiri.
Sikubaliani ASILAN na maelezo yako mkuu.
 
Hapana, nilimsikia mzee mmoja TBC Taifa akifafanua maana na asili ya neno hili ni kumuamuru mkosaji akushike chini ya kikanyagio chako cha mguu ili umsamehe. Mfano umenitukana sasa ili nikusamehe nakuambila 'shikamoo' yaani uniguse sehemu ya chini ya mguu wangu na ntakuwa nimekusamehe.

Mmmh naona pia haileti maana, saa nyingine unamwamkia mtu shikamoo humjui au hakujui sasa akusamehe kwalipi ulomkosea?

Kwa wenzetu wahindi anapokushika mguu ni sawa na kupata baraka kwa mtu aliyekuwa mkubwa kwako......so it makes sense!
 
Mmmh naona pia haileti maana, saa nyingine unamwamkia mtu shikamoo humjui au hakujui sasa akusamehe kwalipi ulomkosea?

Kwa wenzetu wahindi anapokushika mguu ni sawa na kupata baraka kwa mtu aliyekuwa mkubwa kwako......so it makes sense!
Umeelewa sasa! Maana halisi ya SHIKAMOO si kusalimiana ila sisi tumeligeuza/chakachua kama kawaida yetu. Tuna salamu nyingi tu za kusabahiana na zenye heshima ila watunga vitabu vya kiswahili wamepotosha salamu hii.
 
Wadau, labda ni vyema kushare nanyi suryey ambayo tuliifanya muda kidogo, nayo ni kuhusu salam ya 'Shikamoo'.

Katika suryey yetu tukagundua kuwa;

1. Watu wengi hawajui maana ya neno 'Shikamoo' zaidi ya kusema kuwa ni heshima, wengine wakasema ina maana ya 'nipo chini ya miguu yako'

2. Asili yake ni ya kitumwa,yaani walioinzisha hawaitumii kama salamu yao ya kawaida ila walioipokea ndio wanaitumia katika matumizi yao ya kila siku.

3. Ime simama katika kuangalia umri, kitu ambacho muda mwingine ni ngumu kujua au kukisia umri wa mtu sababu waweza muamkia mtu kumbe ni mdogo wako

4. Imejengwa katika nidhamu ya uoga, ndio maana ni rahisi kumkuta mtu mkubwa kiumri ana msalimu mtu mdogo kiumri sababu tu anayeamkiwa ana nguvu kubwa kifedha au kimadaraka.

5. Imepitwa na wakati, yaani wengine hawataki kabisa kuisikia ama wanajishusha umri, ndio maana mtu anaamkiwa anasema poa, au salama.

6.Imesababisha ugomvi au wengine kutosalimiana kwa sababu tu hakuna anayependa kuwa mdogo.

Wadau toeni mapendekezo yenu juu ya kile mliona na mnavyodhani juu ya suala hili...
 
Kwahiyo unapendekeza salamu gani kwa wakubwa wenzako?
 
hujaeleza inakufa kivipi na nini mbadala wake?

kimsingi shikamoo ni salamu ya mdogo kwenda kwa mkubwa, ikiwa ni kweli kwamba inakufa, je, wadogo wanawasalimu vipi wakubwa siku hizi....nipe jibu ambalo utafiti wako ulionyesha!
 
Wewe mzee ni vizuri kukubali tu kwamba umri umekwenda. Pokea shikamoo unazopewa na wadogo zako bila kujiuliza maana kwa umri wako 55+ ni mzee. Na hata shikamoo ikifa, uzee wako uko pale pale.
 
Tunajua na kukubali chanzo cha hii salamu ilikuwa ni utumwa, je kuna aina salamu gani inayoweza kutumika badala ya hii? kusema kweli nilichogundua Baba yangu tangu nikiwa mdogo huwa hataki kupokea shikamoo badala yake anataka tuwe tunamsalimia kilugha.
 
Back
Top Bottom