LGE2024 Askofu Bagonza: Nawaomba radhi niliowahamasisha ili waende wakajiandikishe kupiga kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Jitahidi kuvumilia ukweli. Huu ushenzi mnaofanya kwenye chaguzi za nchi hii lazima wanaojitambua waukemee.
 
Katika andiko lake lenye kichwa cha habari, “Mashindano ya Kujaza Fomu: CCM Mshindi. Mpeni Maua Yake,”

Anasema, kama ni kushindana kujaza fomu nyingi za uchaguzi CCM wameshinda kabla ya kuchaguliwa.

“Mwaka 2019 tulitangaziwa kuna uchaguzi. Likawa shindano la kujaza fomu. CCM wakashinda. Wapinzani wakarudi darasani kujifunza kujaza fomu.”

Anasema; Mwaka huu tumetangaziwa tena lakini idadi ya waliojiandikisha imeonekana kuwa kubwa kuliko idadi halisi ya wapiga kura,

“Wakaandikishwa hata watakaofikisha miaka 18 miaka 5 ijayo. Idadi ya waliojiandikisha ikazidi ya wapiga kura. Tanzania tuna miujiza kweli.”

“Ukimwonya nduguyo ili afunike uchi wake akakataa, jiunge na wanaomcheka”. Sasa nacheka.

“Nimalize tafakuri yangu kwa kuwaomba radhi wote niliowahamasisha kwenda kujiandikisha ili wapige kura, nilidanganywa nami nikawadanganya, sitarudia tena".

"Mungu wetu ana kazi kweli kweli. Mwizi wa Kura anaomba Mungu afanikiwe kuiba, lakini Mungu hadhihakiwi. Ninaipenda nchi yangu hata kama kuna wanaonilazimisha niichukie. Hata mkiniteka, siichukii nchi yangu” Dkt. Benson Bagonza.
 
Ukweli utatuweka huru, sasa nafikiri huu mchezo tuuite Saa100 ujazaji fomu festivals
 
Huyu Askofu ndiye pekee anae haribugi kura kwa makusudi kwenye chaguzi za mkuu wa kanisa la KKKT nchini. Huwa anatamani awe yeye ila ndiyo hivyo tena hakubaliki ni moshi mweusi tu 🤣

Huwa anakasirika sana, na hua anahisi anadhulumiwa na huwa anatamani sana uchaguzi wa Askofu mkuu wa kanisa la KKKT Tanzania usimamiwe na BAKWATA au Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania. Huwa hawaamini kabisa wasimamizi wa kanisa. Sifahamu kama kweli anamuamini hata Mungu 🤣

Baadhi ya Maaskofu wenzake humpamba kweli, kwamba yeye ndie anastahili kua Askofu mkuu wa KKKT Tanzania, Lakini wakifika kwenye uchaguzi wala hakuna alie na habari nae.

Mara nyingine husingizia ana safari ya ghafla mara tu baada ya kupiga kura ambayo huiandika madudu anayojua yeye ili tu kura hiyo iharibike.

Ana gubu na viongozi wa kuu wa kanisa lake, Lakini pia ana gubu na jinsi ambavyo serikali sikivu ya CCM inavyopeleka Maendeleo kwa wananchi kwa kasi ya ajabu...

Actually,
Anakubalika sana Karagwe na kwenye baadhi ya mitandaoni ya kijamii. Nje na hapo ni useless tu 🤣
 
Huyu askofu anajitambua sana, sio wale machawa sijui manabii hovyo kabisa!
 
Wewe wakupuuza
 
Kwani wewe mpumbavu, jambazi akiingia nyumbani kwako kufanya uhalifu ni sahihi, majirani wamuache TU aifanye atakavyo!?
 
Mjukuu wangu wa kike anataka kuwa kama Ph.D Bagonza.
Hakika tumbo lililombeba huyu Askofu lilibeba kitu chema na limebarikiwa sana.
Mungu wa Mbinguni endelea kumbariki Askofu Bagonza zaidi na zaidi.
Amen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…