Askari Polisi Wanawake wahamasisha Wananchi kutembelea Vivutio vya Utalii

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Your browser is not able to display this video.
Afisa Mnadhimu Namba moja wa Polisi Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo Makao Makuu, Mrakibu wa Polisi (SP) Suzan Kidiku akieleza namna ambavyo wamepata fursa ya kujifunza na kufurahia Utalii katika hifadhi za taifa ambapo ameziomba Jamii za kifugaji ambazo zinaishi karibu na hifadhi kulinda na kutunza hifadhi hizo.


ASKARI POLISI WANAWAKE WAHAMASISHA WANANCHI KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kupitia mtandao wa Polisi Wanawake wametembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha kwa lengo la kujionea vivutio vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ambayo inapatikana ndani ya mkoa wa Arusha sambamba na kuhamasisha watu kutembelea vivutio hivyo kuelekea siku ya Wanawake duniani.

Aidha Askari hao wamebainisha kuwa wameona fahari kutembelea hifadhi hiyo yenye vivutio mbalimbali ambapo wametoa wito kwa Watu wengine kuwa na utaratibu wa kwenda kutembelea vivutio vilivyopo hapa Nchini kwani pamoja na kuona uzuri uliopo lakini pia watajifunza mambo mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…