Pre GE2025 Askofu Bagonza: Madai ya mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi yasimilikiwe na chama chochote

Pre GE2025 Askofu Bagonza: Madai ya mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi yasimilikiwe na chama chochote

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
"Si dalili njema kuona vijana wengi wameanza kushabikia uongozi wa kibabe (Trump na Traore) huku wakibeza demokrasia. Na wengine wengi wanamkumbuka JPM na kutamani arudi. JPM alikuwa na mazuri yake lakini si katika eneo hili la demokrasia na utawala bora. Tushtuke na Tuamke. Madai ya mabadiliko ya mfumo wa chaguzi zetu yasimilikiwe na chama chochote bali watu wote wenye mapenzi mema na taifa letu."

Pia soma
- Pre GE2025 - Askofu Bagonza: Naogopa kuamini ahadi za uchaguzi za Rais Samia sababu hazina misingi ya kisheria na kikatiba
Lakini Je Chama cha Queen Sendiga kinawezaje kudai mfumo wa haki wa Uchaguzi?
 
Kwani ni nini 😂😁 siasa na dini ni mafuta na maji.
Pale unapochang'anya siasa na Dini , haiwezi kuwacha salama.
Angalia enzi za Yesu, ilibidi walimu wa dini waungane na wanasiasa wa serikali ya kirumi kumwangamiza Yesu. Very soon, Hata USA, sasa dini-dhehebu wamepewa ofisi kule white House, subiri utasikia bomu litakavyolipuka maana jambo hili haliwezi kuwacha salama.
 
Uaskofu sio cheo cha kiutawala, bali ni utumishi wa kanisa. Usichanganye utawala na huduma.
Ahahahahaha! Maaskofu wa Kanisa Moja Katoliki la Mitume uchaguliwa moja kwa moja na Papa. Na anatakiwa kustaafu akifikisha miaka 75.

Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheli Tanzania (KKKT) hupigiwa kura kila baada ya muda fulani. Jimbo la Kaskazini Magharibi limekuwa na Maaskofu wawili ambao ni Askofu Mstaafu Buberwa na Askofu wa Sasa Askofu Keshomshahara! Yeye Askofu Bagonza, yupoooo!!!
 
Pale unapochang'anya siasa na Dini , haiwezi kuwacha salama.
Angalia enzi za Yesu, ilibidi walimu wa dini waungane na wanasiasa wa serikali ya kirumi kumwangamiza Yesu. Very soon, Hata USA, sasa dini-dhehebu wamepewa ofisi kule white House, subiri utasikia bomu litakavyolipuka maana jambo hili haliwezi kuwacha salama.
Me nawaambia watu awaelewi najua wataelwa siku moja kuwa haya mambo ayatakiwa
 
Mwambie Yule Jamàa wa KAWE aliyeahidi kupeleka Watu Ulaya......
Dini na siasa aviingiliani me naona kamchezo sikuizi kamezuka viongozi wa dini wanaanza kujipa ujiko badala ya kutangaza ufalme wa Mungu na wengi wameenda mbali na kuanza promotion za vyama vya siasa.

Sasa hao waumini utawahubiri nini hilo litakua kanisa au pango la matapele.

Akili za kuambiwa changanya na zako
Usitafute references wakati mambo yanaonekana bayana tena kwa akili ya mchunga mbuzi.

🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Dini na siasa ni mafuta na maji tusijaribu kumixx by YAs 😂😂😁
 
Back
Top Bottom