Askari wa JWTZ kizimbani kwa kukaidi amri halali ya askari wa Usalama Barabarani

Askari wa JWTZ kizimbani kwa kukaidi amri halali ya askari wa Usalama Barabarani

Hii mbuzi inaongea nini? Unayajua maisha mazuri wewe? Maisha mazuri ya kunyenyekea kama mtoto?

Ila kwa kuwa unalinganisha Wanajeshi/ Askari na takataka siyo tatizo!! Kwa level ya takataka za jalalani/ yaani uchafu / Uozo, kwa hapa wanajeshi/askari wanazidi kidogo sana takataka, maana karibia wafanane na huo uozo tu!!

Ila kama unalinganisha Wanajeshi na raia wengine wa Tanzania, wamepitwa mbali sana. Sina uhakika kama kuna mwanajeshi anapokea 10M, wakati wapo watanzania wengi tu hiyo ni hela ya andazi asubuhi,

Sijui unapozungumzia kuliko yoyote unamlinganisha na nani!!?

Mbuzi tu, kapige kwata huko, kujitutumua tu wakati mnanuka mikopo mitupu!!
Arooo...arooo,mbona unareta fujo?Hebu piga magoti hapo uripo muraa!😂😂😂😂😂
 
Bado ushamba haujawatoka ,hasahasa hawa ambao hawana vyeo ,utakuta kwenye "Vibakuli" vyao kwenye dashboard ameweka kofia ya jeshi au kwenye kiti amevalisha kombati lake la jeshi yaani ujinga ujinga.

JWTZ ambaye ameenda shule huwa na nidhamu sana ,hawana mambo ya kijinga na mara nyingi hata hawataki watu wajue kama ni JWTZ ila hawa ambao "makuruti" wana mwembwe sana ,fujo nyingi ili mradi ujue kama yeye ni Mwanajeshi.

Kuna Mjeshi mmoja alikuwa ndani ya kibakuli akawa analeta mwembwe kwa dereva wa bodaboda ambaye alikuwa amempakiza mother mmoja hivi ,alivyoenda mbele akataka kumzingua yule bodaboda kisa ni JWTZ ,yule mother aliyebebwa alishuka akampiga bonge la biti ,akamwambia aache ujinga atamfukuzisha kazi mara moja na akamchana aache ushamba wa kuweka makoti kwenye viti vya gari ili kutisha raia(inaonekana yule mother ni kama mtu wa system ,msoja kumsoma yule mother ikabidi atulie mwenyewe) ,akamwambia ushwahi kumuona mwamnyange ameweka shati kwenye kiti cha gari? JWTZ alinywea mwenyewe

Bado ushamba haujawatoka ,hasahasa hawa ambao hawana vyeo ,utakuta kwenye "Vibakuli" vyao kwenye dashboard ameweka kofia ya jeshi au kwenye kiti amevalisha kombati lake la jeshi yaani ujinga ujinga.

JWTZ ambaye ameenda shule huwa na nidhamu sana ,hawana mambo ya kijinga na mara nyingi hata hawataki watu wajue kama ni JWTZ ila hawa ambao "makuruti" wana mwembwe sana ,fujo nyingi ili mradi ujue kama yeye ni Mwanajeshi.

Kuna Mjeshi mmoja alikuwa ndani ya kibakuli akawa analeta mwembwe kwa dereva wa bodaboda ambaye alikuwa amempakiza mother mmoja hivi ,alivyoenda mbele akataka kumzingua yule bodaboda kisa ni JWTZ ,yule mother aliyebebwa alishuka akampiga bonge la biti ,akamwambia aache ujinga atamfukuzisha kazi mara moja na akamchana aache ushamba wa kuweka makoti kwenye viti vya gari ili kutisha raia(inaonekana yule mother ni kama mtu wa system ,msoja kumsoma yule mother ikabidi atulie mwenyewe) ,akamwambia ushwahi kumuona mwamnyange ameweka shati kwenye kiti cha gari? JWTZ alinywea mwenyewe!
#**Safi Sana.... Heshima lazima iwepo.
Sio kujitia miungu watu, watu wengine bhana.. 🤷
 
JWTZ bado baadhi wana ushamba sana, gari lenyewe la miaka ya 90 ndio anafanyia watu dharau

Ulimbukeni tu,haya maisha ukikaa utafakari ndio maana baadhi ya watu hawapewi maisha mazuri, Mungu anajuaga kabisa

hilo la 90 baba yako analo, bado hata baiskeli huna
 
Habari zenu ndugu,

Kutoka Dar, askari wa JWTZ apandishwa Kizimbani Kwa Kukaidi Amri Halali ya Askari Trafiki wakati akitekeleza Wajibu wake.

Hii safi sana, lazima ieleweke kwamba utii wa Sheria bila shurti ni Kwa Kila raia bila kujali hadhi wala vyeo.

Askari Jeshi hasa JKT mara nyingi Huwa wanapiga raia hivyo na kujifanya wao wako Juu ya Sheria na Wana Haki sana kuliko raia wengine.

Kazi iendelee

==============

ASKARI wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ ) amepandishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam akikabiliwa na mashitaka ya kukataa amri halali ya askari wa usalama barabarani.

Imedaiwa Mahakamani leo, kuwa MT 89487 CPL Hamis Ramadhan alishindwa kusimamisha gari yake katika kivuko cha watembea kwa miguu eneo la Mlimani City, barabara ya Survey.

Wakili wa Serikali, Vailet Kyendesa ameiambia Mahakama kuwa Ramadhani akiwa akiiendesha gari binafsi T 433 ALB Nissan Patrol alikaidi amri ya kusimamisha gari na kujaribu kumsukuma askari wa usalama barabarani kwa gari lake.

Mshitakiwa amekana mashitaka na upande wa mashitaka umedai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

#HabarileoUPDATES
Ule ushahidi wa video ni rahisi kuukana, plate namba zimeeditiwa zile
 
JWTZ bado baadhi wana ushamba sana, gari lenyewe la miaka ya 90 ndio anafanyia watu dharau

Ulimbukeni tu,haya maisha ukikaa utafakari ndio maana baadhi ya watu hawapewi maisha mazuri, Mungu anajuaga kabisa
Mimi trafiki nikipata chance ya kumtengua kiuno na kukimbia nitafanya hivyo.., yaani ni waonevu sijapata ona.., acha tu
 
Unaita watu takataka ? Mimi nimezaliwa jeshini na ninaandika hapa nikiwa kambini, hawana pesa

Angekuwa na pesa asingeendesha hilo li Nissan la miaka ya 90
Nissan kama hizo bei yake mil 7 yametumika watu hawayataki kakopa kalinunua anadharau watembea Kwa miguu
 
Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ ), MT 89487 CPL Hamis Ramadhan (36) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam akikabiliwa na shitaka la kukataa amri halali.

Mshitakiwa huyo amesomewa kosa lake na Wakili wa Serikali, Vailet Kyendesya mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Rahim Mushi, Vailet amedai Februari 07,2023 Mshtakiwa akiwa eneo la Mlimani City Barabara ya Survey, Kinondoni, Dar es Salaam akiendesha gari namba T. 433 ALB Nissan Patrol alisimamishwa eneo la kivuko cha watembea kwa miguu na Askari Polisi ambapo alikaidi na kuanza kumsukuma Askari kwa gari yake.

Kyendesya alidai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo anaiomba Mahakama kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa, baada ya kusomewa shtaka hilo Mshtakiwa alikana makosa yake na kuachiwa kwa dhamana, ambapo kesi imehairishwa hadi March 6, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Itakumbukwa Feb 10,2023 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Jumanne Sagini aliliagiza Jeshi la Polisi kumkamata na kumchukulia hatua Dereva wa gari aina ya Nissan Patrol aliyeonekana kwenye video iliyosambaa mitandaoni akikaidi amri ya kusimama iliyotolewa na Askari wa usalama barabarani.
Inamaana waziri asingesema, ndio ingeisha hivyo !
 
Mwisho wa yote watayamaliza..hawa polisi na wanajeshi huwa hawapendani lkn wakikaa meza moja wanayamaliza

Huyo waziri ameongea tu kisiasa ili aonekane anafanya kazi lkn ukweli ni kwamba meno hayaumani
 
Mwisho wa yote watayamaliza..hawa polisi na wanajeshi huwa hawapendani lkn wakikaa meza moja wanayamaliza

Huyo waziri ameongea tu kisiasa ili aonekane anafanya kazi lkn ukweli ni kwamba meno hayaumani
Kuna jamaa jwtz tulikuwa naye tunalewa si akaanza ushamba kutukana watu , alichezea kichapo kutoka kwa Magereza, kesho yake issue ilimalizwa mezani jamaa akiwa na bandeji

Magereza alijitetea kwa afande wake "ni mambo ya pombe mimi sikumbuki chochote" 🤣
 
Unaita watu takataka ? Mimi nimezaliwa jeshini na ninaandika hapa nikiwa kambini, hawana pesa

Angekuwa na pesa asingeendesha hilo li Nissan la miaka ya 90
Majeshi yetu na serikali ya walamba asali ya miaka 60 Bado hawana mishahara inayotosha kuendesha maisha yao bila kutegemea kwenda Nje kulinda waporaji wa Rasilimali za bara la Afrika wanajificha chini ya mwavuli wa UN.

Kama nchi za Afrika zinagekua na amani hakika serikali nyingi zingepinduliwa mana serikali nyingi haziwalipi mishahara hata Moja ya Kumi ya mishahara ya wanasiasa.
Hii ni hatari sana. Ukiona mwanajeshi au Polisi ana maisha mazuri basi ujue ni Kwa sababu ya kazi za kulinda nchi nyingine lakini sio nchi yake . Kwenye nchi nyingine wanaonufaika sio waafrika Bali ni Majangili ya kimataifa huku waafrika wakiwa wanaachiwa Silaha za kuuana. Wanalindwa waporaji.

Afrika Ina laana Fulani inayotokana na ubaguzi na ubinafsi.
 
Back
Top Bottom