Jitahidi kuvumilia ukweli. Huu ushenzi mnaofanya kwenye chaguzi za nchi hii lazima wanaojitambua waukemee.Kwa hiyo huyo askofu alitaka fomu zisihahakiwe? Aache serikali ifanye kazi yake, km kazi ya uaskof imeshinda na anaona siasa ni rahisi aache uaskofu aingie kwenye siasa. Hv viongozi wa dini wanawashwa na nini mbn serikali hawaingilii wakifanya mapuuzi yao makanisani.
Ukweli utatuweka huru, sasa nafikiri huu mchezo tuuiteKatika andiko lake lenye kichwa cha habari, “Mashindano ya Kujaza Fomu: CCM Mshindi. Mpeni Maua Yake,”
Anasema, kama ni kushindana kujaza fomu nyingi za uchaguzi CCM wameshinda kabla ya kuchaguliwa.
“Mwaka 2019 tulitangaziwa kuna uchaguzi. Likawa shindano la kujaza fomu. CCM wakashinda. Wapinzani wakarudi darasani kujifunza kujaza fomu.”
Anasema; Mwaka huu tumetangaziwa tena lakini idadi ya waliojiandikisha imeonekana kuwa kubwa kuliko idadi halisi ya wapiga kura,
“Wakaandikishwa hata watakaofikisha miaka 18 miaka 5 ijayo. Idadi ya waliojiandikisha ikazidi ya wapiga kura. Tanzania tuna miujiza kweli.”
“Ukimwonya nduguyo ili afunike uchi wake akakataa, jiunge na wanaomcheka”. Sasa nacheka.
“Nimalize tafakuri yangu kwa kuwaomba radhi wote niliowahamasisha kwenda kujiandikisha ili wapige kura, nilidanganywa nami nikawadanganya, sitarudia tena".
"Mungu wetu ana kazi kweli kweli. Mwizi wa Kura anaomba Mungu afanikiwe kuiba, lakini Mungu hadhihakiwi. Ninaipenda nchi yangu hata kama kuna wanaonilazimisha niichukie. Hata mkiniteka, siichukii nchi yangu” Dkt. Benson Bagonza.
View attachment 3155115
Saa100 ujazaji fomu festivalsMajinga yamekaa sehemu nyeti.Poleni Watanzania
Huyu Askofu ndiye pekee anae haribugi kura kwa makusudi kwenye chaguzi za mkuu wa kanisa la KKKT nchini. Huwa anatamani awe yeye ila ndiyo hivyo tena hakubaliki ni moshi mweusi tu 🤣MASHINDANO YA KUJAZA FOMU: CCM MSHINDI. Mpeni Maua yake.
Mwaka 2019 tulitangaziwa kuna uchaguzi. Likawa shindano la kujaza fomu. CCM wakashinda. Wapinzani wakarudi darasani kujifunza kujaza fomu.
Mwaka huu tukatangaziwa, safari hii ni UCHAGUZI KWELI. Tukainuka kuhamasisha watu wajiandikishe. Wakaandikwa hata watakaofikisha miaka 18 miaka 5 ijayo. Idadi ya waliojiandikisha ikazidi ya wapiga kura. Tanzania tuna miujiza kweli.
Ghafla, uchaguzi “ukahairishwa” tukarudi tena kwenye mashindano ya kujaza fomu. CCM wameshinda tena. Wapeni maua yao. Lakini:
1. Nduguyo akikukosea muonye mkiwa wawili. Akikataa, chukua shahidi ukaonye tena. Akikataa liambie kanisa. Akikatalia kanisa, achana naye. Mwone kama mmataifa na mtoza ushuru (Mathayo 18:16-18). CCT, TEC na Bakwata wamesema tayari. Hata wasioomba wanaomba!
2. Wanyambo wana hekima isemayo; “Ukimwonya nduguyo ili afunike uchi wake akakataa, jiunge na wanaomcheka”. Nipo nacheka utadhani mazuri!
3. Tumemaliza ibada Musoma. Tumempata Mkurya mmoja akawa Askofu. Kofia ilitaka kugoma kuingia kichwani tukatamani tutafute ya jeshi. Yesu “aliyemteka” Mkurya akatii, kuna siku atawateka wanaokaidi maonyo ya kanisa lake kuhusu taifa.
4. Mgeni rasmi Prof John Kabudi, katupiga darasa ibadani. Ilani nzima ya chama chake imefunika mpaka wengine tukaondoka bila kula mchele. Katujulisha habari za BWAWA la umeme. Ahsante Prof LAKINI..
5. Watanzania hawa wanatamani Bwawa kubwa la kuzalisha Demokrasia. Bwawa hilo litalinda Bwawa la Umeme. Bila demokrasia wanaohujumu SGR watahamia kwenye umeme.
6. Najiuliza: Waweza kuwa na taifa huru lisilo na watu huru? Na je waweza kuwa na watu huru katika taifa lisilo huru? Niliwahi jibu swali nikiwa darasa la sita, lisemalo “Afrika ni Bara Tajiri lenye watu maskini: Jadili kwa kutoa mifano. Majibu yangu yalisababisha nifukuzwe shule mwaka mzima. Apumzike kwa amani Mwalimu aliyenifukuza.
7. Nimalize tafakuri yangu kwa kutoa pole kwa wahanga wa Kariakoo. Nitoe pole kwa familia Mama Kibiki. Waliomuua “wameishakufa” hata kama wanatembea. Nitoe pole kwa wote walioenda kwenye uchaguzi wakaambulia mashindano ya kujaza fomu. Nitoe pole kwa wote wanaolazimika kucheka wakati moyoni wanatamani kulia.
Nawaomba radhi wote niliowahamasisha kwenda kujiandikisha ili wapige kura. Nilidanganywa nami nikawadanganya. Sitarudia tena.
Mungu wetu ana kazi kweli kweli. Mwizi wa Kura anamuomba afanikiwe kuiba. Mlinzi wa kura naye anakanyaga mafuta ili alinde kura zisiibiwe. Lakini HADHIAKIWI.
Naipenda nchi yangu hata kama kuna wanaonilazimisha niichukie. Hata mkiniteka, SIICHUKII NCHI YANGU.
Huyu askofu anajitambua sana, sio wale machawa sijui manabii hovyo kabisa!Katika andiko lake lenye kichwa cha habari, “Mashindano ya Kujaza Fomu: CCM Mshindi. Mpeni Maua Yake,”
Anasema, kama ni kushindana kujaza fomu nyingi za uchaguzi CCM wameshinda kabla ya kuchaguliwa.
“Mwaka 2019 tulitangaziwa kuna uchaguzi. Likawa shindano la kujaza fomu. CCM wakashinda. Wapinzani wakarudi darasani kujifunza kujaza fomu.”
Anasema; Mwaka huu tumetangaziwa tena lakini idadi ya waliojiandikisha imeonekana kuwa kubwa kuliko idadi halisi ya wapiga kura,
“Wakaandikishwa hata watakaofikisha miaka 18 miaka 5 ijayo. Idadi ya waliojiandikisha ikazidi ya wapiga kura. Tanzania tuna miujiza kweli.”
“Ukimwonya nduguyo ili afunike uchi wake akakataa, jiunge na wanaomcheka”. Sasa nacheka.
“Nimalize tafakuri yangu kwa kuwaomba radhi wote niliowahamasisha kwenda kujiandikisha ili wapige kura, nilidanganywa nami nikawadanganya, sitarudia tena".
"Mungu wetu ana kazi kweli kweli. Mwizi wa Kura anaomba Mungu afanikiwe kuiba, lakini Mungu hadhihakiwi. Ninaipenda nchi yangu hata kama kuna wanaonilazimisha niichukie. Hata mkiniteka, siichukii nchi yangu” Dkt. Benson Bagonza.
CCM wanaweza kumuua aseeHuyu askofu anajitambua sana, sio wale machawa sijui manabii hovyo kabisa!
Ni CCMNa bado tunadanganywa kuwa hawa wanaoteka watu ni "watu wasiojulikna" 😭 😭
Wewe wakupuuzaKwa hiyo huyo askofu alitaka fomu zisihahakiwe? Aache serikali ifanye kazi yake, km kazi ya uaskof imeshinda na anaona siasa ni rahisi aache uaskofu aingie kwenye siasa. Hv viongozi wa dini wanawashwa na nini mbn serikali hawaingilii wakifanya mapuuzi yao makanisani.
BENSON BAGONZA ndiyo ina sound vizuri tumeizoeaSurname ndio uhalisia wa mtu.
Yes ni kifua kipana amempa wajuu wa kutoshaMkwe si alimuita KIFUA KIPANA?!
Kauli inayompa ujasiri.
Kwani wewe mpumbavu, jambazi akiingia nyumbani kwako kufanya uhalifu ni sahihi, majirani wamuache TU aifanye atakavyo!?Kwa hiyo huyo askofu alitaka fomu zisihahakiwe? Aache serikali ifanye kazi yake, km kazi ya uaskof imeshinda na anaona siasa ni rahisi aache uaskofu aingie kwenye siasa. Hv viongozi wa dini wanawashwa na nini mbn serikali hawaingilii wakifanya mapuuzi yao makanisani.
Mjukuu wangu wa kike anataka kuwa kama Ph.D Bagonza.Anaandika Askofu Bagonza kwa masikitiko makubwa juu ya zoezi la uandikishaji wapiga kura, mchakato wa kuchukuwa fomu, kurudisha fomu hadi kuenguliwa wagombea wa vyama vya upinzani.
Mwaka 2019 tulitangaziwa kuna uchaguzi. Likawa shindano la kujaza fomu. CCM wakashinda. Wapinzani wakarudi darasani kujifunza kujaza fomu.
Mwaka huu tukatangaziwa, safari hii ni UCHAGUZI KWELI. Tukainuka kuhamasisha watu wajiandikishe.
Wakaandikwa hata watakaofikisha miaka 18 miaka 5 ijayo. Idadi ya waliojiandikisha ikazidi ya wapiga kura.
Tanzania tuna miujiza kweli. Ghafla, uchaguzi “ukahairishwa” tukarudi tena kwenye mashindano ya kujaza fomu. CCM wameshinda tena. Wapeni maua yao. Lakini:
1. Nduguyo akikukosea muonye mkiwa wawili. Akikataa, chukua shahidi ukaonye tena. Akikataa liambie kanisa. Akikatalia kanisa, achana naye. Mwone kama mmataifa na mtoza ushuru (Mathayo 18:16-18). CCT, TEC na Bakwata wamesema tayari. Hata wasioomba wanaomba!
2. Wanyambo wana hekima isemayo; “Ukimwonya nduguyo ili afunike uchi wake akakataa, jiunge na wanaomcheka”. Nipo nacheka utadhani mazuri!
3. Tumemaliza ibada Musoma. Tumempata Mkurya mmoja akawa Askofu. Kofia ilitaka kugoma kuingia kichwani tukatamani tutafute ya jeshi. Yesu “aliyemteka” Mkurya akatii, kuna siku atawateka wanaokaidi maonyo ya kanisa lake kuhusu taifa.
4. Mgeni rasmi Prof John Kabudi, katupiga darasa ibadani. Ilani nzima ya chama chake imefunika mpaka wengine tukaondoka bila kula mchele. Katujulisha habari za BWAWA la umeme. Ahsante Prof LAKINI..
5. Watanzania hawa wanatamani Bwawa kubwa la kuzalisha Demokrasia. Bwawa hilo litalinda Bwawa la Umeme. Bila demokrasia wanaohujumu SGR watahamia kwenye umeme.