Wengi tumepitia huko ila baada ya kutoboa tunasahau tulikotoka. Tuendelee kuwalea ila si lazima kuwatafutia kazi mijini, vijijini kuna fursa pia.Kwanini usijali shida zako au za ndugu zako?una uhakika maisha yako ni mazuri?
Maisha kwa shemegi
ukwer upi kuna familia naijua kijana ana miaka 34 ana watoto wa 3 ila toka dingi yao avute miaka ya 2005 hana jipya anaishi na maza yake mpaka leo kwel kazi sana kufanikiwa maana umri huo anaona aibu ata kwenda kufanya kazi ya kumuingizia bk 2000Tatizo mnawachekea hao ...
Waambiwe ukweli akili zitawakaa sawa.
Kuna familia nyingi sana zina watu wa namna hiyo...tena wengine wanazaa kabisa mnawalea wao na watoto wao
Sio mbaya maana nao watakuja kuwafuga shemeji zao na hivyo ndivyo walivyoandaliwa.Katika kutathimini namna ambavyo kama taifa linapaswa kuwekeza kwenye elimu ya biashara (ujasiriamali) na ubunifu badala ya vijana kutegemea ajira za serikali, uchunguzi uliofanywa katika miji ya Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Mwanza & Kagera umegundua 88% ya vijana kati ya umri wa miaka 30 na 35 bado hutegemea kwa matumizi yao yote toka kwa wazazi ama Mashemeji zao.
Hii si dalili nzuri tunapoelekea kwenye nchi ya viwanda na kutimiza dira ya Taifa ya maendeleo ya 2025 (Tanzania Vision 2025). Vijana amkeni fanyeni kazi, biashara, kilimo, acheni kubweteka na ku-bet kutwa nzima, kushangilia mipira ya ulaya na siasa za Marekani huku hamna namna ya kuingiza kipato binafsi zaid ya kutegemea mashemeji na wazazi kuwapa pesa ya matumizi.
Hizi starehe tu mkuu..baada ya kazi acha tushabikie mpira..wewe ushawahi fanya kazi masaa 24???unakuta kijana anabishania mpira wa ligi za ulaya utadhani yupo interview ya kazi!!