Asili ya neno Mungu ni nini?

Asili ya neno Mungu ni nini?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Habari wakuu. Kila neno kwenye lugha huwa lina athiri yake. Mfano ukichunguza utaona kuwa God aliabudiwa na jamii nyingi za Ulaya kabla hata ya ukristo. Allah aliabudiwa na waarabu kabla hata ya uislamu. Yahweh/Yehova aliabudiwa na wana wa Isaraeli. Kuna makabila yetu ambayo yana majina yao ya walichoabudu. Wengine waliwaita Kyala, wengine Ruwa, Nguluvi nk nk.

Zilivyodominate dini hizi mbili za mashariki ya kati, watu wakabadili majina ya wanavyoviabudu kumaanisha Allah na Yehova. Sasa inaonekana hata hili neno Mungu lilikuwa kama Nguluvi, Kyala, au Ruwa. Pengine ni kitu waliabudu waswahili.

Wachaga walikuwa wanamuabudu Ruwa. Wanyakyusa walikuwa wanamuabudu Kyala. wazungu walikuwa wanamuabudu God. Ni nnani waliokuwa wanamuabudu Mungu? Neno Mungu lilitoka wapi?
 
Lilizuka tu.
Lugha ni sauti za nasibu...
Ni kweli lakini hata God lilizuka kwa nasibu kumtaja au kumuwakilisha huyo waliomuabudu! Je, neno Mungu lilizuka kwa bahati nasibu kumtaja nani waliyemuabudu??? Ni Mungu huyu huyu Jehova au mwingine?
 
aisee hizi nyuzi za mada hizi zinaongezeka sana
au ndo tuko mwishoni mwishoni nini??
 
Ni kweli wabantu huita Mulungu au Umungu japo sisi twaita Nyamhanga
Huyo Nyamhanga alikuwa nani?

Huyo Nguruwi alikuwa nani?

Huyo Ruwa alikuwa nani?



Musa akamuuliza "niwaammbie jina Lako nani" akamjibu "Mimi Niko Ambaye Niko".
 
Mungu ni lile wazo la Mungu ambalo kila jamii inalo [in fact kila mtu analo] na inaipa jina la kikwao kwa sababu ni kitu kipo wanaishi nacho. Ni kama mawe, kila jamii ililipa jina jiwe kwa sababu ni kitu kipo waziwazi

Sema tu ule ubinafsishaji au utaifishaji wa huyu Mungu wa wote ndio unaoleta mgawanyiko lakini in fact Mungu ni huyo huyo mmoja. Kinachonifurahisha wasukuma walimuita 'Liwerero/Liwelelo' nahisi jamaa walikuwa deep kichizi. Hili jina sio 'Personal', Maana yake [Liulimwengu], hawa jamaa wachunguzwe walijuaje?
 
Mungu ni lile wazo la Mungu ambalo kila jamii inalo [in fact kila mtu analo] na inaipa jina la kikwao kwa sababu ni kitu kipo wanaishi nacho. Ni kama mawe, kila jamii ililipa jina jiwe kwa sababu ni kitu kipo waziwazi

Sema tu ule ubinafsishaji au utaifishaji wa huyu Mungu wa wote ndio unaoleta mgawanyiko lakini in fact Mungu ni huyo huyo mmoja. Kinachonifurahisha wasukuma walimuita 'Liwerero/Liwelelo' nahisi jamaa walikuwa deep kichizi. Hili jina sio 'Personal', Maana yake [Liulimwengu], hawa jamaa wachunguzwe walijuaje?
Lakini kila watu walikuwa na kitu chao tofauti walichokiabudu. Kikiwa na sifa tofauti na nguvu tofauti. Wengine waliabudu vitu vingi sana. Sasa huyu Mungu alikuwa anaabudiwa na nani?
 
Lakini kila watu walikuwa na kitu chao tofauti walichokiabudu. Kikiwa na sifa tofauti na nguvu tofauti. Wengine waliabudu vitu vingi sana. Sasa huyu Mungu alikuwa anaabudiwa na nani?
Aliabudiwa na wote katika sura tofautitofauti kulingana na jamii tofauti, jamii zilitumia viwakilishi tofautitofauti pia. Yaani tuliparanganyika sana hadi alipokuja Mwana wa Mungu kama Mwana wa Mtu kutuunganisha wooooote ulimwenguni kwa Mungu mmoja
 
Aliabudiwa na wote katika sura tofautitofauti kulingana na jamii tofauti, jamii zilitumia viwakilishi tofautitofauti pia. Yaani tuliparanganyika sana hadi alipokuja Mwana wa Mungu kama Mwana wa Mtu kutuunganisha wooooote ulimwenguni kwa Mungu mmoja
Unataka kusema Allah, Mungu, Ruwa, Nguluvi, Kyala, God nk nk ni kitu kimoja?
 
Kwanza inabidi ufahamu Mungu ni jina la cheo sio jina mahusus( Specific), kama vile mtu anavyoweza kusema Rais/Mfalme bila ku specify ni rahisi yupi/nani wa wapi, Rais ni cheo kama tu vile Mungu,mkuu wa mkoa,CEO na kila cheo kina sifa zake.

Katika lugha mbalimbali Mungu kama cheo ametajwa kwa majina mbalimbali mfano God (English) Allah (Arabic) Elohim (Hebrew) sio Yehova/Yahweh Deus na kadhalika

Lakini wayahudi/ wana Waisrael walikuwa na jina specific la Mungu wao ambalo ndio walikatazwa kulitaja bure kwa sababu ya utakatifu wake ambalo ni YHWH ( tetragrammaton) ambalo kwa sababu za kimatamshi westerns walilitohowa na kuliwekea irabu ndio likawa YAHWEH, ila Jina Yehova walilitumia wayahudi katika desturi zao za kumtaja Mungu kwa majina ya sifa badala ya jina lake halisi kwa sababu ya utakatifu wake ili kuepuka kulitamka bure na kijukuta wamevunja ile amri na sifa hizo ziliendana na kitu alichofanya au jinsi alivyo, mfano Yehova Rapha,Mungu mponyaji, Yehova Sabaoth, Mungu wa majeshi n.k.

Lakini kwa wagiriki walikuwa na desturi ya kuwa na miungu wengi tofauti na wayahudi na majina yao yalikuwa mengi pia, mfano Saturn,Venus,Uranus,Apollo etc.

Lakini kwa waarabu wao wamemtaja Mungu kama cheo (ALLAH) bila ku specify jina lake specific (sio la sifa)

Conclusion: Kwa hiyo usihadaike kwa mtu kusema tu Mungu wetu, je ni Mungu gani, unauhakika asilimia ngapi Mungu anayemmaanisha ndio huyo unaye muamini wewe, Ni swala lisilopingika ya kuwa Mungu wa kweli ni mmoja, lakini je ni Mungu yupi, anaitwa nani na wapi na anasifa zote za uungu, Kwa maana hata Lucifer anaitwa Mungu wa dunia hii, lakini je ni Mungu wa kweli?.

Na wengi wetu tumeingizwa katika ibada za miungu tusioijua kwa kigezo cha Mungu ni mmoja, Mungu ni wetu sote, Mungu ni yule yule, bila kujua Mungu ni cheo ambacho kinaweza kuwa na yeyote bila kujali kakidhi vigezo au laa, Ninyi nyote ni mashaidi kuna watu wanajiita marais, mara rais wa wasafi Rais wa manzese Rais wa watu je ni Marais kweli au wamejiita tu hivyo hivyo na kwa Mungu, Kuna Mungu wanajiita,(zumaridi) wengine wanaitwa na watu, hata mtaani kwetu yupo naye mjua anajiita Mungu na watu wanamuita hivyo, Lakini je ni kweli anavigezo

Note: Mungu wa kweli ni mmoja Muumba wa vyote vyenye kuonekana na visivyoonekana, wa milele, mweza yote,mjua yote, afanyaye kila jambo kwa shauri la mapenzi yake pekee, mwenye uwezo wa kuua na kuhuisha hata roho (je Mungu wako ana fit hapo?) Kama hatoshani na sifa hizo tafakari kisha chukua hatua.
Naomba kuwasilisha.
 
Kwanza inabidi ufahamu Mungu ni jina la cheo sio jina mahusus( Specific), kama vile mtu anavyoweza kusema Rais/Mfalme bila ku specify ni rahisi yupi/nani wa wapi, Rais ni cheo kama tu vile Mungu,mkuu wa mkoa,CEO na kila cheo kina sifa zake.

Katika lugha mbalimbali Mungu kama cheo ametajwa kwa majina mbalimbali mfano God (English) Allah (Arabic) Elohim (Hebrew) sio Yehova/Yahweh Deus na kadhalika

Lakini wayahudi/ wana Waisrael walikuwa na jina specific la Mungu wao ambalo ndio walikatazwa kulitaja bure kwa sababu ya utakatifu wake ambalo ni YHWH ( tetragrammaton) ambalo kwa sababu za kimatamshi westerns walilitohowa na kuliwekea irabu ndio likawa YAHWEH, ila Jina Yehova walilitumia wayahudi katika desturi zao za kumtaja Mungu kwa majina ya sifa badala ya jina lake halisi kwa sababu ya utakatifu wake ili kuepuka kulitamka bure na kijukuta wamevunja ile amri na sifa hizo ziliendana na kitu alichofanya au jinsi alivyo, mfano Yehova Rapha,Mungu mponyaji, Yehova Sabaoth, Mungu wa majeshi n.k.

Lakini kwa wagiriki walikuwa na desturi ya kuwa na miungu wengi tofauti na wayahudi na majina yao yalikuwa mengi pia, mfano Saturn,Venus,Uranus,Apollo etc.

Lakini kwa waarabu wao wamemtaja Mungu kama cheo (ALLAH) bila ku specify jina lake specific (sio la sifa)

Conclusion: Kwa hiyo usihadaike kwa mtu kusema tu Mungu wetu, je ni Mungu gani, unauhakika asilimia ngapi Mungu anayemmaanisha ndio huyo unaye muamini wewe, Ni swala lisilopingika ya kuwa Mungu wa kweli ni mmoja, lakini je ni Mungu yupi, anaitwa nani na wapi na anasifa zote za uungu, Kwa maana hata Lucifer anaitwa Mungu wa dunia hii, lakini je ni Mungu wa kweli?.

Na wengi wetu tumeingizwa katika ibada za miungu tusioijua kwa kigezo cha Mungu ni mmoja, Mungu ni wetu sote, Mungu ni yule yule, bila kujua Mungu ni cheo ambacho kinaweza kuwa na yeyote bila kujali kakidhi vigezo au laa, Ninyi nyote ni mashaidi kuna watu wanajiita marais, mara rais wa wasafi Rais wa manzese Rais wa watu je ni Marais kweli au wamejiita tu hivyo hivyo na kwa Mungu, Kuna Mungu wanajiita,(zumaridi) wengine wanaitwa na watu, hata mtaani kwetu yupo naye mjua anajiita Mungu na watu wanamuita hivyo, Lakini je ni kweli anavigezo

Note: Mungu wa kweli ni mmoja Muumba wa vyote vyenye kuonekana na visivyoonekana, wa milele, mweza yote,mjua yote, afanyaye kila jambo kwa shauri la mapenzi yake pekee, mwenye uwezo wa kuua na kuhuisha hata roho (je Mungu wako ana fit hapo?) Kama hatoshani na sifa hizo tafakari kisha chukua hatua.
Naomba kuwasilisha.
Uyo YHWH Ni shetani pia.
 
Back
Top Bottom